MAENDELEO YA KISWAHILI

2y ago
451 Views
12 Downloads
743.56 KB
39 Pages
Last View : 21d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Anton Mixon
Transcription

MAENDELEO YA KISWAHILIKiswahili ni lugha ya kibantu inayozungumzwa katika eneo kubwa la Afrika ya Mashariki. Lughahii ya Kiswahili imesambaa katika eneo kubwa la mwambao wa Afrika ya Mashariki.Lugha: Ni mfumo wa sauti za nasibu zilizobeba maana, zilizokubaliwa na jamii katika kuletamawasiliano. Lugha ni chombo cha mawasiliano baina ya watu.NADHARIA YA KISWAHILIKuna nadharia mbalimbali zinazoelezea asili ya lugha ya Kiswahili. Nadharia hizo ni: Kiswahili ni Kikongo Kiswahili ni pijini au Krioli Kiswahili ni Kiarabu Kiswahili ni lugha ya Vizalia Kiswahili ni KibantuSwali: Fafanua nadharia mbalimbali zinazoelezea asili ya lugha ya Kiswahili. KISWAHILI NI KIKONGOBaadhi ya wataalamu hudai kuwa asili ya lugha ya Kiswahili ni huko Kongo ambayo baadayeiliitwa Zaire na sasa inaitwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Dai hili linaimarishwa na wazojingine linalodai kwamba katika vipindi kongwe vilivyopata kuwako, sehemu za pwani ya AfrikaMashariki hazikuwa zinakaliwa na watu. Kutokana na hali ya vita, uchungaji na biashara,inadaiwa kuwa Wabantu walitoka sehemu za Kongo walisambaa na kuja pwani ya Afrika yaMashariki kupitia Kigoma. Baadhi yao walipitia sehemu za Uganda. Wakati wa kusambaa kwao,walieneza pia lugha zao ikiwemo hii ya Kiswahili.Udhaifu wa nadharia: Wataalamu wa Nadharia hii hawajaweza kueleza na kuthibitishaKisayansi ama Kihistoria juu ya lini hasa watu watu walianza kuishi pwani ya Afrika Mashariki. KISWAHILI NI PIJINI AU KRIOLIBaadhi ya wataalamu hudai kuwa, asili ya Kiswahili ni mwingiliano baina ya wenyeji wa pwani yaAfrika ya Mashariki na wageni wa Kiarabu. Hudai kuwa, Kiswahili ni lugha ya kati iliyozuka ilikurahisisha au kufanikisha mawasiliano katika shughuli ya biashara ya mwanzo. Husisitiza kuwalugha ya Kiswahili haikuwepo kabla ya hapo. Hawa huiona kuwa lugha ya Kiswahili ilianza kamaPijini na baadaye kuwa Krioli.

*Pijini- Ni lugha ambayo huzaliwa kutokana na kukutana kwa makundi mawili yanayotumialugha mbili tofauti. Ili makundi hayo yaweze kuelewana, kunaundwa lugha moja ambayo kitabiani tofauti na zile zinazozungumzwa na makundi yanayohusika. Lugha hii inaweza kuwa namsamiati mwingi kutoka lugha kati ya zile mbili, au inaweza kuwa na msamiati wenye uzitosawa.Swali: Kiswahili ni Pijini. Jadili*Krioli - Ni pijini iliyokomaa. Hii ni hatua ya juu ya pijini. Watu wanaozungumza pijini wanawezakuishi pamoja na kuzoeana na hata wanaweza kuoana. Wakioana watoto wao huikuta lugha yapijini kama lugha yao ya kwanza. Inapofika hatua hii ya watoto kuzungumza lugha hiyo, waohusemekana wanazungumza Krioli.Nadharia hii hutumia kigezo cha msamiati wa Kiswahili kuonesha uhusiano uliopo kati yaKiswahili na Kiarabu. Hawa wanaamini kuwa kwa kiasi kikubwa Kiarabu kimehusika katikakuzaliwa lugha ya Kiswahili.Udhaifu- Udhaifu wa nadharia hii ni kwamba, hutumia kigezo cha msamiati tu bila kuzingatiavipengele vingine vya lugha kama vile matamshi, muundo wa maneno au muundo wa sentensiza Kiswahili.Maswali:1. Kiswahili ni Krioli. Jadili2. Kiswahili si Pijini wala Krioli. Jadili3. Onesha udhaifu wa hoja unaodhihirisha kuwa Kiswahili si Pijini wala Krioli.4. Fafanua hoja zinazodhihirisha kuwa Kiswahili ni Pijini au Krioli. KISWAHILI NI LUGHA YA VIZALIANadharia hii hudai kuwa, Kiswahili ni lugha ya watu wa jamii ya vizalia waliotokana namwingiliano kati ya Waarabu na wanawake wa pwani ya Afrika ya Mashariki. Kutokana nakuingiliana huko palizaliwa watoto wenye mchanganyiko wa damu yaani Waswahili ambaohawakuwa Waarabu wala Wabantu.Nadharia hii inafafanua kuwa, Waarabu waliohamia Afrika ya Mashariki walioa wanawake waKiafrika. Watoto wao walijifunza maneno ya Kiarabu kutoka kwa baba zao na maneno ya kibantukutoka kwa mama zao. Katika jitihada ya kujirekebisha kutoka tamaduni za wazazi wao, vizaliahao walianza kutumia lugha mpya ambayo kwa kiasi kikubwa ilikuwa ni upotoshaji wa lugha yaKiarabu. Lugha hii ndiyo baadaye ilikuwa Kiswahili.

