ATHARI ZA LUGHA YA KINYAMWEZI KATIKA KUJIFUNZA

2y ago
409 Views
2 Downloads
357.28 KB
100 Pages
Last View : 6d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Randy Pettway
Transcription

ATHARI ZA LUGHA YA KINYAMWEZI KATIKA KUJIFUNZA LUGHAYA KISWAHILI ENEO LA UTAFITI : URAMBONYANDA JOSEPHINETASNIFU ILIYOWASILISHWA, IKIWA NI SEHEMU YA MASHARTI YAKUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (M.A. KISWAHILI) YA CHUOKIKUU HURIA CHA TANZANIA2015

iiUTHIBITISHOAliyeweka saini hapa chini anathibitisha kwamba ameisoma tasnifu hii inayoitwaAthari za Lugha ya Kinyamwezi Katika Kujifunza Lugha ya Kiswahili nakupendekeza ikubaliwe na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa ajili ya Kukamilishamasharti ya shahada ya MA. Kiswahili ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.Dkt. Hanna Simpassa(Msimamizi)Tarehe

iiiHAKI MILIKIHaki zote zimehifadhiwa.Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kutafsiri kwa mfumo wowoteule au kutoa hata sehemu ndogo ya tasnifu hii kwa njia yoyote ile bila idhini yamaandishi kutoka kwa mwandishi wa tasnifu hii na / au Chuo Kikuu Huria chaTanzania.

ivTAMKOMimi Josephine Nyanda ninatamka na kuthibitisha kwamba Tasnifu hii iitwayoAthari za Lugha ya Kinyamwezi Katika Kujifunza Lugha Kiswahili ni kazi yangumwenyewe na haijawahi kutolewa popote pale kwa lengo la kutunukiwa shahadayoyote katika Chuo Kikuu chochote.SahihiTarehe

vTABARUKUNinaitabaruku tasnifu hii kwa wanangu wapendwaTumaininaMercyWana kila sababu ya kuhakikisha kuwa wanasoma kwa bidii na kufaulu vizuri sana!

viSHUKURANINinapenda kumshukuru Mungu wangu kwa wema na ukuu wake kwangu.Ama kwahakika yeye amejaa rehema , neema na uweza tele kwani amenijaalia uhai naufahamu ulioniwezesha kukamilisha kazi hii.Shukurani za pekee ninampa msimamizi wangu mpendwa Dkt. Hanna Simpassa,kwa kuutumia muda wake, kwa hali na mali katika kunitia moyo nilipoonekanakukata tamaa. Licha ya mapungufu niliyokuwa nayo aliweza kunivumilia, akaipitiakazi yangu, akaisahihisha na kunielekeza vilivyo ili kuhakikisha kuwa inakuwainavyotakiwa kuwa. Mungu ambariki sana huyu mama! . Ninakishukuru Chuo KikuuHuria cha Tanzania hasa Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii wakiwemo walimuwangu Dkt. Zelda Elisifa, Nestory Pembe Ligembe, Lipembe, Prof.EmmanuelMbogo, James Mdee na Tigiti Sengo kwa taaluma, maarifa na ushauri walionipa nakwa ushirikiano mzuri ulioniwezesha kukamilisha kazi hii.Nasema asantesana,Mungu awajaalie mema.Ninapenda kumshukuru sana mume wangu mpendwa Jonathan Joseph kwakuniruhusu kujiunga na masomo na kunivumilia nilipokuwa mbali na familiayetu.Alijitwika mzigo wa kuikimu familia yetu katika kipindi chote cha masomoyangu.Mungu ambariki sana na kumshindia katika yote.Aidha, ninawashukuru sanawatoto wetu wapendwa Tumaini Jonathan na Mercy Jonathan kwa kunivumiliakwani kipindi ambacho sikuwepo walikuwa wakikosa upendo wa mama.Naye wifiyangu Naomi Daniel tunayeishi naye.Mungu awabariki na kuwashindia katikamasomo yao! Hakika wana kila sababu ya kufaulu.

