YALIYOMO - Revival Ministries Australia

2y ago
213 Views
3 Downloads
659.44 KB
40 Pages
Last View : 1d ago
Last Download : 2m ago
Upload by : Joao Adcock
Transcription

YALIYOMOUtangulizi: Uvuvio unakuja1a & 1b Kainsa la Siku za Mwisho: Fundisho kutoka Kwa Efeso2. Kuurudia Upendo wa Kwanza: Matendo ya kwanza ni gani?3. Kuumega Mkate katika Maandiko Matakatifu.4. Hakikisho la Wokovu wa Sayuni: Nafasi ya kudumu katika maombikulingana na Neno la Mungu5. Wokovu kwa Mataifa: Nyumba Yangu itaitwa Nyumba ya Maombikwa Mataifa Yote.6. Tume Kuu: Mpango wa Uinjilisti.7. Kuingia Katika milango ya Mji Mtakatifu.Pg 2

UTANGULIZI – UVUVIO UNAKUJAUvuvio ambao unakuja na ambao tayari umeanza katika mataifa mengine ni mavunokatika nyakati za mwisho, ambao ulinenwa mara nyingi na Yesu katika MafundishoYake. Sasa Mungu anarejesha huduma ya mitume kwa kanisa na wanaume kwawanawake walio na maono wameanza kujitokeza katika kazi ya mavuno. Wale ambaowanavazi la utume juu yao wamejitolea kikamilifu kuwafundisha watenda kazi katikamavuno na wengine wameanza shughuli za upanzi wa makanisa.Katika muongozo huu na katika vipindi ambavyo vitakavyo jitokeza kupitia katika muongozohuu, tutatembelea mafundisho mengine ambayo Bwana ameweka huru.MASWALA BAYANA YA UVUVIO1.Ukweli wa toba kutokana na dhambi yote na kuungama dhambi kwa Mungu na mtumwingine kunapohitajika (Yakobo 5:16). “Vivyo hivyo nanyi jihesabuni kuwa wafukwa dhambi na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu”, Rum.6:11. Mungu analiitakanisa Lake liwetakatifu.2.Kuishi na kuenenda kwa Roho, kujifunza kumtegemea Yesu na Neno Lake kwetu,kupokea na kuitikia upendo Wake, kumtumikia katika maombi na huduma jinsiAnavyoongoza. Gal.5:16-25, inazungumzia jinsi ya kuishi maisha ya kushinda mwilikwa kuishi kwa Roho, na kuthihirisha matunda tisa ya Roho. [Kol.3:1-4)3.Ufupisho wa kazi ya huduma katika maisha ya watu: jinsi Bwana anvyoifupishawakati wa huduma kwa kuwaleta watu katika kitu kipya ambacho Anafanya. Hudumaya ukombozi ni sehemu ya mpangillio huu, pamoja na mwenendo mkuu wa RohoMtakatifu katika maisha ya watu Wake.4.Wajibu Mkuu wa Roho Mtakatifu katika kanisa, na utiifu usio na swali Kwakekatika huduma ya uvuvio. Roho Mtakatifu ni Mungu miongoni mwetu,2 Kor. 3:17, na kupitia kwa ibada ndani Yake tunabadilishwa, a.18; na kupitia kwaketunawezeshwa kuwa wahudumu wa Agano Jipya, a.5-6. “Kwa kuwa wotewanaoongozwa na Roho hao ndio wana wa Mungu”, Rum.8:14.5.Kufundisha kutoka kwa Maandiko kuhusu kanisa la kimitume, kuanzishwakwake na utekelezaji wa huduma ya kimitume katika kitabu cha Matendo, hasamatendo ya Paulo ya kuanzisha kituo cha mafunzo, ambacho kupitia kwake vuvionyingi kuu zilikua na kuenea, na watenda kazi wengi waliingia katika kazi ya mavuno.(Matendo 19:8-10).6.Maombi kama msingi mkuu katika yale Mungu anafanya: tunakuwa na maombiya kikundi kila mara na pia tumeongozwa na Bwana katika maombi ya kuugua. Watuwengi hunukuu Rum 8:28 bila kujua msingi wa a.26-27 ambao unaonyesha mahalimuhimu pa maombi na maombezi ya Roho Mtakatifu kuyaleta mapenzi ya mungukufanyika.Pg 3

