CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA KITIVO CHA SANAA

2y ago
491 Views
6 Downloads
885.18 KB
141 Pages
Last View : 7d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Albert Barnett
Transcription

CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIAKITIVO CHA SANAA NA SAYANSI ZA JAMIIOSW 101UTANGULIZI WA LUGHA NA ISIMUAhmad Kipacha1

OSW 101UTANGULIZI WA LUGHA NA ISIMUDkt. Ahmad KipachaMhadhiriKitivo cha Sanaa na Sayansi ya JamiiChuo Kikuu Huria cha TanzaniaChuo Kikuu Huria cha TanzaniaS.L.P. 23409,DAR ES SALAAM.Tel: 22-2668992/2668820Fax: 22-2668759E-mail: vc@out.ac.tz, deputyvc@out.ac.tz, registrar@out.ac.tz2

Website: http://www.openuniversity.ac.tzChuo Kikuu Huria cha TanzaniaBarabara ya Kawawa-Manispaa ya KinondoniS.L.P 23409Dar es Salaam.Tanzania. Chuo Kikuu Huria cha Tanzania 2005Toleo la Kwanza, 2005ISBN 9987 0 0134 3Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuigiza, kunakili au kukitoa kitabu hiki kwa njiayoyote ile bila idhini ya maandishi ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.Haki zamwandishi wa kitabu hiki zinalindwa na mkataba baina yake na Chuo Kikuu Huria chaTanzania.3

YALIYOMOSHUKRANIMADHUMUNI YA KOZIMhadhara wa Kwanza: Lugha na Isimu1.1Utangulizi .1.2Lugha ni nini? .1.2.1 Sifa Kuu Bainifu za Lugha za Binadamu .1.2.2 Dhima ya Lugha 1.2.3 Ujuzi wa Lugha: Umilisi na Utendaji .1.2.4 Lugha na Utamaduni: Nadharia ya Sapir-Whorf . .1.3Isimu .1135678Mhadhara wa Pili: Fonetiki2.1Utangulizi .2.2Maana ya Fonetiki .2.3Fonetiki Matamshi .2.3.1 Ala za Sauti . 2.3.2 Aina za Sauti .2.3.2.1 Konsonanti . .2.3.2.2 AKIKI .2.3.3 Irabu 2.3.4. Vipambasauti . .2.3.4.1 Sifa ya Mkazo . 2.3.4.2 Sifa ya Toni . .2.3.4.2 Urefushaji 141517181920212225262627Mhadhara wa Tatu: Fonolojia3.1Utangulizi .3.2Maana ya Fonolojia .3.2.1 Tofauti Baina ya Fonetiki na Fonolojia .3.2.2Fonolojia Vipandesauti .3.2.2.1 Vitamkwa Asilia .3.2.2.2 Upambanuzi wa Vitamkwa .3.2.3Sifa Bainifu za Makundi ya Vipandesauti . .3.2.4Vipashio vya Kifonolojia:Fonimu na Alofoni 3.2.5Unukuzi wa Vitamkwa .3.2.6Michakato na Kanuni za Kifonolojia . .3.2.6.1 Usilimisho .3.2.6.1.1 Michakato ya Usilimisho . .3.2.6.2 Uviringishaji . .3.2.6.3 Usilimisho Pamwe Nazali .3.2.6.4 Utangamano Irabu .3.2.7Fonolojia Vipambasauti (Arudhi) .303131323232343738404141424343464

3.2.7.13.2.7.23.2.7.33.2.7.4Kanuni ya Ufuatano (Fonotakitiki) .Muundo wa Silabi .Mkazo Toni .47474850Mhadhara wa Nne: Mofolojia4.1Utangulizi .4.2Dhana ya Neno, Leksimu na Mofu .4.3Dhana ya Mofimu na Alomofu . .4.3.1 Aina za Mofimu .4.3.1.1 Aina za Viambishi .4.4Uambishaji .4.4.1 Uambishaji Kisarufi .4.4.2 Uambishaji Nyambulishi . .4.4.3 Mwambatano .4.5Uundaji wa Maneno .4.5.1 Ukatizaji . .4.5.2 Uhulutishaji .4.5.3 Vifupisho .4.5.4 Uundaji wa Mashine 5455555657596061626363636363Mhadhara wa Tano: Sintaksia5.1Utangulizi 5.2Mpangilio wa Maneno 5.2.1 Kategoria za Kisintaksia .5.3Uchambuzi wa Virai, Vishazi na Sentensi .5.3.1Mtazamo wa Chomsky . 5.4Muundo wa Kishazi .5.4.1 Aina Mbalimbali za Vishazi 66676871717677Mhadhara wa Sita: Semantikia6.1Utangulizi 6.2Maana ya Maana .6.3Mfumo wa Udhahania 6.3.1Dhana Ficho 6.3.2Umenyu (Typicality) 6.3.3Upanda wa Dhana .6.4Uhusiano wa Maneno 6.4.1Sinonimi (Usawe) .6.4.2Antonimi (Unyume) 6.4.3Polisemia 6.4.4Homonimi .6.4.5Haiponimia .6.4.6Lugha Taswira 6.5Utata .6.5.1Kanuni ya Utungaji (Compositionality) .8384878888899191929293949494945

