KUCHUNGUZA JINSI NAHAU ZA KISWAHILI SANIFU

2y ago
654 Views
8 Downloads
878.92 KB
101 Pages
Last View : 5d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Isobel Thacker
Transcription

KUCHUNGUZA JINSI NAHAU ZA KISWAHILI SANIFUZINAVYOKWAMISHA MAWASILIANO FANISI KWA WAGENI WALUGHAMWANAISHA MUSSA SKUNITASNIFU ILIYOWASILISHWA KWA KUKAMILISHA MASHARTI YASHAHADA YA UZAMILI (M.A KISWAHILI ISIMU) YA CHUO KIKUUHURIA CHA TANZANIA2018

iiITHIBATIAliyeweka saini hapa chini anathibitisha kuwa ameisoma Tasnifu hii iitwayo“Kuchunguza jinsi Nahau za Kiswahili Sanifu zinavyokwamisha Mawasiliano Fanisikwa Wageni wa Lugha” na anapendekeza ikubaliwe na Chuo Kikuu Huria chaTanzania kwa ajili ya kutimiza sehemu ya sharti la kutunukiwa Shahada ya Uzamilikatika Kiswahili ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.--------------------------------Dr. Mohamed Omary Maguo(Msimamizi) . .Tarehe

iiiHAKIMILIKIHairuhusiwi kuiga, kunakili kwa namna yoyote na kwa lengo lolote tasnifu hii bilaya idhini ya mmiliki au Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa niaba

ivTAMKOMimi Mwanaisha Mussa Skuni, natamka kwamba tasnifu hii ni yangu mwenyewena haijawahi kuwasilishwa na wala haitawasilishwa katika chuo kikuu kingineChochote kwa ajili ya kutunukiwa shahada hii au nyingine yoyote. .Sahihi .Tarehe

vTABARUKUNinaitabaruku tasnifu hii kwa wazazi wangu wawili Bw.Mussa Skuni Juma na BibiSafia Nassor Rashid kwa kunilea kwa mapenzi ya hali ya juu. Pia ninaitabaruku kwawatoto wangu; Ummukulthum Iddi moh’d, Suleiman, Yussra, Maryam, Aisha,Mussa,Muhiddin na Rahila . Vile vile ninaitabaruku kwa walezi wangu Bw.Mmanga mgeni Na Bibi Rukia Mussa kwa kunilea kwa moyo wa upendouliochanganyika na huruma pamoja na kunipeleka shule kupata elimu na kunikuzakatika maadili mema ya kiislamu ambayo ndiyo dira ya maisha yangu ya hapaduniani na huko akhera .

viSHUKURANIAwali ya shukurani zangu nazipeleka kwa muumba wa ardhi na mbingu na vyotevilivyomo ndani yake kwa kunijaalia kuwa mwenye akili timamu, nguvu, afyanjema, uwezo na maarifa, ustahamilivu , uvumilivu na utulivu wa moyo katikakipindi chote cha masomo yangu haya ya uzamili na kwa hili ninakiri wazi wazikwamba sio kwa uwezo , uhodari, wala ujanja wangu ila ni kwa idhini yake yeyeALLAH (SW) Hivyo shukurani hizo nazipeleka kwake ingawa kwa kusemaAlhamdulillah Rabbil-Alamina. Pili napenda kumshukuru kwa udhati wa moyowangu msimamizi wangu Dr. Mohamed Omary Maguo kwa kukubali kuwamsimamizi wangu ambapo aliniongoza na kunielekeza kuanzia hatua ya kwanza hadikufikia tamati ya utafiti huu Mungu ambariki. Tatu shukurani zangu zisizo na mfanozimwendee mwalimu wangu mlezi Bw Bakar Kombo Bakar kwa muongozo,maelekezo, na ushauri alioweza kunipa ambao una thamani kubwa katika maishayangu . Na hii ni dalili ya wazi wazi kwamba bila ya usimamizina uelekezi wakeisingeweza kufikia katika hatua hii kwa wakati huu. Hivyo kwa upendo naunyenyekevu mkubwa namuomba ALLAH (SW) amjaalie kila la kheri pamoja naafya njema na aukuze moyo wake wa imani na ujasiri wa kuwatakia mema wenzake,ampe umri mrefu na ajaalie uwe na manufaa kwake ili aweze kuendelea kuwa hazinakubwa inayotegemewa na kufaa kizazi kilichopo sasa na kinachofuata baadae. Nneshukurani za pekee zimwendee mume wangu mpenzi Bw. Iddi Moh’d Juma kwakuniruhusu kusoma masomo haya ya uzamili. Pia kunipa maelekezo na kunitia moyowakati nilipokuwa nakata tama kutokana na ugumu wa kazi hii ya utafiti naenamuomba ALLAH ambariki na ampe kila la kheri. Pia nawashukuru wazazi wanguBw. Mussa Skuni Juma na Bibi Safia Nassor Rashid na walezi wangu Bw. Mmanga