viiNinamshukuru mama yangu mpenzi Sussane Melkizedeck kwa kunishauri,kuniombea mafanikio na kunitia moyo mno katika safari ya masomo yanguhaya.Baba yangu Ezekiel Nyanda pia hakuwa nyuma katika hili bila kuwasahauwapendwa dada yangu Consolata Nyanda na kaka zangu Andes Nyanda, JuliusNyanda na Edgar Nyanda, watoto wetu Ezekiel William na Suzan Nicholaus, wifizangu Neema Mnuo na Sara Seni kwa ushauri wao na misaada ya hali na maliwaliyonipa ili kuhakikisha kuwa ninafaulu.Wabarikiwe mno!Siwasahau wanafunzi wenzangu tulioabiri nao chombo hiki kwa kunitia moyo nakunipa misaada yao ya hapa na pale.Nao ni Wenceslaus Mashaka, NicholausLunyana, Reuben Luhende, Daud Mtega, January Magesa,Salome Mhangilwa,Deusdedit Omchamba na Angela Ghati. Nawashukuru na kuwatakia kila la heri,ushindi na mafanikio tele! Wafanyakazi wenzangu Alex Majenga na JosephineMsonsa, Wabarikiwe pia kwa misaada yao kwangu.Ninajua kuna wengi waliochangia ambao sijawataja kwa ukosefu wa nafasi. Kwaowote ninasema asanteni sana na Mungu awabariki!.

viiiIKISIRIUtafiti huu ulikuwa na lengo la kuchunguza Athari za Kinyamwezi Katika KujifunzaLugha ya Kiswahili.Umetumia nadharia ya Fonolojia Zalishi Asilia ili kuwekabayana athari hizo. Sura ya Kwanza imeshughulikia Utangulizi, Tatizo la Utafiti,Malengo ya Utafiti, Umuhimu wa Utafiti, Mawanda na Mipaka ya Utafiti na Mpangowa Utafiti.Sura ya Pili imeshughulikia Mapitio ya Kitaaluma na ya Kazi Tanguliziambapo imeelezea yaliyoandikwa kuhusu lugha na athari za lugha za kibantu katikaUjifunzaji wa Lugha ya Kiswahili.Aidha, imeelezea yaliyoandikwa kuhusu Ala zaSauti, Sauti za Lugha, Namna ya Utamkaji na Mahali pa Kutamkia Sauti zaKiswahili. Imeelezea Pengo la Maarifa na Kiunzi cha Nadharia.Sura ya Tatuimezungumzia Njia na Mbinu za Utafiti.Imezungumzia Utangulizi, Eneo la Utafiti,Sampuli ya Utafiti na Usampulishaji,Vyanzo vya Data,Ukusanyaji wa Data, Mkabalawa Uchambuzi wa Data,Uchambuzi wa Data na Vikwazo vya Utafiti.Sura ya Nneimeeleza juu ya Uwasilishaji na Uchambuzi wa data,ambapo imeelezea aina zafonimu za Kinyamwezi na Athari ya Lugha ya Kinyamwezi katika Kujifunza Lughaya Kiswahili. Sura ya tano imeeleza juu ya Muhtasari wa Utafiti na Mapendekezo.

ixYALIYOMOUTHIBITISHO. iiHAKI MILIKI . iiiTAMKO . . ivTABARUKU . vSHUKURANI . viIKISIRI . . viiiYALIYOMO . ixVIELELEZO . xiiiSURA YA KWANZA. 1UTANGULIZI . 11.1Utangulizi. . 11.1.1Mada ya Utafiti. 11.1.1.1Usuli wa mada. . 11.1.1.1.1Lugha ya Kinyamwezi. . 11.1.1.1.2Lugha ya Kiswahili. . 11.1.1.1.2Mwingiliano baina ya lugha mbili tofauti. . 21.2Tatizo la utafiti. . 31.3Malengo ya utafiti. . 31.3.1Lengo kuu. . 31.3.2Malengo mahsusi. 41.3.3Maswali ya utafiti. . 41.4.Umuhimu wa utafiti. . 41.5Mawanda na mipaka ya utafiti. . 61.6Mpango wa utafiti. . 6SURA YA PILI. . 7

xMAPITIO YA KITAALUMA NA MAPITIO YA KAZI TANGULIZI. . 72.1Utangulizi . 72.2Mapitio ya Kitaaluma na Mapitio ya kazi tangulizi. . 72.2.1Yaliyoandikwa kuhusu lugha,Lugha ya asili,Lugha mama na Lugha yaPili. . 72.2.2Yaliyoandikwa kuhusu Uamiliaji lugha, Ujifunzaji lugha na Matumizi yalugha ya Pili. 92.2.3Yaliyoandikwa kuhusu athari za lugha za kibantu katika lugha yaKiswahili. . 162.2.4Yaliyoandikwa kuhusu Ala za sauti, Sauti za Lugha, Namna ya utamkajina Mahali pa kutamkia sauti za Kiswahili. . 182.2.4.1Ala za sauti. . 182.2.4.2Fasili ya fonimu, Aina za fonimu za Kiswahili, Mahali pa kuzitamkia naNamna ya kuzitamka. . 192.2.4.2.1Fasili ya fonimu. . 192.2.4.2.2Aina za fonimu za Kiswahili. . 202.2.4.2.2.1 Fonimu za irabu/Vokali za Kiswahili sanifu. . 202.2.4.2.2.2 Fonimu za nusu irabu za Kiswahili sanifu /viyeyusho. 232.2.5Pengo la maarifa. . 252.2.6Kiunzi cha Nadharia. . 262.3Hitimisho. . 28SURA YA TATU . 29NJIA NA MBINU ZA UTAFITI . 293.1Utangulizi . 293.2Eneo la Utafiti. . 293.3Uteuzi wa Walengwa. . 30

