MTIHANI WA PAMOJA WA MOKASA - Stluciekiriri.ac.ke

2y ago
769 Views
29 Downloads
449.53 KB
8 Pages
Last View : 9d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Alexia Money
Transcription

MTIHANI WA PAMOJA WA MOKASAJULAI - 2019KIDATO CHA NNE102/3KISWAHILI--Karatasi ya 3FASIHIJulai. 2019 - Muda: Saa 2 ½Jina . Nambari ya Mtahiniwa Sahihi . Tarehe .Maagizo:a) Andika jina lako na nambari yako ya usajili katika karatasi ya majibu uliyopewab) Jibu maswali manne pekee.c) Swali la kwanza ni la lazima.d) Maswali hayo mengine matatu yachaguliwe kutoka sehemu ya Riwaya, Tamthilia, Ushairi naFasihi Simulizi.e) Usijibu maswali mawili kutoka sehemu mojaf) Majibu yote lazima yaandikwe kwa lugha ya Kiswahili.g) Karatasi hii ina kurasa 8 zilizopigwa chapa.h) Watahiniwa ni lazima wahakikishe kwamba kurasa zote za karatasi hii zimepigwa chapasawasawa na kuwa maswali yote yamo.Kwa matumizi ya mtahini pekeeSwaliUpeo120220320420520620720820Jumla80 MTIHANI WA PAMOJA WA MOKASA 2019AlamaUk. wa 1

SEHEMU YA A: HADITHI FUPIAlifa chokocho na Dumu Kayanda: Tumbo Lisiloshiba1. Lazima“Doa ndio kawaida inayobainisha maisha ya mwanadamu.”Onyesha ukweli wa kauli hii kwamujibu wa hadithi za: Shogake Dada ana Ndevu, Mame Bakari, Shibe Inatumaliza naMtihani wa Maisha.(alama 20)SEHEMU YA B: RIWAYAAssumpta Matei: Chozi la HeriJibu swali la 2 au la 32. Alijiona kama mfa maji ambaye anakabiliwa na mtutumo wa mawimbi ya misiba, mmojabaada ya mwingine.(a) Bainisha muktadha wa dondoo hili.(alama 4)(b) Eleza sifa tatu za anayerejelewa katika dondoo hili.(alama 3)(c) Eleza tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili.(alama 2)(d) Fafanua masaibu yaliyomkumba mrejelewa.(alama 3)(e) Huku ukitolea mifano riwayani, jadili matatizo yanayowakumba wanajamii katika ndoa.(alama 8)3. Eleza ufaafu wa anwani Chozi la Heri. (alama 20) MTIHANI WA PAMOJA WA MOKASA 2019Uk. wa 2

SEHEMU YA C: TAMTHILIAPauline Kea: KigogoJibu swali la 4 au 54. “Hivi vishahada vyao wanavyovipata siku hizi vinawavimbisha vichwa!”(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.(alama 4)(b) Taja tamathali zozote mbili zinazojitokeza katika dondoo hili.(alama 2)(c) Eleza changamoto zilizomkabili mrejelewa na wenzake.(alama 14)5. Mwandishi wa Kigogo amefanikiwa sana katika matumizi yake ya mbinu ya jazanda nakinaya. Fafanua ukweli wa kauli hii kwa kurejelea tamthilia.(alama 20)SEHEMU YA D: USHAIRIJibu swali la 6 au 76. Ipo SikuJua la mashariki limezibwaNa machweo ya magharibiTukabaki kuhesabu sikuNa kila sekunde inayopitaIkilifyatua shaka jipyaAmbalo bado kidogoLitakuwa limeliua tumainiNa sumu yake kulipuka hadharaniUlimwengu ushuhudie.Ni upeo wa sayansi:Waundapo silaha MTIHANI WA PAMOJA WA MOKASA 2019Uk. wa 3

Mabomu ya masafa ya mbaliYanayomwaya yake mimwesoNa kutudonoaKama yule jogooWa radi.Ni upeo wa uhayawani:Tuundapo silahaMabomu ya masafa ya karibuAu zana za kukingia wao jogooAsitudonoe na kututia mautiniKatika yetu ardhiWalipoishi na kuzikwa wetu wahenga.Ni udikteta sisi kuongozana vibayaNi udikteta viongozi kuwaua wapinzaniNi unyama watu kupigwa risasiNi unyama wananchi kuteswaLakiniNi demokrasia wao kutuvamiaNa yetu ardhi kukaliaNi demokrasia kuwaua viongozi wetuPamoja na wananchi kwa yao makomboraYenye kiu ya damu yetu.Ni haki kutukatia mifereji ya majiTukanyauka na kujifia kama vipandoKatika majira magumu ya ukame?Ni utu kuwatesa watoto wetuWaliojisabilia kuipigania nchi katika ushinde MTIHANI WA PAMOJA WA MOKASA 2019Uk. wa 4