7.Kurudia injili na kusikia tena kile Yesu Anasema, kwa sikio la kusikia kileambacho analiambia kanisa leo. Ni injili ya Bwana Yesu Kristo(Marko 1:1) katikamaneno yake amwenyewe. Katika Injili, Yesu anatwambia cha kufanya! Katikakitabu cha Matendo, mitume wanatuonyesha jinsi ya kutii Amri ya Bwana; na katikaNyaraka, mitume wanatwambia kwa nini. Kwa maneno mengine wanafundisha Neno.8.Kupenda kuendelea na Mungu kulingana na Neno Lake, sio kuendelea kufungwana desturi au utawala. Gharama ni mateso na upinzani!Pg 4

KANISA LA SIKU ZA MWISHO:FUNDISHO KUTOKA KWA EFESO – SEHEMU AKANISA LA KIMITUME NI NINI?Ni kanisa ambalo Yesu alisema atalijenga katika Mathayo 16:18:"Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro[Petro ni jiwe, petros; tafsiriwa: Petro, Jiwe)]Na juu ya Mwamba huu {juu ya ufunuo ndani ya Yesu Kristo}[Mwamba Kristo (S.C.Gr.4073 petra, Mwamba]nitalijenga [Yesu] kanisa Langu wala milango ya kuzimu haitalishinda."Nyumba ya Mungu ya Roho inajengwa na mawe yaliyohai (1Pet.2:5). Tunafanyika maweyaliyohai kwa njia ya imani katika Kristo Yesu!Yesu ni mtume, aliyeteuliwa na Mungu kujenga kanisa, nyumba ya Mungu (Ebr. 3: 3-6).Petro kama mtume wa Yesu Kristo, aliteuliwa kuuweka msingi wa kanisa. Mathayo 16:19:"Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga [zuia]duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua [ruhusu, haribu]duniani,litakuwa limefunguliwa mbinguni."Petro alizitumia hizo funguo Siku ya Pentekoste kuwafungua Wayahudi 3,000 kuingia katikaufalme wa Mungu; alizitumia Samaria kuwafungulia Roho Mtakatifu; na pia alizitumia katikanyumba ya Kornelio kuwafungulia Mataifa wa kwanza kuingia katika Ufalme.Kanisa la kimitume ni kanisa la Agano Jipya Lake Bwana Yesu Kristo. Hakuna kanisalingine hakika katika Agano Jipya. Yesu alipatia kanisa mamlaka na uwezo Wake. Aliahidikuwa "milango ya Kuzimu", mamlaka yote na uwezo wa shetani na mapepo wachafu (Luka10:19), hawataweza kushinda kanisa. Ni kanisa ambalo Yesu alituma kuhubiri injili kwamataifa yote (Marko 16:15-20 & Mathayo 28:18-20). Ni kanisa ambalo Yesu aliwekamsingi wake katika kuwalea wale mitume kumi na wawili, mashahidi sabini (Luka 10:1) na500 (1 Kor. 15:6) waliomuona akiwa hai kutoka kwa wafu. Ni "Nyumba ya Mungu, ambayoimejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, Kristo Yesu mwenyewe akiwa jiwe kuu laPembeni, katika yeye jingo lote limeungamanishwa vema na kukua hata liwe hekalu takatifukatika Bwana" (Efe 2:19-21).MPANGO WA MUNGU KWA KANISAKitabu cha Efeso kinatupatia picha kamili ya kanisa. Ni Waraka kwa Waefeso ndio Pauloanatoa vipawa vya huduma vyake Yesu aliyepaa (Efe. 4:8). Vipawa ambavyo Yesu aliyepaaalitoa ni: mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji na waalimu. (aya 11). Kristo nayealishuka mpaka pande zilizo chini (mauti, alishuka na akapaa juu – aya ya 9-10) ili atoevipawa na kuwapa watu kwa ajili ya kujenga na kutimiza makusudi ya Mungu. Kanisa lakwanza la Yerusalemu lilianzishwa na wale mitume kumi na wawili na baadaye, liliongozwana mitume na wazee (Matendo 15:6). Muhubiri wa injili, Filipo, (Matendo 21:8) kwanzaalihubiri Samaria (Matendo 8:5) kisha akaacha uvuvio mikononi mwa mtume Petro naYohana (aya ya 14). Kanisa la Antiokia liliongozwa na manabii na waalimu (Matendo 13:1),ambao miongoni mwao alikuwa Sauli (Paulo). Ni waraka kwa Waefeso tu ndiounaotuonyesha kazi kamilifu ya kanisa lililofunuliwa na wajibu wake kuelezwa wazi.Kitabu cha Waefeso kina mafundisho mengi kuhusu kanisa, ufunuo wa ufasaha ambaounaonyesha mpango wa Mungu kwa kanisa. Paulo anasema (2 Kor. 12:1-4) alinyakuliwa hadimbingu ya tatu na akapokea mafunuo, akasikia maneno mengine yasiyotamkika, ambayoPg 5

