MTAZAMO WA JAMII JUU YA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO

2y ago
327 Views
5 Downloads
786.45 KB
116 Pages
Last View : 1d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Matteo Vollmer
Transcription

MTAZAMO WA JAMII JUU YA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO 2014KUHUSU KUTUMIA KISWAHILI KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIAELIMU YA JUU KATIKA VYUO VYA KATIVEDASTUS LUSATO GEREMU MUNUBI AMBROSETASNIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SEHEMU YAMASHARTI YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI YA KISWAHILIYA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA2018

iiUTHIBITISHINiliyetia saini hapa chini ninathibitisha kuwa nimesoma tasnifu hii iitwayoMtazamo wa Jamii Juu ya Sera ya Elimu na Mafunzo 2014 Kuhusu KutumiaKiswahili Kufundishia na Kujifunzia Elimu ya Juu katika Vyuo vya Kati nakupendekeza ikubaliwe kwa utahini na Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania kwa ajili yakutimiza sehemu ya Masharti ya kutunukiwa Shahada ya Uzamili ya Kiswahili yaChuo Kikuu Huria Cha Tanzania. . Sheikh, Profesa, Dkt. T. Y. M. K. S. Sengo(Msimamizi) Tarehe

iiiHAKIMILIKIHairuhusiwi kuiga au kunakili kwa namna yoyote ile tasnifu hii kwa njia yoyotekama vile kielektroni, kurudufu nakala, kurekodi au kwa njia yoyote nyinginebilaidhini ya mwandishi au Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania kwa niaba

ivTAMKOMimi, Vedastus Lusato Geremu Munubi Ambrose, nathibitisha kuwa tasnifu hii nikazi yangu halisi na haijawahi kuwasilishwa katika Chuo Kikuu kingine chochotekwa ajili ya kutunukiwa Shahada kama hii au nyingine yoyote. Saini .Tarehe

vTABARUKUNatabaruku kazi hii kwa mke wangu Getrude Migani Makene pamoja na wananguGodwin Munubi, Prosper Makene, Ezekiel Nago, Gladness Nakataga na NelsonGunje.

viSHUKURANIKazi hii ni matokeo ya jitihada zangu binafsi pamoja na michango ya watu wengine.Sina budi kutoa japo neno la shukuranikwa wale wote walionishika mkono nakuniongoza katika safari hii ndefu katika uwanja huu wa taaluma.Awali ya yote, ninatoa shukurani zangu za pekee kwa Mwenyezi Mungu ambayeamekuwa ni msaada mkubwa sana kwangu tangu nilipoanza kazi hii hadi kukamilikakwake. Ameniongoza na kunijaalia afya njema katika safari hii iliyojaa vikwazovingina amenifanikishia ndoto yangu ya miaka mingi ya kupata shahada ya Uzamilikatika Kiswahili.Pili, ninatoa shukurani zangu za dhati kwa msimamizi wangu Sheikh, Profesa, Dkt,T.Y.M.K.S. Sengo kwa uongozi, uelekezaji, ukosoaji, ushauri na uvumilivu wakeambao umekuwa chachu ya kukamilisha kazi hii. Kwa hakika amenisaidiasana,amenijenga na kunikomaza kitaaluma na kitaalamu.Tatu, shukurani zangu ninazitoa kwa Maprofesa na wahadhiri wote walionifundishana kuniandaa kitaaluma hadi nikaweza kupata stadi za kuniwezesha kuikabili kazihii. Shukurani hizi ni kwa Prof. James Mdee, Dkt. Elsifa Zelda, Dkt.HannaSimpassa, Dkt Ligembe, Dkt. Kishe na Dkt. Hadija Jilala bila kuwasahau kina Dkt.Hokororo, Mwalimu Sostenes Raphael Mashinji wa Chuo cha Ualimu Butimba.Nne, nimshukru mke wangu Getrude Migani Makene pamoja na wanangu GodwinMunubi, Prosper Makene, Ezekiel Nago, Gladness Nakataga na Nelson Gunje kwa

viisala na maombi yao pamoja na uvumilivu waliouonesha wakati wote walipokosaupendo wangu kutokana na kuhudhuria masomo ya kozi ya Uzamili.Tano, shukurani zangu za dhati zimwendee Bwana Nteminyanda Kisabo kwa ushauriwake na kujitolea kwake muda wa kuchapa kazi hii tangu hatua za awali hadikukamilika kwake.Sita, nawashukuru wanafunzi wenzangu tuliokuwa nao katika safari ya kitaaluma2015 / 2016 katika Chuo Kikuu Huria chaTanzania. Nimefaidika na ushirikiano waonamichango yao imekuwa chachu katika kufanikisha kazi hii.Mwisho, ninatoa shukurani kwa uongozi wa vyuo vya CBE na ADEM pamoja nawanafunzi wote walioshiriki katika utafiti huu.

