SAYANSI - NECTA

2y ago
1.4K Views
115 Downloads
1.39 MB
67 Pages
Last View : 6d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Kelvin Chao
Transcription

BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIATAARIFA YA UCHAMBUZI WA MAJIBU YAWATAHINIWA KATIKA MASWALI YA MTIHANIWA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI MWAKA2019SAYANSI

BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIATAARIFA YA UCHAMBUZI WA MAJIBU YAWATAHINIWA KATIKA MTIHANI WA KUMALIZAELIMU YA MSINGI (PSLE) 2019SAYANSI

Imechapishwa na:Baraza la Mitihani la Tanzania,S.L.P. 2624,Dar es Salaam, Tanzania. Baraza la Mitihani la Tanzania, 2019Haki zote zimehifadhiwa.iii

YALIYOMODIBAJI . v1.0UTANGULIZI . 12.0UCHAMBUZI WA MAJIBU YA WATAHINIWA. 22.1Sehemu A: Maswali ya Kuchagua Jibu Sahihi . 22.2Sehemu B: Maswali ya kujaza nafasi . 473.0UCHAMBUZI WA KUFAULU KATIKA MADA . 574.0HITIMISHO . 585.0MAONI NA MAPENDEKEZO. 58KIAMBATISHO . 59iv

DIBAJIBaraza la Mitihani la Tanzania linafurahi kutoa Taarifa ya UchambuziwaMajibu ya watahiniwa (CIRA) waliofanya Mtihani wa Kumaliza Elimu yaMsingi (PSLE) 2019 somo la Sayansi. Lengo la uchambuzi huu nikutoamrejesho kwa walimu, watunga sera, watunga mitaala na wadau wenginewa elimu kuhusu namna watahiniwa walivyojibu maswali ya mtihani. Hii nikwa sababu ubora wa majibu ya watahiniwa katika mtihani ni miongonimwa viashiria vinavyoonesha kuwa watahiniwa waliweza/hawakuwezakujifunza kwa ufasaha katika kipindi cha miaka saba ya elimu ya msingi.Kwa ujumla, taarifa inaonesha uchambuzi wa majibu kwa kila swali nakubainisha changamoto walizokabiliana nazo watahiniwa wakati wa kujibumaswali husika. Pia, taarifa imeainisha sababu za watahiniwa kuweza aukutoweza kutoa majibu sahihi kulingana na matakwa ya kila swali. Baadhiya sababu zilizofanya watahiniwa waweze kujibu kwa usahihi ni kuwa namaarifa ya kutosha kuhusu dhana zilizopimwa. Kwa upande mwingine,sababu zilizofanya watahiniwa kushindwa kujibu maswali kwa usahihi nikukosa maarifa kuhusu dhana zilizotahiniwa na kushindwa kuelewa vemamatakwa ya swali husika, hivyo kutoa majibu yasiyohusiana nakilichoulizwa.Baraza la Mitihani lina imani kuwa, mrejesho wa taarifa hii utatoa mwangakwa wadau wa elimu kuhusu maendeleo ya kielimu katika ngazi ya elimuya msingi. Hivyo, hatua za kuboresha ufundishaji na ujifunzaji wa somo lasayansi zitachukuliwa ipasavyo, na hatimaye kuboresha matokeo yawatahiniwa katika mitihani ijayo.Mwisho, Baraza la Mitihani linatoa shukrani za pekee kwamaafisa mitihanina wengine wote walioshiriki kuandaa taarifa hii.Dkt. Charles E. MsondeKATIBU MTENDAJIv