viiMgeni na Bibi Rukia Mussa kwa kunilea katika maadili mema ya kiislamu nakunipeleka shule kupata elimu. Vile vile naishukuru familia yangu kuvumilia nakustahamili tabu na shida walizokuwa wakipambana nazi kipindi chote cha masomoyangu haya na kuyakosa malezi ya mama yao mzazi ambayo ni muhimu sana kwao.Kwa hili namuomba Mungu awajaalie dini iliyojaa imani, awaelekeze katika njiailiyonyooka , na mimi niwe kegezo chema kwao cha kufuata katika kutafuta elimuyenye manufaa kwa hapa duniani na huko akhera. Pia shukurani za dhati zimwendeeMachano Mmanga Mgeni kwa kutoa mchango wake mkubwa katika utafiti huu.Mungu amzidishie imani.Vile vile nitakuwa mwizi wa fadhila nikiwachakuwashukuru wakuu wangu wa kazi akiwemo mwalimu wangu mkuu kwakuniruhusu pale ninapoomba ruhusa kwao. Na mwisho napenda kuwashukuruwanafunzi wenzangu Maryam Rashid Ali, Zaitun Hassan Sheha, Miza Hassn Faki,Amina Makame Haji, Riziki Ali Hamad, Aisha Ameir Moh’d, Bishara NassorMoh’d, Bimkuwa Abdalla Hamza na Fatma Hamad Nassor kwa kunisaidia kwa njiamoja au nyengine nasema Ahsanteni sana.

viiiIKISIRIUtafiti huu unalenga“Kuchunguza jinsi Nahau za Kiswahili zinavyokwamishaMawasiliano kwa Wageni wa Lugha”. Nahau hizo zinatumika katika lugha yamaandishi ya Kiswahili na katika mazungumzo ya kila siku. Mtafiti wa utafiti huualiongozwa na malengo mahsusi matatu ambayo ni kubainisha nahau mbali mbali zalugha ya Kiswahili kwa kuzingatia makundi yake kimuktadha, kuchambua maana yanahau Kipragmatiki na maana ya nahau kwa kuzingatia viambajengo vilivyoundanahau hizo (Kisemantiki), na kubainisha jinsi nahau zinavyokwamisha mawasilianokwa wageni wa lugha. Utafiti huu umefanyika katika kisiwa cha Pemba, katikahospitali ya Wete,hopitali ya wakorea Chake chake na hospitali ya Abdalla Mzee nakatika Mtaa wa Mkoroshoni Chake chake. Pia utafiti hu ulifanyika shule yasekondari ya Uwelenina shule ya sekondari ya Utaani na Chuo Cha KiislamuPemba Mbinu ya uwandani na maktabani zilitumika katika kufanya utafiti huu nanjia zilizotumika ni dodoso, mahojiano . Sampuli iliyotumika ni ya wanafunzi nawalimu wa somo la Kiswahili wa shule zilizoteuliwa. Mtafiti alitumia nadharia yamaana katika matumizi na nadharia ya maana katika muktadha. Matokeo ya jumla yautafiti huu yanaonyesha kuwa lugha ya kiswahili ni pana katika matumizi yake. Piamtafiti amegundua kuwa mambo yanayopelekea matumizi ya nahau yasababishekufeli kwa mawasiliano kwa wageni wa lugha ni pamoja na wageni kujifunza zaidisarufi ya lugha na kuiwacha kabisa kabisa fasihi ya lugha.Vile vile Nahau hazitoimaanakisarufi. Hata hiyo matokeo yanaonyesha kuwa nahau hazikwamishimawasiliano kwa wageni wa lugha tu bali pia na wazawa wa lugha wanakabiliwa nataizo hili.

