(Hupigwa Chapa Kwa Amri Ya Serikali)

3y ago
271 Views
4 Downloads
214.53 KB
16 Pages
Last View : 1d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Milo Davies
Transcription

Gazeti Makhsus13GAZETI RASMI LA SERIKALI YAMAPINDUZI YA ZANZIBAR(Hupigwa Chapa kwa Amri ya Serikali)Sehemu ya CXXVII Nam. 670318 Juni, 2018Imekubaliwa na Mkuu wa Posta kuwa ni GazetiYALIYOMOMswada wa Sheria ya Kuanzisha Wakala wa Serikali waUchapaji Zanzibar na kuweka masharti bora yanayohusianana Kazi, Uwezo, Uongozi na mambo mengineyanayohusiana na hayo .Bei Shs. 3,000/ Ukurasa14SEHEMU YA SHERIATangazo la Mswada lililotajwa hapo chini linatangazwa katika GazetiRasmi hili.Tangazo la MswadaNam. :Sheria hii itajulikana kama Sheria ya Wakala wa Serikali waUchapaji Zanzibar, 2018.TAN GAZ OMswada ufuatao utawasilishwa katika Mkutano wa Baraza laWawakilishi utakaoanza tarehe .9 Mei, 2018 kwa kusomwa kwa mara yakwanza na unachapishwa pamoja na Madhumuni na Sababu zake kwa ajiliya kutoa taarifa kwa wananchi.ZANZIBAR10 April, 2018(Dkt. ABDULHAMID Y. MZEE)Katibu wa Baraza la Mapinduzi naKatibu Mkuu Kiongozi.Matangazo yaliyohusu maiti, kuvunjika kwa Ushirika na baadhi ya matangazo ambayo ni muhimu kwa watu kujuayanaweza kutiwa katika Gazeti. Nakala matangazo namna hiyo, zipelekwe kwa Mhariri wa Gazeti Rasmi la Serikali yaMapinduzi ya Zanzibar - Tanzania katika nyumba ya kupiga Chapa, Sanduku la Posta 261. Nakala zisichelewe kulikoJumatatu kila wiki.

14GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR18 Juni, 2018MSWADAWASHERIA YA KUANZISHA WAKALA WA SERIKALI WAUCHAPAJI ZANZIBAR NA KUWEKA MASHARTI BORAYANAYOHUSIANA NA KAZI, UWEZO, UONGOZINA MAMBO MENGINE YANAYOHUSIANA NA HAYOSEHEMU YA KWANZAUTANGULIZIJina fupina kuanzakutumika.1. Sheria hii itajulikana kama Sheria ya Wakala wa Serikali waUchapaji Zanzibar, 2018 na itaanza kutumika mara tu baada ya kutiwasaini na Rais.Ufafanuzi.2. Katika Sheria hii, isipokuwa kama maelezo yatahitaji vyenginevyo:“Wakala” maana yake ni Wakala wa Serikali wa Uchapaji Zanzibarkama ulivyoanzishwa chini ya kifungu cha 3 cha Sheria hii;“Bodi” maana yake ni Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala kamailivyoanzishwa chini ya kifungu cha 8 cha Sheria hii;“Mwenyekiti” maana yake ni Mwenyekiti wa Bodi na inajumuishamtu mwengine anayefanya kazi za Mwenyekiti;“Mkurugenzi Mtendaji” maana yake ni Mkurugenzi Mtendaji waWakala aliyeteuliwa chini ya masharti ya kifungu cha 21 chaSheria hii;“Mjumbe” maana yake ni mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi;“Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana na masuala yaWakala wa Uchapaji;“Wizara” maana yake ni Wizara yenye dhamana na masuala yaWakala;“Rais” maana yake ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Barazala Mapinduzi.SEHEMU YA PILIKUANZISHWA KWA WAKALA NA UONGOZIKuanzishwa3. Kunaanzishwa Wakala wa Serikali utakaojulikana kama ni Wakalakwa Wakala.wa Uchapaji Zanzibar.Uwezo waWakala.4. Wakala utakuwa na uwezo wa:

18 Juni, 2018GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR(a) kupata, kumiliki, kununua au kuhamisha mali yoyoteinayohamishika na isiyohamishika;(b) kuingia kwenye mkataba wowote;(c) kukopa fedha kutoka katika Taasisi yoyote ya fedha kwamujibu wa masharti ya Sheria ya Usimamizi wa Fedha zaUmma; na(d) kutekeleza au kufanya jambo lolote au kitu chochoteambacho Wakala wa aina yake unaweza kukitekeleza kwamujibu wa Sheria.5.(1) Kutakuwa na muhuri na nembo ya Wakala katika muundo naaina kama itakavyoamuliwa na Bodi.Muhuri nanembo yaWakala.(2) Nembo ya Wakala itakuwa ni ufupisho wa jina la Wakalakama ambavyo itaamuliwa na Bodi.(3) Matumizi ya muhuri ya Wakala kwa nyaraka yoyoteyatatambulika ni sahihi ikiwa nyaraka hiyo itasainiwa na MkurugenziMtendaji au afisa yeyote wa Wakala aliyeidhinishwa na MkurugenziMtendaji.(4) Nyaraka yoyote iliyotolewa na kuwekwa muhuri wa Wakala,itakuwa sahihi, na kwa mujibu wa masharti ya kifungu kidogo cha (2)cha kifungu hiki, itatambulika kuwa ni nyaraka ya Wakala.6. Malengo ya Wakala yatakuwa ni:Malengoya Wakala.(a) kutoa huduma za uchapaji katika viwango vya juu na kutatuachangamoto zake kwa upeo mpana na kuhakikisha gharamaza huduma za uchapaji zienda sambamba na hudumazenyewe;(b) kutoa huduma za bohari kuu ya Serikali ya vifaa vya ofisi navya kuandikia kwa ajili ya Taasisi za Serikali na binafsi;(c) kuimarisha uweledi wa wafanyakazi ili kwenda sambambana teknolojia za kisasa za uchapishaji; na(d) kufanya tathmini ya athari za kijamii na kimazingira kwaajili ya kukinga na kutafuta suluhisho la athari hizo katikautekelezaji wa kazi za kiwanda kwa jamii.7.-(1) Katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria hii,Wakala utatoa huduma za Uchapaji na Bohari Kuu ya vifaa vya Ofisi nakuandikia.Kazi zaWakala15

16GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBARya;18 Juni, 2018(2) Katika kutoa huduma za uchapaji, Wakala utakuwa na kazi(a) kuchapisha na kutangaza Gazeti Rasmi, Miswada, Sheria,Kanuni, Matangazo ya kisheria na nyaraka nyengine;(b) kuendesha, kuongoza, kusimamia, kuhifadhi na kuendelezakiwanda cha Uchapaji cha Serikali;(c) kutoa huduma za Uchapaji kwa jamii zenye kiwango chajuu kwa bei nafuu na kwa ufanisi;(d) kutoa machapisho ya Serikali kwa umma kupitia maduka yaSerikali yaliyoopo ndani na nje ya Zanzibar;(e) kuishauri Serikali katika mambo yanayohusiana namabadiliko ya teknolojia katika fani ya uchapaji;(f) kuweka na kuhifadhi kumbukumbu zote zinazochapishwana Wakala.(3) Katika kutoa huduma za Bohari Kuu ya vifaa vya ofisi nakuandikia, Wakala utakuwa na kazi ya;(a) kuuza vifaa vya ofisi na kuandikia kwa taasisi zote zaSerikali na binafsi;(b) kufanya utafiti wa mahitaji ya vifaa vya ofisi na kuandikiakwa taasisi za Serikali;(c) kufanya tathmini ya matumizi ya vifaa vya ofisi na kuandikiakwa taasisi zote Serikali; na(d) kuimarisha mashirikiano na taasisi au kampuni zozote zandani na nje ya Zanzibar zinazozalisha au kutengeneza vifaavya ofisi na kuandikia kwa ajili ya kutoa huduma bora kwataasisi zote za Serikali.(4)Wakala unaweza kutekeleza kazi nyengine yoyoteambayo ni muhimu au inayofaa kuhusiana na kazi zake zilizopewa kwamujibu wa Sheria hii.(5)Katika kutekeleza kazi zake, Wakala utafanya nakusimamia kazi zake kwa utaalamu,ufanisi, usiri na kwa kuzingatiamaadili ya kazi za uchapaji.(6)Wakala unaweza kuingia katika makubaliano na kiwandaau taasisi yoyote ya uchapaji ambayo ina malengo yenye kufananana Wakala kwa ajili ya kuleta ufanisi na kuimarisha huduma bora zauchapaji kwa jamii.

