KUCHUNGUZA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA RIWAYA ZA

2y ago
482 Views
13 Downloads
593.00 KB
100 Pages
Last View : 7d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Farrah Jaffe
Transcription

KUCHUNGUZA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA RIWAYA ZAKISWAHILI:UCHUNGUZI KIFANI WA RIWAYA ZA VIPULI VYA FIGO NA SIRI ZAMAISHASIDORA JOSEPH KIMAMBOTASINIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SEHEMU YAMASHARTI YA KUTUNUKIWA DIGRII YA UZAMILI (M.A KISWAHILIFASIHI) YA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIAOKTOBA, 2015

iiUTHIBITISHOAliyetia saini yake hapa chini, anathibitisha kuwa, amesoma tasnifu hii iitwayoKuchunguza Matumizi ya Lugha katika Riwaya ya Kiswahili: UchunguziKifani wa Vipuli vya Figo na Siri za Maisha na anapendekeza ikubaliwe na ChuoKikuu Huria Cha Tanzania kwa ajili ya kutimiza sehemu ya masharti ya kutunukiwaDigrii ya Uzamili (MA) katika Kiswahili ya Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania.DKT. MOHAMED OMARY .MsimamiziTarehe

iiiHAKIMILIKIHairuhusiwi kuiga au kunakili kwa namna yoyote sehemu yoyote ile ya tasinifu hiikwa njia yoyote kama vile, kielektroniki, kurudufu nakala, kurekodi au njia yoyotenyingine bila ya idhini ya mwandishi au Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa niaba.

ivTAMKOMimi, SIDORA JOSEPH KIMAMBO, nathibitisha kuwa tasinifu hii ni kazi yanguhalisi na haijawahi kuwasilishwa katika Chuo Kikuu kingine chochote kwa ajili yakutunukiwa shahada kama hii au nyingine yoyote.Sahihi: e

vTABARUKUNatabaruku kazi hii kwa Mume wangu Mr. F. Foya

viSHUKURANIKazi hii ya Utafiti ni mchango wa matokeo ya safari ndefu baina yangu mimi nawatu wengine wakiwemo walimu wangu; rafiki na ndugu siyo rahisi kuwashukurukwa kina kila mmoja na mchango wake kwangu katika kukamilisha kazi hii lakinikwanza napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyenipa uhai na afya njema yakuniwezesha katika kipindi chote cha masomo yangu.Pili, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa msimamizi wangu wa tasnifu hii,Daktari, Mohamed Omary kwa kunifuatilia kwa ukaribu sana na kuniongoza vyemakwa kila hatua ya utafiti huu bila kusita wala kuchoka kunishauri na kuniongozakufanya marekebisho ya kazi hii hatua kwa hatua hadi ilipokamilika. Aidha, msaadawa msimamizi huyu, pamoja na moyo wake mkunjufu hauwezi kulipwa walakufananishwa na kitu chochote, bali jambo la msingi ni kumwombea maisha marefuna afya njema kwani wapo watu wengi wanaohitaji msada wake. Ninachowezakusema ni kukushukuru sana Baba, Profesa Sengo, Mwenyezi Mungu akulinde,akupe afya njema na azidi kukutumia ili uwasaidie watu wengine.Tatu, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa walimu wengine wote wa ChuoKikuu Huria Cha Tanzania kwa kunifundisha vizuri na kuniongoza katika kipindichote cha masomo yangu akiwemo profesa, E. Mbogo, Dr. P. P. Lipembe, Prof. S.Mdee, Dr. H. Simpassa na Dr. Z. Elisifa.Nne, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa wanangu Emmanuel, Patrick,Doreen na Lilian ambao wamenipa moyo na msaada mkubwa kuwa karibu sana namimi wakati naiandaa kazi hii. Mungu awape uzima.

viiMwisho, nawashukuru wanachuo wenzangu walionipa ushauri na kutoa mchangowao mkubwa katika kuikamilisha kazi hii. Wanachuo hao ni Rehema Adam, GladysMadoffe na Roxana Mhando. Si rahisi kumtaja kila mmoja kwa kina balinawashukuru wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha kaziyangu.Asanteni sana