ixYALIYOMOITHIBATI . iiHAKIMILIKI . iiiTAMKO . ivTABARUKU . vSHUKURANI . viIKISIRI . viiiORODHA YA MAJEDWALI. xvORODHA YA VIFUPISHO . xviSURA YA KWANZA . 11.0UTANGULIZI WA JUMLA . 11.1Utangulizi wa Sura . 11.2Usuli wa Tatizo . 11.3Tatizo la Utafiti . 31.4Malengo ya Utafiti . 51.4.1 Lengo Kuu . 51.4.2 Malengo Mahususi . 51.5Maswali ya Utafiti . 51.6Umuhimu wa Utafiti. 61.7Vikwazo vya Utafiti . 61.8Utatuzi wa Vikwazo . 71.9Hitimisho . 7SURA YA PILI . 92.0MAPITIO YA KAZI TANGULIZI NA KIUNZI CHA NADHARIA . 9

x2.1Mapitio ya Kazi Tangulizi. 92.2Kazi Tangulizi Zinazohusiana na Semi . 102.2.1 Dhana ya Semi . 102.2.2 Vipera vya Semi . 122.3Dhana ya Maana . 152.3.1 Maana katika Mtazamo wa Kisemantiki . 152.3.2 Maana katika Mtazamo wa Kipragmatiki . 152.4Kazi Tangulizi kuhusu Semi . 162.5Pengo la Utafiti. 182.6Kiunzi cha Nadharia . 192.6.1 Maana ya Nadharia . 192.6.2 Nadharia ya Maana ya Matumizi . 202.6.3 Nadharia ya Maana Kimuktadha . 212.7Hitimisho . 22SURA YA TATU . 233.0MBINU ZA UTAFITI . 233.1Utangulizi wa Sura . 233.2Muundo wa Utafiti . 233.3Kundi Lengwa . 233.4Sampuli. 243.5Usampulishaji . 243.6Maana ya Data . 253.6.1 Aina za Data . 253.7Mbinu za Kukusanyia Data . 26

xi3.7.1 Dodoso . 273.7.2 Mahojiano. 273.8Mbinu za Uchambuzi wa Data . 283.9Maadili ya utafiti . 293.10Hitimisho . 30SURA YA NNE . 314.0UWASILISHAJI NA UCHAMBUZI WA DATA . 314.1Utangulizi wa Sura . 314.2Kubainisha Nahau za Kiswahili kwa Kuzingatia Makundi. 334.2.1 Tafsiri ya Matokeo . 344.2.2 Nahau zinazohusu Mila na Desturi za Jamii . 354.2.3 Nahau Zinazohusu Juhudi katika Kazi . 374.2.4 Nahau zenye Uhusiano wa Dini na Imani . 374.2.5 Nahau Zimazohusu Choyo na Usaliti . 384.2.6 Nahau Zinazohusu Subira na Uvumilivu . 384.2.7 Nahau Zinazohusiana na Mambo ya Maadili . 394.2.8 Nahau Zinazohusu Ushirikiano . 394.2.9 Nahau Zinazohusu Elimu . 394.3Kuchambua Maana ya Nahau Kipragmatiki na kwa Kuzingatia Viambajengovilivyounda Nahau hizo . 394.3.1 Kuchambua Maana ya Nahau Kipragmatiki . 414.3.2 Tafsiri ya matokeo . 434.3.3 Kuchambua Maana za Nahau kwa Kuzingatia Viambajengo VilivyoundaNahau . 44