1.0UTANGULIZIMtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) ni mtihani wa mwishoambao hufanyika wiki ya pili ya mwezi Septemba kila mwaka.Mwaka huu mtihani ulifanyika tarehe 11 na 12 Septemba 2019.Taarifa hii inahusu uchambuzi wakufaulu kwa watahiniwa waliofanyaPSLE 2019 katika somo la Sayansi. Kwa ujumla, taarifa inawasilishatakwimu na ufafanuzi kuhusu viwango vya kufaulu kwa watahiniwakwa kila swali na katika mada.Taarifa ina sehemu tano ambazo ni utangulizi, uchambuzi wakufaulu kwa watahiniwa kwa kila swali, uchambuzi wa kufaulu kwawatahiniwa kwa kila mada, hitimisho na mapendekezo. Muhtasariwa viwango vya kufaulu kwa kila mada umeoneshwa katikakiambatisho. Viwango hivyo vimeoneshwa katika makundi yakufaulu yaliyogawanywa sehemu tatu ambazo nivizuri, wastani nahafifu. Makundi haya yametokana na mfiko wa asilimia kamaifuatavyo: 60 – 100 Vizuri, 40 – 59 Wastani, na 0 – 39 Hafifu.Kwa ujumla, takwimu zinaonesha kuwa, jumla ya watahiniwa947,077walisajiliwa ambapo 933,323 (98.55%) walifanya mtihani.Uchambuzi wa takwimu unaonesha kuwa, watahiniwa 778,331(83.50%) walifaulu. Kiwango hikini ongezeko la asilimia 6.90%kikilinganishwa na cha PSLE of 2018 ambapo waliofaulu walikuwaasilimia 76.60.1

2.0UCHAMBUZI WA MAJIBU YA WATAHINIWASehemu hii inachambua kufaulu kwawatahiniwa katika sehemu A naB.Sehemu A: Maswali ya Kuchagua Jibu SahihiUchambuzi wakufaulu kwa watahiniwa katika swali la 1 hadi 40 nikama ifuatavyo:Swali la 1: Kati ya wanyama wafuatao yupi ni mamalia?A KonokonoB BataC PopoD MjusiE ChuraSwali lilipima uwezo wawatahiniwa katika kutambua mamalia katikakundi la wanyama. Swali lilijibiwa vizuri na watahiniwa wengi,930,847(99.73%)ambapo kati yao, 788,052 (84.44%) walijibu kwausahihi. Watahiniwa waliobaki, 142,795 (15.30%) walishindwakutambua jibu hivyo walichagua kati ya vipotoshi A, B, D na E.Mtawanyiko wa idadi ya watahiniwa kwa kila chaguo umeoneshwakatika Chati Na.1.Asilimia ya C*3.184.570.27DEMengineChaguoChatiNa 1:Kufaulu kwaWatahiniwa katika Swali la 12

Watahiniwa waliochagua jibu sahihi C, popo walitambua sifa zamamaliaambazo ni pamoja nakuwa na viwele na miili yao kufunikwakwa vinyweleo. Hivyo, waliweza kubaini kuwa, miongoni mwawanyama walioorodheshwa, popo ndiye mwenye sifa hizo.Watahiniwa 142,795 (15.30%) walioshindwa kujibu swali hilihawafahamu sifa za makundi mbalimbali ya wanyama. Wanyamawaliotajwa katika vipotoshi A, B, D na Esio mamalia kwani hawanaviwele wala miili yao haijafunikwa na vinyweleo. Pia, wapo katikamakundi mbalimbali ya wanyama.Kwa mfano, chura yupo kundi laamfibia; mjusi kundi la reptilia; bata anatoka kundi la ndegenakonokono kundi la wanyama wasiokuwa na uti wa mgongo.Swali la 2: Usafi wa mwili husaidia kuzuia magonjwa kamaA kaswende na klamidiaB mapunye na vipeleC pepopunda na matendeD dondakoo na kifua kikuuE UKIMWI na kisonono.Asilimia ya WatahiniwaSwali lilipima uelewa wa watahiniwa kuhusu magonjwa na vyanzovyake. Swali hili lilijibiwa na watahiniwa 930,883 (99.75%).Kiwangocha kufaulu kwaujumla kilikuwa kizuri ambapo watahiniwa 802,249(85.96%) walichagua jibu sahihi. Kwa upande mwingine, watahiniwa128,634 (13.78%) walishindwa kuchagua jibu sahihi.Chati Na. 2inaonesha muhtasari wakufaulu kwa watahiniwa katika swali ngineChaguoChati Na. 2: Kufaulu kwaWatahiniwa katika Swali la 23