xi3.3.1Sampuli na Usampulishaji. 303.4Vyanzo vya Data. . 323.4.1Data za msingi. . 323.4.2Data za Upili . 323.5Ukusanyaji wa Data. . 333.5.1Vifaa vya kukusanyia Data. . 333.5.2Mbinu za ukusanyaji wa Data. . 343.5.2.1Mahojiano. 343.5.2.2Mbinu ya Hojaji. . 353.5.2.3Mbinu ya majadiliano. 363.5.2.4Maktabani (Mbinu ya kimaktaba). . 373.6.Mkabala wa uchambuzi wa Data. . 373.7Uchambuzi wa Data. . 383.8Vikwazo vya Utafiti. . 383.9Hitimisho. . 39SURA YA NNE . 40UWASILISHAJI NA UCHAMBUZI WA DATA . 404.1Utangulizi . 404.2Aina za fonimu za Kinyamwezi. . 404.3Athari ya Lugha ya Kinyamwezi Katika Kujifunza Lugha yaKiswahili. . 44SURA YA TANO . 675.1Utangulizi. . 675.2Muhtasari wa Utafiti. 675.3Mchango wa Utafiti . 685.4Mapendekezo: . 69

xiiMAREJELEO . 71VIAMBATANISHO. 74

xiiiVIELELEZOKielelezo na.2.1: Jedwali la Irabu za Kiswahili Sanifu na Sifa Zake Bainifu .22Kielelezo na.2.4: Jedwali la Konsonanti na Nusu irabu za Kiswahili Sanifu .24Kielelezo na.3.1: Jedwali la Mchanganuo wa Watafitiwa . 31Kielelezo na.4.1: Fonimu za irabu fupi za Kinyamwezi . .41Kielelezo na 4.2: Fonimu za irabu ndefu za Kinyamwezi .41Kielelezo Na.4.3: Matriki ya irabu za Kinyamwezi 42Kielelezo na.4.4:: Jedwali la Konsonanti na Nusu Irabu za Kinyamwezi .43Kielelezo na. 4.5: Jedwali la Watafitiwa Linaloonyesha Idadi na Majibu Yao 44Kielelezo Na.4.6: Jedwali la Watafitiwa Linaloonyesha idadi na Majibu Yao .45Kielelezo na.4.7: Jedwali la Watafitiwa Linaloonyesha Idadi na Majibu Yao .45Kielelezo na.4.8: Jedwali la Watafitiwa Linaloonyesha Idadi na Majibu Yao .46Kielelezo na.4.9: Jedwali la Watafitiwa Linaloonyesha Idadi na Majibu Yao .40Kielelezo na.4.10: Jedwali la watafitiwa linaloonyesha idadi na majibu yao .48Kielelezo na.4.11: Jedwali la watafitiwa linaloonyesha idadi na majibu yao .49Kielelezo na.4.12: Jedwali linaloonyesha mifano ya Athari katika matumizi ya/Ɵ/ .Kielelezo na.4.13: Jedwali linaloonyesha mifano ya Athari katika matumizi ya /ð/ .50

xiv51Kielelezo na.4.14: Jedwali linaloonyesha mifano ya Athari katika matumizi ya /b/ .Kielelezo na.4.15: Jedwali linaloonyesha mifano ya Uchopekaji wa silabi katikaNeon Kielelezo na.4.1653: Jedwali linaloonyesha mifano ya Uchopekaji wa silabi katikaNeon .Kielelezo na.4.175253: Jedwali linaloonyesha mifano ya Uchopekaji wa sautikatika Neon .54Kielelezo na.4.18: Jedwali linaloonyesha mifano ya Athari za kimaana 55Kielelezo na.4.19: Jedwali linaloonyesha mifano ya Athari za kimaana 57Kielelezo na.4.20: Jedwali linaloonyesha mifano ya Athari za kimaana 58Kielelezo na.4.21: Jedwali la Watafitiwa Linaloonyesha Idadi na Majibu yao .63Kielelezo na.4.22: Jedwali la Watafitiwa Linaloonyesha Idadi na Majibu yao.63Kielelezo na.4.23: Jedwali la Watafitiwa Iinaloonyesha Idadi na Majibu yao. .64

xvISHARA NA VIFUPISHO VILIVYOTUMIKA[ ] Mabano ya fonimu.// Mabano ya fonetiki.TATAKI Taasisi ya Taalimu za Kiswahili.

