MASWALI YA SARUFI NA UTUMIZI WA LUGHA NECTA 2007-2017 1 .

3y ago
2.5K Views
203 Downloads
48.48 KB
21 Pages
Last View : 1d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Karl Gosselin
Transcription

MASWALI YA SARUFI NA UTUMIZI WA LUGHA NECTA 2007-20171.Katika kila moja ya sentensi zifuatazo onesha kosa la kisarufi kisha andikasentensi hiyo kwa usahihi:a)Kiboko kinaogeleab)Arusi ya kaka yenu zitakuwa Disemba 2006.c)Mwaka huu mvua zinanyesha sanad)Tafadhali nikope shilingi elfu kumi nitakurudishia kesho2.Tunga tungo yenye vipashio vifuatavyoa)Nomino Kishazi tegemezi Prediketa Shamirishob)Kiimakapa prediketa chagizoc)Kirai nomino kishazi huru kishazi tegemezi.3.Eleza dhima ya kiambishi "ni" kilichopigiwa mstari katika sentensi zifuatazoa)Alinisaidia.

b)Wajumbe wapo mkutanoni.c)Wakubalienid)Yeye ni mvivue)Ninakalamu4.Bainisha kauli tano (5) za vitenzi na kila kauli itungie sentensi moja.5.Kwa kutumia mifano ya sentensi eleza dhima tano (5) za mofimu(necta2007)"ku"6.Viambishi awali na viambishi tamati vina uwezo wa kubadili umbo na maana yaneno. Katika maneno yafuatayo eleza dhima ya kila nisho wa kisarufi hufanya nomino mbalimbali kuwa katika kundi moja.Fikiria nomino tano na kwa kutumia sentensi moja kwa kila nomino zipange katikamakundiyake.

8.Uchanganuzi wa sentensi hufanyika kwa hatua hatua. Ukitumia hatua hizochanganua sentensi ifuatayo kwa njia ya jedwali."Wale wawili watakuwa wamepimwa virusi vya UKIMWI hivyo afya zaozitakuwa mapembed)Pembetatue)Mtutu.10."Vitenzi vifuatavyo vinatofautiana kiasili" .Toa sababu za kuthibitisha jibu lako,kisha vipange vitenzi hivyo kutegemeana na uasili wake.(a)Lima (b)Arifu (c)Ruka (d)Sali ( e)Pamoja (f)Adhibu (g)weka (h)Buni(i)Stahimili (j)Chambua. (2008)

11.Vitenzi vya Kiswahili vina tabia zake. Kwa kutumia mifano ya sentensi tano (5)onesha tabia tano (5) tofauti za vitenzi.12.Kuna tofauti gani kati ya mofimu huru na mofimu tegemezi? Eleza kwakutumia sentensinne (4), mbili (2) kwa kila mofimu.13.(a)Eleza maana ya vidahizo Sandali(v)Uzimbezimbe(b)Tunga sentensi moja (1)kwa kila kidahizo.14.Vitenzi vishirikishi hukamilisha ujumbe katika sentensi. Kwa kutumia mifanomitano(5) thibitisha ukweli huo.15.Fafanua dhana ya kiunganishi huru. Kwa kutumia mifano dhihirisha tofauti katiya kiunganishi huru na aina nyingine ya kiunganishi.(2009)

16.Eleza tofauti za msingi mbili (2) zilizopo kati ya kirai na kishazi.Toa mifanomiwili kwa kila tofauti.17.Ni kigezo kipi kinachotumika katika kuunda ngeli za kimapokeo? Dhihirishautumiaji wa kigezo hichokwa kutunga sentensi tano (5) za ngeli tofauti.18.Kwa kutoa mifano, taja matumizi matano (5) tofauti ya kiunganishi "kwa".19.Eleza tofauti kati ya viambishi awali na viambishi tamati. Toa maoni yakokuhusu dhana ya viambishi "kati" katika Kiswahili.20."Mofimu huru zina hadhi ya neno."Fafanua usemi huu kwa kutumia sentensitano tofauti. (2010).21.Tumia kiambishi "KA"kuonesha matukio kumi (10)22."Kila lugha ina tabia ya kuchukua maneno kutoka lugha nyingine ili kukidhimahitaji yake kimsamiati". Fafanua kauli hii ukitumia maneno kumi ya Kiswahili.23.Yapange maneno yafuatayo kama yanavyoonekana katika kamusi, kisha elezamaana ya kila neno kwa kutoa mfano mmoja (1) wa sentensi.