Chati Na. 2 inaonesha kuwa watahiniwa wengi walichagua jibusahihi B, mapunye na vipele. Watahiniwa hawa waliweza kutambuakuwa, mapunye na vipele ni magonjwa yanayoathiri ngozi nayanasababishwa na uchafu wa mwili. Hii inathibitisha kuwawatahiniwa hao walikuwa na maarifa ya kutosha kuhusu aina zamagonjwa, na vyanzo vyake.Uchambuziwa takwimu ulibaini pia kuwa, watahiniwa 128,634(13.78%) walishindwa kujibu swali hili kwa usahihi. Watahiniwahawa walikosa maarifa kuhusu visababishi vya magonjwa. Kwamfano, watahiniwa waliochagua A, kaswende na klamidia na E,UKIMWI na kisonono hawakujua kuwa hayo ni magonjwa ya zinaa.Kwa upande mwingine, watahiniwa waliochagua C, pepopunda namatende na D, dondakoo na kifua kikuu hawakufahamu ambukizwa na bakteria na ugonjwa wa matendehuambukizwa na minyoo iitwayo filaria isambazwayo na mbu jike.Swali la 3: Matunda na mboga za kijani vipo kwenye kundi lavyakula vyenyeA protiniB kabohaidretiC mafutaD vitaminiE wanga.Swali lilipima uwezo wawatahiniwa kutambua vyakula mbalimbalikwenye makundi husika. Swali lilijibiwa na watahiniwa 929,348(99.57%). Kiwango cha kufaulu kilikuwa cha wastani, kwaniwatahiniwa 598,850 (64.16%) walijibu kwa usahihi. Watahiniwawaliobaki, 330,498 (35.4%) walishindwa kujibu swali hili kwa usahihikwa kuchagua kati ya vipotoshi A, B, C na E kama ilivyooneshwakatika Jedwali Na. 1.4

Jedwali Na.1: Idadi na asilimia ya watahiniwa katika kila chaguoChaguoIdadi yaWatahiniwa% 049,4573,97520.007.342.7764.165.300.43Uchambuzi watakwimu unaonesha kuwa, asilimia 64.16 yawatahiniwa waliweza kuchagua jibu sahihi D, vitamini. Watahiniwahawa walikuwa nauelewa wa kutosha kuhusu virutubisho vilivyopokatika aina mbalimbali za vyakula.Uchambuzi zaidi unaonesha kuwa, watahiniwa walioshindwa kujibuswali hili kwa usahihi walichagua vipotoshi A, B, C na E. Watahiniwahawa hawakuwa na uelewa kuhusu virutubisho vilivyoko kwenyeaina mbalimbali za vyakula. Watahiniwa hao walishindwa kuelewakuwa, protini hupatikana katika vyakula kamavile nyama za ainazote, maziwa na mimea aina ya kunde. Kabohaidreti hupatikanakatika nafaka za aina zote na sukari.Mafuta hupatikana katikavyakula vyenye mafuta, nyama yenye mafuta na karanga wakatiwanga hupatikana katika nafaka na vyakula vya mizizi kamamihogo.Swali la 4:Kwanini mimea hutawanya mbegu zake baada yakukomaa?A Ili zichukuliwe na wanyamaB Ili zistawi vizuriC Ili ziongeze virutubishoD Ili kupunguza uzaziE Ili ziote haraka.Swali lililenga kupima uelewa wawatahiniwa kuhusu umuhimuwamimea kutawanya mbegu. Swali lilijibiwa na watahiniwa 933,323(99.10%). Kiwango cha kufaulu katika swali hili kilikuwa hafifu kwaniwatahiniwa 317,242 (33.99%) tu walijibu swali hili kwa usahihi.Watahiniwa 616,081 (66.01%) walishindwa kujibu swali hili kwausahihi. Jedwali Na. 2 linaonesha muhtasari wa takwimu za kufaulukwa watahiniwa.5