xii4.4Kubainisha jinsi Nahau zinavyokwamisha Mawasiliano kwa Wageni waLugha ya Kiswahili . 464.4.1 Nahau “ Amevunja Chupa” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha ya Kiswahili . 474.4.2 Nahau “Kuchimba Dawa” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha ya Kiswahili . 484.4.3 Nahau “Amepata jiko” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwa Mgeniwa Lugha ya Kiswahili . 494.4.4 Nahau “Jamvi la Wageni” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha . 504.4.5 Nahau “Amepata Ua” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha. 504.4.6 Nahau “Kenda Kombo” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha . 514.4.7 Nahau “Andika Meza” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha . 524.4.8 Nahau “Kuchungulia Kaburi” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha . 524.4.9 Nahau “Amevunja Ungo” Inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha . 534.4.10 Nahau “Ameacha njia” Inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha . 544.4.11 Nahau “Aliniunga Mkono” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha . 54

xiii4.4.12 Nahau “Ameanguka mtungi” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha . 554.4.13 Nahau “Kutapikia sandani ” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha . 564.4.14 Nahau “Amaemlanda baba yake” inavyoweza Kukwamisha Mawasilianokwa Mgeni wa Lugha . 574.4.15 Nahau “ Ameukata” inavyoweza Kukwamisha Mawasilianokwa . 574.4.16 Nahau “ Bao la Mkahawani”inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha ya Kiswahili . 584.4.17 Nahau “ Kata maini” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwa Mgeni waLugha ya Kiswahili . 584.4.18 Nahau “Chomea utambi” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha ya Kiswahili . 594.4.19 Nahau “Kaza buti” ” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwa Mgeniwa Lugha ya Kiswahili . 604.4.20 Nahau “Ana Ndimi Mbili” Inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha. 604.4.21 Nahau “Kujipalia Makaa” inavyoweza Kukwamisha Mawasiliano kwaMgeni wa Lugha . 614.4.22 Nahau “Kupigwa fyagio la chuma” inavyoweza KukwamishaMawasiliano kwa Mgeni wa Lugha . 614.5Hitimisho la Sura . 62SURA YA TANO . 645.0MUHUTASARI HITIMISHO NA MAPENDEKEZO . 64

xiv5.1Utangulizi . 645.2Muhtasari wa Utafiti. 645.3Matokeo ya Utafiti kwa Kila Lengo . 655.3.1 Lengo la Kwanza . 655.3.2 Lengo la Pili . 655.3.3 Lengo la Tatu . 665.4Matokeo ya Jumla . 675.5Mchango wa Utafiti . 685.6Mapendekezo kwa Tafiti Fuatishi . 685.7Hitimisho . 69MAREJELEO . 70VIAMBATANISHO. 73

xvORODHA YA MAJEDWALIJeduweli Na :4.1:Watafitiwawa Kigeni . 32Jeduwali Na.4.2:Watafitiwa Wanafunzi . 32Jeduwali Na. 4.3:Watafitiwa Walimu . 32Jeduwali Na. 4.4:Mgawanyiko wa Majibu ya Watafitiwa . 34Jeduwali Na 4.5:Makundi ya Nahau Zilizobaininishwa . 35Jeduweli Na 4.6:Maana ya Nahau Kipragmatiki . 41Jeduweli Na. 4.7:Mfano wa Nahau Katika Kiwango Cha Neno . 42Jeduweli Na. 4.8:Mfano wa Nahau Katika Kiwango Cha Kirai . 43Jeduwali Na 4.9:Maana ya Nahau Kwa Kuzingatia Viambajengo VilivyoundaNahau . 45

xviORODHA YA VIFUPISHOBAKITABaraza la Kiwahili TanzaniNNahauNaNambariSnSerial numberSW:Subhana WataalaTTafsiriTAKILUKITaasisi ya kiwhili na lugha za kigeniTATAKITaasisi ya Taaluma za KiwhiliTUKITaasisi ya Uchunguzi wa KiwhiliTUMITaasisi ya Ukuzaji MitaalaUKUkurasaUKIMWIUkoefu wa Kinga MwiliniW KEWanawakeWUWanaume