(a)Falsafa (b)Barizi (c)Anuwai (d)Barubaru (e)Kinda (f)Ajuza (g)Fanusi (h)Ghaibu(i)Goigoi(j) Kinanda24.Eleza maana ya upatanisho wa kisarufi. Fafanua jibu lako kwa kutoa mifanominne.25.Misemo mingi hutumika kwa madhumuni ya kulinda heshima na kuvuta makiniya watu". Fafanua usemi huu kwa kutumia misemo mitano (5).(2011)26.Kwa kutumia mifano dhahiri, fafanua dhana zifuatazo:(a)Kiima (b)Chagizo (c)Shamirisho (d)Utohoaji (e)Urudufishaji27."Maneno huweza kubadilika kutoka aina moja na kuwa aina nyingine."Dhihirisha kauli hii kwa kubadili maneno yafuatayo kwa kuzingatia maelekezoyaliyo katika mabano.(a)Mkono(badili kuwa kielezi)(b)Kwenda(badili kuwa nomino)(c)Bora(badili kuwa kitenzi)(d)Ogopa(badili kuwa kivumishi)(e)Mzazi(badili kuwa kitenzi)(f)Bisha(badili kuwa kivumishi)

(g)Refu(badili kuwa kitenzi)(h)Linda(badili kuwa nomino)(i)Kabati(badili kuwa kielezi)(j)Uguza(badili kuwa nomino)28.Kamusi ni muhimu kwa mtumiaji yeyote wa lugha. Taja hoja tanozinazothibitisha umuhimuhuo29.Kwa kutumia mifano ya lugha ya Kiswahili taja sababu tano za utata katikamawasiliano.30.Kwa kutumia mifano taja miundo mitano ya kirai nomino. (Necta 2012).31.Onesha nomino katika tungo zifuatazo kisha bainisha ni aina gani ya nomino:(a)Hatuna budi kumshukuru Mola(b)Mazao yamestawi shambani.(c)Uzalendo usisitizwe shuleni(d)Mpeleke mtoto ndani

(e)Nimechoshwa na upweke.32.Andika tungo zifuatazo kwa usahihi:(a)/Mwenyekiti aliahirisha kikao(b)Mtoto amedumbukia shimoni(c)Kila mwanafunzi anatakiwa kuchangia deski(d)Mama amenunua dazeni ya sufuria(e)Mwanafunzi msafi amepewa zawadi33.Tambulisha viambishi vyenye dhima zilizowekwa kwenye mabano katikamaneno yafuatayo (a)Hakukumbuka (njeo/wakati uliopo)(b)Wamekamatana (kauli ya kutendana)(c)Akisema (hali ya masharti)(d)Ananiona (kurejesha mtendwa)

(e)Tuliwashangilia (kurejesha watenda)(f)Huimba (hali ya mazoea)(g)Wamelima (wakati uliopita hali timilifu)(h)Wanatucheka (urejeshi wa watendwa)(i)/Hawakusoma (ukanushi)(j)Amenipigisha (kauli ya kutendesha)34.Onesha maana tano za neno "kata" na kwa kila maana tunga sentensi moja.35."Upatanisho wa kisarufi ni kigezo kimojawapo kati ya vigezo vya kuunda ngeliza nomino."Thibitisha daihilo kwa kutunga sentensi ukitumia ngeli zifuatazo:(a)U-I(b)LI-YA(c)U-ZI(d)I-ZI

(e)U-YA35.Kwa kuzingatia tungo ulizopewa, bainisha aina za maneno yaliyopigiwa mstari:(a)Juzi tulishiriki maandamano ya amani.(b)Kucheza kwake kunaburudisha(c)Kijana mlevi amepata ajali.(d)Hamisi alikuwa amekwishakwenda kulima(e)Wale vikongwe wamepata msaada(f)Mawazo hayo si yangu(g)Sitakwenda kwake asilani!(h)Amekwenda kazini ijapokuwa ni mgonjwa(j)Mbuzi amekwishakata kamba.