18 Juni, 2018GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR(7)Kwa madhumuni ya kazi zake na kutekeleza majukumuyake, Wakala unaweza kuanzisha matawi sehemu yoyote itakayoonainafaa.SEHEMU YA TATUUONGOZI NA UTAWALA WA WAKALA8. Kutakuwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala ambayoitakuwa na wajumbe wafuatao:Bodi yaWakurugenzi.(a) Mwenyekiti ambaye atateuliwa na Rais;(b) Mkurugenzi Mtendaji;(c) Ofisa mmoja mwandamizi kutoka Wizara ya fedha;(d) Ofisa mmoja mwandamizi kutoka Wizara yenye dhamanana Wakala;(e) Mwanasheria Mwandamizi wa Serikali kutoka Afisi yaMwanasheria Mkuu wa Serikali;(f) Wajumbe wengine wawili (2) ambao watateuliwa na Waziri,katika uteuzi huo Waziri atazingatia jinsia na sifa katikafani ya Uongozi wa Uchapaji, Mawasiliano ya Umma,Usimamizi wa Biashara, Teknolojia ya mawasiliano yaUmma na sifa nyengine zinazohusiana na hizo.9. Kazi za Bodi zitakuwa ni:(a) kusimamia uendeshaji wa Wakala;(b) kumshauri Waziri katika uandaaji wa sera na mikakatiinayohusiana na huduma za uchapaji;(c) kupitia na kuidhinisha sera, mpango kazi, bajeti, ripotina taarifa ya ukaguzi ya fedha ya Wakala kwa kuzingatiaMadhumuni ya Wakala yaliyowekwa katika Sheria hii;(d) kusimamia utekelezaji wa usimamizi wa Wakala;(e) kutoa miongozo ya kimkakati;(f) kusimamia masuala ya kiutawala;(g) kuhakikisha utekelezaji wa sera na Utawala bora;(h) kuhakikisha matumizi mazuri ya rasilimali; naKazi za Bodi.17

18GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR18 Juni, 2018(j) kufanya kazi nyengine yoyote kwa mujibu wa Sheria hiiau ambayo ni muhimu katika kufikia madhumuni ambayoWakala umeanzishwa.Kukasimukazi za Bodi.10. Bodi inaweza, ikiwa itaona inafaa kwa ajili utekelezaji bora wakazi zake, kukasimu baadhi ya kazi zake kwa kamati ya Bodi.Uwezo waBodi.11. Bodi itakuwa na uwezo wa jumla wa usimamizi kuhusiana nautekelezaji wa kazi za Wakala, na itakuwa na uwezo maalumu wa:(a) kuanzisha na kusimamia Kanuni za Wafanyakazi na Kanuniza Fedha kwa ajili ya Wakala;(b) kuamua muundo wa uongozi wa Wakala;(c) kupendekeza kwa Mamlaka husika mabadiliko yoyote yamishahara au vigezo na masharti mengine ya huduma zawaajiriwa wa Wakala;(d) kuajiri au kuteua wafanyakazi wa Wakala kwa mujibu waSheria ya Utumishi wa Umma;(e) kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya mfanyakazi yeyoteatayekwenda kinyume na maadili ya kazi zake kwa mujibuwa Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma pamoja naSheria hii;(f) kuidhinisha bei, viwango na malipo mengine; na(g) kupendekeza kwa Waziri uamuzi wa vikao vya bodi,mabadiliko yoyote ya kazi na uwezo wa Wakala; naMakamuMwenyekiti.12. Wajumbe wa Bodi watamteua mjumbe mmoja miongoni mwaokuwa Makamo Mwenyekiti wa Bodi.Muda waBodi.13. Mwenyekiti wa Bodi atatumikia nafasi kwa kipindi cha miakaminne na anaweza kuteuliwa tena, na wajumbe wengine wa Bodiwatatumikia nafasi zao kwa kipindi cha miaka mitatu na wanawezakuteuliwa tena.Nafasi yamjumbekuwa wazi14. Nafasi ya mjumbe wa Bodi itakuwa wazi:(a) akifariki;(b) akiwa, bila ya sababu za msingi, atashindwa kuhudhuriavikao vitatu vilivyofuatana vya Bodi;(c) akiwa atajiuzulu au atakuwa kwa namna yoyote amepotezasifa za kuwa mjumbe wa Bodi; au

18 Juni, 2018GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR(d) akiwa hana uwezo kutokana na sababu za kimwili au kiakilikutekeleza majukumu yake.15. Bodi itamteua Afisa wa Sheria ambaye ni muajiriwa wa Wakalamwenye angalau Shahada ya kwanza ya Sheria na uzoefu usiopunguamiaka mitatu kuwa Katibu wa Bodi.Katibu waBodi.16.(1) Bodi itafanya vikao vyake vya kawaida angalau mara mojakwa kila kipindi cha mienzi mitatu na inaweza kukutana muda wowoteikiwa ipo haja ya kufanya hivyo kwa ajili ya utekelezaji wa shughulizake.Vikao vyaBodi.(2) Vikao vyote vya Bodi vitaitishwa na Mwenyekiti au ikiwahayupo Makamu Mwenyekiti.(3) Vikao vya Bodi vitaongozwa na Mwenyekiti na ikiwahayupo Makamo Mwenyekiti ataendesha kikao hicho, na ikiwa hawapowote wawili Mwenyekiti na Makamo Mwenyekiti, wajumbe waliopowatamteu mmoja miongoni mwa wajumbe kuongoza kikao.(4) Zaidi ya nusu ya wajumbe wa Bodi wanaweza kuomba kwamaandishi kwa Mwenyekiti kuitisha kikao, baada ya kupokea ombi,Mwenyekiti anaweza kuitisha kikao ndani ya siku ishirini na moja.17. Akidi ya kikao cha Bodi itakuwa ni zaidi ya nusu ya Wajumbewa Bodi kwa kila kikao.Akidi yaKikao.18. Maamuzi ya Bodi yatafanywa kwa makubaliano na ikiwamakubaliano hayatofikiwa, maamuzi yatafanyika kwa kupiga kura naendapo kura zitakuwa sawa, Mwenyekiti au mjumbe anayeendesha kikaoatakuwa na kura ya maamuzi.Maamuzi yaBodi.19. Kumbukumbu za kila kikao cha Bodi zitathibitishwa katikakikao kinachofuata cha Bodi na kuwekwa saini na Mwenyekiti wa kikaona Katibu wa Bodi.Kumbukumbuza vikao.20. Mwenyekiti na wajumbe wengine wa Bodi watapewa posho namalipo mengine kama Waziri atakavyoamuwa kila baada ya muda kwamujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma, Kanuni na Miongozo.Posho zawajumbe.21.(1) Kutakuwa na Mkurugenzi Mtendaji atakayeteuliwa na Rais.ikiwa:(2) Mtu atakua na sifa za kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji(a)ni Mzanzibari;(b) ana angalau shahada ya kwanza ya Teknolojia ya Uchapaji,Teknolojia ya Mawasiliano ya Umma, Ufundi na UhandisiUteuzi waMkurugenziMtendaji.19

20GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR18 Juni, 2018wa Umeme, Utawala au fani inayofanana na hizo kutokachuo kikuu kinachotambulika; na(c)Kazi zaMkurugenziMtendaji.Kuanzishaana uzoefu angalau miaka saba (7) katika fani zilizotajwakatika aya ya (b) ya kifungu hiki.22.(1) Mkurugenzi Mtendaji atakuwa Afisa Mtendaji Mkuu naMchapaji Mkuu wa Serikali na atawajibika na majukumu ya kila siku yauendeshaji, utekelezaji na usimamizi wa Wakala.(2) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu kidogo cha (1) cha kifunguhiki, Mkurugenzi Mtendaji atakuwa na kazi zifuatazo:(a) kuwa na dhamana ya mapato na matumizi ya Wakala;(b) kutoa machapisho yenye viwango na kuingia kwenyemikataba kwa ridhaa ya Bodi;(c) usimamizi bora wa fedha na mali za Wakala;(d) kuhakikisha kuwa sera za Wakala zinatekelezwa namalengo, shabaha na viwango vilivyokubaliwa vinafikiwa;(e) kupendekeza na kutekeleza Mpango Mkakati, Mpango waKibiashara na Mpango wa Utekelezaji wa Wakala;(f) kusimamia masuala ya Wakala kwa ufanisi na umakinikatika utoaji wa huduma zilizo na ubora;(g) kutoa msaada wa kitaalamu kwa Bodi;(h) Kutengenezakwamba:mifumoya uchapajikwa kuhakikisha(i) huduma za uchapaji zinatolewa katika hali ya usalama;(ii) miundo mbinu ya uchapaji inafanya kazi;(iii) kuhakikisha upatikanaji wa mfumo wa uchapaji, vitendeakazi na vifaa vyengine vya Wakala;(iv) upatikanaji wa huduma za uchapaji endelevu zinazotolewakwa kiwango cha juu katika hali ya kitaalamu kwa kuletamaendeleo endelevu na uongozi bora;(v) uzalishaji wa bidhaa kwa usahihi na wakati, na kutoataarifa za masuala ya uchapaji kwa ajili ya kupanga na kutoamaamuzi husika;