viiiIKISIRIUtafiti huu ulilengakuchunguza mtazamo wa jamii juu ya Sera ya Elimu na Mafunzo2014 kuhusu matumizi ya Kiswahili katika kufundishia na kujifunzia katika vyuo vyakati. Utafiti huu ulikuwa na madhumuni mahsusi matatu ambayo ni kubaini tamko lasera ya elimu kuhusu matumizi ya Kiswahili kama lugha ya kufundishia, Kubainishachangamoto za utekelezaji wa sera ya Elimu kuhusu matumizi ya Kiswahili kama lughaya kufundishia, Kutoa mapendekezo juu ya utekelezaji wa sera ya elimu kuhusumatumizi ya Kiswahili kama lugha ya kufundishia.Utafiti huu umeongozwa nanadharia ya kijamii na utekelezaji. Utafiti huu ulifanywa katika wilaya zaNyamaganana Ilemela katika vyuo vya CBE na ADEM kwa kutumia watafitiwa 95waliosailiwa na kujibu maswali. Watafitiwa waliteuliwa kwa kuzingatia kigezo chanasibu na makusudi.Mbinu ya utafiti iliyotumika katika kukusanya data ilikuwa niusaili, hojaji na utalii wa machapishi.Uchambuzi wa data zilizokusanywa umefanyikakwa kutumia mkabala wa kimaelezo na kitakwimu.Matokeo ya utafiti yanaoneshakuwa lugha ya Kiswahili inakidhi vigezo vyote vya kutumika kama lugha yakufundishia na kujifunzia elimu katika vyuo vya kati. Matumizi ya lugha inayotumiwana wazungumzaji wengi inaweza kuwa ni nyenzo muhimu katika kuinua ubora waelimu itolewayo katika vyuo hivyo. Kutotumika kwa lugha ya Kiswahili kufundishiaelimu nchini Tanzania hakuwasaidii wanafunzi kufikia viwango vinavyotakiwa. Aidha,hakusaidii kuendeleza vipaji na ubunifu wa wanafunzi katika kuikuza lugha yaKiswahili ili iendane na mahitaji ya kutumika kufundishia na kujifunzia elimu ya kati.

ixYALIYOMOUTHIBITISHI . iiHAKIMILIKI . iiiTAMKO . ivTABARUKU . vSHUKURANI . viIKISIRI . viiiORODHA YA MAJEDWALI . xiiiSURA YA KWANZA . 11.0UTANGULIZI . 11.1Utangulizi . 11.2Usuli wa Mada . 11.3Tatizo la Utafiti . 51.4Makusudio ya Utafiti. 61.4.1 Lengo Kuu . 61.4.2 Madhumuni Mahsusi. 61.4.3 Maswali ya Utafiti . 61.5Umuhimu wa Utafiti . 71.6Mawanda ya Utafiti . 71.7Mipaka ya Utafiti . 81.8Vikwazo vya Utafiti . 81.9Mpangilio wa Tasnifu . 91.10Hitimishi. 9

xSURA YA PILI . 112.0UTALII WA MACHAPISHI NA MKABALA WA KINADHARIA . 112.1Utangulizi . 112.2Utalii Kuhusu Lugha ya Kufundishia na Kujifunzia Katika Elimu . 112.3Utalii wa Sera ya Lugha . 142.3.1 Lugha Rasmi ya Kufundishia na Kujifunzia Tanzania . 152.3.2 Sera ya Lugha ya Afrika Kusini . 202.3.3 Sera ya Lugha ya Ghana . 212.4Utalii waUtafiti Uliyokwishafanyika . 222.5Pengo la Maarifa . 322.6Mkabala wa Kinadharia . 322.6.1 Nadharia ya Kijamii . 332.6.2 Nadharia ya Utekelezaji . 342.7Hitimisho . 37SURA YA TATU . 393.0MBINU ZA UTAFITI . 393.1Utangulizi . 393.2Mpango wa Utafiti . 393.3Eneo la Utafiti . 393.4Kundi Lengwa . 403.5Usampulishaji na Mbinu za Usampulishaji . 403.5.1 Usampulishaji. 403.5.2 Mbinu za Usampulishaji . 413.6Aina za Data Zilizo Kusanywa . 42