Nadharia hii inashindwa kuthibitisha Kiisimu na Kihistoria kuwepo kwa lahaja mbalimbali zaKiswahili katika mwambao wa Afrika ya Mashariki na visiwa vya jirani ambazo zinahusiana katikamatamshi, msamiati na sarufi kwa ujumla. KISWAHILI NI KIARABUBaadhi ya wananadharia wanaamini kuwa asili ya lugha ya Kiswahili ni Kiarabu. Hawa wanakujana hoja kuu tatu ambazo wanazitumia, Hoja hizo ni:(a) Maneno mengi ya lugha ya Kiarabu katika Kiswahili, hawa wanaamini kwamba uwepowa maneno mengi yenye asili ya Kiarabu katika lugha ya Kiswahili ni ishara tosha kuwaKiswahili kilianza kama pijini ya Kiarabu.(b) Neno lenyewe Kiswahili, inadaiwa kuwa asili ya neno Kiswahili limetokana na neno laKiarabu. Neno Kiswahili linatokana na neno “Sahil” (Umoja) na “Swahil” (Wingi)(c) Inadaiwa kuwa Kiswahili kilianzia pwani na idadi kubwa ya watu wa pwani ni waislamu,na kwa kuwa uislamu uliletwa na waarabu, basi Kiswahili nacho kililetwa na Waarabu.Udhaifu(a) Tukianza na dai la kwanza, Lugha ya Kiswahili haina maneno ya Kiarabu pekee, yapomaneno ya Kiingereza, Kiajemi, Kijerumani n.k. Hivyo lugha yoyote huwa na maneno yamkopo.(b) Kigezo cha dini hakina mashiko, kwani lugha haiwi lugha kwa sababu ya imani.Ikumbukwe pia lugha zilianza kabla ya majilio ya Uislamu. Pia ikumbukwe kwambatunaweza kutumia lugha kufasili dini lakini hatuwezi kutumia dini kufasili lugha.Maswali:1. Fafanua madai yanayodai kwamba, “Kiswahili ni Kiarabu”2. “Kiswahili ni Kiarabu kwa jina lake lakini ni Kibantu kwa tabia yake.” Jadili3. Fafanua udhaifu wa hoja unaosema kwamba,” Asili ya lugha ya Kiswahili ni kibantu.” KISWAHILI NI KIBANTUNadharia hii huchunguza lugha ya Kiswahili katika mfumo mzima wa historia ya mgawanyowa kusambaa kwa lugha za Kibantu. Nadharia hii huhitimisha kuwa, Kiswahili ni mojawapoya lugha katika jamii kubwa ya lugha za Kibantu. Katika kuthibitisha kuwa Kiswahili niKibantu, nadharia hutumia ushahidi wa Kiisimu na Kihistoria.

01: Ushahidi wa KihistoriaUshahidi wa kihistoria unathibitisha kuwa lugha ya Kiswahili ilianza kuzungumzwa katika upwawa Afrika Mashariki kabla hata ya ujio wa wageni kama vile Waarabu na Wazungu. Ushahidi huuulitolewa na wageni mbalimbali waliofika hapa Afrika Mashariki. Wote wanathibitisha kuwalugha ya Kiswahili ilizungumzwa hapa Afrika Mashariki kabla ya ujio wa wageni. Ushahidi huo ni:Ugunduzi wa Ali – IdrisUgunduzi huu yasemekana ulifanywa huko Sicily yapata mwaka 1100-1166, kwenye mahakamaya mfalme Roger II. Licha ya kufahamika kuwa, Kiswahili kilipata kuandikwa kabla ya karne ya10bk, Ali- Idris alikuwa wa kwanza kugundua jina la zamani la Zanzibar kuwa ni Unguja. Katikamaelezo yake anaandika majina kama vile kikombe, mkono wa tembo, muriani na sukari ambazoni ndizi mbalimbali zilzokuwa zikipatikana huko.Ushahidi wa Marco poloHuyu ni mzungu ambaye alijishughulisha sana na masuala mbalimbali ya kijiografia na alisafirisehemu nyingi duniani. Marco polo aliandika hivi:“ Zanzibar ni kisiwa kizuri ambacho kina ukubwa maili 200. Watu wake wanaabudu(Mungu).Wana mfalme na wanatumia lugha yao na hawalipi kodi (Ushuru) kwa mtu.”(Safari za Marcopolo 1958:301)Marco Polo inasemekana aliandika kitabu cha Jiografia ambacho hakikupatwa kuchapishwalakini sehemu zake zimeweza kutafsiriwa kwa Kirusi na Kifaransa. Mfano mmojawapo ni huuufuatao:“Katika visiwa cha Djawaga vilivyoshughulikiwa katika sura hii, ni kile kisiwa cha Andjabaambacho mji wake mkuu unaitwa kwa lugha ya kwao- Zanzibar- Ungudya na wakazi wakejapokuwa ni mchanganyiko, kwa sasa wengi wao ni waislam chakula chao kikuu ni ndizi. Kunandizi za aina tano ambazo zinajulikana kama kundi, Fili ambazo uzito wake waweza kuwa wakia12,Omani, Mariyani, Sukari ”Maelezo haya ya Marco Polo yanathibisha mambo ya msingi kuhusu wakazi wa mwambao wapwani ya Afrika ya Mashariki na lugha yao.