18 Juni, 2018GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR(vi) kuhakikisha usalama wa wafanyakazi, mashine na mazingiramazuri ya kazi; na(i) kufanya kazi nyengine yoyote halali ambayo ni muhimu auinafaa katika utekelezaji wa kazi zake kwa mujibu wa Sheriahii kama atakavyoelekezwa na Bodi.23.(1) Kutakuwa na Idara, vitengo au divisheni ndani ya Wakala kamaitakavyoamuliwa na Bodi na kuidhinishwa na Kamisheni ya Utumishi waUmma.Idara.(2) Kwa mujibu wa masharti ya kifungu kidogo cha (1), Idara zaWakala zitakuwa:(a) Idara ya uwendeshaji Kiwanda na Bohari Kuu ya Vifaa vyaOfisi na kuandikia;(b) Idara ya Masoko na Uhusiano kwa Umma; na(c) Idara ya Mipango na Utawala;(3) Bila ya kuathiri kifungu kidogo cha (2) cha kifungu hiki, Bodiinaweza kuanzisha Idara nyengine kama itakavyoona inafaa.(4) Idara, vitengo au divisheni zitazoanzishwa chini ya kifungukidogo (1) cha kifungu hiki zitafanya kazi kwa mujibu wa muundo waWakala ulioidhinishwa na Kamisheni ya Utumishi wa Umma.(5) Mkuu wa Idara atateuliwa na Bodi na atakuwa mtu mwenyetaaluma na uzoefu wa kutosha kufanyakazi za Idara husika.(6) Mkuu wa Idara, kitengo au divisheni atatekeleza majukumuyake chini ya usimamizi wa Mkurugenzi Mtendaji.24.(1) Wakala utakuwa na Afisi ndogo ya Pemba ambayo itaongozwana Mkuu wa Afisi hiyo ambaye atateuliwa na Bodi.Afisi ndogoya Pemba.(2) Mkuu wa Afisi ndogo ya Pemba atafanya kazi zake chini yauangalizi na maelekezo ya Mkurugenzi Mtendaji.Wafanyakazi wa Wakala25. Bodi inaweza kuajiri wafanyakazi wengine kama ikihitajika kwautekelezaji bora wa kazi za Wakala kwa mujibu wa Sheria ya Utumishiwa Umma na Kanuzi zake.26. Katika kutekeleza majukumu yake, Waziri atakuwa na uwezo wakusimamia utekelezaji wa Sera zinazohusiana na Wakala kutoa maelekezona maagizo ya jumla kwa Wakala na Bodi.Wafanyakaziya Wakala.Uwezo waWaziri naMahusiano yaWakala.21

22GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBARUhusianobaina yaWakala naWizara.18 Juni, 201827. Kwa kuzingatia masharti ya Sheria ya Utumishi wa Umma naSheria hii, Wakala utawajibika kuwasilisha taarifa zozote za kiutawala nakiuendeshaji kwa Wizara kila zinapohitajika.SEHEMU YA NNEMASHARTI YA FEDHAFedha zaWakala.28. Fedha na rasilimali za Wakala zitajumuisha:(a) fedha zilizoidhinishwa na Baraza la Wawakilishi kwa ajiliya matumizi ya Wakala;(b) ada au tozo zinazolipwa Wakala kutokana na utowaji wahuduma zake;(c) ruzuku, zawadi, msaada, michango, mikopo, au uwekezajihalali kama itakavyopokewa kutoka kwa mtu yoyote aujumuiya; na(d) fedha nyengine yoyote halali itakazopewa au kuzipatakatika utekelezaji wa kazi zake au vyenginevyo.Hesabu zaWakala.29. (1) Wakala utaweka vizuri vitabu vya hesabu si zaidi ya miezimitatu baada ya mwisho wa kila mwaka wa fedha na utaandaa:(a) taarifa ya mali na madeni ya Wakala ya siku ya mwisho yamwaka wa fedha, kuwasilishwa na kukaguliwa na Mdhibitina Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali;(b) taarifa ya mapato na matumizi ya mwaka huo wa fedha; na(c) taarifa nyengine yoyote ya fedha kama itakavyo hitajika.(2) Mapato yote yaliyokusanywa kutokana na huduma zilizotolewana Wakala yatawekwa katika akaunti ya benki kwa kuzingatia na kwamujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Fedha za Umma.Taarifa yaUtekelezajiya Mwaka.30. Wakala ndani ya miezi sita ya kila mwaka wa fedha baada yakuidhinishwa na Bodi utawasilishwa kwa Waziri taarifa inayohusiana namwaka huo ikijumuisha:(a) kivuli cha hesabu za Wakala zilizokaguliwa, pamoja na taarifaya Mkaguzi ya hesabu hizo;(b) taarifa ya utekelezaji ya malengo makuu na taarifa nyengineyoyote inayohusiana na hizo;(c) taarifa ya uendeshaji wa Wakala kupitia mwaka wa fedha;na(d) taarifa nyengine juu ya shughuli za Wakala Waziriatakapohitaji.