1SURA YA KWANZA1.0 UTANGULIZI WA JUMLA1.1Utangulizi wa SuraSura hii inatoa taarifa za awali zinazohusiana na mada ya utafiti ambayo ni“Kuchunguza jinsi Nahau za Kiswahili zinavyokwamisha Mawasiliano kwa Wageniwa Lugha”. Sura hii imeundwa na sehemu kumi. Sehemu ya kwanza inaelezautangulizi wa jumla kuhusu mada ya utafiti. Sehemu ya pili inatoa taarifa kuhusuusuli wa tatizo la utafiti. Sehemu ya tatu inaeleza tatizo la Utafiti. Sehemu ya nneinaeleza pengo la utafiti. Sehemu ya tano inaeleza malengo. Sehemu ya sita nimaswali ya utafiti, sehemu ya saba ni umuhimu wa utafiti. Sehemu ya nane inahusuchangamoto za utafiti na jinsi ya kutatua changamoto hizo na sehemu ya tisa inaelezahitimisho la sura hii.1.2Usuli wa TatizoKihistoria, Kiswahili ni miongoni mwa lugha ambazo hukua na kupokea mabadilikotofauti (Masamba 2006). Katika karne tulizonazo wanaisimu wa lugha ya Kiswahilipamoja na watumiaji wengine wa lugha hiyo wameshuhudia mabadiliko makubwaya lugha ya Kiswahili kutokana na kuongezeka kwa idadi ya semi, nahau ikiwa nimiongoni mwao. Inasadikiwa kuwa idadi kubwa ya wageni wanaotumia Kiswahiliwamekabiliwa na tatizo la matumizi ya nahau katika matumizi yao ya lugha hii,jambo ambalo hupelekea ugumu mkubwa kimawasiliano. Kiisimu, hakunaanayekataa kuwa kuongezeka kwa idadi ya nahau katika lugha ya Kiswahili ndikokunakopelekea kuibuka kwa tatizo la ugumu wa kujifunza lugha kwa wasiokuwa

2wazawa wa lugha hii (Kitiso 1988). Licha ya jitihada mbali mbali za kuhakikishakuwa lugha ya Kiswahili inapata watumiaji wengi duniani na kuikuza hadhi yakekuwa ni lugha ya kimataifa, bado majibu ya tatizo la kuibuka kwa nahauzinazosababisha ugumu wa kujifunza lugha hiyo kwa wageni ni kitendawilikinachohitaji kuteguliwa (BAKIZA, 2008).Kuna kazi nyingi zilizoandikwakuhusiana na mada ya semi za Kiswali nahau zikiwemo. Mfano wa kazi hizo ni ileya (Kiiza (2004), ambaye aliandika kuhusu jinsi semi za Kiswahili zinavyozaliwa nakukua katika Lugha ya Kiswahili na aligundua kuwa baadhi ya semi huzaliwa,hukuwa na kufa, kutegemeana na mabadiliko ya wakati na mahitaji ya watumiaji walugha . Mbunda (1992) alifanya utafiti juu ya namna gani nahau zinavyotumikakatika lugha ya Kiswahili na alithibitisha kuwa nahau zinatumika kuipamba lugha nakupunguza ukali wa maneno. Kwa upande mwengine Balisidya (1976) yeye alitafitijuu ya umuhimu wa nahau zinazoibuka katika maendeleo ya Kiswahili na kugunduakuwa nahau zina umuhimu mkubwa katika kukuza lugha kwani husaidia kuibuamisamiati mipya katika lugha.Kiukweli, pamoja na jitihada za watafiti hawa, mtafitiwa kazi hii anaona ipo haja ya kuchunguza zaidi kwa sababu maandiko yotealiyoyabainisha hapo juu hayajamuonesha andiko mahsusi lililolenga katikakuchunguza jinsi nahau za Kiswahili zinavyokwamisha mawasiliano kwa wageni walugha. Waandishi walio wengi walizungumzia vipengele vyengine vya nahau hasavile vinavyohusiana na uchambuzi wa kifasihi na bado hawajachunguza kipengelekinachohusiana na nahau kwa kuangalia mtazamo wa Kiisimu. Kwa msingi huu,mtafiti wa kazi hii anakusudia kufanya utafiti katika kuchunguza jinsi nahau zaKiswahili Sanifu zinavyokwamisha mawasiliano fanisi kwa wageni wa lugha ilikutoa andiko mahsusi ambalo litasaidia kwa namna tofauti kufahamu jinsi hali hii