36.Unganisha tungo zifuatazo kwa kutumia O-rejeshi: (a)Mafisadi wamekamatwa.Mafisadi wamefikishwa ahalihapatoshi.37.Bainisha kauli zinazowakilishwa na vitenzi vilivyotumika katika sentensizifuatazo:(a)Refa alichezesha mechi vizuri(b)Mtoto amevunjwa mguu(c)Wanafunzi wanasomeana kitabu(d)Mafuta yamemwagika(e)Walevi wanapigana kilabuni(f)Mtoto analia sana(g)Babu alisomewa kitabu(h)Dada anampikia mtoto uji.

(i)Kaka alimtuliza rafiki yake.(j) Gazeti linasomeka vizuri.38.Vishazi tegemezi hufanyakazi ya vivumishi viwapo katika tungo. Oneshaukweli wa kauli hiyo kwa kutumia mifano minne ya sentensi.39.Toa maana ya kamusi kisha fafanua sehemu kuu tatu zinazounda kamusi.(Necta2013)40.Soma sentensi zifuatazo kisha kwa kila moja taja ni aina gani ya sentensi.(a)Mtoto alikuwa anakimbizana na wenzake.(b)Akisema ukweli atasamehewa(c)Wanafunzi wanasoma kitabu na mwalimu anaandika ubaoni.(d)Kitabu kilichonunuliwa jana kitaletwa kesho darasani.(e)Ingelikuwa vyema tungelifahamiana leo.

41.Taja njia iliyotumika kuunda maneno (d)Kasimawimbi(e)Nyau(f)Uzalishaji (g)Pekepeke (h)Pedeli (i)Ufagio (j)Kingamwili42.Badilisha nomino zifuatazo ili ziwe vitenzi vilivyokatika kauli ya kutenda.(a)Hakimu (b)Msamaha (c)Msuluhishi (d)Kinyambuo (e)Uhamiaji (f)Mafichoni(g)Shuhuda (h) Masimulizi (i)Vichekesho (j)Upendo43.Tungozifuatazo ni tata, toa maana mbili kwa kila tungo:(a)Wewe una ua?(b)Watoto wanamkimbilia babu(c)Kaka amenunua taa.(d)Kumbe ni tembo.(e)Sawa, sasa unaweza kuandaa sherehe. (Necta 2014 P)44.Fafanua utata uliopo katika sentensi zifuatazo:

(a)Mama anafurahia pango(b)Mwalimu analima barabara(c)Alimpigia ngoma.(d)Kijana amepata fomu.(e)Baba ana unda.45.Tumia neno "Paa" katika sentensi kuunda dhana zifuatazo (a)Nomino(b)Kitenzi(c)Kielezi (d)Kivumishi (e)Shamirisho46.Bainisha mzizi wa asili kwa kila neno katika maneno yafuatayo:(a)Anawaandikisha (b)Mkimbizi (c)Mlaji (d)Muumbaji (e)Nisingelipenda(f)Kuburudika (g)Sadifu (h) Aliokota (i)Walichopoka (j)Kipambanuliwe47.Vibadilishe vitenzi vifuatavyo viwe katika kauli ya kutendeka: (a)Badili(b)Kata (c)Komboa (d)Zuia (e)Fika (f)Zoa (g)Jenga (h)Remba (i)Tumia (j)Lima48.Fafanua maana ya neno "Chenga" kwa kutumia sentensi tano tofauti.(Necta2014S)

49.Sentensi zifuatazo zina makosa. Onesha kosa kisha andika upya sentensi hizokwa usahihi.(a)Nimekwenda kwa Kondo na nimemkuta hayupo(b)Dhumuni la Ali ni kuishi mjini.(c)Tunachukua nafasi hii kuwakaribisha hapa nyumbani(d)Mahusiano mazuri hujenga undugu(e)Ni muhimu tukaelewa taratibu za lugha yetu.50.Kuna njia nyingi za kuunda maneno katika lugha ya Kiswahili.Eleza njia zilizotumika kuunda maneno yafuatayo:(a)Misikwao (b)Jografia (c)Chemshabongo (d)Mchezaji (e)Kisimbuzi.51.Tumia maneno yaliyowekwa kwenye parandesi kuunganisha sentensi zifuatazo:(Kwa; lichaya; pasina; pamojana; kwasababu)(a)Kijana huyu anaingia chumbani.Kijana anaingia bila hodi.(b)Juma hakusalimu wazee.Juma hakuwaona wazee.(c)Rashidi ni mrefu.Mimi ninamshinda kwa mbio.