haijuzu mwnadamu ayanene. Je! Kama Musa, aliweza kuonyeshwa mfano wa kanisa laBwana Yesu Kristo?EFESO 1 – SISI NI NANI KATIKA KRISTOAya ya 1: Paulo anaandika waraka huu kama mtume wa Yesu Kristo lakini wenginewanaweza kusema kuwa pia ni nabii kwa ajili ya mafunuo ya Mungu na hivyo inamuwekaPaulo kama mtume na nabii wa msingi wa kanisa la Bwana Yesu Kristo la Agano Jipya.Anawaandikia watakatifu walioko Efeso, wanaomwamini Kristo Yesu. Watakatifu niwaaminio wa kweli wa Mungu, waliotakaswa na Mungu kwa njia ya wokovu Wake.Aya ya 2: Paulo anawatumia salamu za kweli za NEEMA na AMANI kutoka kwa MunguBaba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo. Bwana anataka tupokee kutoka kwake neema naamani kila siku. Hii neema na amani ni kweli kila siku – ipokee kwa imani na shukuru Mungukwa Neema Yake na Amani anayotupatia.KANISA LIMEBARIKIWA NA BARAKA ZOTE ZA ROHONIAya ya 3-14: Paulo anatwambia sote kwa jumla, anaponukuu Baraka nyingi za rohoniambazo tumepokea kutoka kwake Kristo. Anasema kuwa Mungu ametubarikina kila Baraka za rohoni katika ulimwengu wa roho!Baraka hizo ni gani?1. Aya ya 4: Alituchagua katika Kristo Yesua. kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu;b. ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika upendo2. Aya ya 5: Alitangulia kutuchagua ili tufanywe wanawe kwa njia ya Kristo Yesusawasawa na Uradhi wa mapenzi yake;3. Aya ya 6: Ametuneemisha katika huyo Mpendwa;4. Aya ya 7: katika Yeye huyo tunao ukombozi wetu, msamaha wa dhambi, sawa sawa nawingi wa Neema yake.5. Aya ya 8:Aya ya 9:Alituzidishia hiyo neema katika hekima yote na ujuzi;Akiisha kutujulisha siri ya mapenzi yake, sawa sawa na Uradhi wakealioukusudia katika yeye huyo;Aya ya 10: kuleta madaraka ya wakati mkamilifu atavijumulisha vitu vyote katika Kristo,vitu vya mbinguni na vitu vya duniani pia- katika Yeye huyo.6. Aya ya 11: ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi.Aya ya 12: sisi tuliotangulia kumuwekea Kristo tumaini letu, tupate kuwa sifa ya utukufuwake.7. Aya ya 13: tumetiwa muhuri na Roho Yule wa ahadi aliye Mtakatifu, tukisha mwaminiyeye kwa kulisikia Neno Lake la kweli, habari njema za wokovu wetu;Aya ya 14: Roho Mtakatifu ndiye arabuni ya urithi wetu, ili kuleta ukombozi wa milkiyake, kuwa sifa ya utukufu wake (Rum 8:23: ukombozi wa miili yetu).Pg 6

