N14/2/ABSWA/SP1/SWA/TZ0/XX/T

2y ago
238 Views
7 Downloads
789.47 KB
7 Pages
Last View : 5d ago
Last Download : 1m ago
Upload by : Rosemary Rios
Transcription

N14/2/ABSWA/SP1/SWA/TZ0/XX/T88142319SWAHILI B – STANDARD LEVEL – PAPER 1SWAHILI B – NIVEAU MOYEN – ÉPREUVE 1SWAHILI B – NIVEL MEDIO – PRUEBA 1Wednesday 12 November 2014 (morning)Mercredi 12 novembre 2014 (matin)Miércoles 12 de noviembre de 2014 (mañana)1 h 30 mTEXT BOOKLET – INSTRUCTIONS TO CANDIDATES Do not open this booklet until instructed to do so. This booklet contains all of the texts required for paper 1. Answer the questions in the question and answer booklet provided.LIVRET DE TEXTES – INSTRUCTIONS DESTINÉES AUX CANDIDATS N’ouvrez pas ce livret avant d’y être autorisé(e). Ce livret contient tous les textes nécessaires à l’épreuve 1. Répondez à toutes les questions dans le livret de questions et réponses fourni.CUADERNO DE TEXTOS – INSTRUCCIONES PARA LOS ALUMNOS No abra este cuaderno hasta que se lo autoricen. Este cuaderno contiene todos los textos para la prueba 1. Conteste todas las preguntas en el cuaderno de preguntas y respuestas.8814-23197 pages/páginas International Baccalaureate Organization 2014

–2–Blank pagePage viergePágina en blanco8814-2319N14/2/ABSWA/SP1/SWA/TZ0/XX/T

–3–N14/2/ABSWA/SP1/SWA/TZ0/XX/TKIFUNGU AEPHRAIM SEKELETI: MSANII MWENYE MAFANIKIO YA NYIMBO ZAINJILI ZAMBIA ANAYEIMBA KWA KISWAHILINyota wa muziki wa Injili* wa nchini Zambia,Ephraim Sekeleti, ni kati ya waimbaji wa muzikihuo wanaokubalika sana nchini Tanzania.510152025Ni mtunzi na muimbaji mzuri; uwezo wa kuimbabaadhi ya nyimbo zake kwa lugha ya Kiswahilini kati ya sifa zinazochangia umaarufu wakezaidi nchini.Licha ya kufanya muziki wake nchini Zambia,amewahi kuja nchini Tanzania na kurekodi albamuyake nzima kwa lugha ya Kiswahili. Kati yanyimbo zake zinazotamba hapa nchini ni pamojana “Baraka Zako”, “Uniongoze” na “ Mwaka Huu”.Ephraim hajui Kiswahili fasaha lakini nyimbozake hizo alifundishwa kuziimba kwa lugha yaKiswahili na mchungaji ambaye pia ni muimbaji wanyimbo za Injili kutoka Tanzania, Ency Mwalukasa.Muimbaji huyo amesema ataendelea kuimbanyimbo za injili kwa sababu zimempa changamotoambazo zimemfanya kuwa mtu wa nguvu zaidi.Ephraim Sekeleti alizaliwa mwaka 1983 katika mji wa Kalulushi nchini Zambia. Alimaliza elimuyake ya sekondari katika shule ya Kalulushi mwaka 2001. Yeye ni mtoto wa pili kutoka mwisho katiya watoto sita wa familia yao na aliingia kwenye muziki wa Injili tangu akiwa kinda. Alifundishwakupiga kinanda na mmishionari alipokuwa bado mdogo.Mwaka 2002 akiwa na kiu ya kurekodi albamu yake, aliamua kwenda Afrika Kusini kwa kutumiakiasi kidogo tu cha pesa alichokuwa nacho. Nia ilikuwa kurekodi albamu yake ya kwanza.Pamoja na jitihada hizo baada ya kufika nchini Afrika ya Kusini, alijikuta anarekodi nyimbo mbili tukati ya albamu nzima.Hivyo akaamua kujiingiza katika jukwaa la Pretoria na ndipo akapata fursa ya kuimba mbele yaRais wa Afrika Kusini wakati huo, Nelson Mandela.3035Karibu aamue kuacha kuendelea na muziki wa Injili ili aimbe muziki wa kidunia lakini akawamuaminifu kuendelea na uimbaji wa Injili. Mlango ulifunguka na kumruhusu kurekodi albamu yakwanza iitwayo “Temba Baby”.Baada ya kurekodi na kuuza nakala za kutosha za albamu hiyo ya “Temba Baby”, aliamua kurudinyumbani kuwekeza fedha zake. Aliona awekeze zaidi kwenye albamu yake ya pili iliyopatamafanikio makubwa iliyoitwa “Limo Ndanaka”. Albamu hii ilifanya vizuri kwenye chati mbalimbaliza muziki wa Injili. Anafurahi kuona nyimbo zake zikiwa na athari nzuri kwa watu.Imetoholewa kutoka na mwandishi wetu wa Nipashe (2013)*Injili: aina ya Muziki wa kidini8814-2319Turn over / Tournez la page / Véase al dorso