Ushahidi wa Al- Masudi (915BK)Katika moja ya maandishi yake,Al-Masudi anazungumzia juu ya wakazi wa mwambao ambaowalijulikana kwa jina la “Wazanji”. Kwa dhana hii neno Zanzibar linatokana Zenjibar yaani pwaniya “Zanji” . Katika maelezo yake Al- Masudi anaonesha kwamba, Wazenji walikuwa watawalawakilimi ambao waliaminiwa kuwa walitawala kwa nguvu za Mungu. Kuna maelezo kwambahuenda neno Wakilimi lina maana ya Wafalme. Al- Masudi alisisitiza katika maelezo yake kuwa,Wazenji walitema lugha kwa ufasaha na walikuwa na viongozi waliowahutubia kwa lughayao.Kutokana na neno “Zenji” kuna uwezekano kuwa kabla majilio ya Waarabu, Kiswahili kiliitwa“Kiazania” au “Kizanji” na wageni waliofika pwani.Historia ya KilwaKimsingi habari zinaeleza historia ya Kilwa karne ya 10-16BK na zinahusisha na kutaja majina yautani kama vile Mkoma watu, nguo nyingi n.k ambayo walipewa masultani wa kwanza wa KilwaAli Ibn Hussein na mwanae Mohamedi Ibn Ali. Kutokana na habari hizi, huenda lugha yaKiswahili ilishaanza kusemwa mnamo karne ya 10 au ya 11BK. Maelezo ya kihistoria yanaelezajuu ya Sultan aliyeitwa Talt ibn Al Husaini ambaye alipewa jina la utani la Hasha hazifikiVitabu vya Peryplus na Yu-Yang-Tsa-TsuKitabu cha Peryplus kinahusu mwongozo wa bahari ya Hindi. Inadhaniwa kiliandikwa karne yakwanza huko Alexandaria. Kinataja habari za Azania (Afrika Mashariki) na habari za vyombokama vile ngalawa, madema na mitepe. Kinaeleza kuwa, wageni walitozwa ushuru nawafanyabiashara wenyeji, wanaijua pia lugha ya wenyeji vizuri. Kitabu cha Yu-Yang-Tsa-Tsukinaelezea habari za upwa wa Afrika ya Mashariki na Shughuli mbalimbali za wachina hapaAfrika Ya Mashariki. Kitabu kingine kiitwacho Chu-fan-chi kilichapishwa 1226 kinaelezea habariza Zanzibar. Kinaelezea habari za biashara, vyakula, dini na wanyama wa pwani ya AfrikaMashariki.Ushairi wa Kiswahili(a) Utenzi wa Fumo LiyongoShairi la zamani kabisa lillilopata kuandikwa la Kiswahili, linalojulikana ni lile la la utenzi wa FumoLiyongo. Utenzi huu inasemekana uliandikwa karne ya 13BK. Kuweko kwa shairi hilikunadhihirisha kuweko kwa lugha ya Kiswahili kabla ya hapo. Huenda Kiswahili kilianza kutumikakabla ya karne ya 10BK. Miongoni mwa ubeti wa utenzi nii huu:

Liyongo KitamkaliAkabalaghi vijaliAkawa mtu wa kweliNa hiba huongeya(Kutoka E.A. Swahili Committee) Lugha hii ndio mfano wa lugha iliyokuwa ikitumika kunakokarne ya 13BK. Ni wazi kuwa, lugha ilianza kusemwa mapema kabla ya muda huo.(b) Utenzi wa tambuka karne ya 18 BKUtenzi huu uliandikwa mnamo karne ya 18 kuanzia 1700 na kuendelea (tarehe kamilihaijulikani). Utenzi huu umeandikwa kwa kutumia lugha (lahaja ya kimvita) ambayo ni moja yalahaja za lugha ya Kiswahili.Ushahidi wa Ibn Batuta Karne ya 14 KBMohammad bin Batuta ana asili ya taifa la kiarabu.Alifika upwa wa Afrika Mashariki kunako1331 BK. Katika maandishi yake anaelezea maisha ya watu wan chi hii ya Afrika masharikiingawa yeye aliita nchi ya waswahili. Anataja miji kama vile Mogadishu na Kilwa .Anadai kuwa,“Basi nilianza safari baharini kutoka Mogadishu kwenda nchi ya waswahili na mji wa Kilwaambao umo katika nchi ya Zanji. Tulifika Mombasa kisiwa kikubwa , mwendo wa siku mbilikutoka nchi ya waswahili .watu hawajishughulishi na kilimo, ingawa huagiza nafakakutoka kwa waswahili”.Maelezoyaliotolewa hapa yanahusu eneo au mahali ambapo waswahili walikuwa wakiishi.Lakinimaelezo mengi ya msingi yanaonesha kuwa ,watu huwa walikuwa wakiishi katika upwa waafrika Mashariki kuanzia sehemu za bara upande wa kaskazini hadi msumbiji na Bukini kwaupande wa kusini.Maandishi ya Morice (Karne ya 18 BK)Maandishi haya yalijitokeza mwaka 1776. Katika maandishi haya , Morice anawagawa wakazi waAfrika Mashariki katika makundi matatu ambayo ni; Waarabu, Masuriyama na Waafrika.Anaendelea kusisitiza kuwa, Masuriyama na Waafrika walishakaa na kuungana kama jumuiamoja, wakaoleana na kusema lugha moja ya kiasuriama. Kuna wazo kuwa, huwenda Kisuriyamandicho Kiswahili cha leo.