Kuna baraka 7 kuu ambazo ametoa kwa ufupi. Hii sehemu ya Maandiko Matakatifu,kuanzia Aya ya 2 ni sehemu muhimu kukaririrwa.1.chaguliwa kabla ya misingi ya ulimwengu;2.Tufanywe wanawe;3.Tumekubalika;4.ukombozi - tumesamehewa;5.tumejulishwa siri;6.Tuna urithi;7.Tumetiwa muhuri na Roho Mtakatifu.PAULO ANATUOMBEA: Efeso 1:15-20Aya ya 15kulingana na imani yetu katika Bwana Yesu na upendo kwa watakatifu wote;Aya ya 16pamoja na shukrani tunatakikana kuwaombea watakatifu kwa majina!Aya ya 17Paulo anamuomba Baba wa utukufu, Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo,atupatie Roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye [Kristo],Aya ya 18na macho ya mioyo yetu yatiwe nuru:i.mjue tumaini la Mwito wake. Linganisha na ombi la Paulo katikaFilipi 3:10-14;ii.Na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu – Munguanaurithi wa utukufu ndani yetu, watakatifu wake, “Kristo ndani yetu!”(Kol 1:27);Verse 19:na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio (kwa sababutunaamini uweza wa ukuu wake ndani yetu katika Kristo): kwa kadri yautendaji wa nguvu za uweza wake.Urithi huja tu wakati mtu anapoaga. Mungu anatakatufe ili tuweze kuupokeaurithi Wake, yaani, Kristo ndani yetu. Tufe ili aishi ndani yetu, utukufu wakendani yetu na wote wauone. Tunaweza kusema, ‘ukiniona mimi umemuonaYesu?’Aya ya 20Aliotenda katika Kristo Yesu alipomfufua katika wafu akamweka mkono wakewa kuume katika ulimwengu wa roho.KRISTO YUKO WAPI? Ameketishwa mkono wa kuume wa Mungu katika ulimwengu waroho!Aya ya 21Juu sana kuliko ufalme wote (utawala) na mamlaka na nguvu (uweza) nausultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu bali katika uleujao pia.Kumbuka, hapa ndipo alipo Yesu!Aya ya 22Mungu amevitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe Kichwa juuya vitu vyote kwa ajili ya kanisa (kama kichwa juu ya vitu vyote vya Munguambavyo Mungu amepatia kanisa),Aya ya 23Ndilo Mwili Wake (sisi ni Mwili Wake)(sisi ni) ukamilifu wa Kristo anayekamilika kwa vyote katika vyote.Kama Mwili wake tunatakikana tumuthihirishe Kristo kikamilifu duniani: Je!Twaweza kusema ukiniona mimi umemuona Yesu?’Tunajifunza nini kuhusu kanisa katika sura ya kwanza ya Waefeso? Tumechaguliwa na Kristo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, yaani, kanisa wakatiwote limekuwa wazo la milele la Mungu – watu watakatifu wasio na lawama, Tumefanyika jamii ya MunguPg 7