3inavyokwamisha mfumo wa mawasiliano kwa wageni wa lugha hiyo jambo ambalohusababisha kupungua kwa ufanisi wa mawasiliano kwa watumiaji wapya wa lughaya Kiswahili.1.3Tatizo la UtafitiKutokana na tafiti rejelewa na maandiko mbali mbali yaliyokwisha wasilishwa juuya semi za Kiswahili, mtafiti wa mada hii anakiri wazi wazi kuwa kuna tafiti nyingizilizokwishafanywa juu ya mada ya semi katika vipengele mbali mbali. Kwa mfanoMahenge (2009) alichunguza semi zilizoandikwa kwenye tiketi za daladala jijini Dares salaam. Katika utafiti wake aliangalia kipengele cha fani na maudhui . Migodella(2011) alichunguza ufasihi wa misemo au semi ziliziandikwa katika sehemu zaumma, akitolea mifano misemo iliyoandikwa katika kuta za vyoo. Matokeo ya utafitiwake yanaonyesha kwamba semi zilizoandikwa katika kuta za vyoo zina utajirimkubwa wa matumizi ya lugha ya kitamathali kama vile tashbiha, tafsida, sitiari,taswira, ishara, picha nakadhalika. Uledi (2012) nae alichunguza muundo wavipengele vya lugha katika methali na vitendawili kwa jamii ya wamakunduchi. Kaziyake ilikuwa ni kulinganisha semi hizo na zile za Kiswahili sanifu na kugunduakuwa katika kila methali na vitendawili kuna vipengele mbali mbali vya lughavinavyotumika katika ujenzi wake. Hassan (2013) alichunguza dhima za methalikatika jamii ya Wapemba na kubaini kwamba methali zinatumika katika jamii yaWapemba kwa kuangalia dhima ya methali ili kudumisha dhamira na maadili katikajamii. Vile vile Alhabib (2012) alichunguza matumizi ya taswira katika nyimbo zataarab na kugundua kuwa kipengele cha misemo kinajidhihirisha katika nyimbo zataarab .Vile vile Rajab (2012) alifanya utafiti juu ya dhima za misemo iliyoandikwa