(d)Wewe ni mwanafunzi lakini lazima ulipe nauli.(e)Mchezaji amerusha mpira. Mchezaji amefuata utaratibu.52.(a)Eleza kwa kifupi dhana ya utumizi wa lugha.(b)Taja mambo matatu ya kuzingatia wakati wa kuteua lugha ya kutumia, kisha toamifano miwili kwa kila moja.53.Fafanua maana ya neno "bichi" kama lilivyotumika katika tungo zifuatazo kwakuzingatia muktadha husika:(a)Niletee shuka la kijani kibichi(b)Hili embe bado ni bichi(c)Msichana huyu ni mbichi kabisa.(d)Chakula hiki ni kibichi.(e)Koti lake ni bichi. (Necta2015P)54.Watumiaji wa lugha ya Kiswahili hufanya makosa mengi bila ya kudhamiria.Taja aina mbili za makosa hayo kwa kutoa mfano wa sentensi mbili kwa kila kosa.

55.(a)Eleza maana yarejesta.(b)Kwa kutoa mifano, taja mambo muhimu matatu yanayomwongoza mtumiaji walugha katika uteuzi wa rejesta.56.Katika kila sentensi andika neno moja lenye maana sawa na maelezo yasentensi husika.(a)Mtu anayechunguza uhalifu.(b)Ng'ombe dume aliyehasiwa.(c)Chombo cha usafiri kinachopita juu ya vyuma.(d)Mti unaozaa matunda yanayotengenezwa kinywaji cha kahawa.(e)Sehemu ndogo ya nchi iliyochongoka na kuzungukwa na bahar i katika sehemuzake tatu.57.Eleza dhima za mofimu "li" kama ilivyotumika katika sentensi zifuatazo:(a)Shamba letu li kubwasana.(b)Walichelewa kurudi.

ka sentensi zifuatazo katika hali ya ukanushi:(a)Ameshiba sana.(b)Watoto wengi wanaogelea(c)Mvua ilinyesha kwa wingi(d)Kijana anakula chakula kingi.(e)Mimi nasoma polepole.(Necta2015S.)59.(a)Eleza maana ya utohoaji.(b)Maneno yametohelewa kutoka lugha gani?(i)Picha (ii)Duka (iii)Shule (iv)Rehema (v)Shati (vi)Trekta (vii)Ikulu (viii)Bunge(ix)Achali.

60.Taja aina za sentensi zifuatazo kisha eleza muundo ujengao kila sentensi.(a)Maisha ni safari ndefu.(b)Ukisoma kwa bidii utafaulu kwa kiwango cha juu.(c)Mtoto aliyelazwa hospitalini ameruhusiwa kwenda nyumbani.(d)Nitakuja leo ingawa nitachelewa sana.61.(a)Eleza maana ya urejeshi katika kitenzi. (b)Tunga sentensi tatu zinazooneshaurejeshi wa: (i)Mtenda nafsi ya tatu umoja. (ii)Mtendwa (idadi-wingi)(iii)Mtenda(kitu)62.Andika maneno matano ambayo yameundwa kutokana na kufananisha sauti.Kwa kila neno tunga sentensi moja.63.(a)Eleza maana ya kiambishi. (b)Bainisha viambishi vilivyopo katikavitenzivifuatavyo (i)Tunalima (ii)Wanatembea (iii)Godoro. (Necta2016)64.Katika kila sentensi uliyopewa, orodhesha vishazi huru katika safu A na vishazitegemezi katika safu B.(a)Ngoma hailii vizuri kwa kuwa imepasuka.

(b)Watoto walioandikishwa watakuja kesho. (c)Kiongozi atakayefunga mkutanoamepelekewa taarifa.(d)Mtawatambua waliowasikivu (e)Kitabu ulichopewa kina kurasa nyingi.65.(a)Eleza maana ya kielezi kwa kutoa mfano mmoja wa sentensi.(b)Kwa kila tungo uliyopewa pigia mstari kielezi na kisha taja ni cha aina gani.(i)Darasani kuna utulivu mkubwa.(ii)Wanafunzi wanaimba kimasihara.(iii)Mwalimu amerudi tena.(iv)Nitaondoka wiki ijayo66.Toa maana tano tofauti za neno "kibao" kisha tunga sentensi moja kwa kilamaana uliyoitoa.68.Moja ya faida za misimu ni kuhifadhi historia ya jamii. Toa mfano mmoja wamisimu zagao iliyovuma Tanzania katika vipindi vifuatavyo:(a)Muda mfupi baada ya kupata uhuru.