–4–N14/2/ABSWA/SP1/SWA/TZ0/XX/TKIFUNGU BSERIKALI: UHAMIAJI WA ANALOJIA KWENDA DIJITALI UFANYIKEKWA AWAMU51015202530Mfumo wa mawasiliano Tanzania unabadilika kutoka mfumo mmoja (analojia)hadi mwingine (dijitali) ambao unafaa zaidi. Serikali imeitaka Mamlaka yaMawasiliano Tanzania (TCRA) kuhakikisha kwamba zoezi la uhamiaji wa mfumowa matangazo ya analojia kwenda dijitali unafanyika kwa awamu ili kuondoahofu ya wananchi kukosa matangazo ifikapo Desemba 22 mwaka huu.Agizo hilo limetolewa jana na Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. FenellaMukangara, wakati akizungumza na baadhi yaviongozi wakuu wa TRCA, ambao waliwasilishataarifa na mabadiliko ya mfumo huo ofisinimwake. Aidha, Waziri huyo aliusisitizia uongozihuo kuendelea kutoa elimu sahihi kwa ummakwa kuzingatia ratiba ya uzimaji wa mitambohiyo iliyotolewa.Mkurugenzi wa Utangazaji wa TRCA HabiGunze akiwasilisha taarifa hiyo kwa Wazirialisema, uzimaji wa matangazo hayoutafanywa kwa awamu tano. Alisema kwakanda ya Dar es Salam, mitambo ya analojiaitazimwa Desemba 31, mwaka huu saa sita usiku na maeneo husika ni jiji laDar es Salaam, Kibaha, Bagamoyo Vituo vitakavyohusika ni TBC1, ITV, EATV naCapital TV. Vituo vingine vitakavyoathiriwa eneo la Dar es Salaam ni pamoja naTumaini TV, ATN, Mlimani.Katika kanda ya Dodoma na Tanga mitambo hiyo itazimwa Januari 30, 2013.Maeneo husika yakiwa ni Manispaa ya Dodoma Kibaigwa, Mvumi Mtera naMkinga likiwa eneo la kumalizia. Vituo vitakavyohusika ni: TBCI, ITV, EATV, TV yaManispaa ya Tanga na ATN.Dkt. Mukungara alisema wananchi wanaoishi katika maeneo ambayohayakutajwa katika ratiba hiyo, wataendelea kupata matangazo kupitiamfumo wa matangazo ya televisheni kama ilivyo sasa hadi hapo mitambo yakupokea mfumo wa matangazo ya dijitali itakapokamilika kwenye maeneo yao.Alizitaka kampuni zinazoweka mitambo ya dijitali kuongeza kasi ili kuhakikishakuwa ujenzi wa mitambo hiyo unakamilika nchini kote kabla ya mwaka 2015.Imetoholewa kutoka Hellen Mwango, Nipashe (2013)8814-2319