6.5.1.16.5.1.26.5.26.5.3Utata wa Kimuundo .Utata wa Kileksika Dhima za Kisemantiki .Uainishaji wa Viwakilishi .95959697Mhadhara wa Saba: Isimujamii7.1Utangulizi .7.2Chimbuko na Maana ya Isimujamii .7.3Launi za Lugha 7.4Matabaka ya Kijamii .7.5Ulumbi .7.5.1Ulumbi Taifa 7.5.2Ulumbi Taasisi 7.5.3Ulumbi Binafsi .7.6Ustawi, Mabadiliko na Ufaji wa Lugha . 100101102104106106106107107Mhadhara wa Nane: Isimuhistoria8.1Utangulizi .8.2Chanzo cha Mabadiliko ya Lugha 8.3Kanuni na Nadharia za Mabadiliko ya Lugha 8.4Mabadiliko ya Kileksika na Kisemantika .8.4.1Ukopaji .8.4.2Uundaji wa Maneno Mapya 8.4.3Mabadiliko Katika Maana ya Maneno 8.4.4Mabadiliko ya Kifonolojia .8.4.5Mabadiliko ya Kimofolojia .8.4.5.1 Analojia na Usawazisho .8.4.5.2 Usarufishaji .8.4.6Mabadiliko ya Kisintaksia .111112113116116117117118119119120121Mhadhara wa Tisa: Isimunafsia9.1Utangulizi .9.2Maana ya Isimu-nafsia .9.2.1Matawi ya Isimu-nafsia 9.3Kuteleza Ulimi .9.4Mpangilio wa Maneno Katika Ubongo 9.5Michakato ya Lugha na Isimu .9.5.1Michakato ya Kifonetiki na Kifonolojia 9.5.2Mchakato wa Kimofolojia .9.5.3Mchakato wa Kisintaksia .1241251261271281291291301306

SHUKURANIKazi ya uandishi wa kozi hii imechochewa na mwitikio wa wanafunzi wetu kujiunga kwawingi katika kujifunza lugha ya Kiswahili na Isimu kwa ujumla. Ili kuwasheheneza namada mbalimbali kuendana na mabadiliko ya sasa tumeamua kuandika kitangulizi hikicha Lugha na Isimu kwa kuzingatia kozi mbalimbali ambazo wanafunzi watakuwa nauhuru wa kuzisoma katika ngazi ya shahada ya kwanza na hata uzamili. Hivyoninawashukuru wanafunzi wote wa somo la Kiswahili na Isimu kwa kutupa changamotokuandika kozi hii kwa mtazamo mpya kabisa.Pili ninawashukuru walezi wangu hususan Prof. Kahigi, Prof, Massamba, Prof. Rubanza,Prof. Yahya-Othman na Dr. Kiango kwa kunipa moyo na kunikubalia kubadilishana naomawazo kila maji yanifikapo pomoni. Nawashakuru vilevile Dick Hayward, MichaelMann na Lutz Martin kwa kuniingiza katika maeneo ya Isimu ambayo sikuwahi kuyapitiahapo awali hivyo kutanua uoni wangu wa taaluma hii. Hata hivyo kila mapungufu ya kazihii hayawahusishi wakongwe niliowataja na nisiowataja hapa juu.Bila kumsahau mwandani wangu, Joseline na wana wetu Lut, Ishaq, Waqia na Mwanashakwa kunipa moyo wa kuendelea na kazi hii ya kujitolea mhanga katika mazingira yakukatisha tamaa.Tuendeleze Kiswahili.AkipachaNshupu, Arumeru.7

1.0 UTANGULIZI WA KOZIKila mmojawetu kwa kawaida ana ujuzi wa lugha moja au kadhaa zinazotusaidiakuwasiliana na wenzetu katika kuendesha maisha yetu ya kila siku. Hata hivyo kujualugha hiyo au hizo hakupelekei kufahamu kinagaubaga undani wa miundo ya lugha hiyoau hizo. Ujuzi wa miundo ya lugha ni taaluma inayowashughulisha wanaisimu ambaokila kukicha hujaribu kuibua kanuni na ruwaza zijengazo lugha asili za binadamu.Ushahidi wa ugumu wa kuielezea miundo hiyo unathibitishwa na jitihada mbalimbali zawakongwe wa uchambuzi wa lugha kisayansi kama vile Edward Sapir, Otto Jerspersonna Leornard Bloomfield ambapo katika miaka ya 1920 na 1930 wote waliandika vitabuvyenye kujihusisha na mada moja tu ya lugha yaani Language. Haikuwa bahati nasibukwao kufanya hivyo, kila mmojawao aliona umuhimu kuifafanua dhana hiyo ya lughana kujenga nadharia, kanuni, na mbinu za uchambuzi wa lugha kisayansi. Huo haukuwamwisho kwa wanataaluma, kwani bado jitihada hizo ziliendelea kupitia kazi mbalimbaliza wanaisimu mahiri kama vile Kenneth Pike, Noam Chomsk na wengineo.Muundo wa kozi hii unazingatia mfumo uliozoeleka ambapo vipengele vya vijenzivya lugha huzungumziwa mwanzoni kwa kuanza na vitamkwa viundavyo sauti,mpangilio wake, namna ya kuunda maneno, sentensi, maana ya maneno na sentensi,tumeongezea vilevile taaluma uchambuzi wa maingiliano baina ya lugha na muktadhajamii na mwishoni tumeweka taaluma ya uchambuzi wamabadiliko ya lugha.Tumeukadiria kila mhadhara kukuwezesha wewe mwanafunzi kuusoma na kukupa fikrakwa kipindi kifupi na kukuachia muda wa kufanya mazoezi na kudurusu marejeotuliyoyapendekeza.MADHUMUNI YA KOZIUnatarajiwa mwishoni mwa kozi hii :(i)Ufasili dhana za lugha na Isimu kisarufi(ii)Ubaini sifa za lugha-asili za wanadamu(iii)Kujua muundo wa lugha kuanzia daraja ya chini ya vitamkwahadi sentensi(iv)Ubainishe matawi mbalimbali ya isimu.Tunakutakia kila la kheri masomoni.8