02: Ushahidi wa KiisimuUshahidi wa kiismu ni ushahidi unaothibitishwa kwa misingi ya sayansi ya lugha. Isimu nitaaluma inayoangalia lugha kwa undani (Kisayansi). Ushahidi huu unadhihirisha kuwa asili yalugha ya Kiswahili ni Kibantu, ushahidi huu unadhihirisha hayo kwa hoja zifuatazo:Utafiti wa Marcom GuthrieHuyu ni mwanaisimu kutoka chuo kikuu cha London, Uingereza. Alitumia miaka 20 kuchunguzauhusiano uliopo baina ya lugha za Kibantu zilizoko katika eneo ambalo hukaliwa na Wabantu.Sehemu hii ni ile inayojulikana Afrika, kusini mwa jangwa la Sahara.Alifanya uchunguzi wa mashina/mizizi ya maneno 22,000 kutoka lugha 200 za Kibantu. Katikauchunguzi wake alikuta mizizi (mashina)2,300 imezagaa katika lugha mbalimbali za Kibantu naKiswahili kikiwemo. Mashina/mizizi 500 yalilingana katika lugha zote 200. Mashina hayayalipatikana katika lugha zote za Kibantu. Mashina haya yalikuwa ya asili moja.MsamiatiMsamiati wa msingi wa lugha ya Kiswahili na lugha za Kibantu unafanana kabisa. Msamiati wamsingi ni ule unaohusu mambo ambayo hayabadilikibadiliki kutokana na mabadiliko yautamaduni. Tofauti zinaweza kujitokeza katika matamshi au mabadiliko kidogo ya viambishivyake, lakini si o (Sentensi) za KiswahiliMiundo ya tungo (Sentensi) za maneno ya Kiswahili zinafanana sana na miundo ya tungo zamaneno ya Kibantu. Sentensi za Kiswahili na lugha za Kibantu zina Kiima na JumaJumaJumaJumaAanakula ugaliadya ugalialelya bugaliakulya ubhugalikalya ubusima

Ngeli za majinaHapa kuna makubaliano kufuatana na ngeli katika maumbo ya nomino (Umoja na wingi wamajina) pamoja na upatanisho wa kisarufi.(a) Kigezo cha maumbo ya majinaKigezo hiki hufuata maumbo ya umoja na wingi katika kuyaainisha majina. Majina yaliyo mengikatika lugha ya Kiswahili na lugha za Kibantu hufuata mkondo wa umoja na wingi. Majina yalugha za Kiswahili na lugha za Kibantu yaliyo mengi yana maumbo dhahiri ya umoja na tuWingiWatuBanto (abanto)Bhantu(b) Kigezo cha Upatanisho wa KisarufiKatika kigezo hiki tunaangalia uhusiano uliopo kati ya nomino/vivumishi na viambishi awali vyanafsi katka vitenzi vya Kiswahili na Kibantu. Vivumishi,majina pamoja na vitenzi hivyo hubadilikakutokana na maumbo ya umoja na wingi.MfanoKiswahiliKindaliKikuryaKijitaUmojaBaba analimaUtata akulimaTata araremaTata kalmiaWingiBaba wanalimaAbhatata bhakulimaBata(Tata) bararemaBatata abalima

Vitenzi vya Kiswahili na KibantuKuna uhusiano mkubwa sana kati ya vitenzi vya Kiswahili na vile vya Kibantu. Vipengelevinavyothibisha uhusiano huu ni:(a) ViambishiLugha ya Kiswahili na lugha za Kibantu, vitenzi vyake hujengwa na mzizi pamoja na viambishivyake(awali na tamati)MfanoKiswahili - Analima A-na-lim-aKikuyu - Arerema A-re-rem-aKindali - Akulima A- ku-lim-a(b) Mnyumbuliko wa vitenziMnyumbuliko wa vitenzi vya Kiswahili unafanana na ule wa vitenzi vya lugha za ashaKuhekeshaKusekashakusekesha(c) Mwanzo wa vitenziMwanzo wa vitenzi vya Kiswahili na Kibantu huanza na Viambishi vya nafsi.Mfano:Kiswahili – Analima A-na-lim-aKikuyu - Arerema A -re-rem-aKindali - Akulima A - ekelela

(d) Mwisho wa vitenziVitenzi vingi vya lugha za Kibantu na lugha ya Kiswahili huishia na irabu –aKiswahili – analim –a A-na-lim-aKikuyu - arerem –a A-re-rem-aKindali - akulim - a A- ku-lim-aMaswali:1. “Kiswahili ni Kibantu.” Thibitisha kwa ushahidi wa Kiisimu na Kihistoria.2. “ Kiswahili ni Kiarabu.” Jadili kwa kutumia ushahidi wa Kiisimu na kihistoria3. Thibitisha kwa ushahidi wa Kihistoria kuwa Kiswahili ni KibantuLAHAJALahaja ni tofauti ndogondogo zinazojitokeza katika lugha kuu yenye asili moja. Tofauti hizo zikokatika matamshi ,Lafudhi, maumbo au matumizi ya maneno. Lahaja ni vilugha vidogovidogo vyalugha moja. Lahaja ni mojawapo kati ya lugha ambazo kusema kweli huhesabika kama lughamoja isipokuwa zinatofautiana katika baadhi ya vipengele kama vile: Lafudhi, fonolojia, msamiatiusiokuwa wa msingi au miundo.Watu wanaozungumza lahaja moja wanajisimamia kama kundi mahsusi la kijamii au wanaishipamoja katika sehemu mahsusi ya kijiografia. Lahaja zinaweza kufanana sana au kutofautianamno. Lahaja hutofautiana katika matamshi, muundo wa kisarufi na msamiati.Chanzo cha Lahaja(a) Utengano wa watu kijiografia: Wazungumzaji wa lugha fulani wanapoongezekaidadi huanza kusambaa na kuenea kutoka eneo moja kwenda lingine kutafutamahitaji yao ya asili. Kusambaa huko huweza kusababishwa na matatizo mengikama vile njaa, ukame, vita, shughuliza uvuvi, shughuli za kilimo na ufugaji,elimu, kazi, n,k. Watu wanapohamia kwenye eneo jipya hutengwa na makundimbalimbali ya wazungumzaji wengine. Makundi hayo huwa wana lugha zaoambazo humletea athari katika uzungumzaji wake. Kwa hiyo basi, kitendo hichohusababisha kutokea kwa utofauti katika uzungumzaji wa lugha hiyo.Ikumbukwe watu wanaweza kutenganishwa kwa milima, mabonde, mito nakadhalika.