Katika ardhi hii tulopawaNaye Mola Moliwa?Lakini fahamuni:Tofauti kati ya hadithi fupi na ndefuNi kuwa ndefu huchukua mrefu wakati kuishaNa ile fupi huchukua muda mfupiZote lakini zina miishoNa hii nayo ipo sikuUkingoni itafikaHatimaye watoto wetu wapate tenaJioni kuitamaniJioni isiyo na mimwesoMimweso ya kutishia wao uhaiNa mingurumo na mirindimoYa kutangaza yao maangamizo!Najua sitokuwepo hili kushuhudiaLakini kwangu itakuwa si kituMuhimu ni wajukuu wafahamishweKuwa hapa nilipita na kushuhudiaBinadamu akiutekeleza unyamaAlioupindua juu chini, nje ndaniKama funzo la demokrasiaKwa ulimwengu kipofu! MTIHANI WA PAMOJA WA MOKASA 2019Uk. wa 5

Maswali(a) Eleza toni ya shairi hili.(b) Taja na kueleza nafsi – neni katika shairi hili.(c) Jadili matumizi ya mbinu zifuatazo katika shairi hili.(alama 1)(alama 2)(i) Kinaya(alama 3)(ii)Usambamba(alama 3)(iii)Jazanda(alama 3)(d) Andika ubeti wa mwisho kwa lugha nathari.(e) Eleza muundo wa shairi hili.(alama 4)(alama 4)7. INSANI TWAJILAANIYa wapi silika hino, ya kwenda kinyumenyume?Nilijibu hata kwa wino, majibuyo niyasome,Kuno ‘geuza maneno, na kuyafanya maleme,Haramu kuwa halali, insani twajilaani.Insiya jilaani, ni bora wazi niseme,Kukubalia idhini, mimba wakazikateme,Hiyo nayo haki gani, wasiyoona mit ume,Haramu kuwa halali, insani twajilaani.Twajilaani laana, kijitakia ujume,Nayo habari hatuna, twajiletea ukame,Pia habari hatuna, ni wana sio vimeme, MTIHANI WA PAMOJA WA MOKASA 2019Uk. wa 6

Haramu kuwa halali, insani twajilaani.Muswada siyo halali, wakuviavya vikembe,Utawapea halali, mabinti wetu watambe,Magulamu ja fahali, nao wakame pembe,Haramu kuwa halali, insani twajilani.Kuavya mimba ni dhambi, ya kumuudhi Rahimu,Laana twajaza tumbi, ya moto wa jahanamu,Tuache vino vitimbi,turudie utimamu,Haramu kuwa halali, insani twajilani.Jambo hili nawambia, litazidisha ukware,Ni ya uvundo tabia, ni afueni tuisare,Tuweze kuitubia, tuwache zino parare,Haramu kuwa halali, insani twajilani.Muida ndio sinao, nina mengi ya kusema,Wapigania hakio, zingatia nayosema,‘sipashe mswada huo , ni madhambi ya kuchoma,Haramu kuwa halali insani twajilani. MTIHANI WA PAMOJA WA MOKASA 2019Uk. wa 7

MASWALIa) Eleza dhamira ya mtunzi wa shairi hili(alama 1)b) Eleza muundo wa shairi hili(alama 4)c) Kwa kutolea maelezo mwafaka,tambua bahari tatu katika shairi hili(alama 3)d) Eleza tamathali mbili za usemi zinazojitokeza katika shairi na utolee ithibati(alama 2)e) Onyesha jinsi idhini ya mtunzi ilivyotumika kutimiza arudhi katika shairi hili (alama 4)f) Bainisha toni ya shairi hili(alama 1)g) Tambua maudhui mawili yanayotawala shairi hili(alama 2)h) Tambua madhara matatu ya uavyaji mimba( alama 3)SEHEMU YA E: FASIHI SIMULIZI8. Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.Mtu A: Tulienda kwa hiyo sherehe jana Mtu B: Ooh! Kumbe ulipata ngiri mbili za kiingilio?Mtu A: Nilivaa chupa woiyee!Mtu B: Ulimuona yule kijana Kamba?Mtu A: Hehehe! Yule huringa mbaya Mtu B: Huyo alitoka mbio aliposikia kumethuka Maswali(a) Tambua kipera cha utanzu wa semi kinachohusishwa na kifungu hiki.(alama 1)(b) Fafanua umuhimu wa kipera hiki.(alama 5)(c) Ngomezi ni nini?(alama 2)(d) Jadili sababu ambazo zimesababisha kuzorota kwa matumizi ya ngomezi katika jamii yakisasa.(e) Jadili sifa za sogora zinazojitokeza nyanjani wakati wa utafiti. MTIHANI WA PAMOJA WA MOKASA 2019(alama 6)(alama 6)Uk. wa 8