MHADHARA WA KWANZALUGHA NA ISIMU1.1 UTANGULIZIHivi lugha ni nini? Je, watu wote hutumia lugha ili kuwasiliana? Je, kuna baadhiya sifa ambazo kila lugha huwa nazo yaani kuna kufanana kwa namna fulani kwalugha zote duniani? Je, tunaweza kutambua sehemu ambayo lugha hupatikanakatika ubongo wetu? Je, wanyama wana lugha? Haya ni maswali ya anayanaendeleakutafutiwa majibu kila kukicha. Na ni madhumuni ya kozi hii kutoa baadhi yamajibu ya maswali hayo ingawa ni katika kiwango cha utangulizi tu. Mhadharahuu utagusia kwa uchache majibu ya baadhi ya maswali hayo.MALENGO YA MHADHARAUnatarijiwa mwishoni mwa mhadhara huu:(v)Ufasili dhana za lugha na Isimu kisarufi(vi) Ubaini sifa za lugha-asili za wanadamu(vii) Ubainishe waziwazi maana ya ujuzi wa lugha.(viii) Ufasili dhana ya isimu na kujua kazi za mwanaisimu.1.2LUGHA NI NINI?Mawazo ya nini chanzo cha lugha yamekuwa ni msingi katika kujenga fasili yalugha. Mawazo hayo yalikuwa kama yafuatayo: kwamba lugha ni ishara nakwamba ishara hizo huhusisha ala za sauti, na kwamba ishara hizo zipo katikamfumo maalumu, na mfumo huo ni wa bahati nasibu tu, na kwa mfumo huo wabahati nasibu wa ala za sauti, binadamu huwasiliana. Mawazo haya na fasiliiliyoambatana na mawazo hayo yamekuwepo takriban tangia miaka ya 1920 na9

1930 hususan katika skuli ya wanaisimu miundo i.e Leonard Bloomfield naEdward Sapir. Naye Crystal (1992) anafasili lugha kama:mfumo wa sauti nasibu, ishara au maandishi kwa ajili ya mawasiliano nakujielezea katika jamii ya watu.Katika fasili yake ametaja mambo kadhaa ya msingi:(i) MfumoKila lugha ina muundo. Kwa upande mwingine, kila lugha ni kijisehemu tu chamiundo iliyopo katika jozi nzima ya miundo ya lugha duniani. Miundo hiyo kamavile jinsi maneno yanavyoundwa, au jinsi vishazi vinavyofuatana n.k hufuataruwaza maalumu.(ii) Sauti nasibuUhusiano baina ya sauti za maneno au umbo linalowakilisha alama katika lugha yaalama na ule wa maana inayowakilisha ni wa kinasibu tu au ulitokana namakubaliano ya wanajamii wazungumzao lugha fulani.(iii) Sauti, alama na isharaKila lugha huteua sauti au ishara zinazowakilisha wazo au ujumbe fulani. Isharaza maandishi ni sehemu ndogo ukilinganisha na lugha za mazungumzo ambazozipo takriban lugha zaidi ya 6800 za duniani kati ya hizi ni 70 tu ndiyo lugha zaalama kwa mujibu wa Ethnologue (Grimes 2000).(iv) Jamii ya wanadamuNi watu ndio watumiao lugha na ni jamii zao ndizo zinazoteua na kuyapa manenomaana wayatakayo na jinsi gani miundo ya lugha zao iwe. Lugha za wanadamuzina tofauti za msingi dhidi ya njia nyengine za mawasiliano za viumbe wengine.10

(vi) MawasilianoNjia mojawapo ya kuelezea ni kwa namna gani lugha huitumikia jamii ni kuwainawasaidia watu kuwasiliana yaani kutoa na kupokea ujumbe pamoja na kutoleahisia zao. Kwa kutumia lugha tunasema tunachotaka ili kukidhi mahitaji yetu.Kuandika, kusoma, kusema na hata kutumia mfumo wa ishara. Zote hizo ni njiaza lugha.(vi) KujielezeaPamoja na kuwa wanadamu hutumia lugha kwa mawasiliano kiujumla lakiniieleweke kuwa watu hutumia lugha kama njia ya kujitambulisha na kamawanakundi-jamii fulani mahsusi. m.f. Wapemba au Wasiu.Kwa kutumia fasili hii sasa tuangalie sifa kuu za lugha za binadamu ambazo ndiyomalengo ya kozi yetu hii. Katika uchunguzi wa fasili mbalimbali zihusuzo lughaza binadamu sifa zifuatazo zinajitokeza kwa ujumla.1.2.1 Sifa kuu Bainifu za Lugha za WanadamuLugha za wanadamu zina sifa kuu nne zinazoipambanua na mfumo wamawasiliano wa wanyama: Sifa hizo ni:(a) Unasibu(b) Utabaka(c) Uhamisho(d) UzalishajiTunapozungumzia unasibu katika lugha za wanadamu huwa tunamaanisha ile haliambapo sauti fulani zinawakilisha maana fulani katika jamii. Hata zile sautiambazo zinasemekana kuigizia mlio wa sauti halisi ‘onomatopea’ nazo piahukaribia tu ile sauti halisi inayowakilisha. Mengi ya maneno ni sehemu tu yasauti inayotumika kama ishara inayowakilisha maana ya yale yaliyokusudiwa.11