(b) Utengano wa watu kitabaka: Katika jumuiya moja kunaweza kumea au kuibukakwa matabaka mbalimbali ya watu. Kila tabaka hujihisi na kujitambulisha kwa namnaya pekee japokuwa matabaka hayo huishi katika eneo moja la kijiografia. Msingi wautabaka unaweza kuwa ni wa kiuchumi, kijamii, kisiasa, kielimu, kiutamaduni, aukidini. Aidha mawasiliano ya mara kwa mara baina ya watu walio katika matabakambalimbali hupungua. Hivyo nafasi hiyo ikishapotea hupelekea kuchipuka kwaupekee wa usemaji au uzungumzaji miongoni mwa watu hao. (c) Kupita kwa wakati: Jamii ya wazungumzaji inapohamia kwenye mazingira mapyahukutana na mambo mapya yenye utamaduni mpya. Hivyo ni lazima hali hiyoisababishe kutokea kwa utofauti wa uzungumzaji wa lugha zao. Kwa mfano, jamiiinapohamia karibu na vyanzo vya maji hujishughulisha zaidi na mamboyanayohusiana na mazingira kama hayo. Pia jamii inapohamia mijini vivyo hivyohujishughulisha sana na mambo yanayohusu shughuli kadhaa za mijini. Na endapojamii hiyohiyo itaamia mikoani itakuwa anajishughulisha na masuala ya shambani.Kwa hiyo, hali kama hiyo nayo hupelekea kutokea kwa utofauti katika uzungumzajiwao. Kwa mfano, jamii ile iliyohamia kwenye vyanzo vya maji itajishughulisha nashughuli kama vile kilimo, uvuvi, uwindaji, ufinyanzi, uhunzi, ujenzi, ufugaji, n.k.Hivyo basi, shughuli zinazofanyika katika eneo fulani huathiri hata namna yauzungumzaji wa lugha inayotumiwa na wazungumzaji wa aina tofauti tofauti.Matokeo yake husababisha kuzaliwa kwa maneno mapya yatakayoendana namazingira husika na kusababisha kutokea kwa lugha tofauti.Aina za LahajaKuna aina kuu mbili (2) za Lahaja. Aina hizo ni:1. Lahaja za kijamiiNi lahaja ambazo huzuka kutokana na vigezo vya kijamii kama vile tofauti za mielekeo yakitabaka, elimu, jinsia au umri. Lugha moja inaweza kuzua lahaja mbalimbali kwa misingi yakitabaka. Aghalabu watu wa tabaka moja mfano, wasomi huwa na lahaja yao tofauti na watuwasiokuwa wasomi. Ajira pia huwagawa watu kitabaka, watu wenye ajira moja huweza kuzalishalahaja yao.2. Lahaja za kijiografiaLahaja kijiografia ni mgao wa lugha uliozuka kutokana na vizuizi vya kijiografia, hususani milima,mito, maziwa au jangwa na hata upana wa eneo la lugha. Lahaja za kijiografia ndizo tunazionakatika lugha ya Kiswahili. Lahaja hizi zimeenea katika eneo la pwani ya Afrika Mashariki na tabia

zinaonesha kuwa zote zina msingi mmoja wa lugha ya Kiswahili ambayo ni asili ya kibantu.Lahaja hizo ni:(i) KingoziLugha hii ilikuwa ikizungumzwa tangu kale huko Kismayu na Kaskazini mwa Lamu. Inasemekanakuwa asili ya lugha ya Kingozi inatokana na jamii ya watu walioishi katika mji wa zamani ulioitwa‘Ngozi’ na kabila watu wake liliitwa ‘Wangozi’ Kuna ushahidi kuwa, lugha hiyo ilipata katikabaraza kuu la nchi ya Pate(bunge) na serikali ya nchi hiyo.(ii) KiungujaLugha hii ilitumika unguja mjini na viunga vyake.(iii)Kihadimu na KitumbatuLugha ya Kihadimu na Kitumbatu, kama zilivyo lugha nyingine za Kiswahili, zina manenomachache ya asili ya kigeni. Kihadimu pia huitwa Kikae au Kimakunduchi, kina maneno mengi yaasili ya Kiswahili. Kimsingi Kitumbatu na Kihadimu zinatofautiana sana na Kiunguja, lakinizinakaribiana sana na Kipemba.(iv) KingaoHii ni lugha inayotumika sehemu za Kilwa na kuendelea kusini mwake. Lugha hii inafanana nalugha za makabila yanayoizunguka Kilwa.(v) KimrimaLugha ya Kimrima inazungumzwa sehemu za mwambao kuanzia Vanga, Tanga, Pangani, Dar esSalaam, Rufiji na Mafia. Kimrima kinafanana na Kimtang’ata, Kivumba na Kiunguja kwa kiasiFulani.(vi)KipembaLugha hii hutumika kisiwani Pemba. Lahaja hii inachanganya maneno mbalimbali kama vileKimvita, Kimtang’ata au Kitumbatu.(vii)Kimtang’ataLugha hii inasemwa sehemu za Mrima, hasa za Tanga na Pangani na inayopakana nayo.Kimtang’ata vilevile kinafanana na Kimvita na Kijomvu.(viii)KivumbaLugha hii husemwa katika sehemu za Vanga na Wasini. Sehemu hizi ziko kusini mwa pwani yaKenya.