viiiIKISIRIRiwaya za Vipuli vya Figo na Siri za Maisha ni riwaya mpya, kwa maana ya riwayaza karibuni zenye kusheheni matukio ya kusisimua na kutoa mafunzo kwa yeyotealiyewahi ama atakayezisoma aidha kwa kujiburudisha au kujifunza. Ni kazi nzuri naza kuvutia za Profesa Emmanuel Mbogo. Utafiti huu ulifanywa kwa lengo lakuchunguza matumizi ya lugha katika riwaya hizi mbili na kuibua dhamirambalimbali zilizojitokeza. Utafiti huu ulikuwa na malengo mahususi matatu ambayoni, kuchambua matumizi ya lugha ya kitamathali katika riwaya za Vipuli vya Figo naSiri za Maisha, kuchambua matumizi ya lugha yasiyo ya kitamathali katika riwaya zaVipuli vya Figo na Siri za Maisha na kuwasilisha dhamira zinazojitokeza katikariwaya za Vipuli vya Figo na Siri za Maisha. Katika kutimiza malengo haya,tulikusanya data kwa kutumia mbinu za usomaji makini na upitiaji wa nyarakamaktabani na kufanya uchambuzi wa data kwa kutumia mbinu ya mkabala wakimaelezo na nadharia ya Simiotiki.Maokeo ya utafiti yanaonyesha kwamba, matumizi ya lugha yaliyojitokeza katikariwaya za Vipuli vya Figo na Siri za Maisha ni tamathali za usemi na zisizo tamathaliza usemi. Matumizi ya lugha ya kitamathali ni tashibiha, tashihisi, tafsida, sitiari,kejeli na dhihaka. Matumizi ya lugha yasiyokuwa ya kitamathali ni misemo, nahau,takriri, tanakali sauti na taharuki. Pamoja na matumizi haya ya lugha ya kitamathalina yasiyokuwa ya kitamathali pia kuna dhamira mbalimbali zimejitokeza katikariwaya tafitiwa. Dhamira hizo ni biashara haramu, umuhimu wa elimu katika jamii,Dhamira ya malezi katika jamii, hali ngumu ya maisha, siasa na uchumi na nafasi yamwanamke katika jamii.

ixYALIYOMOUTHIBITISHO . iiHAKIMILIKI . iiiTAMKO . ivTABARUKU . vSHUKURANI . viIKISIRI . . viiiYALIYOMO . ixSURAYA KWANZA . 1UTANGULIZI . 11.0Utangulizi wa Jumla . 11.1Usuli wa Tatizo la Utafiti . 11.2Tamko la Tatizo la Utafiti . 51.3Lengo Kuu la Utafiti . 51.3.1Malengo Mahususi ya Utafiti . 51.3.2Maswali ya Utafiti . 61.4Umuhimu wa Utafiti . 61.5Mipaka ya Utafiti . 71.6Mpangilio wa Tasinifu. 71.7Hitimisho . 8

xSURA YA PILI . 10MAPITIO YA KAZI TANGULIZI NA MKABALA WA KINADHARIA . 102.0Utangulizi . 102.1Maana ya Riwaya . 102.2Historia na Chimbuko la Riwaya ya Kiswahili . 132.3Kazi tangulizi Juu ya Riwaya ya Kiswahili . 152.3.1Kazi Tangulizi za Fani ya Riwaya ya Kiswahili . 152.3.2Kazi Tangulizi za Dhamira katika Riwaya . 202.3.3Kazi Tangulizi Kuhusu Riwaya za Emmanuel Mbogo . 242.4Mkabala wa Kinadharia . 252.4.1Nadharia ya Simiotiki . 252.5Hitimisho . 27SURA YA TATU . 28MBINU ZA UTAFITI. 283.0Utangulizi . 283.1Umbo la Utafiti . 283.2Eneo la Utafiti . 293.3Kundi Lengwa la Utafiti . 293.4Sampuli na Mbinu za Uteuzi wa Sampuli . 303.5Mbinu ya Uteuzi wa Madhumuni Maalumu. 303.6Data za Utafiti . 313.6.1Data za Msingi/Awali . 313.6.2Data za upili . 31