Muundo sarufi wa lugha vilevile ni wa kinasibu kwani hakuna muundo wa ainamoja mfano wa kishazi au kirai ambao kila lugha hauna budi kuufuata (isipokuwakwa zile kanuni ubia).Sifa ya utabaka inamaanisha ile hali ya lugha kuwa ni muunganiko wa vipande aujozi za kanuni zinazounda lugha. Sauti zinajenga silabi, silabi zinajenga neno lakifonolojia, maneno nayo yanakuwa virai, n.k. Kwa upande sarufi, mofimuinajenga shina na maneno, maneno yanakuwa virai, virai navyo vinakuwa vishazi,vishazi vinakuwa sentensi n.k. Hata kwa upande wa semantiki, tunaona utabakawa chini wa vijenzi kujenga ule wa juu zaidi.Mawazo ya utabaka wa lugha ya mwanadamu yanaonekana waziwazi pale Pinker(1994:334) aliposema kuwa:Mfumo wa mawasiliano ya viumbe wasio wanadamu yana muundo wa ainatatu: Milio yenye ukomo .ishara za kianolojia zenye kuendelea ambazozinaonyesha namna ya hali ilivyo au seti isiyo na utaratibu ya mabadilikoya mada. Wakati lugha ya mwanadamu zinamuundo tofauti kabisa ambapotabia ya mfumo wa muungano uitwao ‘sarufi’ huifanya lugha yamwanadamu kuwa iso ukomo enye kuherufika (digital) na kutungika(compositional).Vilevile ikumbukwe kuwa kipande sauti mfano [k] hakitamkiki kwa namna mojatu. Twaweza kuwa na mpasuo kidogo mfano /kh/ au /k/ na tukapata maana tofautikatika /khaa/ ‘kiumbe wa baharini’ au /kaa/ ‘amri ya kukaa chini’ n.k.Sifa ya uhamisho nayo ni ya lugha za binadamu pekee. Katika sifa hii tunaonakuwa mwanadamu anaweza kuongelea jambo ambalo halipo machoni mwao,mfano kuongelea tukio, watu au kitendo kilichopita au hata ambacho kingewezakutokea.12

Sifa ya uzalishi pia hupatikana katika lugha za wanadamu kwani wazungumzajiwaweza kuongeza vishazi, sentensi au hata kisawe katika mazungumzo na hivyokutoa ujumbe kwa kutumia mfumo wa maneno ambao haujawahi kutolewa na mtumwingine yeyote yule duniani. Ili mradi ana uhuru wa kujieleza na kufafanuajambo kwa njia aitakayo yeye na kwa namna yake na wasikilizaji wakamuelewahata kama ni kwa mara ya kwanza kusikia muundo wa sentensi kama huo.ZINGATIALugha za binadamu zina sifa kuu nne: Unasibu, Utabaka, Uhamisho,na Uzalishaji.1.2. 2 Dhima ya LughaLugha hutumika kwa dhima mbalimbali: Nida (1986) ameonyesha dhima nanenazo risha(f)Kushirikiana(g)KuonyeshaWatu hutumia lugha kwa dhima ya Ujumi, yaani wanatumia maneno kwa ustadiili kuburudisha na kuwavutia wengine mfano katika lugha ya matangazo auushairi. Vilevile tunapokokotoa ubongoni mwetu na kutoa majibu yake chombokikuu kitumikacho hapo ni lugha. Hivyo, lugha hutumika kama chombo chautambuzi. Tunapotaka kuonyeshea hisia zetu na vilevile kuwavuta wengine kwamaneno mazito yanayoweza kumtoa msikilizaji machozi ya huzuni au furaha13