4katika fulana, ambapo alishughulikia zaidi kipengele cha dhamira na matumizi yalugha katika jiji la Dar es salaam. AIichogundua ni kwamba maandishiyaliyoandikwa katika vazi la fulana yamejaa dhamira mbali mbali, alitaja baadhi yadhamira hizo kuwa ni umaskini, hali ngumu ya maisha, UKIMWI, dini, elimu, chuki,maisha, wivu, pesa, umuhimu wa kufanya kazi, vita dhidi ya magonjwa. Nassor(2016) akafanya utafiti juu ya kuchunguza fani na dhamira za semi zilizoandikwakatika vyombo vya safari vya baharini kisiwani Pemba. Katika kazi yake hiyoaligundua kuwa katika semi zilizoandikwa katika vyombo vya safari zimetumikambinu mbali mbali za kisanaa kama vile tashtiti, taswira, kejeli, methali, misemo,simo, misimu nakadhalika .Vile vile aligundua kuwa dhamira inayotumika katikasemi hizo ni dhamira ya maisha ya kila siku pamoja na maisha ya baadae hukoakhera. Dhamira hizo ziliwasilishwa na kujitokeza katika semi zilizoandikwa katikavyombo vya baharini kisiwani Pemba.Tafiti zote hizo kwa kiasi anachoelewamtafiti wa kazi hii bado hazijabainisha ni kwa kiasi gani semi kupitia kipengele chanahau zinavyokwamisha mfumo wa mawasiliano kwa wageni wa lugha ya Kiswahili.Kama hivyo ndivyo ilivyo, basi mtafiti amebaini kuwa bado wanaisimu wa Kiswahilihawajawahi kuweka bayana namna gani nahau za Kiswahili zinavyokwamishamfumo wa mawasiliano kwa wageni wa lugha hiyo. Kwa maana hiyo, mtafiti wakazi hii amelazimika kuichagua mada hii ili wadau wa isimu ya Kiswahili wawezakufahamu kwa kuweka bayana namna nahau zinavyokwamisha mfumo wamawasiliano kwa wageni wa lugha hiyo. Utafiti huu umekuwa ni wa lazimakufanywa kwa lengo la kupata andiko mahsusi lenye sifa za kipekee na lenyekutafautiana na maandiko mengi yaliyotolewa na wataalamu ambalo litasaidia wahilisanifu

5zinavyokwamisha mfumo wa mawasiliano kwa wageni wa lugha hiyo. Hii inatokanana ukweli kwamba wakati wa mapitio ya maandiko mbali mbali mtafiti hakubahatikakuona andiko mahasusi ambalo linazungumzia juu ya mada kama hii.1.4Malengo ya UtafitiUtafiti huu umeongozwa na malengo yafuatayo:-1.4.1 Lengo KuuLengo kuu la utafiti huu ni kuchunguza jinsi Nahau za Kiswahili Sanifuzinavyokwamisha aawasiliano fanisi kwa wageni wa lugha.1.4.2 Malengo MahususiKwa ajili ya kukamilisha lengo kuu lililoanishwa hapo juu, utafiti huu umejumuishamalengo mahsusi yafuatayo:i)Kubainisha nahau mbali mbali za lugha ya Kiswahili kwa kuzingatia makundiyake.ii)Kubainisha maana ya nahau kipragmatikia na maana ya nahau kwa kuzingatiaviambajengo vilivyounda nahau hizo (kisemantikia).iii)Kubainisha jinsi nahau zinavyokwamisha mawasililiano kwa wageni wa lugha.1.5Maswali ya UtafitiUtafiti huu una jumla ya maswali matatu ambayo yalimuongoza mtafiti kukamilishaau kufikia malengo yake ya utafiti. Kila swali linahusiana na lengo mahsusi moja.Maswali hayo ni kama yafuatayo:i) Ni zipi nahau za lugha ya Kiswahili?

6ii) Ni maana zipi za kipragmatikii na maana zipi za kisemantiki za nahau zaKiswahili Sanifu?iii) Ni jinsi gani nahau za Kiswahili zinakwamisha mawasiliano kwa wageni walugha?1.6Umuhimu wa UtafitiKwanza kabisa, utafiti huu unatarajiwa kutumika kama chanzo cha maarifakinachoonesha jinsi gani nahau za Kiswahili zinavyokwamisha mawasiliano kwawageni wa lugha. Pili, utafiti utaweza kutumiwa na wataalamu wa lugha, isimu nawengineo kama chanzo cha maarifa au kama marejeleo kwa ajili ya tafiti zabaadaye ama kwa kurekebisha au kukosoa kazi hii. Pia, hivi sasa lugha hii ipokatika mchakato wa kuwa lugha ya mawasiliano katika Jumuiya ya Afrika Masharikina dunia kwa ujumla, wakati miongoni mwa sifa za lugha ni kuwa na watumiajiwengi. Hivyo, utafiti huu utawasaidia wanaisimu wa lugha ya Kiswahili katikakutatua tatizo la ugumu wa kujifunza lugha linalosababishwa na kuibuka kwa Nahauza Kiswahili. Mwisho, utafiti huu utakuwa ni rejeleo muhimu ambalo litatumiwa nawahadhiri pamoja na wanafunzi wao wa shahada za awali, uzamili na uzamivu. Kwaupande wa wahadhiri utafiti huu utawawezesha kuandaa mihadhara yao juu yamasuala ya nahau za Kiswahili na jinsi zinavyokwamisha mawasiliano kwa wageniwa lugha.1.7Vikwazo vya UtafitiKatika utafiti huu mtafiti alikutana na vikwazo tofauti ambavyo kwanza kab