1SURA YA KWANZAUTANGULIZI1.1 Utangulizi.1.1.1 Mada ya Utafiti.Athari za Kinyamwezi Katika Kujifunza Lugha ya Kiswahili.1.1.1.1 Usuli wa mada.1.1.1.1.1 Lugha ya Kinyamwezi.Maendeleo ya lugha ya Kiswahili huchangiwa pia na lugha za kibantu, Kinyamwezikikiwa miongoni mwazo.Kinyamwezi ni lugha ya kibantu nchini Tanzaniainayozungumzwa na wanyamwezi. Mwaka wa 2006 idadi ya wasemaji waKinyamwezi imehesabiwa kuwa watu 980,000.Kutokana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcom Guthrie Kinyamwezi kikokatika kundi la F20 na kinafanana na Kisukuma. Wanyamwezi ni kabila la Tanzaniawanaoishi katika mikoa ya Tabora na Shinyanga.Lugha yao ni Kinyamwezi. Kukuakwa mji wa Tabora ambako ndiko kabila la Kinyamwezi liliko na kutokana na kuwakituo kikubwa na kitovu cha biashara ya misafara ya watumwa, kulichangia sanaWanyamwezi kutumia lugha ya Kiswahili katika mawasiliano.1.1.1.1.2 Lugha ya Kiswahili.Lugha ya Kiswahili ni lugha ya Kibantu ambayo chimbuko lake ni upwa wa AfrikaMashariki. Lugha hii iliainishwa na Guthrie (1948) kama lugha ya Kibantu ya kundila G. (Polome, 1967; Mbaabu, 1991; Chimerah, 1998).

2Kiswahili ni lugha ambayo awali ilianza kutumiwa na watu wachache walioishikatika mwambao wa Afrika Mashariki. Kwa wakati huo idadi ya watu hao ilikuwandogo. Leo hii lugha ya Kiswahili imekua na matumizi yake yameenea kwa harakakatika bara la Afrika, Ulaya, Marekani, Asia na Australia.Ghanen (2005), anaeleza kuwa lugha ya Kiswahili ni miongoni mwa lugha hayakidiplomasia.Matumizi ya lugha ya Kiswahili katika maswala kidiplomasiayatakifanya Kiswahili kuenea kwa kasi kubwa zaidi na kupata wazungumzaji wengikuliko ilivyo leo. Nafasi ya lugha ya Kiswahili ni kule kupata fursa yakuzungumzwa. Lugha hii huzungumzwa si tu Afrika Mashariki, Kati na Kusini balihata ulimwenguni kiasi cha kufundishwa katika vyuo vikuu mbalimbali. Ni dhahirikuwa Kiswahili kina nafasi ya kuwa miongoni mwa lugha zinazotambuliwa Afrikana duniani kwa ujumla. Hutumika pia katika umoja wa mataifa.1.1.1.1.2 Mwingiliano baina ya lugha mbili tofauti.Mwingiliano baina ya lugha mbili tofauti husababisha kuathiriana kwa lugha hizokutokana na kwamba kila lugha huchukua baadhi ya msamiati toka lugha nyingine nakuuingiza katika lugha yake.Lugha huathiriana na lugha nyingine endapo kutakuwa namwingiliano baina ya wanajamii wa lugha hizo.Waongeaji wa lugha hizowazungumzapo huwakuna baadhi ya tofauti zinazojitokeza katika viwango vyakiisimu kuanzia fonolojia, mofolojia, sintaksia na semantiki. Mwingiliano huuulisababisha msamiati wa Kinyamwezi kuingia katika lugha ya Kiswahili. .