tunachagua maneno makali yenye hisia. Lugha pia hutumika kujielezea hali mtualiyonayo ‘ninafuraha kweli kweli’. Hapa mtu anatumia msisitizo wa kuonyeshakiwango cha furaha yake. Jaji anamuhukumu mshtakiwa kwa kumuamuru‘Ninakufunga miaka mitatu jela’; hapa lugha inatenda. Watu pia huweza kutumialugha kuwa na siri baina yao na huweza kujitengenezea njia zao za kuwasilianapasina wengine kuelewa. Unapotaka kuonyesha jambo ni lazima utumie lughakwa njia moja au nyengine.1.2. 3 Ujuzi wa Lugha: Umilisi na UtendajiJe, tunamaanisha nini tunaposema fulani anajua lugha fulani?Jibu ni kuwa hapa tunamaana mtu huyo(a) Ana ujuzi wa aina na mpangilio wa sauti za lugha hiyo.(b) Ana ujuzi wa maana ya maneno na sentensi za lugha hiyo.(c) Ana ujuzi wa sentensi na zisizo sentensi katika lugha hiyo.Ujuzi wa hayo hapo juu unajulikana kama umilisi wa kisarufi ambaounatofautishwa na hali halisi ya matumizi ya lugha hiyo tuiitayo utendaji wakisarufi. Ikumbukwe kuwa ujuzi huu hunaswa katika mapango yaliyokwishatayarishwa katika ubongo wetu kuanzia utoto wetu pale tunapoanza kujifunzalugha kutoka kwa mama zetu. Hakuna darasa la waziwazi la kuwa sasa tunajifunzaaina ya sauti na kesho maana ya sauti hizo na kesho kutwa jinsi ya kutumia sautihizo katika muktadha husika. Haya huzuka pengine bila sisi wenyewe kujuatumejifunza lini. Suala hili la ujuzi wa lugha katika ubongo wetu limezua tawimaalumu liitwalo Isimu-neva ambalo ni mapema mno kulishughulikia katikamadarasa yetu kwa sasa.Kabla ya kukamilisha mjadala wetu unaohusu maana ya lugha ningependaKumalizia kwa kujadili mada ya mahusiano baina ya lugha na utamaduni kwamujibu wa nadharia ya Sapir-Whorf.14

1.2. 4 Lugha na Utamaduni- Nadharia ya Sapir- WhorfMnamo karne ya 20 wanaisimu mahiri waitwao Edward Sapir na Benjamin Whorfwalitafiti lugha za Amerindia za Amerika Kaskazini na kugundua kuwa miundo yamisamiati na ya kisarufi ya lugha hizi haifanani kabisa na ile ya lugha yaKiingereza na lugha nyenginezo za Ulaya na Asia. Hivyo, wakapendekezanadharia isemayo kuwa lugha hutawala namna wazungumzaji wake waionavyodunia. Ukichunguza misamiati ya Kimakunduchi utakuta kuwa maneno yaoyanawakilisha yale wayaonayo mbele ya macho yao au mazingira yao kwa ujumlana kutokuwepo kwa neno kunamaanisha jambo hilo halipo ‘machoni’ pao. Nisawa na kusema ‘lisilo kuwepo machoni na moyoni halipo’.Nadharia hiyo ya Sapir- Whorf, inayojulikana kama nadharia ya Taathira-lughainaunga mkono mawazo ya awali ya William von Humboldt (1767-1835) palealiposema kuwa ‘lugha ya mtu hutawala mawazo yake’. Si wote wanaokubalianamoja kwa moja na ule mtazamo kuwa lugha hufinyanga uoni wetu wa dunia; waohuchukulia kwamba lugha ‘huakisi’ utamaduni wa wazungumzaji wake. Mjadalahuu unaendelea na wanafunzi wanayo fursa ya kuendelea nao na kuuchambua kwakufuatilia kazi mashuhuri ya hivi karibuni ya George Lakoff na Mark Johnson(1980) iitwayo ‘Metaphors We Live By’ ambayo inaunga mkono mawazo kuwalugha hutawala uoni wetu wa mazingira yanayotuzunguka.Wanasema kuwa:Dhana tulizonazo huunda kile tukionacho, kutuzunguka na kinachotuhusu.Hivyo mfumo wa dhana ndio mhimili wa jinsi tuionavyo dunia yetu ya kilasiku (Angalia Lakoff na Johnson 1980:3).Kinyume na kazi ya Eugene Nida (1986) inayosisitiza kuwa lugha ni kielelezo chautamaduni wa wazungumzaji wake na siyo mhimili wa uoni wao. ‘Lugha hufuatajamii wala sio kuiongoza jamii hiyo’ (Nida 1986:11).15

Kwako wewe mwanafunzi hii ni fursa yako na wewe kutoa mawazo yakokuhusiana na uhusiano baina ya lugha na utamaduni.MAZOEZI1.Je, unadhani lugha inatawala uoni wa maisha yetu?Je, haupo uwezekano wakukifikiria kitu (bila ya kukiona) nakukielezea ?Je, nadhariatete ya taathira lugha inaathari gani katika kujifunza lughambalimbali duniani?Hadi hapa tumeona kwa kifupi mambo yafuatayo:MUHTASARI Kila jamii ina lugha lugha kamili Ujuzi wa lugha huambatana na kuelewa mpangilio wa sauti,muundo na maana yake Uhusiano baina ya sauti, ishara na maana ni wa kinasibu tu Lugha za dunia zina kanuni fulani zinazofanana kwa lugha zote Watu hutumia lugha kwa dhima mbalimbali Lugha inaakisi utamaduni wa wazungumzaji wakeSasa na tuangalie namna ya kuchambua lugha kwa kuzingatia vigezo vyakisayansi chini ya taaluma iitwayo Isimu.1.3 litutakayoyashughulikia katika sehemu hii. Jibu ni kwamba Isimu ni ‘taaluma yauchunguzi wa lugha kisayansi’. Ipo taaluma kama vile ya Falsafa ambayo nayoinaweza kujishughulisha na uchambuzi wa masuala ya lugha lakini si kwa kutumia16