xi3.7Mbinu za Kukusanya Data . 323.7.1Usomaji Makini . 323.7.2Upitiaji wa Nyaraka . 333.8Uchambuzi wa Data. 333.9Maadili ya Utafiti. 333.10Hitimisho . 34SURA YA NNE . 35UWASILISHAJI, UCHAMBUZI NA MJADALA WA DATA ZA UTAFITI . 354.0Utangulizi . 354.1Wasifu wa Emmanuel Mbogo . 354.1.1Muhtasari wa Riwaya ya Vipuli vya Figo . 364.1.2Muhtasari wa Riwaya ya Siri za Maisha . 374.2Matumizi ya Lugha ya Kitamathali katika Riwaya Teule . 384.2.1Matumizi ya Tashibiha katika Riwaya Teule . 384.2.2Matumizi ya Tashihisi katika Riwaya Teule . 404.2.3Matumizi yaTafsida katika Riwaya Teule . 444.2.4Matumizi ya Sitiari katika Riwaya Teule . 464.2.5Matumizi yaKejeli au Kinaya katika Riwaya Teule . 484.2.6Matumizi ya Dhihaka katika Riwaya Teule . 504.3Matumizi ya Lugha Isiyokuwa ya Kitamathali . 514.3.1Matumizi ya Misemo katika Riwaya Teule . 514.3.2Matumizi ya Nahau katika Riwaya Teule . 544.3.3Matumizi ya Takriri katika Riwaya Teule . 55

xii4.3.4Matumizi ya Tanakali Sautikatika Riwaya Teule . 574.3.5Matumizi ya Lugha yaKitaharuki katika Riwaya Teule . 594.4Dhamira katika riwaya ya Vipuli vya Figona Siri za Maisha . 624.4.1Biashara Haramu . 634.4.2Umuhimu wa Elimu katika Jamii . 654.4.3Malezi katika Jamii. 684.4.4Siasa na Uchumi katika Jamii . 704.4.5Nafasi ya Mwanamke katika Jamii . 714.5.6Hali ngumu ya Maisha katika Jamii . 754.6Hitimisho . 76SURA YA TANO . 78MUHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO . 785.0Utangulizi . 785.1Muhtasari . 785.1.1Matumizi ya Lugha ya Kitamathali katika Riwaya Teule . 785.1.2Matumizi ya Lugha yasiyo yaKitamathali katika Riwaya Teule . 795.1.3Dhamira katika Riwaya Zilizoteuliwa . 795.2Hitimisho . 795.3Mapendekezo . 80MAREJELEO . 82

1SURAYA KWANZAUTANGULIZI1.0Utangulizi wa JumlaWataalamu wengi wa fasihi ya Kiswahili wamefanya tafiti mbalimbali zikiwemo zakuchunguza matumizi ya lugha katika riwaya, tamthilia, na ushairi kwa ujumla,lakini tafiti hizo kwa upande mwingine bado hazijagusa uteuzi wa lugha kwa namnainavyotumika kulingana na makusudio ya mwandishi (Wamitila, 2002).Kwa maanahiyo, utafiti huu umefanywa kama sehemu mojawapo ya kuchangia kujazia pengo lautafiti ili kukuza na kuimarisha utafiti hasa katika riwaya ya Kiswahili. Sura yakwanza imeelezea vipengele vya kiutangulizi kama vile; usuli wa tatizo la utafiti,tamko la tatizo la utafiti, lengo kuu na madhumuni mahususi ya utafiti. Aidhamaswali ya utafiti, umuhimu wa utafiti, mipaka ya utafiti na mpangilio wa tasnifu piavimewasilishwa katika sura hii.1.1Usuli wa Tatizo la UtafitiBinadamu katika kuishi kwake anakutana na mambo mbalimbali ambayo hana budikupambana nayo ili aweze kuyamudu mazingira anamoishi. Mambo ambayobinadamu hukutana nayo katika maisha ni mengi na yanaweza kuelezwa kwakutumia utanzu wa fasihi hususani riwaya (Msokile, 1992). Kwa kupitia utanzu wariwaya mtunzi huiumba na kuifinyanga hadithi yake kwa kutumia usaniiunaowajenga wahusika wake kwa kutumia kanuni na taratibu za uzuri,upendezaji,uozo na ubaya na kwa hiyo humwathiri binadamu katika kuvuta ama kuchukizamilango yake ya fahamu(Khamis, 2007).