–5–N14/2/ABSWA/SP1/SWA/TZ0/XX/TKIFUNGU CSAMAHANI YAWEZA KUONDOA KINYONGO NA KUOKOA UHUSIANOHuwa inasemwa kuwa tenda wema nenda zako usingoje shukrani. Na kwamba binadamu nikiumbe asiyekumbuka wala kujali wema. Ubinadamu huweza kuthibitishwa kwa vitu vidogoambavyo wakati mwingine unaweza kuvidharau. Pia hakuna binadamu kamili, wote tuna udhaifu.510Kutokana na udhaifu tulio nao ndiyo maana wakati mwingine tunajikuta tunafanya au kusemamambo ambayo yanawaumiza wengine. Vitendo hivi vya kikatili huwa vinauma zaidi vinapotendwana ndugu ama jamaa wa karibu kuliko vinapotendwa na mtu wa mbali.Kuna jirani wangu ambaye yalimkuta haya ya kufadhili ndugu zake na hatimaye wakamtendana kumdharau kama vile sio ndugu yao. Huyu kaka akanisimulia jinsi alivyojibebesha jukumula kuwalea, kuwatunza na kuwasomesha ndugu zake hadi wakapata kazi na kujitegemea nawengine kufunga ndoa na kuanza maisha yao.Huku akitikisa kichwa kwa huzuni akasimulia alivyoweka pembeni mambo yake mengi kimaishaikiwemo kumaliza shahada yake ya kwanza ili apate kuwasomesha ndugu zake nao wawezekujitegemea.15Kawaida katika maisha kuna kupanda na kushuka na huyu kaka shughuli zake za kibiasharahazikumwendea vizuri. Akajikuta anaandamwa na madeni na huku asiwe na njia yakudumu ya kumwingizia kipato. Hivyo akajaribu kutafuta jinsi ya kujisimamia tena kimaisha.Na katika shughuli zake akasafiri nje ya nchi kujaribu kuangalia uwezekano wa biashara.Ndiposa wakati akiwa kwenye harakati, ndugu zake wakafanya njama, wakaleta dalali wakasombavitu vyote vya nyumbani na kwenda kuvipiga bei wakidai wanataka kulipa madeni yake.20Kwa kifupi ni kwamba wale aliowaita ndugu zake wamemsafisha na kumwacha mweupebila chochote. Na hivi sasa anaanza tena maisha upya akijaribu kujitibu majeraha ya moyo wake.Hivyo nilipopata nafasi ya kuzungumza naye nilimsisitizia umuhimu wa kusamehe na kuwekahuru roho yake. Nikamkumbusha kwamba waliompora mali zake hawajampora nguvu, akili nauwezo wa kutafuta mali nyingine zaidi ya zile alizokuwa nazo.25Unaposamehe unajipunguzia [ – X – ] ambayo umeyapata kwa uliyotendewa. Kawaida watuwanapokutenda na kukufanyia ukatili wanakuwa [ – 27 – ] sana kuomba [ – 28 – ] wakidhani kwakufanya hivyo watakuwa wamejishusha sana. Hawataki kuonekana kuwa ni [ – 29 – ] na kukubali[ – 30 – ] walio nao kwa kuomba msamaha.Imetoholewa kutoka Sizarina, Taifa Leo (2013)8814-2319Turn over / Tournez la page / Véase al dorso

–6–N14/2/ABSWA/SP1/SWA/TZ0/XX/TKIFUNGU DJANUARI YAANZA NA IDADI NDOGO YA WATALII PWANIMombasa na Mathias RingaHoteli za pwani zimekumbwa na upungufu mkubwa wa watalii baada ya msimu wa Krismasi na MwakaMpya kuisha. Wakati wa Krismasi na Mwaka Mpya, hoteli katika mji wa Mombasa, Malindi, Watamu naDiani zilijaa kutokana na idadi kubwa ya watalii kutoka humu nchini.5Baadhi ya hoteli za Mombasa zilikuwa na asilimia 80 ya watalii kutoka humu nchini wakati wa msimuwa sherehe. Lakini baada ya msimu wa sherehe kuisha, hoteli za Mombasa na Lamu zina wageni wachachemno baada ya watalii kutoka humu nchini kurudi kazini na wanafunzi kurudi shuleni.Kulingana na Mwenyekiti wa Chama cha Utalii, Mombasa na Pwani (MCTA) Bw. Mohammed Hersi, hotelinyingi za Mombasa zina asilimia 40 ya wageni.Ugaidi10Kati yao, alisema, ni watalii kutoka nchi za nje na wageni ambao wanahudhuria mikutano na warsha.Bw. Hersi alituarifu kuwa idadi ya watalii kutoka Ulaya ni ndogo kwa sababu ya tisho la ugaidi na kuzorotekakwa uchumi barani Ulaya.“Baada ya msimu wa sherehe kuisha, hoteli nyingi za Mombasa zina wageni wachache mno kutokana nawageni wa humu nchini kurudi kazini na vile vile shule kufunguliwa”, akasema.1520“Kwa sasa hoteli zinategemea maandalizi ya mikutano na warsha na watalii wachache kutoka mataifa yakigeni”, akaarifu. Hata hivyo, Bw. Hersi alisema kuwa hoteli za Lamu ndizo ambazo zinakumbwa na uhabamkubwa wa watalii. Bw. Hersi ambaye pia ni Afisa Mkuu wa Hoteli za Heritage aliarifu kuwa hoteli katikaKaunti ya Lamu zina asilimia 20 ya wageni kutokana na athari ya visa vya ugaidi vilivyotokea miaka yahivi majuzi.Mkuu wa Utalii katika Kaunti ya Kwale, Bw. Adam Sheikh, alisema kuwa hoteli za Pwani Kusini zina asilimia60 ya wageni baada ya msimu wa sherehe kuisha.8814-2319