vigezo vya kisayansi. Wanaisimu huhakikisha kuwa wakati wa kutafiti na hatimaekuwasilisha matokeo ya utafiti wao wanatumia vigezo vya kisayansi hatua kwahatua. Kwanza huchunguza na kukusanya data, Halafu, wanafanya malinganishokabla ya kuunda nadharia na kuzipima nadharia na kuonyesha matokeo yake.Baadaye hujiundia nadharia na kutoa kanuni ambazo zinapimika. Taaluma hii inamatawi mawili makuu:(a)Isimu Fafanuzi(b)Isimu MatumiziIsimu fafanuzi ni taaluma ya uchambuzi wa vipengee vya lugha au namna gani lughaimepangilika. Isimu Matumizi yenyewe inajishughulisha na kutumia nadharia, mbinuna maarifa ya kiisimu katika kuelezea matumizi ya lugha. mfano katika kufundishalugha, kutunga kamusi, kuunda sera za lugha, leksikografia, tafsiri, lugha zamatangazo, mahakama n.k.Kozi hii itajishughulisha na kujadili baadhi ya matawi ya Isimu fafanuzi pekee. Ndaniya taaluma hiyo kuna vitawi vidogo vidogo ambavyo baadhi yake tutavishughulikiakatika kozi hii nzima. Vitawi hivyo ni kama vile: Fonetiki, Fonolojia, Mofolojia,Sintaksia, Semantikia, Isimu Amali, Isimu Historia, Isimu Jamii, Isimu Nafsia, IsimuNeva, Isimu Kokotozi n.kTunaorodhesha baadhi yake hapa chini na kuonyesha tofauti zake:FonetikiNi tawi linaloshughulikia sauti za vitamkwa ikiwa nipamoja na kuchunguza ala za matamshi, namna yakutamka, uelewa wa sauti, aina za vitamkwa, kusafirikwa sauti na za kiakustika.FonolojiaNi tawi linaloshughulikia uchambuzi wa mfumo wasauti zinazotumiwa katika lugha fulani.17

MofolojiaNi tawi linaloshughulikia uchunguzi wa maneno naaina za manenoSintaksiaNi tawi linaloshughulikia uchanganuzi wa mpangiliona uhusiano wa vipashio katika sentensiIsimu HistoriaTawi linalofuatilia mabadiliko katika lugha kama vilemabadiliko ya sauti, leksika, maumbo ya maneno nahata mabadiliko ya maana.Isimu JamiiTawi llinaloshughulikia uhusiano baina ya lugha najamii.Isimu AmaliTawi linaloshughulikia uchanganuzi wa lugha kwakutegemea maoni ya mtumiaji, hasa uchaguzi wamiundo ya maneno anaoufanya, vikwazo vya kijamiianavyokabiliana navyo katika kutumia lugha, na athariza kijamii katika matumizi ya lugha yake.Isimu NevaTawi linaloshughulikia uchunguzi wa jinsi ubongounavyozalisha, fasiri na kunasa lughaIsimu NafsiaTawi linalochunguza jinsi mtu anavyojifunza lughakwa kutumia misingi ya kisaikolojia.Isimu AnthropolojiaTawi linaloshughulikia mahusiano baina ya lugha nautamaduniIsimu KokotoziTawi linaloshughulika na uchanganuzi wa vipengeevya kiisimu kwa kutumia mbinu za ukokotozi.Haya ni matawi yanayojumuisha Isimu fafanuzi. Hivyo tunaweza kuona kuwakazi ya mwanaisimu ni kuchambua jinsi lugha ilivyoundika na inavyotumikakatika jamii. Sifa kuu katika fasili ya lugha ni kuwa lugha ni mfumo. Ili ujue lughani nini hunabudi utafiti mfumo huo na kubaini miundo yake. Na kwa namna mojaau nyengine lugha zote duniani zina kanuni zinazofanana na ni kazi ya18

mwanaisimu kuzibainisha kanuni hizo huku tukizitofautisha na zile kanuni zalugha au kundi lugha binafsi.Skuli ya wanaisimu mtindo iliweka mkazo tangu awali kushughulikia uchambuziwa lugha kwa kuanzia daraja ya chini kabisa katika mfumo huo, ikianzia utamkajina usikivu wa vitamkwa ambapo tangu awali maelezo na nadharia za fonimu nafonemiki (fonolojia kwa sasa) zilishashughulikiwa kwa kiasi kikubwa. Hakukuwana utata kwamba ni vijenzi hivyo vidogo vya sauti viitwavyo fonimu ndivyovilivyopelekea kuundwa kwa vijenzi vikubwa zaidi viitwavyo mofimu, hadimaneno, virai, vishazi na hadi sentensi. Nadharia za uchambuzi wa lugha kwamsingi wa madarajia ziko wazi, rahisi kutumika na zimeendelea kufanya kazi nakukubalika na wengi.ZINGATIAJambo kuu linajolitokeza hadi sasa kuwa lugha ina muundo namuundo huo unaweza kuchambuliwa kwa kuanzia katika vijenzivyake vidogo kabisa hadi vile vikubwa ambavyo kwa ujumlavinajenga dhana ijulikanayo kama sarufi ya lugha.Hivyo kujua lugha ni kujua sarufi ya lugha hiyo.MUHTASARIKatika muhadhara huu tumeona kuwa: wanadamu walipo popote pale wana mfumo kamili wa mawasilianouitwao lugha. Na hakuna lugha iliyobora zaidi ya nyengine. Dhana ya lugha imenasibishwa na mambo kadhaa: mfumo wamawasiliano, kitambulisho cha utamaduni wa taifa au jamii-lughafulani, na njia ya kufikisha ujumbe ama kwa sauti au maandishi19