2Hata hivyo, Senkoro (1982) anatoa ufafanuzi wa kina wa utanzu huu na kuelezeakuwa, visa na matukio ndio msingi na uti wa mgongo wa riwaya ya Kiswahili nanyingeine zote duniani. Kisa ndiyo sehemu ya asili ambayo imekuwepo toka wakatiwa ngano hadi katika riwaya. Vilevile, visa na matukio hayo yanayowahusuwahusika na matendo yao huelezwa kwa mchangamano na mwingiliano mkubwaambao si rahisi kuupata katika utanzu mwingine wowote wa kazi ya fasihi kamaushahiri na tamthiliya. Aidha, kuwepo kwa utanzu wa riwaya katika kuelezea maishana matukio anayopambana nayo mwanadamu hakumaanishi kutokuwepo kwa utanzumwingine wa fashihi ya kiswahili na fasihi kwa ujumla duniani kote. Ndungo (1991)katika maelezo yake anaamini kuwa, fasihi simulizi ni sehemu ya fasihi ambayo niya zamani sana ambayo masimulizi yake yalihifadhiwa katika maandishi. Kwaupande wa riwaya, Msokile (1992) anasisitiza kwa kusema kwamba, utanzu wariwaya ulianza kustawi wakati wa mageuzi ya viwanda na utamaduni huko ulaya.Kwa maana hiyo, utanzu huu ulizuka baadaye sana ukilinganishwa na tanzu nyingineza kifasihi Kama vile, ushairi na nyimbo. Utanzu huu ulizuka wakati maalumu wahistoria ya jamii, wakati huo jamii ilikwisha kuwa kubwa yenye makao maalumu nalugha ya jamii hiyo ilikuwa imekwisha pevuka kiasi cha kuweza kueleza dhana,imani na amali mbalimbali za jamii kwa wasanii.Mlacha na Madumulla (1991) wanaeleza kuwa, historia ya riwaya ya Kiswahilihaikupishana sana na hali hiyo ya kutanguliwa na tanzu nyingine za fasihi ingawakwa hakika umejitokeza mapema zaidi kabla ya tamthiliya ya Kiswahili. Maelezohaya yanaonyesha kuwa, utanzu wa riwaya ulikuwepo tangu zama za kale lakiniukawa umefungamanishwa katika tungo za kishairi simulizi hususani katika tenzi.

3Kwa maelezo haya,inaonyesha kwamba,utanzu wa riwaya uliokuwepo ndani yaushairi uliokuwa bado haujafahamika kwa maana ya uainishaji wake ambao leo hiiunafahamika kutokana na kazi kubwa waliyoifanya wataalamu wa fasihi yaKiswahili.Uainishaji wa riwaya za mwanzo ni zile zilizoandikwa mwanzoni mwa karne yakumi na tisa (19) kutokana na matumizi ya hati za Kilatini na Kiarabu kutumikakuandika na kusoma katika madarasa(Ndungo, 1991). Riwaya zilizoandikwa kipindihicho zilihusu masimulizi na fikra za ki-magharibi lakini kwa lugha za Kiswahili.Miongoni mwa waandishi wa mwanzo kuandika riwaya ya Kiswahili ni ShaabanRobert. Baadhi ya kazi zake za mwanzo ni riwaya ya Kusadikika, Adili na nduguze,Maisha Yangu Baada ya Miaka Hamsini, Siku ya Watenzi Wote na Siti binti Saad.Visa na matukio pamoja na uchangamano uliomo ndani ya riwaya, huelezwa kwakutumia lugha ya kisanii. Mlacha na Madumulla (1991) wanaeleza kuwa, lugha nikipengele muhimu sana kinachotegemewa na wahusika walivyoundwa, lengo ladhamira pamoja na maudhui yaliyoko katika kazi ya fasihi. Mlacha na Madumulla(1991) wanasema kwamba, umuhimu wa lugha ni katika kuchambua riwaya nakufanya uhakiki kimuundo sio katika utamu, urahisi au ugumu wake. Muundo walugha hujumuisha vipengele vingi vya lugha kama vile tamathali za semi, misemo,methali, taswira zilizojitokeza pamoja na dhamira kuu.Umuhimu wa kuangalia lugha kipekee ndimo yanamojitokeza mawazo ya juu na yaukito ya mwandishi. Kuangalia lugha katika muundo ukito ni kuangalia maana zandani za maneno au sentensi ambazo zinaweza kujitokeza pamoja na kuwa maana zakawaida zitakuwa zimepewa uzito wake katika kuiangalia lugha katika muundo wa