xi3.6.1 Data za Msingi . 433.6.2 Data za Upili . 433.7Mbinu za Utafiti . 433.7.1 Mbinu za Kukusanya Data . 433.7.2 Mbinu za Uchambuzi wa Data . 453.8Maadili ya Utafiti . 463.9Hitimishi. 46SURA YA NNE . 474.0UWASILISHAJI NA UCHAMBUZI WA DATA . 474.1Utangulizi . 474.2Sera ya Lugha ya Elimu na Mafunzo Kuhusu Kiswahili Kama LughaKufundishiana Kujifunzia . 474.2.1 Uelewa wa Wadau wa Elimu Kuhusu Tamko la Kutumia Lugha yaKiswahili . 494.2.2 Uwazi wa Sera Kuhusu Matumizi ya Lugha ya Kiswahili Kufundishia naKujifunzia. 524.3Changamoto za Utekelezaji wa Sera . 534.4Mapendekezo . 624.4.1 Mchango wa Lugha ya Kiingereza katika Kufundishia na Kujifunzia . 624.4.2 Manufaa ya Kutumia Lugha ya Kiswahili katika Kufundishia naKujifunzia . 664.4.3 Athari ya Kutotekelezwa kwa Matamko ya Sera ya Elimu na Mafunzo Juu yaMatumizi ya Lugha ya Kiswahili Kufundishia Vyuo vya Kati. 684.4.4 Changamoto za Utekelezaji Tamko la Sera ya Elimu juu Yamatumizi ya Lughaya Kiswahili Kufundishia na Kujifunzia Vyuo vya Kati . 71

xii4.5Hitimishi. 75SURA YA TANO . 765.0MUHTASARI, HITIMISHI NA MAPENDEKEZO . 765.1Utangulizi . 765.2Muhtasari Kuhusu Utafiti. 765.3Matokeo ya Utafiti . 785.4Mapendekezo . 805.5Maeneo Yanayohitaji Utafiti Zaidi . 825.6Hitimishi. 83MAREJELEO . 84VIAMBATANISHO . 91

xiiiORODHA YA MAJEDWALIJedwali 3.1:Idadi ya Uteuzi wa Watafitiwa . 42Jedwali 4.1:Maoni ya Watafitiwa Kuhusu Tamko la Kutumia Lugha yaKiswahili . 49Jedwali 4.2:Majibu Yaliyotolewa na Watafitiwa Waliosema Wamesoma AmaKusikia Tamko la kutumia Lugha Kiswahili . 50Jedwali 4.3:Uwazi ya Sera ya Elimu Kuhusu Lugha ya Kiswahili Kufundishia naKujifunzia. . 52Jedwali 4.4:Kutekelezeka Kwa Sera ya Elimu na Mafunzo Juu ya KiswahiliKama Lugha Kufundishia na Kujifunzia . 54Jedwali 4.5:Hatua Zilizochukuliwa na Serikali Kuhakikisha Matumizi yaKiswahili . 55Jedwali 4.6:Maoni ya Watafitiwa Kuhusu Mikakati ya Utekelezaji Iliyowekwa naSerikali . 57Jedwali 4.7:Maoni ya Watafitiwa Juu ya Kutumia Lugha Kiswahili KatikaKufundishia na Kujifunzia . 59Jedwali 4.8:Matumizi Yalugha ya Kiswahili ama Kiingereza Katika Mijadala yaMada Wanazojifunza. 61Jedwali 4.9:Maoni ya Watafitiwa Kuhusu Mchango wa Lugha ya KiingerezaKatika Kufundishia na Kujifunzia. 63Jedwali 4.10: Maoni ya Watafitiwa Kuhusu Manufaa ya Kutumia Lugha yaKiswahili katika Kufundishia na Kujifunzia . 66

xivJedwali 4.12: Maoni ya Watafitiwa Kuhusu Athari ya Kutotekelezwa kwa Tamkola Matumizi ya Lugha ya Kiswahili katika Kufundishia na Kujifunziakatika Vyuo vya Kati. 69