Kujua lugha maana yake ni kujua sarufi ya lugha hiyo. Ni pale tuunapojua sarufi hiyo kwenye ubongo wako ndipo uzalishaji wamaneno na sentensi za namna namna zinapojijenga katikamazungumzo. Na sarufi ndiyo inayotawala utamkaji, usikivu na upangaji wa sauti,uundaji na umaana wa maneno na sentensi hizo.MAZOEZI1. Lugha ni nini?2. Je, tunamaana gani tunaposema fulani anajua Kiingereza auKimatumbi?3. Nini maana ya Isimu na bainisha kazi za mwanaisimu kwa mifanohalisi.4. Elezea ni kwa namna gani lugha ni kielelezo cha utamaduni wajamii husika.5. Ni kwa vipi taaluma ya Isimu ni sayansi ?MAREJEOCrystal, D. (1992), An Encylopedic Dictionary of Language andLanguages. Oxford. Blackwell.Eastman, C. (1990), Aspects of Language and Culture. 2nd edition.Novato, CA: Chandler and Sharp Publishers.Grimes, B. Ethnologue 14th ed. Dallas. SIL.Lakoff, G na M. Johnson. (1980), Metaphors We Live By. Chicago.University of Chicago Press.Nida, E. (1986), Sociolinguistics and Translating. Katika Louw, J(Mha.) Sociolinguistics and Communication. UBS MonographSeries, No 1. London United Bible Societies. 1-49.Pinker, S. (1994), The Language Instinct. New York. William Morrowand Company, Inc20

MAREJEO YA ZIADABesha, R. (1994), Utangulizi wa lugha na Isimu. Dar es salaamUniversity Press.Dobrovolsky, M, Katamba F na O’Grady, W (Wah.) (1997),Contemporary Linguistics An Introduction. Longman Londonand New York.Lyons, J. (1999), Language and Linguistics: An Introduction.Cambridge University Press.Kihore Y, D. Massamba na Y. Msanjila (2003), Sarufi Maumbo yaKiswahili Sanifu (Samakisa) Sekondari na vyuo. TUKI.Massamba, D (1990), Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha, TUKI.Massamba, D. (2004), Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha. TUKI.21

MHADHARA WA PILIFONETIKI: UCHAMBUZI WA SAUTI ZA LUGHA2.1 UTANGULIZIJe, sauti zinatamkwaje na msikilizaji anazisikiaje hizo sauti?. Je ni kwa namnagani taaluma hii itatusaidia kuchambua na kubainisha sauti za lugha mbalimbaliduniani? Muhadhara huu utajishughulisha na majibu ya maswali hayo. Vilevile,tunawashauri wanafunzi kupitia kazi zifuatazo kama kiambatanisho cha majibuhayo. Kazi hizo ni Dobrovolsky na wenzake (1997:18-62) , Lyons (1999: 66-98),Massamba, D na wenzake (2004: 1-6) na Besha (1984: 18-28). Taaluma hii nimuhimu kwako wewe mwanafunzi kwani bila kuwa na uwezo wa kubainishavitamkwa mbalimbali na kuwa na ujuzi wa kunukuu itakuwa vigumu kuwezakuchambua na kutofautisha sarufi ya lugha mbalimbali. Ujuzi wa kunukuuvitamkwa utakusaidia kuweza kubainisha sauti ya lugha fulani kwa kutumia alamaza kimataifa zinazotambulika duniani kote. Ujuzi huo pia utakusaidia kuwezakusoma na kuelewa chambuzi nyenginezo zilizofanywa na wanaisimu mbalimbalihasa wanapoandika juu ya monografia ya lugha au lahaja ngeni. Kwa ufupi ujuziwa foneniki ndio msingi wa taaluma zote za isimu ziwe za kijarabati aukinadharia.MALENGO YA MHADHARAUnatarijiwa mwishoni mwa mhadhara huu:(i)Ufasili dhana ya fonetiki na matawi yake(ii)Ubaini namna sauti zinavyozalishwa(iii) Ubaini tofauti kati ya utamkaji wa Konsonanti na ule wa Irabu(iv) Ubaini namna ya kunakili kifonetiki sauti mbalimbali za lughaza binadamu(v)Ubainishe sifa za vipambasauti22