Jedwali Na.2: Idadi na asilimia ya watahiniwa katika kila chaguoChaguoIdadi yaWatahiniwa% 45186,8978,4018.4633.9924.0312.5920.020.90Takwimu katika jedwalizinaonesha kuwa, ni theluthi moja pekee yawatahiniwa waliweza kutambua kuwa B, ili zistawi vizuri ndilo jibusahihi. Watahiniwa hao walielewa kuwa ili mimea istawi vizuriinahitaji maji, virutubisho, hewa na mwanga wa kutosha. Mbeguzinadondoka chini ya mti husika huweza kushindwa kustawikutokana nakuwa na ushindani mkubwa wa upatiakanaji mahitajihayo.Aidha, theluthi mbili ya watahiniwa walishindwa kujibu swali hili kwausahihi. Watahiniwa hao, hawakufahamu umuhimu wa mimeakutawanya mbegu. Kwa mfano, asilimia 36.62 walichagua vipotoshiC, ili ziongeze virutubisho na D, ili kupunguza uzazi kwanihawafahamu kuwa utawanyaji wa mbegu ni kitendo chakuzisafirisha toka eneo moja hadi jingine. Kitendo hicho huwezeshambegu kupata mahitaji muhimu kwa ajili ya kuota na kustawi.Halikadhalika, waliochagua kipotoshi A, ili zichukuliwe nawanyamawalishindwa kujua kuwa, wanyama ni mawakala waubebaji mbegu kutoka eneo moja hadi jingine.Swali la 5: Tunda lipi halitokani na uchavushaji?A Tikiti majiB NyanyaC NdiziD ChungwaE LimaoSwali lilipima uwezo wawatahiniwa katika kubaini tunda ambalohalizalishwi kutokana na uchavushaji. Jumla ya watahiniwa 927,492(99.37%) walijibu swali hilo. Kiwango cha kufaulu kilikuwa chawastani, kwani nusu ya watahiniwa (50.04%) waliweza kujibu kwausahihi. Aidha, watahiniwa (49.33%) walishindwa kujibu swali hili6

kwa usahihi. Jedwali Na. 3 linaonesha muhtasari wa takwimu zakufaulu kwa watahiniwa.Jedwali Na.3: Idadi na asilimia ya watahiniwa katika kilachaguoChaguoIdadi yaWatahiniwa% 084,97058,3125.339.6350.045.279.100.62Watahiniwa walioweza kuchagua jibu sahihi C, ndizi walifahamumchakato wa uchavushaji katika mimea. Walijua kuwa, matundayaliyotokana na uchavushaji huwa na mbegu zilizokomaazinazoweza kuzalisha mmea mwingine. Maarifa haya yaliwasaidiakubaini kuwa, ndizi hazitokani na uchavushaji.Kwa upande mwingine, watahiniwa waliochagua vipotoshi A, B, Dna E hawakufahamu dhana ya uchavushaji katika mimea.Walishindwa kubaini tunda ambalo uzalishaji wake haupitiiuchavushaji. Matunda yaliyotajwa katika vipotoshi yanabeba mbeguambazo zinapokomaa huweza kuzalisha mmea mwingine kwasababuyametokana na uchavushaji.Swali la 6: Wakati mbegu ya mmea inapoota kiinitetehukua kwakuelekea upande gani?A JuuB KuliaC KushotoD KatikatiE ChiniSwali lilipima uelewa wawatahiniwa kuhusu mchakato wa ukuajikatika mimea. Swali hili lilijibiwana watahiniwa wengi, 927,051(99.32%) ambapo 547,011 (58.61%) waliweza kujibu kwa usahihi.Aidha, watahiniwa 380,040 (40.71%) walishindwa kujibu swali kwausahihi.Takwimu za kufaulu kwawatahiniwa katika swali hilizimeoneshwa katika Chati Na.3.7

Asilimia ya .430.670A*BCDChaguoEMengineChatiNa. 3: Kufaulu kwaWatahiniwa katika Swali la 6ChatiNa. 3 inaonesha kufaulu kwawastani (58.61%)katika swali hili.Watahiniwa hao waliochagua jibu sahihi A, juu hawa walikuwa naufahamu kuwa, wakati wa ukuaji mmea huelekea juu kufuatamwanga wa jua kwa ajili ya mchakato wa fotosinthesisi. Pia,waliweza kutumia maarifa ya ukuaji wa mimea mingi wanayoionakatika mazingira ya kila siku.Watahiniwa waliobaki (40.7%) hawakuelewa kuwa, mimea hukuakuelekea juu kufuata mwanga wa jua. Aidha, walishindwa kutumiauzoefu kuhusu ukuaji wa mimea hali iliyowafanya washindwe kujibuswali kwa usahihi.Swali la 7: Binadamu ana figo ngapi?A MojaB TanoC TatuD MbiliE NneSwali lilipima uelewa wa watahiniwa juu ya ogani zinazounda mwiliwa binadamu. Swali lilijibiwa na watahiwa 930,055 (99.65%),ambapo kati ya hao watahiniwa 791,712 (84.83%) walijibu kwausahihi na watahiniwa 138,343 (14.82%) walishindwa. Takwimuzinaonesha kuwa swali hili lilijibiwakwa usahihi na watahiniwa wengi.8