(ix)Chimbalazi/ ChimiiniLugha hii hutumika kaskazini karibu na Mogadishu, Somalia. Mahali ambapo lugha hiihuzungumzwa sana ni Marka na Barawa(x)KingazijaHii ni lugha ambayo inazungumzwa sehemu na wenyeji wa Kisiwa cha ngazija (Comoro)(xi)KitikuuLugha hii inapatikana kaskazini mwa Lamu na katika visiwa vingine vinavyokaribiana. Sehemu hiiinaendelea hadi huko Somalia sehemu ya Kismayu. Hii ndiyo sehemu inayoitwa Shungwaya naambapo wengi wanaamini kuwa ni chimbuko la lugha ya Kiswahili.(xii)KisiuLugha hii husemwa kuzunguka mji wa Siu. Kisiu ni lugha inayofanana na lugha ya Kiamu naKipate.(xiii)KipatePate ni Kisiwa maarufu chenye historia ya muda mrefu katika pwani ya Afrika Mashariki. Kisiwahiki kiko kaskazini mwa pwani ya Kenya, mashariki ya Lamu.(xiv)KiamuLugha hii huzungumzwa katika kisiwa cha Amu (Lamu). Kiamu kina maneno mengi ya lugha zaKibantu.(xv)KimvitaChimbuko la lugha hii ni kisiwa cha Mombasa. Kimvita ni lugha iliyo katikati, yaani inatengalugha za kaskazini (Kiamu, kisiu, kipate n.k) na zile za kusini (Kimtang’ata, Kivumba, Kipemba n.k)(xvi)Kingare, Kijomvu na ChichifundiChichifundi huzungumzwa sehemu zilizo kusini ya Gazi na kati ya mito ya Mkurumiji na Ranisi.Lugha hii imekaribiana na Kivumba. Kingare, lugha hii huzungumzwa eneo la Mombasa, sehemuya bandari ya Kilindini. Kijomvu huzungumzwa kaskazini mwa Mombasa. Kijomvu hukaribianasana na Kimvita.

MGAWANYO WA LAHAJALahaja zinaweza kugawanywa katika makundi manne kama ifuatavyo:1. Lahaja za kaskaziniLahaja hizi ziko mwambao wa Somalia na Kenya. Hujumuisha lahaja ndogondogo kama vilekiamu, Kitukuu, Kipate, Kingozi, Kisiu, Chimbalazi/Chimiini2. Lahaja za kusiniLahaja hizi ziko Pemba, Unguja na Komoro na hujumuisha Kiunguja, Kihadimu, Kipemba,Kingazija, Kitumbatu n.k3.Lahaja za katikatiLahaja hizi hujumuisha lahaja za Kivumba, Kimtang’ata, Kimrima, Kimvita, Kingao n.k4.Lahaja za baraHizi hujumuisha lahaja za Kingwana (Kongo) na misemo ya wageni kama vile wazungu nawahindi.MAMBO YANAYODHOOFISHA LAHAJA(a) Maendeleo ya njia za usafiri kama vile barabara, reli, meli n.k(b) Maendeleo ya njia za upashanaji habari kama vile redio, televisheni na magazeti.(c) Kuwepo chini ya utawala wa dini moja(d) Usanifishaji: Hasa inaposanifishwa lahaja moja(e) Biashara: Kwa kuwa huwakutanisha watu pamojaDHIMA YA LAHAJA KATIKA LUGHA(i) Kukuza lugha: Lugha ya Kiswahili imechukua baadhi ya misamiati yake kutokabaadhi ya lahajaMfanoKivumbaKiswahili sanifuKawashindi -Aliwashinda