2.2MAANA YA FONETIKIFonetiki ni taaluma ya uchambuzi wa sauti za lugha. Etimolojia ya neno fonetikiimebeba dhana mbili kuu. ‘foni na ‘etiki’. Foni maana yake ni ‘sauti’ na dhana ya‘etiki’ ni pana kidogo. Mara nyingi dhana ya etiki inakinzanishwa na ile ya ‘emiki’(Angalia Eastman 1990:25). Kwa kifupi, ‘etiki’ ni uchambuzi wa tofauti za sautikatika hatua ya awali ya ukusanyaji wa data. Hapa mwanaisimu ananukuu kilasauti aisikiayo kutoka kwa mzungumzaji wa lugha wakati wa ukusanyaji huo.Baada ya hapo inafuatia hatua ya ‘emiki’ ambapo anazibainisha sauti hizo katikangazi mbalimbali za muundo wa sauti ambazo zinatambulika. Kutokana na dhanahizo tunapata kuona tofauti kati ya ‘fonetiki’ na ile ya ‘fonemiki’. Besha (1994:18)anasema kuwa taaluma ya fonetiki huchunguza sauti zozote zile za lugha fulani nakuzitolea sifa zake (yaani etiki) na kisha zinaweza kupangwa katika makundi nakuzipa au kuzitolea sifa ambazo zinaweza kutofautishwa na sauti za lughanyengine (yaani emiki).Hakuna mgongano katika kufasili fonetiki. Ukiangalia fasili za wanaisimu karibuzote zinazungumzia juu ya kuwa taaluma hii ni ya uchambuzi na uchunguzi wataratibu zote zinazohusiana na utoaji, utamkaji, usafirishaji, usikiaji na ufasili wasauti za mwanadamu (Angalia Masamba na wenzake (2004:5) na Besha(1994:18).ZINGATIAFonetiki ni taaluma ya uchambuzi na uchunguzi wa taratibu zotezinazohusiana na utoaji, utamkaji, usafirishaji, usikiaji na ufasili wasauti za mwanadamu.Kwa mujibu wa mwanafonetiki Ladefoged (1975:1), kazi ya kwanza yamwanafonetiki ni kujaribu kujua je, watu hufanya nini wanapozungumza nakusikiliza sauti. Hivyo utakuta kwamba tutawajibika kujua sauti inatolewaje au23

viungo vya sauti ni vipi. Pili, tutaangalia jinsi tunavyovitumia viungo hivyokutolea sauti za namna mbalimbali. Hii ni taaluma ndogo iitwayo fonetikimatamshi au utamkaji. Vile vile tunaweza kuchambua sauti kwa namnaunavyoisikia. Ili tuweze kusikia, tunahitaji kuwa na muundo wa kiakustiki. Niahasa ya kuchambua sauti kiakustiki ni kwa sababu tuweze kubainisha kwa niniwazungumzaji wanajikanganya katika kutofautisha sauti za aina fulani. Aukubainisha sauti ambazo si rahisi kuzitofautisha kwa kuangalia namna yautamkaji. Sauti twaweza kuzisikia na kuzitofautisha kwa namna tatu: kidatu,ukelele na urefu a

Uhusiano baina ya sauti za maneno au umbo linalowakilisha alama katika lugha ya alama na ule wa maana inayowakilisha ni wa kinasibu tu au ulitokana na makuba

Related Documents:

Chuo Kikuu cha Morogoro cha Kilimo kuwa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo. Seneti ya Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo (SUA) mwaka 1991 ilipitisha uamuzi kwamba kila mwaka Chuo kitakuwa kinamuenzi Hayati Edward Moringe Sokoine kwa kuadhimisha kumbukizi ya kifo chake kilichotokea tarehe 12 Aprili, 1984.

1 CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI SHIRIKISHI MUHIMBILI 12 Mei, 2020 TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI Makamu Mkuu wa Chuo, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) anapenda kuwataarifu Waombaji kazi waliotuma maombi ya kujaza n

ii UTHIBITISHO Aliyetia sahihi hapa chini anathibitisha kuwa amesoma Tasnifu hii iitwayo " Athari ya Kimakunduchi Katika Kiswahili Sanifu"" na kupendekeza ikubaliwe na Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania kwa ajili ya kukamilisha masharti ya shahada ya

mada ya utafiti: athari za lugha ya kijita katika kujifunza kiswahili mashaka wenceslaus tasnifu hii imewasilishwa kwa ajili ya kukamilisha masharti ya shahada ya uzamili m.a (kiswahili) kiti vo cha sanaa na sayansi ya jamii.chuo kikuu huria cha tanzania. novemba, 2015

i. Baba yangu ni dereva wa basi. ii. Mama yangu ni mwalimu wa Kiswahili. iii. Dada yake Peter anafundisha katika Chuo Kikuu cha Kyambogo. iv. Bin yangu anaitwa Haba. v. Kaka yangu anasomea katika Chuo cha walimu cha Nakaseke. vi. Binti yake Yusuph ni mrembo sana. vii. Tafadhali niitie yule kaka yangu. viii. Eve ni binti yake mzee Lutaaya. ix.

kuchambua maudhui yanayopatikana katika hadithi za watoto katika jamii ya wapemba mwanaika madi mzee tasnifu iliyowasilishwa kwa ajili ya kutimiza sehemu ya la pekee la kutunukiwa digrii ya uzamili (m.a. kiswahili) ya chuo kikuu huria cha tanzania 2015

ii UTHIBITISHO Aliyetia saini hapo chini anathibitisha kuwa amesoma na anapendekeza tasnifu hii inayohusu athari za kiisimu za lahaja ya Kitumbatu katika Kiswahili Sanifu kinachotumika katika shule za Tumbatu Zanzibar, ipokelewe na ikubaliwe na Chuo Kikuu Huria cha Tanzani

M. Peskin and D. Schroeder, An Introduction to Quantum Field Theory This is a very clear and comprehensive book, covering everything in this course at the right level. It will also cover everything in the \Advanced Quantum Field Theory" course, much of the \Standard Model" course, and will serve you well if you go on to do research. To a large extent, our course will follow the rst section of .