Alifa chokocho na Dumu Kayanda: Tumbo Lisiloshiba 1. Lazima “Doa ndio kawaida inayobainisha maisha ya mwanadamu.”Onyesha ukweli wa kauli hii kwa mujibu wa hadithi za: Shogake Dada ana Nd

Related Documents:

MTIHANI WA PAMOJA WA SHULE ZA EKSIKA Hati ya kuhitimu kisomo cha sekondari Kenya(K.C.S.E) MAAGIZO: a) Jibu maswali yote. b) Andika majibu yote katika nafasi zilizoachwa. c) Karatasi hii ina alama 30. d) Hakikisha kurasa zote zimepigwa chapa. Swali Upeo Alama Ufahamu 15 Ufupisho 15 Lugha 40 Isimu Jamii 10 Jumla 80

MTIHANI WA PAMOJA WA SHULE ZA UPILI WILAYANI MAKINDU, 2014 Kenya Certificate of Secondary Education (K.C.S.E) MAAGIZO KWA MTAHINIWA . Urafiki wa namna hii ndio uletao baraka ya Mungu, kuwashukia viumbe hao kama umande wa asubuhi. Urafiki ni lazima sana katika maisha ya wanadamu. Urafiki ni mfano wa mishipa ipitishayo damu

MTIHANI WA PAMOJA -MECS 2021 Jina: _ Nambari ya mtahiniwa:_Darasa: _ Tarehe: _ Sahihi: _ 102/2 Kiswahili Karatasi ya 2 Muhula wa Pili - 2021 Muda: Saa 2½ . kweli kwamba sera ya elimu bila malipo katika shule za msingi nchini humu inaendelea kutekelezwa. Hata hivyo, asilimia ya watoto na hata watu wazima wasiojua kusoma na .

JARIBIO LA TATHMINI YA PAMOJA MTIHANI WA CEKENAS MUHULA WA PILI MWAKA 2015 Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari KISWAHILI INSHA KARATASI YA KWANZA MUDA: SAA 1 ¾ MAAGIZO 1. Andika insha mbili. 2. Insha ya kwanza ni ya lazima. 3. Chagua insha nyingine moja kutoka hizo tatu zilizosalia. 4. Kila insha isipungue maneno 400 5. Kila insha ina alama 20.

2015 Mtihani wa Tathmini eneo la Bondo 102/1 Insha Fungua ukurasa 102/1 KISWAHILI Karatasi ya 1 Julai/Agosti - 2015 MUDA: SAA 1 ¾ MTIHANI WA KUTATHIMINI WILAYA YA BONDO - 2015 . Ardhi ndiyo chanzo cha riziki zote. Fauka ya hayo, ardhi ni dafina kubwa. . Fupisha aya ya kwanza kwa maneno 50.

4.0 KISWAHILI (102) 4.1 MATOKEO YA MTIHANI WA SOMO LA KISWAHILI Jedwali hili linaonyesha matokeo ya mtihani wa somo la Kiswahili katika muda wa miaka minne (2005 hadi 2008). Jedwali 6: Matokeo ya mtihani wa Kiswahili (2005 - 2008) Mwaka Karatasi Watahiniwa Alama ya Juu Alama ya Wastani Alama ya Tanganisho 2005 1 2 3 Jumla 259,301 40 80

FASIHI Julai / Agosti 2018 Muda: Saa 2½ MTIHANI AW MWISHO AW MUHULA AW PILI Kidato cha Nne KISAW HILI Karatasi - 102/3 Julai / Agosti 2018 Muda : Saa 2½ MAAGIZO 1. Jibu maswali MANNE pekee. 2. Swali la KWANZA ni la LAZIMA. 3. Kisha chagua maswali mengine matatu kutoka sehemu zilizobakia; yaani Riwaya, Hadithi Fupi, na Ushairi 4.

EMC Overview 43 Immunity Issues Can Exist Due To The Following Most of today’s electrical and electronic systems rely on active devices such as microprocessors and digital logic for: –Control of system functions. –User convenience / features. –Legislated system requirements (such as mobile telephone location reporting). With today’s vast networks for data communication there .