4jamii (Wamitila, 2008).Baada ya kufahamu maelezo ya wataalamu hawa wa lugha,tukaona ipo haja ya msingi ya kufanya utafiti wa kina wa kuchunguza matumizi yalugha kama yalivyotumika katika riwaya mbili ambazo ni Siri za Maisha na Vipulivya Figo.Kimsingi, uchunguzi wa kifasihi katika riwaya zilizoandikwa na Emmanuel Mbogohaujafanyiwa utafiti wa kina zaidi ya baadhi ya waandishi kuishia katika kuzitaja tubaadhi ya Riwaya za mwandishi huyu pale wanapoandika vitabu au utafiti kwa lengola kushadadia hoja na malengo yao. Njogu na Chimerah (1999), Wamitila (2008) naMadumulla (2009) ndio baadhi ya waandishi waliozitaja riwaya hizi katikauchambuzi wao walioufanya kwa malengo tofauti nay a utafiti huu. Tumejaribukutafuta sababu ya hali hi na kubaini kuwa Emmanuel Mbogo ni mwandishi maarufuzaidi katika tasinia ya tamthiliya kuliko riuwaya na hivyo watafiti na wahakikikadhaa wakavutiwa katika kuchunguza tamthiliya za Emmanuel Mbogo kulikoriwaya (Massoud, 2013). Sababu nyingine ni kuwa mwandishi huyu aliondokaTanzania na kwenda Kenya alikofundisha katika Vyuo Vikuu kadhaa na hivyokusahaulika Tanzania katika ulimwengu wa riwaya.Ni baada ya kurudi Tanzania katika miaka ya 2000 na kuandika riwaya yake yaWatoto wa Mama Ntiliye ndiposa alipotambulika kuwa ni mwandishi wa riwaya.Riwaya hii ni maarufu na inasomwa kama kitabu cha kiada katika shule za sekondarikidato cha tatu na nne na kama kitabu cha ziada katika kidato cha tano na sita navyuo vikuu. Kwa kipindi alichokaa Tanzania amefanikiwa kuandika riwaya nyingineza Vipuli vya Figo na Siriza Maisha lakini hakuna mtafiti hata mmoja mpaka kufikia

5sasa ambaye amechunguza matumizi ya lugha katika riwaya hizi mbili. Utafiti huuwetu umeona kwamba hili ni pengo la utafiti na umefanywa ili kuziba.1.2Tamko la Tatizo la UtafitiRiwaya ni kazi ya sanaa inayotumia lugha ya kinathari ambapo inaweza kuwamasimulizi ya mtu ya kweli au ya kubuni. Ni kazi ya mtu ama ya mwandishi yenyemwigo wa kiyakinifu ambao umefungamana na wakati, mazingira na mfumo wajamii (Msokile, 1992).Utafiti na uhakiki wa riwaya ya Kiswahili umefanywa nawatafiti kadhaa ambao ni Nkwera(1981) na Madumulla(2009), Senkoro(1982),Senkoro na Kahigi(2006), Mulokozi (1996) na Wamitilla (2002). Kati ya watafitiwote hao hakuna hata mmoja kwa mujibu wa ufahamu wangu aliyeteua kipengelecha lugha na kukitathimini ili kuona namna kilivyotumika katika kazi za kubuni zariwaya za mwandishi Emmanuel Mbogo kama sehemu ya madhumuni ya kazi zao.Utafiti huu umefanywa kwa lengo la kuzibapengo hilo kiutafiti kwa kuchunguzamatumizi ya lugha katika kazi za kubuniza Vipuli vya Figo na Siri za Maisha.1.3Lengo Kuu la UtafitiLengo kuu la utafiti huu ni kuchunguza matumizi ya lugha katika riwaya za Vipulivya Figo na Siri zaMaisha.1.3.1Malengo Mahususi ya UtafitiUtafiti huu uliongozwa na malengo mahususi yafuatayo:i.Kuchambua matumizi ya lugha ya kitamathali katika riwaya zaVipulivyaFigonaSiri za Maisha.

6ii.Kufafanua matumizi ya lugha yasiyo ya kitamathali katika riwaya zaVipulivya Figo na Siri za Maisha.iii.Kuwasilisha dhamira kutoka katika riwaya za Vipuli vya Figo na SirizaMaisha.1.3.2i.Maswali ya UtafitiNi vipengele gani vya matumizi ya lugha ya kitamathali vilivyotumika katikariwaya za Vipuli vya Figo na Siri za Maisha?ii.Ni vipengele gani vya lugha isiyo ya kitamathali vilivyofafanuliwa katikariwaya zaVipuli vya Figo na Siri za Maisha?iii. Ni dhamira zipi zilizowasilishwa katika riwaya za Vipuli vya Figo na Siri zaMaisha?1.4Umuhimu wa UtafitiKitaalimu: Matokeo ya utafiti huu yatakuwa marejeleo muhimu kwa wasomi wangazi zote za taaluma ya fasihi ambao ni walimu, wahadhiri na maprofesa katikataalimu ya fasihi. Kwa walimu wa wanafunzi wa sekondari, utafiti huu ni muhimukwani watautumia katika kuhakikia na kuchambulia vipengele vya lugha katika kaziza fasihi.Kinadharia: utafiti huu utaonesha kwamba upo uhusiano wa moja kwa moja bainaya matumizi ya lugha uwasilishaji wa dhamira mbalimbali katika kazi za riwaya. Hililitabainika pale ambapo katika utafiti huu tumebainisha namna lugha ya kitamathalina isiyo ya kitamathali zilivyotumiwa na mwandishi katika kuwasilisha dhamirambalimbali. Utafiti huu umetumia nadharia ya Simiotiki katika kuchambua data zake