18 Juni, 2018GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR31. Wakala unaweza, baada ya kupata ruhusa ya Waziri anayehusikana fedha na kwa mujibu wa masharti ya Sheria ya Usimamizi wa Fedhaza Umma, kufungua akaunti katika Benki yoyote kwa ajili ya kuwekafedha zake kwa matumizi na kutekeleza kazi za Wakala kwa mujibu waSheria.UfunguajiwaAkaunti.SEHEMU YA TANOMAKOSA NA ADHABU32.(1) Mtu yeyote aliyeajiriwa kutekeleza jukumu lolote chini yaSheria hii ambaye:(a) kutokana na nafasi yake ya kazi akapata taarifa zozote naakazitumia taarifa hizo kwa maslahi yake binafsi au kwamiamala ya kibiashara ambayo itachochea au kuhatarishausalama, maslahi au miamala ya kibiashara kabla yakutumika kwa umma taarifa hizo au akazitumia taarifa hizokwa kupata faida binafsi;(b) bila ya amri halali akachapisha au kumpatia mtu mwenginetaarifa za kiwanda kinyume na utaratibu wa kazi ambazotaarifa hizo alizipata wakati anatekeleza kazi za Wakala;(c) kwa makusudi anashiriki katika jambo au kuharibu taarifaau kuwasilisha taarifa za uongo;atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatia atawajibika kulipa fainiya fedha za kitanzania zisizopungua milioni tano na zisizozidi milionikumi au kifungo kisichopungua miaka miwili na kisichozidi miakaminne au vyote viwili faini na kifungo kwa pamoja.(2) Mtu ambaye anazo taarifa au nyaraka za Wakala kwa makusudiakazitoa taarifa au nyaraka hizo kinyume na masharti ya Sheria hii,akazichapisha au kumpatia mtu mwengine, atakuwa ametenda kosana akipatikana na hatia atawajibika kulipa faini ya fedha za kitanzaniazisizopungua milioni tatu na zisizozidi milioni tano au kifungo kwakipindi kisichopungua miaka miwili na kisichozidi miaka mitatu auvyote viwili, faini na kifungo kwa pamoja.(3) Mtu ambaye atatumia malighafi za Wakala au mashine kwamatumizi yake binafsi atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatiaatawajibika kulipa faini isiyopungua milioni mbili na isiyozidi milionitano fedha za kitanzania au kifungo kisichopungua miezi sita nakisichozidi miaka miwili au vyote viwili faini na kifungo kwa pamoja.(4) Mtu atakayeuza, kutumia au kuruhusu kutumika kwa mashinebila ya ruhusa na kuidhinishwa na Wakala, atakuwa ametenda kosa naakipatikana na hatia atawajibika kulipa faini ya fedha za kitanzaniazisizopungua milioni tano na zisizozidi milioni kumi au kifungokisichopungua miaka miwili na kisichozidi miaka mitano au vyote viwilifaini na kifungo kwa pamoja.Makosa naAdhabu.23

24GAZETI RASMI LA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR18 Juni, 2018(5) Mtu yeyote ambaye atatumia mashine au vifaa vya Wakalabila ya ruhusa ya Mkurugenzi Mtendaji, atakuwa ametenda kosa naakipatikana na hatia atawajibika kulipa faini ya fedha za kitanzaniazisizopungua milioni tatu na zisizozidi milioni tano au kifungokisichopungua miaka miwili na kisichozidi miaka mitatu au vyote viwilifaini na kifungo kwa pamoja.(6) Mtu yeyote au taasisi itakayotumia muhuri au alama yaWakala bila ya ridhaa ya Mkurugenzi Mtendaji atakuwa ametendakosa na akipatikana na hatia atawajibika kulipa faini fedha zakitanzania zisizopungua Milioni tatu na zisizidi milioni tano au kifungokisichopungua miaka miwili na kisichozidi miaka mitatu au vyote viwilifaini na kifungo kwa pamoja.SEHEMU YA SITAMASHARTI MENGINEYOKinga.33. Mjumbe wa Bodi, mfanyakazi au mtu yeyote aliyeajiriwa naWakala hatowajibika yeye binafsi kw