Jedwali laNa.4linaonesha muhtasari wakufaulu kwa watahiniwakatika swali hili.Jedwali Na.4: Idadi na asilimia ya watahiniwa katika kila chaguoChaguoIdadi yaWatahiniwa% 13,5193,2688.452.991.9484.831.450.35Kama ilivyooneshwa katika Jedwali Na. 4, watahiniwa wengi(84.83%) waliweza kujibu swali hili kwa usahihi. Watahiniwa hawawalichagua jibu sahihi D, mbilikwasababu walijua kwamba figo zikombili ndani ya mwili wa binadamu.Kwa upande mwingine, watahiniwa wachache (14.82%)waliochagua vipotoshi A, B, C na E hawakuwa na maarifa juu yaogani mbalimbali zinazounda mwili wa binadamu. Walishindwakubaini kuwa katika mwili wa binadamu ziko figombili na sivinginevyo.Swali la 8: Nini kitatokea iwapo mfumo wa fahamu katika mwili wabinadamu hautafanya kazi?A Mtu atatetemeka.B Mtu atajihisi dhaifu.C Mtu atasikia maumivu makali.D Mawasiliano mwilini hayatakuwepo.E Mtu atapungua uzito.Swali lilipima uelewa wa watahiniwa kuhusu kazi ya mfumo wafahamu katika mwili wa binadamu. Swali hili lilijibiwa na watahiniwa929,366 (99.58%) ambapo kati ya hao watahiniwa 738,014 (79.07%)walijibu kwa usahihi na watahiniwa 191,352 (20.50%) hawakuwezakujibu kwa usahihi. Kwa ujumla ufaulu huu ni mzuri kamaunavyooneshwa katika Chati Na. 4.9

Asilimia ya .540.42ChaguoChati Na.4: Kufaulu kwaWatahiniwa katika Swali la 8Chati Na. 5 inaonesha kuwa, watahiniwa wengi (79.07%) waliwezakujibu swali hili kwa usahihi. Watahiniwa hawa walielewa kazi zamfumo wa fahamu. Walifahamu kwamba, mfumo wa fahamu nimtandao wa neva na seli zinazobeba taarifa kutoka maeneombalimbali ya mwili kwenda kwenye ubongo na uti wa mgongo nakuzirudisha. Waliweza kubaini kuwa, chaguo D, hakutakuwa namawasiliano mwilini ndio jibu sahihi kwani mfumo wa fahamuunahusika na mawasiliano mwilini.Hata hivyo, watahiniwa wachache 191,352 (20.50%) walichagua katiya vipotoshi A, B, C na E. Watahiniwa hawa hawakuwa na maarifajuu ya kazi za mfumo wa fahamu. Hawakufahamu kuwa, mfumo wafahamu huratibu mawasiliano mwilini hivyo, ukishindwa kufanya kazihakutakuwa na mawasiliano.Swali la 9: Ipi ni sifa ya mmea wa monokotiledoni?A Kurutubisha ardhi.B Kutunza maji ardhini.C Kuwa na mzizi mkuu.D Kuwa na mizizi mingi.E Kuwa na ghala mbili.Swali lilipima uwezo wa watahiniwa katika kubaini sifa za mimeailiyopo katika kundi la monokotiledoni. Kiwango cha kufaulu chawatahiniwa katika swali hili ni hafifu kwani kati ya watahiniwa10