Baada ya kukombolewa na kusamehewa Na kutiwa muhuri na Roho Mtakatifu.Mungu hufunulia kanisa kusudi lake la milele, siri, ambayo ni kuvikusanya vitu vyote katikaKristo. Ili kanisa lifahamu kusudi Lake na mpango, Mungu anatupatia Roho wa hekima naufunuo katika kumfahamu Yesu Kristo na anataka tujulishwe mambo matatu muhimu (Aya ya18-20).KANISA LIKO WAPI KATIKA KRISTO?Kanisa ni Mwili wa Kristo ambaye ameketishwa katika ulimwengu wa roho juu sana kulikonguvu zote za upinzani. Tunaanza kujifunza kuhusu mahali petu katika Kristo.Waefeso Sura ya 2: Mengi kuhusu mahali petu katika KristoAya ya 1Tulikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zetu (kwa mwanafunzianayemaanisha, Walawi 5:1 - 6:7 inatuonyesha juu ya dhambi ya hatia nasadaka ya kutoa)Aya ya 2ambazo tulizoziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu nakumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katikawana wa kuasi,Aya ya 3ambao zamani, sisi sote tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu,tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu ya watotowa hasira kama na hao wengine.(Ni wakristo wangapi bado wanatafuta kutimiza tamaa za mwili na za nia,wakisisitiza kuwa lazima waelewe mambo yote katika nia zao kabla wahusike,bila kupambanu nia ya Roho?)Aya ya 4Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuualiyotupenda,Aya ya 5hata wakati ule tulipokuwa bado wafu kwa sababu ya makosa yetu;alituhuisha pamoja ka Kristo, yaani, tumeokolewa kwa neema,Aya ya 6Akatufufua pamoja Naye, akatuketisha pamoja Naye katika Ulimwengu waRoho, katika Kristo Yesu,NEEMA YA MUNGU IMEFUNULIWAAya ya 7ili katika zamani zinazokuja audhihirishe wingi wa neema yake upitao kiasikwa wema wake kwetu sisi katika Kristo Yesu. (Mungu atadhihirisha neemaYake kupitia kwetu sisi).Aya ya 8kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ni kipawa chaMungu,Aya ya 9wala si kwa matendo.Mungu anatonyoshea NEEMA na kutupatia imani ya kuipokea hiyo imani nandipo tunavyookoka. Neema ni kile ambacho Mungu anatupatia; uweza wakewa kimungu ambayo pasipo hiyo tutahukumiwa. Neema ni kile Munguamefanya; imani ni upande wetu!Aya ya 10sisi tu kazi ya mikono yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendomema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.Pg 8

REHEMAAya ya 4AKATUFUFUAAya ya 6UPENDOAya ya 4AMETUHUISHAAya ya 5AKATUKETISHA KATIKAKRISTO Aya ya 6KWA NJIA YA IMANITUMEOKOLEWAAya ya 8KWA NEEMAAya ya 5WINGI WA NEEMA YAKEAya ya 7KAZI YA MIKONO YAKE,MATENDO MEMA YALITENGENEZWA,TUENENDE NAYO Aya ya 10Efe.2:11-13. Tumeletwa karibu na Mungu kwa nji ya damu yake Kristo;tulikuwa wageni wasio na maagano ya ahadi, tumefarakana na jamii ya israeli Mataifakatika Mwili, bila tumaini, bila Kristo hamna Mungu duniani.Aya ya 14-17 Yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja;akibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga, na kuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyosheria ya amri zilizo katika maagizo;[ambazo hatungeweza kutimiza] ili afanye wale wawilikuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani kwa njia ya msalaba (tunawezasote kuja kwa njia ya msalaba; hakuna njia nyingine; kuna mwili mmoja, kwa hivyo kanisamoja). Anakuja kwetu na kutuhubiria amani sisi tuliokuwa mbali, na amani kwa walewaliokuwa karibu. HALLELUYAH!Aya ya 18 Kwa maana kwa yeye sisi sote tumepata njia ya kumkaribia Baba katika Rohommoja.WATU WA NYUMBANI MWA MUNGU Efe.2:19-22a.19 “Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja nawatakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu.” Watakatifu ni wenyeji wa Yerusalemu yambinguni inayoshuka chini duniani kudhihirishwa, na watakatifu ni wenyeji wa nyumbani[nyumba] mwa Mungu.a.20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu Mwenyewe ni jiwekuu la pembeni.” Mitume na manabii ni huduma muhimu ambayo inaweka kanisa kwa msingisawa sawa juu ya Mwamba ambao ni Kristo. Yesu ni jiwe la msingi na tena jiwe kuu lapembeni. Wakati huduma ya mitume na manabii inapokuwa mahali pake basi kujengwa kwawatakatifu ndani ya Yesu Kristo jiwe la pembeni litalainisha – mjengo huu wa kanisa.a.21 “katika yeye jingo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe hekalu takatifukatika Bwana.” Kanisa liko linajengwa ulimwenguni kote kuwa hekalu la Mungu.a.22 “Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja kuwa maskani ya Mungu katika Roho.”Kanisa la Mungu ulimwenguni kote lina jumuisha Shirika zote, mahali ambapo watakatifuwanaushuhudia uwepo wa Mungu katika Roho.Pg 9