(ii) Kusanifisha lugha(iii) Kuonesha mitindo mbalimbali ya wazungumzaji(iv) Kupamba mazungumzo ya wazungumzaji mbalimbali: Kwa kuwa wazungumzajihuibuka na misemo mbalimbali.MASWALI1. Lahaja ni nini? Jadili ukizingatia maana, dhima na manbo yanayosababisha kutokea kwake.2.Fafanua lahaja tano (5) za Kiswahili3.Chora ramani ya Afrika ya Masharika kisha onesha mgawanyo wa LahajaUSANIFISHAJI WA KISWAHILIKusanifisha lugha ni kulinganisha lugha na kuifanya lugha ikubalike kwa watu wote wanaohusikakimatumizi. Mambo muhimu katika usanifishaji wa lugha ni pamoja na kuangalia usahihi wakekisarufi na kimatamshi. Usanifishaji wa lugha unahitajika ikiwa kuna jami ya vikundi mbalimbalivya watu wanaozungumza lugha moja lakini vina matamshi na maandishi tofautitofauti baina yavikundi hivyo. Kiswahili cha leo ni matokeo ya usanifishaji wa lahaja nyingi zilizokuwazikipatikana pwani ya Afrika Mashariki. Hapo mwanzo hatukuwa na aina moja ya Kiswahiliambacho kilikuwa na maandishi na matamshi ya aina moja. Hivyo, usanifishaji wa Kiswahiliulihitajika ili kuweza kupata Kisawhili cha leo.Katika usanifishaji wa lugha ya Kiswahili, makundi yaliyohusika zaidi ni madhehebu ya kidinikama vile; Church Missionary Society (C.M.S), Universities Mission to Central Africa (U.M.C.A),London Society na Free Methodist. Madhehebu haya yalijenga makao yao katika sehemumbalimbali za nchi za Afrika Mashariki. Kutokana na hali hiyo, walipoanza kueneza dini zaowaliwajibika kutumia Kiswahili cha wenyeji wa sehemu za makao yao. Kwa hiyo, wale waliofikaUnguja(U.M.C.A) walitumia Kiunguja na wale waliofika Mombasa (C.M.S) walitumia Kimvita. Halihii ilizusha mgogoro miongoni mwa madhehebu haya. Madhebu hayo yalianza kuzozana kuhusunjia ya mwafaka ya kuendeleza Kiswahili. Dhehebu la Edward la U.M.C.A lilitumia Kiungujakatika mahubiri yao. Dhehebu la Krapf la C.M.S lilitumia Kimvita. Kati ya madhehebu haya mawilikulizuka mgogoro kuhusu lahaja iliyofaa kustawisha Kiswahili.Kutokana na mgogoro huo Gavana wa Tanganyika aliitisha mkutano mwaka 1925 ili kujadililugha ambayo ilifaa kustawishwa kama lugha ya mawasiliano nchini Tanganyika. Lengo lamkutano huo lilikuwa kutafuta lugha moja ya Kienyeji ambayo ingetumiwa katika shule zote zaAfrika Mashariki. Katika mkutano huo, uamuzi ulifikiwa kwamba Kiswahili kitakuwa lugha

itakayotumiwa. Baada ya mkutano huo kulibuniwa kamati kuu ya kupiga chapa (CentralPublishing Committee).Kazi ya kamati hii ilikuwa ni kujishughulisha na azma zote za kupigisha chapa vitabu vya shulevisivyokuwa vya dini ambavyo vingetumika katika sehemu zote ambako Kiswahili kilikuwakinatumiwa katika Afrika Mashariki.Hatua ya kwanza iliyochukuliwa na kamati hiyo ya Afrika ni kuzishauri nchi zingine za AfrikaMashariki kufuata mtindo mmoja wa kukiendeleza Kiswahili kwa hati za Kilatini. Katika mkutanohuo, uamuzi wa kutumia Kiunguja badala ya Kimvita ulitiliwa mkazo. Mwaka 1929, katibu waHalmashauri wa magavana wa Afrika Mashariki aliziandikia serikali nne zilizohusika kuhusu sualala kubuni kamati ya lugha ya Afrika Mashariki. Mnamo tarehe 01-01-1930 kamati ya AfrikaMashariki ilianzishwa iliyoitwa INTER- TERRITORIAL LANGUAGE (Swahili) COMMITTEE.MASWALI:(1) Eleza sababu zilizofanya kiunguja kiteuliwe kuwa msingi wa lahaja ya usanifishaji.(2) “Kuteuliwa kwa lahaja ya Kiunguja kulidumaza lahaja nyingine za Kiswahili.” ThibitishaUmuhimu wa usanifishaji(i) Kupata aina moja ya lugha itakayotumika katika shughuli zote muhimu kama vile;mwawasiliano, ufundishaji n.k(ii) Kukuza msamiati wake na kuhakikisha kuwa kuna aina moja ya msamiati.(iii) Kurahisisha mawasiliano miongoni mwa watumiaji wa lugha hiyo; kwa kuweka manenokiarabu na ya kigeni katika muundo wa maneno ya kibantu.(iv) Kurahisisha maneno yote ambayo yameishilia kuendelezwa kimakosa kutokana na haliya kutumiwa mara kwa mara.(v) Kiswahili kilisanifiwa kwa lengo la kuandikwa kamusi na vitabu vya Kiswahili.(vi) Kiswahili kilisanifiwa ili kuwa na hati moja ya kuandikia.Hatua zilizochukuliwa wakati wa usanifishaji(i) Kuteua lahaja ya usanifishaji miongoni mwa lahaja nyingi: Mfano, Kiswahili, lahja yaKiunguja iliteuliwa(ii) Kurahisisha matamshi ili yawe ya aina moja nchi nzima: Kwa mfano, mwaka 1926palitolewa mapendekezo kadha wa kadha kuhusu maandishi ya Kiswahili katika gazeti la“Mamboleo” Ilipendekezwa kuwa, herufi “C” itumike badala ya herufi “ch” Mfano