926,625 (99.28%) waliojibu swali hili, watahiniwa 257,813 (27.62%)waliweza kuchagua jibu sahihi D, kuwa na mizizi mingi. Aidha, wengiwao 668,812 (71.66%) walichagua mojawapo kati ya vipotoshi A, B,C na E. Jedwali Na. 5 linaonesha muhtasari wa takwimu za kufaulukwa watahiniwa.Jedwali Na.5: Idadi na asilimia ya watahiniwa katika kila chaguoChaguoIdadi yaWatahiniwa% ya 75,2206,6987.289.2225.6727.6229.490.72Kwa ujumla watahiwa wengi (71.66%) walishindwa kujibu swali hilikwa usahihi. Asilimia 55.16 ya watahiniwa walichagua vipotoshi C,kuwa na mzizi mkuu na E, kuwa na ghala mbili. Watahiniwa hawahawakufahamu sifa za monokotiledoni kwani hizo ni sifa zadaikotiledoni. Vilevile, asilimia 16.50 walichagua vipotoshi A,kurutubisha ardhina B, kutunza maji ardhini. Hawakufahamu kuwaudongo unaweza kupata mbolea kwa kuongeza mbolea ya sulfeti yaammonia lakini sio kupitia mimea ya monokotiledoni. Hivyo, uhifadhiwa maji katika udongo unaweza kufanyika kwa kutandaza majani nasi kwa kutumia mimea ya monokotiledoni.Aidha, watahiniwa 257,813 (27.62%) walioweza kuchagua jibusahihi walizifahamu sifa za mimea iliyopo katika kundi lamonokotiledoni. Walijua kuwa, mimea hiyo ina ghala moja katikambegu zake, ina mizizi mingi na majani yake yana vena sambamba.Swali la 10: Viini vya ugonjwa wa kipindupindu huingia mwilini kwakupitiaA kwenye ngoziB kwenye jerahaC jichoniD mdomoniE sikioni.Swali lilipima uwezo wa watahiniwa katika kubaini njia inayotumiwana viini vinavyoeneza ugonjwa wa kipindupindu kuingia mwilini.Jumla ya watahiniwa 928,399 (99.47%) walijibu swali hili kati ya hao,11

watahiniwa 485,247 (51.99%) walijibu kwa usahihi na watahiniwa443,152 (47.48%) walishindwa kujibu kwa usahihi. Kiwango chakufaulu katika swali hili ni cha wastani kama inavyoonekana katikaJedwali Na. 6.Jedwali Na. 6: Idadi na asilimia ya watahiniwa katika kilachaguoChaguoIdadi yaWatahiniwa% ya 7.2615.572.5951.992.07Mengine4,9240.53Takwimu katika Jedwali Na. 6 zinaonesha kuwa, asilimia 51.99 yawatahiniwa walijibu swali hili kwa usahihi. Watahiniwa hawawalifahamu kuwa viini vinavyoeneza ugonjwa wa kipindupindu(bakteria) huingia mwilini kupitia kula vyakula au vinywaji vyenyebakteria hao. Hivyo, waliweza kubaini jibu sahihi D, mdomoni.Aidha, asilimia 47.48 ya watahiniwa hawakutambua kuwa viinivinavyoeneza ugonjwa wa kipindupindu huingia mwilini kupitiamdomo. Watahiniwa hawa walichagua kati ya vipotoshi A, kwenyengozi, B, kwenye jeraha, C, jichonina E, sikioni. Hiki ni kiashiriakuwa, watahiniwa hawakuwana maarifa kuhusu ugonjwa wakipindupindu. Hawakutambua kuwa ugonjwa wa kipindupindu nimojawapo ya magonjwa yanayoenezwa kwa kunywa maji au kulavyakula vyenye vimelea vya ugonjwa huo.Swali la 11: Aina ipi ya vyakula mgonjwa wa kisukari anapaswa kulakwa wingi?A Kabohaidreti na protini.B Vitamini na mafuta.C Matunda na mafuta.D Protini na mboga za kijani.E Chumvi za madini na mboga za kijani.Swali lililenga kupima uelewa wa watahiniwa kuhusu huduma yamgonjwa wa kisukari. Swali lilijibiwa na watahiniwa 924,772(99.08%) ambapo kati yao, 377,702 (40.47%) walijibu kwa usahihi12