1SURA YA KWANZA1.0 UTANGULIZI1.1UtanguliziSehemu hii inahusika na usuli wa mada, tatizo la utafiti, makusudi ya utafiti,madhumuni mahsusi, maswali ya utafiti, umuhimu wa utafiti, mawanda na mipakaya utafiti, vikwazo vya utafiti na hitimishi.1.2Usuli wa MadaHoja ya matumizi ya lugha ya Kiswahili kufundishia mfumo rasmi wa elimu inahistoria ndefu nchini Tanzania. Ifahamike kuwa Tanzania ina lugha kati ya mia mojana ishirini na mia moja hamsini ambazo ni za jamii au asili.Kiswahili ni lughainayozungumzwa na watu wengi kama lugha ya pili.Tafiti nyingi zinaoneshakuwashughulisha wataalam mbalimbali juu ya uteuzi wa lugha rasmi inayowezakurahisisha mchakato wa kufundishia na kujifunzia katika muktadha kama waTanzania.Kihistoria,kabla ya kuanzishwa kwa utawala wa kikoloni wa Wajerumani,wamisionari waliofika Tanganyika walianzisha shule. Mojawapo ya shule hizo ni afuasiwao.Wamisionari hao walitumia Kiswahili na lugha za wenyeji wao katika kutoleaelimu (Gottneid, 1976). Wao waliamini kuwa lugha huwasilisha fikra za watu,utamaduni na mifumo ya utawala katika jamii hizo. Hivyo, namna bora narahisi yakuelewa mila na dasturi za jamii ni kupitia lugha zao. Kiswahili kilikuwa

2mojawapoya lugha iliyozungumzwa na wenyeji wa Tanganyika kama lugha ya pili(Morrison 1971).Hata hivyo suala la lugha ya kufundishia nchini Tanzania limekuwa na mjadalamrefu ambapo tafiti mbalimbali zimefanyika kuhusu ni lugha gani inapaswakutumika katika kufundishia kati ya Kiswahili na Kiingereza. Kwa mujibu waUNESCO (1953), Lugha za jamii ni bora katika kufundishia kuliko zile za kigenikwa sababu kiushunuzi, lugha ya jamii ni mfumo wa alama zenye maana ambazokatika akili ya mwanafunzi hufanya kazi haraka katika kuelewa na kujieleza.Kiushunuzi, lugha ya mtu ni njia ya kujinasibisha na jamii yake. Kielemu,mwanafunzi hujifunza kwa haraka kwa kutumia lugha anayoielewa kuliko lughangeni. Mfano, lugha ya Kiswahili ina mizizi sawa na lugha za kienyeji kama vileKikwere, neno mama ni mama kama lilivyo katika Kiswahili.Kutokana na maelezo hayo, inaonesha kuwa, upo umuhimu wa kutumia lugha yenyenasaba na lugha za asili katika kufundishia na kujifunzia.Kwa Tanzania, Kiswahili,ni lugha ya taifa na inayokidhi kuwa lugha ya pili kwa jamii pana yaWatanzania.Pamoja kuwa Kiswahili si lugha ya jamii kwa Tanzania, lakini ni lughainayozungumzwa na Watanzania wengi na hata kuwa lugha ya kwanza kwa baadhiya watu. Hivyo,matumizi ya Kiswahili kufundishia ngazi zote za elimu yatawezeshawanafunzi kujinasibisha na jamii zao za Kitanzania na kurahisha kujifunza maarifamapya kwa kuondoa kikwazo cha lugha ya mawasiliano katika muendelezo wakufundisha na kujifunza. Walimu watafundisha maarifa mapya kwa lughawanayoifahamu.