–7–N14/2/ABSWA/SP1/SWA/TZ0/XX/TUghaibuniBw. Sheikh alidokeza kuwa idadi kubwa ya wageni ni watalii kutoka Ujerumani, Uingereza, Italia, Ufaransana Australia. Hoteli za Pwani Kusini, alisema, zitaendelea kupokea watalii kutoka Ulaya hadi Machimwaka huu.25“Ijapo idadi ya watalii kutoka humu nchini imeshuka mno, bado tuko na watalii kutoka Ulaya ambaowataendelea kuwasili hadi Machi.” Ili kuimarisha sekta ya utalii nchini, Bw. Sheikh aliomba serikalikuu kuruhusu mashirika zaidi ya ndege ya kimataifa kuanzisha safari za moja kwa moja kutoka Ulayahadi Mombasa.Afisa Mkuu wa Chama cha Kutoa Huduma za Hoteli Nchini (KAHC) tawi la Pwani Bw. Sam Ikwaye alisemakuwa hoteli za Malindi na Watamu zina kati ya asilimia 50 na 60 ya wageni kutokana na watalii kutoka Italia.Imetoholewa kutoka Mathias Ringa, Taifa Leo (2014)8814-2319

Ephraim hajui Kiswahili fasaha lakini nyimbo zake hizo alifundishwa kuziimba kwa lugha ya Kiswahili na mchungaji ambaye pia ni muimbaji wa nyimbo za Injili kutoka Tanzania, Ency Mwalukasa. Muimbaji huyo amesema ataendelea kuimba nyimbo za injili kwa sababu zime

Related Documents:

installations on n14 plus cummins engines. application notes the cbrake by jacobs model 455b and 455c engine brakes are for use on cummins n14 plus engines only. consult your local cummins distributor or dealer to verify your engine cpl is an n14 plus engine. misapplication could result in engine and/or engine brake damage. refer to cummins .

Cummins N14 SERIES MODELS N14 / NTA14 ENGINES INTERSTATE-McBEE, LLC 5300 Lakeside Avenue Cleveland, Ohio 44114 U.S.A. . N14 PARTS LISTING ENGINE KITS Part # QTY Description Comment M-4955558 1 Inframe Kit - .020"/.040" M-4955555 Cylinder Kit M-4955559 1 Inframe Kit - .020"/.040" M-4955556 Cylinder Kit .

Page 2 2014-03-27 TIA Portal V13 - Introduction TIA Portal V13 SP1 Egy fejleszt szoftver minden automatizálási feladatra WinCC V13 SP1 SIMATIC HMI Startdrive V13 SP1 SINAMICS STEP 7 V13 SP1 SIMATIC PLC Safety V13 SP1 Safety Totally Integrated Automation Portal One common engin

Stop Work Authority (SWA) Award Program Goal – Enhance safety awareness and worker safety through promotion of SWA and presentation of: 1. A WOGISA SWA Recognition Award(s) at General Membership Meetings 2. The Annual Governor’s SWA Award at the An

8814-2331 – 4 – n14/2/abtam/sp1/tam/tz0/xx/t புவ் b இகணயவி விைிற கனயால ஏற ு் ஆ துை்

Ten reasons why to move to SCCM 2012 R2 SP1 Reasons not to upgrade, yet . Agenda What do we need? SCCM 2012 SP2? SCCM 2012 R2 SP1? SCCM 2012 SP2 is the update itself SCCM 2012 R2 SP1 is a small package that enables (hidden) features in SCCM 2012 SP2 when coming from SCCM 2012 SP1

rpll/mnl.star. atis 126.4 alt set: hpa trans level: fl130 trans alt: 11000'. 4200' 7000' 5000' 2 90 1 9 0 0 2 0 adnim manila 113.8 miamia n14 30.5 e121 01.3 d rodat n14 58.8 e121 19.6 manila 113.8 miamia n14 30.5 e121 01.3 d cabanatuan cab112.7 cab n15 28.9 e121 01.5 d tarta n15 02.1 e1

the American Board of Radiology (ABR) Core and Certifying examinations administered between January 1 – December 31, 2018. The guide has undergone a few minor changes compared to the 2018 version, which was significantly revised com- pared to earlier versions, reflecting changes in NIS content on the examinations. The primary change in this study guide is the addition of Core Concepts of .