na watahiniwa 547,070 (58.61%) walishindwa. Idadi naasilimia yawatahiniwa katika kila chaguo imeoneshwa kwenye Jedwali Na. 7.Jedwali Na. 7: Idadi na asilimia ya watahiniwa katika kilachaguoChaguoIdadi yaWatahiniwa% ya 21,5818,55120.738.465.6840.4723.740.92Jedwali Na. 7linaonesha kuwa,kiwango cha kufaulu kwa watahiniwakatika swali hili kilikuwa wa wastani. Asilimia 58.61 ya watahiniwawalishindwa kuchagua jibu sahihi D, protini na mboga za kijani. Hiiilichangiwa na kukosa maarifa kuhusu namna ya kumtunza mgonjwawa kisukari. Kwa watahiniwa waliochagua kipotoshi A, kabohaidretina protini hawafahamu kuwa,mgonjwa wa kisukari hapaswi kulakabohaidreti nyingi kwani huongeza sukari katika damu. Pia,waliochagua B, vitamini na mafuta na C, matunda na mafutahawafahamu kuwa,ongezeko la mafuta kwa wingi mwilini huletamadhara. Vile vile matunda huongeza sukari katika damu. Kwa walewaliochagua E, chumvi za madini na mboga za kijani hawakuelewakuwa vyakula hivyo haviwezi kutumiwa kila siku kama mlo mkuukwani vitadhoofisha mwili.Kwa upande mwingine, asilimia 40.47 ya watahiniwa waliwezakutambua kuwa chaguo D, protini na mboga za kijan

sayansi zitachukuliwa ipasavyo, na hatimaye kuboresha matokeo ya watahiniwa katika mitihani ijayo. Mwisho, Baraza la Mitihani linatoa shukrani za pekee kwamaafisa mitihani na wengine wote walioshiriki ku

Related Documents:

coffee groups 1192043 infusion chamber with plug for coffee assembly for necta vending astro-astrop-brio250-brio3-brioc colibri-granmattino-kikko-kikkomax-kikkory-oblo spazio-venezia-zenith for lavazza lb3400zenith necta vending 0v17

1 CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI SHIRIKISHI MUHIMBILI 12 Mei, 2020 TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI Makamu Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) anapenda kuwataarifu Waombaji kazi waliotuma maombi ya kujaza n

sayansi ya leo lakini haijakuwa bado mathalan roketi za kinuklia. Tunaweza kuamini kuwa ulimwengu unaorejelewa kwenye hadithi waweza kuwa katika siku zijazo. Kuna aina ya sayansi bunilizi iliyo burudani tupu. Katika utangulizi wa riwaya ya Isaac Asimor (1955), hadithi ya sayansi bun

elimu ya juu, Sayansi na Teknolojia. Ilitoa jumla ya tuzo 119 kwa wanafunzi wa kike kutoka shule 20 zilizofanya vizuri katika masomo ya Sayansi na Hisabati katika mitihani ya kumaliza kidato cha nne mwaka 2006 (18); kidato cha sita mwaka 2006 na 2007 (25); vyuo vikuu, taasisi za serikal

Awali ya yote, NECTA inaishukuru kwa dhati Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WEST), Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) pamoja na wabia wa maendeleo hususan DF

P a g e 1 of 6 by Mong are Teachers College, Hai Kilimanjaro,March 2020 www.mongarecollege.ac.tz for Online Downloads. WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA MONG ARE TEACHERS COLLEGE S.L.P 215 HAI, KILIMANJARO. SIMU: Mapokezi-0755 679 228 , Msajili-0

3.0 VIPAUMBELE VYA WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI 10. Mheshimiwa Spika, Dira ya Maendeleo ya Taifa (2 025) imelenga kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025. Katika juhudi za kufikia lengo hili, Wizara ya E

ACCOUNTING 0452/11 Paper 1 May/June 2018 1 hour 45 minutes Candidates answer on the Question Paper. No Additional Materials are required. READ THESE INSTRUCTIONS FIRST Write your Centre number, candidate number and name on all the work you hand in. Write in dark blue or black pen. You may use an HB pencil for any diagrams or graphs. Do not use staples, paper clips, glue or correction fluid. DO .