KANISA LA SIKU ZA MWISHO:FUNDISHO KUTOKA KWA EFESO – SEHEMU BEFESO 3: SIRI YA KRISTO NA KANISA LAKEAya ya 2Aya ya 3-4Aya ya 5Aya ya 6Aya ya 7Aya ya 8Aya ya 9Aya ya 10Aya ya 11Paulo alipokea habari ya uwakili wa neema ya Mungukwamba kwa kufunuliwa alijulishwa siri ya Kristo;Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kamawalivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi wa AganoJipyaNi siri ya Mwili, unaojumuisha Myahudi na Myunani, kuwa sisi ni washirikipamoja na warithi wa ahadi Yake iliyo katika Kristo Yesu kwa njia yainjili.[kuwa Mungu anawainua waaminio duniani kuwa watu Wake]Paulo alikuwa muhudumu wa injili kwa kadri ya kipwa cha neema ya Mungualiyopewa kwa kadri ya utendaji wa uweza Wake.Hii neema inapatikana [kwetu pia] kuwahubiri mataifa utajiri wake Kristousiopimika(wasioamini);na kuwaangaza wote wajue habari za madaraka[uwakili] ya siri hiyo, ambayotangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote katikaKristo Yesu;ili sasa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulikane na falme namamlaka kwa njia ya kanisa katika ulimwengu wa Roho,kwa kadri ya kusudi la milele alilolikusudia katika Kristo Yesu Bwana wetu.Siri ambayo Imefunuliwa Inakabiliana na UpinzaniKuhubiri kristo kunapingwa katika ulimwengu wa roho na falme na mamlaka. Unatafutakuendelea kumiliki mahali pao kutumia udanganyifu na uoga. Kuhubiri kwa injili [siriiliyofunuliwa] kuna uweza na mamlaka kufichua udanganyifu na kuvunja ngome zao zotejuu ya nia za wasioamini (soma funzo hili katika 2 Kor 10:3-6).Aya ya 12Aya ya 13hii ni kwa sababu katika yeye tunao ujasiri (wa kukaribia Mungu) katikatumaini kwa njia ya kumuamini Kristo.hii injili kuu inafaa kuteseka kwa ajili yake, maana huuleta utukufu kwetu nandani yetu.OMBI LA PILI LA PAULO KWA AJILI YETU: WAEFESO 3:14-21Aya ya 14 Paulo anampigia magoti Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo (tunafaa kupigamagoti pia).Aya ya 15 ambaye kwa Jina lake ubaba wote wa mbinguni na duniani unaitwa(tumepokea jina jipya, Jina la Mungu wetu); na sisi ni watu wa jamaa Yake.Aya ya 16-19 atujaliaye kwa kadri ya utajiri wa utukufu wake,1. kufanywa imara kwa nguvu, kwa kazi ya Roho wake katika utu wa ndani;(Matendo 1:8)2. Kristo akae mioyoni mwetu kwa imani; (2 Kor 13:5)3. tukiwa shina na msingi katika upendo, ili tupate kufahamu pamoja nawatakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina – na kujuaupendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi;4. Tupate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu (Yoh.3:34, Luka 4:18-19).Pg 10