7na hivyo watafiti wengine wa baadaye wataona namna nadharia hii inavyotumikakatika kuchambua data na wao wakaitumia kwa namna kama hii au nyingine katikauchambuzi wa data za utafiti wao.Kijamii: utafiti huu utakuwa na umhimu mkubwa katika jamii kutokana na kuelezakwake masuala muhimu katika maendeleo ya jamii. Kwa mfano, katika utafiti huutumeeleza umuhimu wa elimu katika jamii, malezi katika jamii, athari za biasharaharamu na masuala ya siasa na uchumi. Mambo haya ni muhimu katika maendeleoya jamii na kwa hiyo wanajamii watakaopata fursa ya kuisoma kazi hii watafaidikana maarifa haya na watakapoyatumia watajipatia maendeleo.1.5Mipaka ya UtafitiUtafiti huu umeshughulikia vipengele vya lugha, jinsi vilivyotumika katika riwaya zaVipuli vya Figo na Siri za Maisha tu kati ya riwaya nyingi zilizoandikwa naEmmanuel Mbogo. Matumizi ya lugha yaliyochunguzwa katika utafiti huu ni yale yakitamathali na yasiyo ya kitamathali tu. Tunafahamu kuwa matumizi ya lugha nitaaluma pana ndio maana tukateua aina hizi mbili za matumizi ya lugha ilikufanikisha malengo mahususi ya utafiti wetu. Uchambuzi uliofanywa katika utafitihuu ni wakifasihi ambapo umeongozwa na nadharia teule ya uhakiki wa kifasihiambayo ni nadharia ya Simiotiki.1.6Mpangilio wa TasinifuTasinifu hii ina jumla ya sura tano ambapo katika sura ya kwanza kumeelezewavipengele vya kiutangulizi katika utafiti. Vipengele hivyo ni pamoja na utangulizi wajumla, usuli wa tatizo la utafiti, tamko la tatizo la utafiti, lengo kuu la utafiti,

8malengo mahususi ya utafiti na maswali ya utafiti. Vipengele vingine ni umuhimuwa utafiti, mipaka ya utafiti, mpangilio wa tasinifu na hitimisho. Sura ya pili nimapitio ya kazi tangulizi na mkabala wa kinadharia. Vipengele vilivyowasilishwakatika sura hii ya pili ni pamoja na utangulizi, maana ya riwaya na historian achimbuko la riwaya. Vipengele vingine ni kazi tangulizi katika fani ya riwaya yaKiswahili, kazi tangulizi katika dhamira za riwaya ya Kiswahili na kazi tangulizikatika riwaya za Emmanuel Mbogo.Sura iliyofuatia ni ya tatu ambayo imewasilisha mbinu za utafiti ikiwemo utangulizi,umbo la utafiti, eneo la utafiti, kundi lengwa la utafiti na sampuli na mbinu za uteuziwa sampuli; mbinu ya uteuzi wa madhumuni maalumu. Vipengele vingine ni data zautafiti; data za msingi na data za upili na mbinu za kukusanyia data; usomaji makinina upitiaji wa nyaraka. Vipengele vingine ni uchambuzi wa data, maadili ya utafiti nahitimisho. Sura ya nne imewasilisha vipengele vya utangulizi, matumizi ya lugha yakitamathali yaliyohusisha tashibiha, tashihisi, tafsida, sitiari, kejeli na dhihaka.Matumizi ya lugha yasiyo ya kitamathali yaliyohusisha misemo, nahau, takriri,tanakali sauti na taharuki. Pia katika sura hii ya nne kumewasilishwa dhamira zabiashara haramu, umuhimu wa elimu katika jamii, malezi katika jamii, siasa nauchumi, nafasi ya mwanamke na hali ngumu ya maisha katika jamii. Sura ya tanondiyo ya mwisho ambayo imetoa muhutasari, hitimisho na mapendekezo.1.7HitimishoKatika sura hii tumefafanua vipengele vilivyoonesha haja ya kufanyika kwa utafitihuu. Aidha, tumeonyesha na kubainisha pengo la utafiti na kisha kujenga hoja yakufanyika kwa utafiti huu. Kwa fahamu zangu, hakuna utafiti wa kina ambao