mujibu wa masharti ya Sheria ya Usimamizi wa Fedha za Umma; na (d)kutekeleza au kufanya jambo lolote au kitu chochote ambacho Wakala wa aina yake unaweza kukitekeleza kwa mujibu wa Sheria. 5.(1) Kutakuwa na muhuri na nembo ya Wakala katika muundo na aina kama itakavyoamuliwa na Bodi. (2) Nembo ya Wakala itakuwa ni ufupisho wa jina la Wakala

Related Documents:

Kwa nini tunakosa kui mwito wa Mungu kuwa mawakili wema. 1. Mtazamo wetu potovu kuhusu fedha. Kwanza tunaona kuwa mali ni yetu na sio ya Mungu. Pili twafikiri kutoa kwetu ni kitendo cha huruma kwa kazi ya Mungu wala sio amri. na Si amri. Tatu ,twafikiri kwa kufanya huvyo twamfanyia Mungu huruma kwa kupeana kwa Kanisa lake. 2.

7. Onyesha kwa vitendo maisha yako mapya kwa kuonyesha upendo na shauku ya kuwajali wengine. Maisha inayotawaliwa na Kristo Maisha ya Mkristo yanaweza kuwakilishwa na picha ya msalaba. Kristo ndiye kiini cha maisha yetu mapya. Tunaishi kwa kujisalimi-sha kwake.Mstari ulio wima, unawakilisha ushirika wetu pamoja na Mungu kwa maombi na kwa kusoma .

KI 214 UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI MBINU ZA UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI I. Malengo ya ufundishaji lugha kwa wageni Lengo kubwa ni kwamba ili mwanafunzi aweze kujua lugha hiyo kwa stadi zote za lugha ile. Stadi za lugha ni 1. Kusikiliza 2.kuzungumza

Yesu aliwaacha waamini na utume mkuu wa kuufikia ulimwengu kwa Injili ya Ufalme. Kazi hii haitakamilishwa kwa maneno pekee. Kama katika kanisa la kwanza, lazima pia kuwe na . Hizi zote ni nguvu kubwa zinazofanya kazi katika ulimwengu wetu wa leo. Lakini mwito kutoka kwa Yesu sio kwa mamlaka ya kidunia. Ni kwa nguvu za kiroho. Ni nguvu ambayo .

MASWALI YETU MUHIMU KWA SERIKALI YA TANZANIA. MASWALI YETU MUHIMU KWA SERIKALI YA TANZANIA Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Bajeti cha Policy Forum Mchora Katuni: Regis Maro Kimechapishwa na Policy Forum Toleo la Kwanza: Oktoba, 2015 ISBN: 978-9987-708-19-2 Kimesanifiwa na kupigwa chapa na; i

(3) Beatriz Treviño (Juan Bautista Chapa) in 1653. (Monterrey, N.L. Mx) Children: Juan, (1660) Nicolas (1655) Gaspar, Jose Maria, Maria, Juana As noted earlier, Juan or Giovanni Schiapapria (Chapa) 1627-1695, was born in Villa Albisola on the coast of Genoa, Italy. He migrated in 1647 to Mexico. There he shortened the family name to Chapa. In

CHAPA-DE News MAY 2021 3 HEPATITIS C CAN BE CURED: HEP C TREATMENT NOW AVAILABLE AT CHAPA-DE Chronic hepatitis C (HCV) is a viral infection

Description Logic RWTH Aachen Germany 4. Introduction to DL I A Description Logic - mainly characterised by a set of constructors that allow to build complex concepts and roles from atomic ones, concepts correspond to classes / are interpreted as sets of objects, roles correspond to relations / are interpreted as binary relations on objects, Example: Happy Father in the DL ALC Manu (9has-child .