3Wakati wa utawala wa Wajerumani, walianzisha shule nyingi katika utawala waokuleTanga, mwaka 1892 (Gottneid, 1976) na Bush schools nyingi vijijini. Kiswahilikilitumika katika kufundishia ngazi za chini za Elimu ya Msingi hasa katika Shule zaWaafrika (Whiteley, 1969). Kiswahili kilitumika pia kama lugha ya shughuli zakiutawala (Gottneid, 1976).Mtaalam huyu anaendelea kufafanua kuwaWajerumaniwalisisitiza kila akida na kila jumbe kukifahamu Kiswahili ili waweze kufanya kazimahali popote kwa lengo la kutekeleza shughuli za kiutawala.Zuri moja na kubwawalilofanikiwa kulifanya wakoloni hao ni kukikuza na kukiendeleza Kiswahiliingawa lugha yenyewe, kwa asili yake, ina nguvu zake yenyewe ya kujitanua nakujipeleka mbele.Aidhani, utawala wa Waingereza (1919 -1961) uliweka msisitizo katika matumizi yalugha yao ya Kiingereza katika mfumo wa elimu.Waingereza walitumia piaKiswahili katika kufundishia ngazi za chini za elim

MTAZAMO WA JAMII JUU YA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO 2014 . wake na kujitolea kwake muda wa kuchapa kazi hii tangu hatua za awali hadi . nawashukuru wanafunzi wenzangu tuliokuwa nao katika safari ya kitaaluma 2015 / 2016 katika Chuo Kikuu Huria chaTanzania. Nimefaidika na ushirikiano wao

Related Documents:

inayojadiliwa hapa ni: Fasihi ni Hisi, Fasihi ni Kioo cha Jamii, Fasihi ni Mwavuli wa Jamii, na Fasihi ni Zao la Jamii husika na Mielekeo yake ya maisha. 3. Mitazamo inayofafanua Uhusiano wa Fasihi na Jamii Kama lilivyo lengo la makala haya kwamba mchango wake ni kuongeza mchango katika kufafanua uhusiano uliopo baina ya fasihi na jamii.

WAZEE NA WATOTO KWA MIAKA 60 YA UHURU WA TANZANIA BARA. Ndugu Wananchi, Disemba 2021 nchi yetu inaadhimisha miaka 60 ya Uhuru tangu tarehe 09 Desemba, 1961 tulipoanza kujitawala hivyo, . Kufikia mwaka 2016 Wizara mbili ziliunganishwa ambazo ni Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, hivyo kutengeneza Idara Kuu ya

elimu ya juu, Sayansi na Teknolojia. Ilitoa jumla ya tuzo 119 kwa wanafunzi wa kike kutoka shule 20 zilizofanya vizuri katika masomo ya Sayansi na Hisabati katika mitihani ya kumaliza kidato cha nne mwaka 2006 (18); kidato cha sita mwaka 2006 na 2007 (25); vyuo vikuu, taasisi za serikal

wahusika wakuu wa kazi ya fasihi na wahusika wadogo. Wahusika hao ndio wanaoipamba kazi fasihi na kuifanya iweze kuakisi mambo ya yaliyomo katika jamii (Msokile, 1992). Kwa muktadha huo tabia za wahusika wa kazi ya fasihi ndio ambao husawiri matukio na mambo mbalimbali yanayofanywa katika jamii inayohusika.

(1990s). Toleo hilo la Ghana lilitayarishwa kutokana na mitaala ya mafunzo mingine mbalimbali ya PATH, ikiwemo Kuelekea kwenye Utokomezaji wa Ukeketaji: Mawasiliano kwa Ajili ya Mabadiliko – Mtaala kwa ajili ya Wakufunzi wa Wafanyakazi wa Afya ya Jamii, Watayarishaji wa Afya ya Jamii, Watetezi wa Vijana, na Waalimu (PATH:2001).

Migororo katika jamii: kusuluhisha migogoro katika maeneo yenye mifugo, kilimo na wanyamapori 5 Sura ya Utangulizi 1 HADI

za taifa hasa katika nchi yenye lugha nyingi za kikabila.Lugha ya taifa ni muhimu sana kwa maisha na maendeleo ya taifa lolote lile.Lugha hii huwa ndiyo kiungo cha kuenezea umoja na uelewano miongoni mwa jamii nyingi tofauti na huwa kama kitambulisho kwao kuwa wao ni ndugu wa jamii moja

The abrasive water jet machining process is characterized by large number of process parameters that determine efficiency, economy and quality of the whole process. Figure 2 demonstrates the factors influencing AWJ machining process. Shanmugam and Masood (2009) have made an investigation on the kerf taper angle, generated by Abrasive Water Jet (AWJ) machining of two kinds of composite .