3Masebo na Nyangwine (2008), wanaeleza kuwa lugha ya Kiswahili imeingiliana sanana lugha nyingine za Kibantu. Kwa kuwa lugha ya Kiswahili ni ya pili katika jamiinyingi za kibantu, athari ya lugha ya kwanza inaonekana sana katika matamshi.Vilevilelugha za kibantu zimeathiri lugha ya Kiswahili katika maana, msamiati na sarufi.1.2 Tatizo la utafiti.Taasisi ya Elimu Tanzania (1996) inaeleza kuwa, Sarufi ni mfumo wa taratibu nakanuni zinazotawala matumizi sahihi ya matamshi ya maneno, maumbo ya maneno,miundo ya tungo na maana ya miundo.Lugha ndicho chombo kikuu cha mawasiliano baina ya watu.Ili watu wawezekuitumia lugha kwa kuelewana, lazima kuwe na taratibu au sheria zinazotawalautumiaji wa lugha.Mzungumzaji akikiuka kanuni za lugha anazungumza lughapotofu. Taratibu za lugha hutawala matamshi ya maneno na vipengele vingine vyakisarufi.Watu hukosea kanuni za Kiswahili kutokana na athari za lugha za awali aulugha nyingine.Utafiti huu umelenga Kuchunguza Athari za Lugha ya KinyamweziKatika Kujifunza Kiswahili.1.3 Malengo ya utafiti.Utafiti huu ulikuwa na malengo ya aina mbili, nayo ni lengo kuu na malengomahsusi.1.3.1 Lengo kuu.Kuchunguza athari za lugha ya Kinyamwezi katika kujifunza lugha ya Kiswahili.

41.3.2 Malengo mahsusi.i).Kufafanua athari za lugha ya Kinyamwezi Kimsamiati, Kimatamshi naKimaana katika kujifunza Kiswahili.ii).Kubaini sababu zinazofanya lugha ya Kinyamwezi kuathiri ujifunzaji walugha ya Kiswahili Kimsamiati, Kimatamshi na afunziwanyamweziwanaojifunza lugha ya Kiswahili kama lugha yao ya pili.1.3.3 Maswali ya utafiti.i)Ni athari zipi za Kimsamiati, Kimatamshi na Kimaana za Lugha yaKinyamwezi zinajitokeza katika kujifunza lugha ya Kiswahili?.ii)Zipi ni sababu za athari za lugha ya Kinyamwezi Kimsamiati, Kimatamshina Kimaana katika kujifunza lugha ya Kiswahili?.iii) Mbinu gani zitumike ili kuwasaidia wanafunzi wanyamwezi wanaojifunzalugha ya Kiswahili kama lugha yao ya pili?.1.4.Umuhimu wa utafiti.Kufanyika kwa utafiti huu kumetoa mchango mkubwa wa kitaalamu,kinadhariana kiutamaduni.Kwa upande wa taaluma, utafiti huu utapunguza pengo la kiutafiti juu ya athari zalughaya Kinyamwezi katika lugha ya Kiswahili ambalo kwa ufahamu wa mtafiti,hakuna utafiti uliofanyika kwa kina juu ya mada hii. Hivyo utawasaidia wadau waelimu kama vile wanafunzi, walimu, Maafisa Elimu kuwa na uelewa juu ya madahiyo ya utafiti na hivyo kuweza kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokezawakati wa kufundisha lugha ya Kiswahili.

5Matokeo ya uchunguzi huu ni ya manufaa kwa walimu watakaoyarejelea ili kutabiriuwezekano wa kutokea kwa makosa wakati wa ufundishaji wa lugha ya Kiswahilimiongoni mwa wanafunzi wanaozungumza Kinyamwezi. Hivyo basi watawezakuyatafutia ufumbuzi matatizo hayo kwa njia mwafaka.Kupitia utafiti huu jamii itakuwa na ufahamu juu ya athari za Kinyamwezi katikakujifunza lugha ya Kiswahili na hivyo kushirikiana kwa ukaribu na wadau wa elimukuhamasisha uzungumzaji wa Kiswahili Sanifu. Wizara ya Elimu na Mafunzo yaUfundi ikiwa na ufahamu juu ya mada hiyo, itashirikiana na wakuza mitaala katikakuandaa mtaala wa elimu ambao utaridhia uzungumzaji wa lugha sanifu ya Kiswahilina uendelezaji wa lugha hiyo.Utafiti huu utamsaidia mtafiti kama mwalimu, wanazuoni na wataalamu wa isimukuelewa kwa undani zaidi juu ya athari za lugha ya Kinyamwezi katika kujifunzalugha ya Kiswahili na hivyo kuielimisha jamii izitambue athari chanya na kishakuchangia kukiendeleza Kiswahili , vilevile changamoto zitokanazo na athari hasi ilikuwawezesha kukabiliana nazo.Utafiti huu utakuwa na utaendelea kuwa kichocheo cha tafiti nyingine kuhusukuathiriana kwa lugha ya Kinyamwezi na Kiswahili katika jamii za Tanzania, Afrikana dunia nzima kwa ujumla.Utawasaidia watifiti wengine watakaoamua kufanyautafiti juu ya athari za lugha mama mbalimbali katika kujifunza Kiswahili na hivyokuweka wazi njia nyingine mbalimbali za kuwasaidia wazawa wa lugha hiyo katikakujifunza lugha ya Kiswahili.Vilevile utakuwa rejea mojawapo kwa tafiti nyinginekuhusu isimu ya lugha.