Mawasiliano kwa Wageni wa Lugha”. Nahau hizo zinatumika katika lugha ya maandishi ya Kiswahili na katika mazungumzo ya kila siku. Mtafiti wa utafiti huu aliongozwa na malengo mahsusi matatu ambayo ni kubainisha nahau mbali mbali za lugha ya Kiswahili k

Related Documents:

mawazo ya wanamsambao hususani katika ugawaji wa ngano bila kuchunguza kwa umakini sifa ya kila kundi. Propp anaamini kuwa ili kuchunguza asili ya ngano ni vema kuanza kuchunguza aina za ngano kwa kuangalia maumbo ya ngano. Hivyo mtazamo huu unaangalia asili ya ngano kwa kuchunguza maumbo ya ngano husika. Ubora wa nadhairia hii, nadharia hii inasaidia kujua aina za ngano kutokana na dhima zake .

Kiswahili dialects are endangered by, among other factors, the onslaught of standard Kiswahili, English, and Sheng, and so they are likely to be dying. The paper holds the position that the Kiswahili dialects are vital for the development of standard Kiswahili and, therefore, their endangerment is the endangerment of standard Kiswahili.

Introduction to Kiswahili Poetry KSX 2102 Kiswahili Oral Literature KSX 2104 (with Mr Innocent Yerindabo) Introduction to Kiswahili Novels KSX 2202 History and Development of Kiswahili KSX 3101 Kiswahili Teaching Methods KSX 3201 Drafts Reviewed: Advanced Proficiency in Kiswahili KSX 1102 by Boaz Mutungi.

Mathalan, chimbuko la hadithi za fasihi ya Kiswahili linatokana na chimbuko la ngano za Kiswahili (Kenguru, 2013). Baada ya wageni wa Kimagharibi kuingia Afrka mashariki, hasa Wamishionari, ngano kadhaa wa kadhaa zilifasiriwa na kuwa ndio msingi wa hadithi ndefu za Kiswahili. Baina ya mwaka 1940 na kuendelea hadi miaka ya 1960, hadithi ndefu nyingi za Kiswahili zilifuata mkondo wa ngano za .

na namna ya kufundisha na kujifunza Kiswahili, kukuza uwezo wa wanafunzi katika ufundishaji na ujifunzaji, jinsi ya kushughulikia masuala mtambuka na inatoa mwongozo kuhusu tathmini. Sehemu ya pili ni sampuli ya andalio la somo ambayo inaonyesha vipengele vya somo na jinsi ya kuandaa somo hilo.

Song as an aspect of Kiswahili poetry. Origin and development of modern Kiswahili classics such as taarab. Leading founders of Kiswahili popular song in East Africa, history and development of Kiswahili solo, choral and orchestra composition. Themes, style and language use in popular Kiswahili songs.

Kiswahili) na Shahada ya Umahiri/Uzamili ya Sanaa katika Kiswahili (MA. Kiswahili – akitamilikia Fasihi) zote kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania. Chuoni anafundisha kozi za Kiswahili - Lugha, Isimu na Fasihi ikiwemo kozi ya Uandishi wa Kubuni. Pia, hufundisha Kiswahili

The broadcasting industry regularly erects and dismantles structures of a temporary nature, which require a significant amount of work at height. This can often involve working in outdoor environments, when building temporary concert arenas or working indoors, building stages inside existing concert halls. Typically work at height involves structural riggers, responsible for the structural .