9umefanyika katika ngazi ya uzamili wa kutathimini lugha kama alivyo itumiaEmmanuel Mbogo katika kazi zake mbili za kubuni zaVipuli vya Figo naSiri zaMaisha. Kwa sababu hiyo, tukaona kwamba kuna haja ya msingi ya kufanya utafitihuu katika ngazi ya uzamili ili kuziba pengo hili la kiutafiti kwa kuchunguzamatumizi ya lugha katika kazi za kubuni zaVipuli vya Figona Siri za Maisha.

10SURA YA PILIMAPITIO YA KAZI TANGULIZI NA MKABALA WA KINADHARIA2.0UtanguliziSura hii imejadili utalii wa maandiko yanayohusu mada iliyofanyiwa utafiti. Katikasehemu hii, tumesoma na kuchambua kazi za watafiti waliotangulia; tukitarajiakupata maarifa na ujuzi utakao tuwezesha kuendelea na utafiti wetu. Katika kusomakazi hizo, wataalamu mbalimbali wanatoa maelezo gani kuhusu riwaya ya Kiswahilikwa ujumla. Aidha, utafiti huu umetupatia maarifa ya kubaini pengo la utafiti pamojana nadharia zilizotumika katika kuongoza kuchambua data za utafiti. Hivyo basi,sura hii imegawanyika katika sehemu kuu tatu ambazo ni maana ya riwaya, historiana chimbuko la riwaya ya Kiswahili. Aidha, katika sura hii tumewasilisha nadhariakadhaa zilizotumika katika kuongoza uchambuzi wa data za utafiti.2.1Maana ya RiwayaMaana ya riwaya imefafanuliwa na wataalamu mbalimbali wa lugha na kila mmojaakitoa maelezo yanayotofautiana na mwingine katika vipengele vinavyounda riwayakwa ujumla. Baadhi ya wataalamu walioelezea dhana ya riwaya akiwemo Senkoro(1982) amefafanua riwaya kwa kusema kwamba, riwaya ni kisa mchanganyikoambacho huweza kuchambuliwa na kupimwa kwa mapana na marefu kifani na kimaudhui. Ni hadithi ndefu ya kubuni yenye visa vingi, wahusika zaidi ya mmoja nayenye mazungumzo na maelezo yanayozingatia kwa undani na upana. Riwaya inatoapicha yote ya ujumla ya maisha ya mtu toka nyumbani hadi katika kiwango cha taifana hata dunia nzima.

11Mlacha na Madumulla, (1991) wametoa maelezo ya dhana ya riwaya na kusema:riwaya ni hadithi iliyotungwa ambayo ina urefu wa kutosha, visa vinavyoana naambayo imezingatia swala la muda. Ukubwa wa riwaya unaweza kuwa kurasa zozotekwani si idadi ya maneno au kurasa tu ambavyo vinatufanya tuiite hadithi fulanikuwa ni riwaya na nyingine kuwa ni hadithi fupi. Wataalamu hawa wa Lughawametoa maelezo ya kina zaidi pale walipolinganisha riwaya zenye manenomachache kama riwaya ya Nyota ya Huzuni(1981) yenye maneno 54,000 na ile yaBwana Muyombekele na Bibi Bugonoka (1980) yenye maneno 195,000 na kusemakuwa bado zote hizo ni riwaya. Kwa uhakika, maneno haya yanatia changamoto kwawasanii wanaoibukia na uandishi wa riwaya na hadithi fupi, kwamba riwaya siyolazima iwe na maneno mengi kama ilivyo riwaya ya Bwana Muyombekele na BibiBugonoka (Msokile, 1992).Pamoja na maelezo ya wataalamu hao, Nkwera (1981) amezingatia vigezovinavyoijenga riwaya na kusema, riwaya ni hadithi iliyo ndefu kutosha kufanyakitabu kimoja au zaidi. Habari iliyomo ni ya kubuniwa tu, na imejengwa juu ya tukiola kihistoria. Yaweza kuandikwa kwa maelezo ya ujazo (au nathari) au kwa mtindowa ushairi. Riwaya ni hadithi iendayo mfululizo na kwa kinaganaga. Hueleza maishaya mtu au kikundi cha watu katika jumla yao au vipengele fulani fulani vya maishayao. Kila riwaya ina mhusika wake mkuu mmoja au hata wawili. Maelezo haya kwaupande mwingine yametiliwa mkazo na Mlacha (1989) pale alipoonyesha umahiriwa mtunzi wa riwaya kwa jinsi anavyoonyesha usanii katika kazi yake kiasi chakuifanya jamii iamini kile wasichoamini na kukubaliana na mawazo ya mwandishi.