6Data zilizopatikana katika utafiti huu zitasaidia kutatua baadhi ya matatizoyaliyojitokeza na yatakayojitokeza katika tafiti nyingine zihusianazo na utafiti huu.1.5Mawanda na mipaka ya utafiti.Lugha ya Kiswahili na Kinyamwezi ndizo zilizohusika katika utafiti huu ilikuchambua athari mbalimbali za Kinyamwezi katika kujifunza lugha ya Kiswahili.Hiiina maana kwamba, mtafiti anafahamu kwamba lugha ya Kiswahili imeathiriwa nalugha kadhaa, lakini yeye alishughulikia athari ya Lugha ya Kinyamwezi peke yakekatika kujifunza lugha ya Kiswahili kwani kama alivyokwishasema hapo juu , kwaufahamu wake mada hii haikuwa imefanyiwa utafiti kwa kina.1.6 Mpango wa utafiti.Tasnifu hii ina jumla ya sura kuu tano zenye mada kuu na mada ndogondogo ndaniyake.Sura ya kwanza inaelezea vipengele mbalimbali vya kiutangulizi.Sura ya piliinaelezea Mapitio ya kitaaluma na Mapitio ya kazi tangulizi huku Sura ya tatuikiwasilisha Mbinu za utafiti.Sura ya nne imeelezea Uchambuzi wa data za utafiti naSura ya tano ikitoa Muhtasari wa utafiti,Mchango wa utafiti,Mapendezo ya jumla,Mapendekezo ya tafiti zijazo na Hitimisho.1.7 . Hitimisho.Katika sura hii mambo yaliyozungumziwa ni Mada ya utafiti,Lugha yaKinyamwezi,Lugha ya Kiswahili,Mwingiliano wa lugha mbili tofauti,Tatizo lautafiti,Malengo ya utafiti,Umuhimu wa utafiti,Mawanda na mipaka ya

7SURA YA PILI.MAPITIO YA KITAALUMA NA MAPITIO YA KAZI TANGULIZI.2.1 UtanguliziSura hii inajadili Mapitio ya kitaaluma na Mapitio ya kazi tangulizi. Marejeleo yavitabu na Machapisho yanayohusiana na mada ya utafiti huu yamehusika. Sura hiiinaonyesha mtazamo wa watalaam mbalimbali ulimwenguni kuhusiana na mada hii yaya utafiti. Sehemu ya kwanza ya sura hii ni Utangulizi, inafuatiwa na sehemu ya pili,ambayo ni Mapitio ya kitaaluma na ya Kazi tangulizi na sehemu ya mwisho niHitimisho. Aidha, Pengo la utafiti na Kiunzi cha nadharia vimeonyeshwa ndani yasehemu hii.2.2 Mapitio ya Kitaaluma na Mapitio ya kazi tangulizi.Katika sehemu hii Fasili ya lugha, Lugha ya asili, Lugha ya kwanza na Lugha ya pili,Uamiliaji lugha, Ujifunzaji lugha na Matumizi ya lugha ya Pili, Ala za sauti, Sauti zalugha, Namna ya utamkaji na Mahali pa kutamkia sauti za Kiswahili, Pengo lamaarifa na Kiunzi cha nadharia vimeelezewa.2.2.1 Yaliyoandikwa kuhusu lugha,Lugha ya asili,Lugha mama na Lugha yaPili.Kabla ya kuongelea juu ya lugha fulani,ni jambo la muhimu kuelewa kwanza fasiliya lugha.Wataalam mbalimbali wameielezea lugha kwa namna zinazotofautiana kwakiasi kidogo sana.Wafuatao ni miongoni mwa wataalamu hao.Habwe na Karanja ( 2004 ), wakiinukuu TUKI (1990), wanasema kuwa lugha nimfumo wa sauti nasibu zinazotumiwa na watu katika jamii wenye utamaduniunaofanana ili kuwasiliana.Masamba na wenzake (2009), wanaeleza kuwa lugha ni