(b)Miaka ya Azimio la Arusha.(c)Njaa ya mwaka 1974/1975(d)Miaka ya vita vya Kagera.(e)Kipindi cha hali ngumu ya maisha baada ya vita vya Kagera.67.(a)Eleza maana ya kiarifu.(b)Kwa kutumia mifano taja miundo minne ya kiarifu. (Necta2017)

5.Kwa kutumia mifano ya sentensi eleza dhima tano (5) za mofimu "ku" (necta2007) 6.Viambishi awali na viambishi tamati vina uwezo wa kubadili umbo na maana ya neno. Katika maneno yafuatayo eleza dhima ya kila kiambishi. a)Watakapotupambanisha b)Sielekezi 7.Upatanisho wa kisarufi hufanya nomino mbalimbali kuwa katika kundi moja.

Related Documents:

4. Biblia inajibu maswali tunayojiuliza Mwanamke fulani alitambua kwamba Biblia ina majibu ya maswali yaliyomhangaisha kwa miaka mingi.OnyeshaVIDEO,kisha mzu-ngumzie maswali haya: Katika video hiyo, mwanamke huyo alijiuliza maswali gani? Kujifunza Biblia kulimsaidiaje? Biblia inatutia moyo tuulize maswali.SomaMathayo 7:7, kisha mzungumzie .

MASWALI NA MAJIBU ميِحِرلا َّنِمَٰحْرلا َِّالل َّمِسِْب NENO LA MCHAPISHAJI M aswali na Majibu ni kitabu kinachotoa mwongo-zo kwa njia ya maswali na majibu. Kitabu hiki ni mkusanyiko wa maswali aliyoulizwa Sheikh Hasan al-Saffar katika programu yake ya maswali na majibu ili-yoandaliwa katika tovuti yake.

MASWALI NA USAHIHISHO 102 1B KISWAHILI KARATASI 1B OCT/ NOV 1995 2 ½ HOURS Jibu maswali yote 1. UFAHAMU Soma Makala yatuatayo kisha ujibu maswali Ama kweli maisha ya vijana wa kisasa yanatofautiana na kuhitilafiana pakubwa na yale ya wazee wao. Sio katika mavazi, lugha, mienendo, mitazamo, mawazo tu bali pia katika kipengele kingine chochote

MTIHANI WA MWIGO KAUNTI NDOGO YA KAKAMEGA KUSINI-2016 Hati ya Kuhitimu Masomo ya Sekondari – Kenya (K.C.S.E) Maagizo a) Jibu maswali yote. b) Majibu yote yaandikwe katika nafasi zilizoachwa katika kijitabu hiki cha maswali. c) Hakikisha kuwa kurasa zote za kijitabu hiki zimepigwa hapa sawasawa na kuwa maswali yote yamo.

MASWALI YETU MUHIMU KWA SERIKALI YA TANZANIA. MASWALI YETU MUHIMU KWA SERIKALI YA TANZANIA Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Bajeti cha Policy Forum Mchora Katuni: Regis Maro Kimechapishwa na Policy Forum Toleo la Kwanza: Oktoba, 2015 ISBN: 978-9987-708-19-2 Kimesanifiwa na kupigwa chapa na; i

Maswali ya Kutafakari Jibu maswali yafuatayo ili kujaribu mafunzo yetu kutoka katika sehemu hii: 1. Linganisha awamu ya muda ya mafunzo (kulingana na Wilson na Biller) na maelezo yake sahihi: a. Kujifunza kwa ajili ya kitendo i. Kujifunza rasmi maarifa mapya b. Kujifunza kwenye kitendo ii. Kujifunza kutokana na uzoefu na kutafakari

maswali haya yanayoelekezwa kwa vijana wa kundi la Shia Ithnasheria. Huenda yakachangia kuwarejesha katika haki wale wenye akili miongoni mwao, kama watazitafakari hoja na maswali haya, ambayo hayana upenyo wa kuyakwepa na kujitakasa nayo ila kwa kukubali wito wa kushikamana na Kitabu na Sunna visivyokuwa na kupingana.

Agile Development in a Medical Device Company Pieter Adriaan Rottier, Victor Rodrigues Cochlear Limited rrottier@cochlear.com.au Abstract This article discuss the experience of the software development group working in Cochlear with introducing Scrum as an Agile methodology. We introduce the unique challenges we faced due to the nature of our product and the medical device industry. These .