Chai –caiChumba- cumbaChatu – catu(iii) Kuundwa kwa chombo cha usanifishaji: Kwa mfano katika usanifishaji wa lugha yaKiswahili kamati ya usanifishaji iliundwa “ The Interterritorial Swahili LanguageCommittee” (01-01-1930)(iv) Kutayarisha kamusi na vitabu vya sarufi ya lugha inayohusika: Kwa mfano, wakati wausanifishaji wa lugha ya Kiswahili, Mwaka 1930-1942, kamati ya lugha ilishughulikiakamusi ya Madan ya Kiswahili –Kiingereza(v) Kuandaa wataalamu wa usanifishaji watakaoshughulikia shughuli zote za usanifishaji:Mfano kabla ya uhuru- Wataalamu wa kizungu ndio walioshughulikia usanifishaji waKiswahili. Baada ya uhuru- TUKI, BAKITA na vyombo vingine vya ukuzaji wa lugha yaKiswahili.Sababu za kuteuliwa kwa lahaja ya Kiunguja kuwa Kiswahili Sanifu(i) Kiunguja kilienea kwa kasi katika sehemu nyingi za Pwani ya Afrima Mashariki.Kuenea huko kilikuwa ni kigezo cha kwanza kuteuliwa kuwa Kiswahili sanifu.(ii) Lahaja ya Kiunguja ilionekana kuwa ina matamshi mepesi na yasiyotatanisha kwawakaazi wa Pwani ya Afrika Mashariki.(iii) Kiunguja kilionekana kuwa na uhusiano mkubwa sana na lahaja nyingine zaKiswahili pamoja na lugha za Kibantu. Hivyo Kiswahili kingeweza kuelewekakiurahisi zaidi kuliko lahaja nyingine.(iv) Kiunguja kilikuwa kilishaanza kutumika katika maandishi mathalani katika magazetina vitabu mbalimbali.(v) Lugha ya Kiunguja ilikuwa ina utajiri mkubwa wa misamiati. Hivyo ilikidhi zaidihaja za watumiaji kama ilivyokusudiwa.Kuteuliwa kwa lahaja ya Kiunguja kulivyodumaza lahaja nyingineMoja ya hasara ya kuteuliwa kwa lahaja ya Kiunguja kuwa msingi wa Kiswahilisanifu ni kudumaza, kuua, kufifisha au kuviza lahaja nyingine za Kiswahili. Hiiilitokana na sababu mbalimbali kama zifuatazo;Lahaja teule ilipata hadhi ya juu hivyo matumizi ya lahaja nyingine yakaonekanakama ni ya watu wa hali ya chini.Lahaja sanifu iliweza kuandika vitabu vya sarufi, kamusi na fasihi. Hivyo kutumikakatika mfumo rasmi wa elimu. Hali hii ikasababisha lahaja nyingine kubaki nyuma nakutokutiliwa maanani au mkazo.

Lahaja iliyosanifiwa iliendelea kuteka fursa ya kuendesha mawasiliano katikaNyanja mbalimbali kama vile utawala, dini, biashara na hivyo kuzinyima lahajanyingine fursa ya kukua.Lahaja zisizosanifishwa zilipwaya na kuonekana kudumaa na kutoweka kabisa katikamifumo ya kupashana habari, vyombo vya habari, dini, elimu, utawala na biashara.Lahaja inayosanifishwa huchukua maneno ya lahaja nyingine hivyo kusababishalahaja ya usanifishaji kujiongezea misamiati na kusababisha l

Wazenji walitema lugha kwa ufasaha na walikuwa na viongozi waliowahutubia kwa lugha yao.Kutokana na neno “ Zenji ” kuna uwezekano kuwa kabla majilio ya Waarabu, Kiswahili kiliitwa “ Kiazania ” a

Related Documents:

Kiswahili dialects are endangered by, among other factors, the onslaught of standard Kiswahili, English, and Sheng, and so they are likely to be dying. The paper holds the position that the Kiswahili dialects are vital for the development of standard Kiswahili and, therefore, their endangerment is the endangerment of standard Kiswahili.

Introduction to Kiswahili Poetry KSX 2102 Kiswahili Oral Literature KSX 2104 (with Mr Innocent Yerindabo) Introduction to Kiswahili Novels KSX 2202 History and Development of Kiswahili KSX 3101 Kiswahili Teaching Methods KSX 3201 Drafts Reviewed: Advanced Proficiency in Kiswahili KSX 1102 by Boaz Mutungi.

Song as an aspect of Kiswahili poetry. Origin and development of modern Kiswahili classics such as taarab. Leading founders of Kiswahili popular song in East Africa, history and development of Kiswahili solo, choral and orchestra composition. Themes, style and language use in popular Kiswahili songs.

Kiswahili) na Shahada ya Umahiri/Uzamili ya Sanaa katika Kiswahili (MA. Kiswahili – akitamilikia Fasihi) zote kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania. Chuoni anafundisha kozi za Kiswahili - Lugha, Isimu na Fasihi ikiwemo kozi ya Uandishi wa Kubuni. Pia, hufundisha Kiswahili

4.0 KISWAHILI (102) 4.1 MATOKEO YA MTIHANI WA SOMO LA KISWAHILI Jedwali hili linaonyesha matokeo ya mtihani wa somo la Kiswahili katika muda wa miaka minne (2005 hadi 2008). Jedwali 6: Matokeo ya mtihani wa Kiswahili (2005 - 2008) Mwaka Karatasi Watahiniwa Alama ya Juu Alama ya Wastani Alama ya Tanganisho 2005 1 2 3 Jumla 259,301 40 80

Kwa mantiki ya nadharia hii, wataalamu hawa hukiona Kiswahili kuwa kilianza kama Pijini kwani ni tokeo la mwingiliano baina ya wenyeji wa pwani ya Afrika Mash

AKS 301: Kiswahili Structure AKS 302: Theories of Literary Criticism AKS 303: Contemporary Kiswahili Novel and Play AKS 400: Sociolinguistics AKS 401: Second Language Learning AKS 402: Kiswahili Poetry AKS 403: Oral Literature in Kiswahili History AHT 102: Introduction to Political Science AHT 200: A History of Kenya AHT 201: Themes in African

Mchango wa Fasihi ya Kiswahili katika Kuudumisha Utambulisho wa Kiswahili : Mifano Kutoka Kazi za Fasihi za Kiswahili Dk. Wael Nabil Ibrahim Othman* Abstract This study emphasizes that the Swahili literature has a very big role in consolidating and maintaining Swahili identity. In the field of Swahili poetry