8mfumo wa sauti nasibu ambazo zimebuniwa na jamii kwa madhumuni yamawasiliano kati yao.Hivyo basi, kulingana na maelezo ya wataalam hao, lugha ni mfumo wa sauti nasibuambazo hutumiwa na watu wa jamii fulani wenye utamaduni unaofanana kwamadhumuni ya mawasiliano miongoni mwa jamii hiyo.Msanjila na wenzake (2009), wanaeleza kuwa lugha ya asili ni lugha inayotokana nawanajamii wa eneo fulani ambao wana mila, desturi na utamaduni wa ainamoja.Lugha ya asili huelezea mambo yahusuyo wanajamii hao kwa kina na kwakujitosheleza.Hivyo basi, lugha ya Kinyamwezi ni lugha inayotokana na wanajamii waTabora.Wanajamii hao ni Wanyamwezi ambao lugha yao ya asili ni Kinyamwezi.Msanjila na wenzake (wameshatajwa), wanasema kuwa lugha mama ni lugha yakwanza anayojifunza mtoto baada ya kuzaliwa. Masebo na Nyangwine (2008),wanaeleza kuwa lugha ya kwanza ni lugha ambayo mtu hujifunza utotoni mwakewakati anakua kabla hajaanza kujifunza lugha ya pili.Ni lugha ambayo jiraniwanaomzunguka,kama wanazungumza lugha hiyo hiyo.Mtoto huigiza taratibumpaka anapoufikia umilisi wa lugha ya kwanza (lugha mama).Masebo na Nyangwine (2008), wanasema kuwa lugha ya pili ni lugha ambayobinadamu hujifunza baada ya kujifunza lugha ya kwanza. Kiswahili ni lugha ya pilikwa watu wengi wa Tanzania.

9Msanjila na wenzake (wameishatajwa), wanaendelea kueleza kuwa lugha ya pili nilugha anayojifunza mtu baada ya lugha yake ya kwanza au lugha mama. Kimsingilugha ya pili huwa ni lugha rasmi inayotumiwa katika elimu, utawala na serikali.Kwa wazungumzaji wengine, lugha ya kwanza huwa pia ndio lugha ya pili kwamaana kwamba ndiyo lugha ya elimu, serikali na mawasiliano mapana. Hivyo basi,kwa wanyamwezi walio wengi lugha yao ya pili ni Kiswahili.2.2.2Yaliyoandikwa kuhusu Uamiliaji lugha, Ujifunzaji lugha na Matumizi yalugha ya Pili.Binadamu anapozaliwa anakuwa na bohari la sauti mbalmbali zisizo na maanayoyote.Mara anapoanza kuishi katika jamii ndipo huanza kuibua sauti hizo katikamazingira bila mwenyewe kutarajia na kuanza kuzitafutia maana.Wataalam mbalimbali wameongelea juu ya Uamiliaji lugha. Krashen na Tracy(1983), wanasema kuwa Uamiliaji lugha ni mchakatounaotokea katika nafsiiliyofichika akilini mwa mtu ambayo ndiyo imuongozayo kuongea au kuandika kwaurahisi.Hivyo wao wanaona kuwa uamiliaji hujitokeza kwa mtu katika hali yaung’amuzi bwete pasipi mhusika mwenyewe kujitambua.Jean(1992:123) anasema, katika uamiliaji lugha watoto wachanga wanakuwamakini katika lugha tangu wanapozaliwa.Wanaanza kutoa maneno yanayotambulikakatika kipindi cha miezi 12 hadi 15 na kuanza kuyaunganisha maneno hayo kuanziamiezi 18. Anaendelea kusema kuwa watoto wote wasio na matatizo ya kimaumbilena baadhi wenye matatizo, wataanza kuongea ikiwa watasikia lugha ikizungumzwakatika mazingira waliyomo.

10Massamba (2004), anasema kuwa, ujifunzaji lugha ni utaratibu wa kufanya jitihadarasmi za kuijua na kuitumia lugha fulani. Mtu yeyote ana uwezo wa kujifunza lughana kuifahamu ikiwa tu atakuwa na akili timamu pamoja na alasauti zotezinazohusiana na ujifunzaji lugha. Kikubwa tu ziwe hazijaathiriwa au kuathirika.Flyn (1984 -1987) kama alivyonukuliwa na Ellis (1996:453), kifaa cha uamiliajilugha ya kwanza kitahusika na mchakato wa ujifunzaji lugha ya pili.Yeye anakubalikuwa Sarufi Majumui ni wezeshi katika ujifunzaji wa lugha ya pili kwani anaaminibado maarifa ambayo mjifunzaji wa lugha ya kwanza anayatumia katika ujifunzajiwa lugha hiyo ndiyo yale anayoyatumia mjifunzaji wa lugha ya pili. Waamiliaji walugha ya kwanza huwa na maarifa asilia ambayo huwawezesha kuiamili lugha yaokwa kutumia maarifa hayo.Sifa za mjifunzaji wa lugha ya kwanza ndizo anazokuwanazo mjifunzaji wa lugha ya pili.Jedwali lifuatalo linaonyesha baadhi ya tofauti zilizopo kati ya uamiliaji lugha naujifunzaji lugha.