MSTARI WA KUKARIRI: Efeso 3:20-21 “Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mamboya ajabu mno kuliko yote tuombayo au tuyawazayo, kwa kadri ya nguvu itendayo kazindani yetu; naam atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milelena milele. Amina.”SiriMungu anafunua siri na kusudi lake na anatupatia uweza wa Roho Wake, imani katika Kristona upendo wake wa karibu, akitujaza na ukamilifu wake ili kwamba hii siri ifunuliwe kwaulimwengu mzima kuona kwa njia ya Kanisa Lake.Yesu Krito ni siri!WAEFESO 4: KUENENDA KATIKA SIRI1. Jamii Ni Moja Na Inatakikana Kukaa PamojaAya ya 1kama jamaa ya Mungu, walioitwa Naye, tuenende kulingana na witotulioitiwa.Aya ya 2kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu tukichukuliana katikaupendo;Aya ya 3na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.Aya ya 4KUNA MWILI MMOJA NA ROHO MMOJA, KAMA MLIVYOITWAKATIKA TUMAINI MOJA LA WITO WETU;Aya ya 5BWANA MMOJA, IMANI MOJA UBATIZO MMOJA;Aya ya 6MUNGU MMOJA, NAYE NI BABA WA WOTE, ALIYE JUU YA YOTENA KATIKA YOTE NDANI YA YOTE.2. Kuujenga Mwili, KanisaAya ya 7 kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo.Kila mmoja wetu ana sehemu [kipimo] katika kipawa cha Kristo: utume, unabii, uinjilist,uchungaji na uwalimu. Hivi vipawa sio vya watu wachache walichaguliwa ila kwa wote(kila mmoja). Kuna neema maalum ambayo tunapokea kutokana na kila kipawa kwa kila mtuanayepokea huduma hiyo.Vivyo hivyo, vipawa vya Roho Mtakatifu vinadhihirika kwa kila mmoja wetu (1 Kor. 12:7)Mungu amampa kila mmoja wetu kipimo cha imani; (Rum 12:3) na katika Aya ya 6tumepokea kipawa cha Baba kulingana na neema aliyotupatia kila mtu binafsi.Vipawa vyote ambavyo vimeandikwa katika Agano Jipya vinapatikana kwa kila mmoja nakwa wote, kwa kadri ya neema na imani. Watu wengi bado hawajafahamu vipawa vyahuduma ambav

Aya ya 15 kulingana na imani yetu katika Bwana Yesu na upendo kwa watakatifu wote; Aya ya 16 pamoja na shukrani tunatakikana kuwaombea watakatifu kwa majina! Aya ya 17 Paulo anamuomba Baba wa utukufu, Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, atupatie Roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye [Kristo], Aya ya 18 na macho ya mioyo yetu yatiwe nuru: i.

Related Documents:

Revival is the resurrection life of Christ coursing through the Church 19. Revival is the Church crowding the upper room in mighty conquering power 20. Revival is our mouth filled with laughter and our tongue with singing 21. Revival is the falling of God’s fire upon the Church 22. Revival

Revival Preparation Guide The purpose of this guide is to help you and your church prepare for revival. It is important to note from the outset that revival is not simply a series of evangelical meetings but is the work of the Holy Spirit, Whom God has sent to guide us into all truth. You can hold revival services without ever having true revival.

FIVE STUDIES IN SPIRITUAL REVIVAL Reading: Psalm 44:1-8 2. THE MEANING AND REALITY OF REVIVAL (1) My personal position and involvement. (a) Conversion of my parents in 1947 after a lifetime of involvement in Church work. Consequent discovery of the Person of the Holy Spirit. My father joined Baptist Revival Fellowship. I was

Ministries. Pray that many girls will receive the baptism in the Holy Spirit through Girls Ministries. Pray that Girls Ministries will enable girls to develop their gifts and become godly young women. Pray for Girls Ministries leaders and workers, that t

PERSONAL REVIVAL CHECKLIST Praying through the Sermon on the Mount Matthew 5-7. 2 Jesus’ Sermon on the Mount (Matthew 5-7) clearly reveals the essential elements for personal revival. If you will live in the light of these truths, you can experience daily, continuous revival. To fail to heed

The first revival disclosure, Revival(1), was designed by the Bureau to succinct ly capture the key behaviors that can trigger revival: “The law limits how long you can be sued for a debt. Because of the age of this debt, we will not sue you for it unless you make a payment or ackn

revival styles: Tudor and Colonial. Colonial Revival architec-ture has endured and remains popular because of its simplicity in design and ornamentation, and its affordability. Examples of the revival styles can be found in many of Nashville's early suburban neighborhoods i

Loughborough College Local Offer Des Gentleman Learner Services Manager des.gentleman@loucoll.ac.uk . 2 Regulation 3 Special Educational Needs and Disability (Information) Regulations (2014) School/College Name: Loughborough College Address: Radmoor Road, Loughborough, Leicestershire Telephone Number: 01509 618375 Principal and CEO: Jo Maher Executive Lead Learner Services: Heather Clarke .