12Kwa upande wake Mlacha (1989) anaeleza kuwa riwaya ni hadithi ambayo imekitwakwenye dhamira moja kuu. Dhamira hiyo inaweza kuwa imejengwa na dhamirakadhaa pamoja na visa tofauti. Dhamira hizo ndogo kama vile visa, huwavinahusiana katika kujenga riwaya nzima. Vilevile, riwaya sio maelezo halisi yamaisha ya binadamu bali ni maelezo ya mtunzi kuhusu anavyoyaona maisha ambayoangetaka yawe hata ambavyo angependa yasiwe. Kwa h

tamko la tatizo la utafiti, lengo kuu na madhumuni mahususi ya utafiti. Aidha maswali ya utafiti, umuhimu wa utafiti, mipaka ya utafiti na mpangilio wa tasnifu pia vimewasilishwa katika sura hii. 1.1 Usuli wa Tatizo la Utafiti Binadamu katika kuishi

Related Documents:

Data zilirekodiwa katika kinasa sauti na kunukuliwa kwa maandishi. . Tofauti za Matumizi ya Lugha katika Miktadha Mbalimbali ya Mazungumzo 13 sehemu ya pili inahusu tofauti ya matumizi ya lugha katika miktadha mbalimbali. Sehemu ya tatu inafafanua mkabala wa kinadharia uliotumika katika uch

Nyenzo za kufundisha huwa viungo muhimu wakati wa utoaji wa mafunzo. Utafiti ulichunguza matumizi ya nyenzo katika ufundishaji wa Kiswahili katika shule za msingi za umma katika Jimbo la Nyandarua, Kenya. Madhumuni ya utafiti yalikuwa: Kuainisha nyenzo zinazotumika kufundisha Kiswahili, Kutathimini kiwango cha matumizi ya

inafuata mchango wa baadhi ya wanaisimu wa lugha ya Kiingereza, Kiarabu na Kiswahili walivyobainisha uwepo wa kategoria ya nomino (majina) katika lugha hizi. 1.1.2 Majina Katika Lugha ya Kiingereza Wataalamu mbalimbali wa lugha ya kiingereza wamebainisha kuwepo kw

Wapemba. Surahii pia inatoa taarifa za awali kuhusu mada ya utafiti ambapo mtafiti ataelezea kuhusu usuli wa mada,tatizo la utafiti,malengo ya utafiti yakiambatana na mswali ya utafiti ,umuhuimu wa utafiti mipaka ya utafiti hatimae hitimisho , haya yote yameelezewa juu ya kuchunguza matumizi ya tafsida katika lahaja

mawazo ya wanamsambao hususani katika ugawaji wa ngano bila kuchunguza kwa umakini sifa ya kila kundi. Propp anaamini kuwa ili kuchunguza asili ya ngano ni vema kuanza kuchunguza aina za ngano kwa kuangalia maumbo ya ngano. Hivyo mtazamo huu unaangalia asili ya ngano kwa kuchunguza maumbo ya ngano husika. Ubora wa nadhairia hii, nadharia hii inasaidia kujua aina za ngano kutokana na dhima zake .

Mawasiliano kwa Wageni wa Lugha”. Nahau hizo zinatumika katika lugha ya maandishi ya Kiswahili na katika mazungumzo ya kila siku. Mtafiti wa utafiti huu aliongozwa na malengo mahsusi matatu ambayo ni kubainisha nahau mbali mbali za lugha ya Kiswahili k

katika tamthiliya za Kinjeketile na Nyerere na Safari ya Kanaani: Utafiti linganishi. Ili kufanikisha utafiti huu, mtafiti ametumia mbinu za maktabani katika kukusanya na kuwasiilisha data kimaelezo. Pia marejeleo mbalimbali kutoka tamthiliya za Kiswahili yalipitiwa. Nadharia ya fasihi ya jamii ndiyo iliyotumika katika

P, produced by A02. Next, A01 asks A03 for every such component to get offers from companies that are able to supply the component. So, a number of exploring transactions T03 may be carried out within one T01, namely as many as there are components of P which are not produced by the tier n company. In order to execute