11KIELELEZO 2.1 : Jedwali linaloonyesha tofauti iliyopo kati ya Uamiliajilugha na Ujifunzaji lugha:NAMBA UAMILIAJI LUGHA1.UJIFUNZAJI LUGHAUamiliaji lugha hutangulia kisha Ujifunzaji lugha hufuata baada yakufuatiwa na ujifunzaji lugha.Yaani uamiliaji lugha. Baada ya kujuamtoto huanza kuzungumza pasipo kuzungumza ndipo hufundishwakujua taratibu za lugha kama vile sheriambalimbalizalughamuundo na utamaduni wa lugha husika.husika.2.Hutokea katika ung’amuziyaanipasipomtotobwete Ni tukio la kiutambuzi yaani mtumwenyewe anajua fika kwamba anajifunzakujitambua kiakili, anajikuta tu ana lugha.uwezo wa kuzungumza vizuri bilakujua kwa nini anazungumza hivyo.3.Hapa huwa hahitajiki mtaalam wa Lazima kuwepo na mwalimulugha wala mazingira maalumu kama ambaye ni mtaalamu wa jifunzajilughayulekuwezakujifunza lugha kwa urahisi zaidi.4.Si lazima kufuata sheria na kanuni za Ni lazima mtu aelewe vipengelelugha au vipengele vya lugha.5.Utamaduniwahauzingatiwi sana.jamiivyote vya lugha.husika Nilazimamjif

Ujifunzaji wa Lugha ya Kiswahili.Aidha, imeelezea yaliyoandikwa kuhusu Ala za Sauti, Sauti za Lugha, Namna ya Utamkaji na Mahali pa Kutamkia Sauti za Kiswahili. Imeelezea Pengo la Maarifa na Kiunzi cha Nadharia. Sura ya Tatu imezungumzia Njia na Mbinu

Related Documents:

inafuata mchango wa baadhi ya wanaisimu wa lugha ya Kiingereza, Kiarabu na Kiswahili walivyobainisha uwepo wa kategoria ya nomino (majina) katika lugha hizi. 1.1.2 Majina Katika Lugha ya Kiingereza Wataalamu mbalimbali wa lugha ya kiingereza wamebainisha kuwepo kw

Kukuza lugha. Aghalabu tungo zote za fasihi hutumia lugha. Isitoshe, fasihi hutumia mbinu nyingi za lugha. Wasimulizi na waandishi wa fasihi huhitaji kuwa na ukwasi wa lugha. Kuhifadhi mila, tamaduni na itikadi za jamii. Aghalabu kazi za fasihi (hasahasa Fasihi Simulizi) huambatanishwa na desturi mbalim

mada ya utafiti: athari za lugha ya kijita katika kujifunza kiswahili mashaka wenceslaus tasnifu hii imewasilishwa kwa ajili ya kukamilisha masharti ya shahada ya uzamili m.a (kiswahili) kiti vo cha sanaa na sayansi ya jamii.chuo kikuu huria cha tanzania. novemba, 2015

tabianchi katika maendeleo ya sasa na unatia maanani fursa za kupunguza ongezeko la hewa mkaa. Katika kutathimini athari za muda mrefu za mabadiliko ya tabianchi ya siku za baadae ,hasa maeneo ambayo yanahitaji hatua za mapema, yaani miundombinu (ya kudumu ) kwa ajili ya athari kubwa na kuc hukua hatua za kukabiliana na hali hiyo

Ikiwa una wasiwasi kuhusu dalili zozote zisizo za kawaida ambazo unaweza kuwa nazo, au una maswali kuhusu mchanganyiko wa athari kutokana na kupata chanjo zaidi ya moja kwa wakati mmoja. Ikiwa una wasiwasi kuhusu athari zako au ikiwa athari haziishi baada ya siku chache.

KI 214 UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI MBINU ZA UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI I. Malengo ya ufundishaji lugha kwa wageni Lengo kubwa ni kwamba ili mwanafunzi aweze kujua lugha hiyo kwa stadi zote za lugha ile. Stadi za lugha ni 1. Kusikiliza 2.kuzungumza

iii) Sauti iv) Ishara za mwili. Ni mfumo wa sauti za nasibu zinazotumiwa na wanadamu katika mawasiliano. Sifa za lugha. i) Hakuna lugha iliyo bora kushinda zingine. –zote ni sawa. ii) Kila lugha ina sifa zake. iii) Lugha hubadilika kutegemea mazingira, aina ya

Paper-and-Pencil Assessments INCLUDING Reading Comprehension Items English/Language Arts (ELA) Directions for Administering the Part 1 ELA Paper Practice Test- Section 1 . If the Mathematics practice test was previously administered, make sure you redistribute the practice test books to the correct students according to their names on the front covers. The passage and questions in this section .