ABU HURAIRA SAHABA WA MTUME - IslamHouse

3y ago
127 Views
2 Downloads
345.47 KB
82 Pages
Last View : 14d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Maxton Kershaw
Transcription

ABU HURAIRA (r.a)SAHABA WA MTUME (S.A.W)Kimeandikwa na Dkt.Haarith bin SulaimanMfasiri:Juma Yusuf KhamisKimepitiwa na: Ustadh Talib Juma AliAFRICA MUSLIMS AGENCYZANAIBAR1431-2010 ( ا أ ه ة ) ر ا

2

ا ا ا KWA JINA LA NWENYE ENZI MUNGUMWENYE REHEMA NA RAHIMU3

4

YALIYOMOUTANGULIZI WA MTUNZI4MLANGO WA KWANZA7MAELEZO YANAYOMUHUSU NA SIRA YAKE7Jina na Nasabu Yake7Kusilimu na Usahaba Wake8Mapenzi Yake Kwa Mtume(S.A.W) na Huduma Zake Kwake9Elimu na Ubora Wake12Ibada na Taqwa Yake14Wema wake kwa mama yake na Mapenzi ya Watu Kwake17Pupa lake Juu Ya Kumfuata Mtume wa Allah(S.A.W)18Kauli na Hekima zake19Riwaya na Hifadhi Yake21Uadilifu na Hifadhi Yake25Al-marfuu na Mawquuf katika riwaya za Abu Huraira (r.a):30Kutolea kwake Umuimu Suala la Daa’wa na Kufikisha Elimu30Mbinu ya Kuhamasisha:33Mbinu ya Kutisha:34Mbinu ya Kukabili na Uwazi:34Pili-Yaliyosimuliwa toka kwake katika sifa za Ja’afar bin Abi Talib.38MLANGO WA PILI415

SHUBUHATI ZA BATILI ZILIZOENEZWA DHIDI YAKE41Shubuha ya Pili49Kupingwa na Baadhi ya Masahaba49Shubha Ya Tatu52Kushughulika kwake na shibe ya tumbo lake52Shubha Ya Nne57Kuficha kwake Baadhi ya aliyoyapokea toka kwa Mtume(S.A.W)57Na shubuha hii hujibibiwa kama ifuatavyo:57Shubha Ya Tano60Kuuzuliwa toka kwenye uongozi wa Bahrein na Omar (r.a)60Shubuha Ya Sita62Kutuhumiwa Kwake kwa Kuwaunga Mkono Bani Umayyah62MLANGO WA TATU66Sababu za Kuenezwa Shubuha kuhusu dhidi yake (r.a )66MWISHO69KIAMBATISHI71Yaliyosemwa Kuhusiana na Abu Huraira Katika Mashairi Kwa Sahaba71MSHAIRI USTADH :ABDIL JALIIL RASHIID73MSHAIRI USTADH SWALIH H’AYYAAWY766

ا ا ا UTANGULIZI WA MTUNZIShukrani zote zimemthibitikia Allah Mola wa viumbe vyote,na Sala na Salamu zimshukie Bwana wetu Muhammad alieletwa kuwani Rehema kwa waja wote na ziwashukie jamaa na Masahaba wote,ama baada ya hayo :Hakika baadhi ya watu wamezowea ima kwa ujinga au kwakufuata kwa wale kilichopekewa akili zao na matamanio ya nafsi juuya kuwatukana Masahaba wa Mtume (S.A.W) walimuamini,waliojipatia hadhi kwa usuhuba wake wakamuunga nguvu nakumnusuru, wakashiriki pamoja nae kwa kila kilichotolewa juhudikatika kujenga maendeleleo ya umma huu, utukufu na historia yakewaliojifakharishia, mataifa mengine yakajisifia kwayo, au sio waobaada matashi ya Allah Taala Uislamu usingelipatia ushindi, usingeeakwenye maeneo ya Ardhi, wala nuru yake kuenea kwenye anga, hivyoumma na kaumu zikaongoka juu ya tabia ndimi, rangi na asili zake,zikafanikiwa zilizofanikiwa juu ya nyenginezo, kwa sababu ya hayomengine katika amali njema ambayo nafasi hii haitoshi kuyataja,Allah (S.W) aliwasifu, kuwaridhia kwake na malipo yake makubwakatika Aya nyingi katika Qur’ni Tukufu, na miongoni mwa hizo ni:Kauli yake Taala { Na waliotangulia wa awaliMuhajirina na Ansari ambao waliwafuata kwa wema,amewaridhia na wao wamemridhia na amewaandaliazinazopitiwa na mito chini yake waishi humo milele, hukokufuzu kuliko kukubwa }[At Tawbah:100]katikaAllahPepondikoNa kauli yake Taala {Hakika Allah ameshawaridhia waumini palewalipokupa ahadi ya utii chini ya mti hivyo Allah alishaelewayaliyomo ndani ya nafsi zao akawateremshia utulivu juu yao nakuwalipa ushindi uliokaribu}[Al Fat-h 18].7

Na kauli yaake Taala {Hawawi sawa miongoni mwenu yulealiehama kabla ya ukombozi na kupigana vita: hao wanayo darajakubwa kuliko wale waliotoka baadae na wote Allah amewaahidimalipo mema; na Allah kwa yale muyafanyayo ni Mwenye kuwa nahabari} [Al Hadiid:10] Kama walivyostahiki sifa za Nabii (S.A.W), nakujitukuza kwa sababu yao na kuwafanya bora juu ya wengine kwahadithi nyingi, miongoni mwao ni, kauli yake (.SA.W) ( Watu waliobora ni wa karne yangu, kisha wanaowafuatia wao, kisha ambaowanaowafuatia wao, kisha ambao wanaowafuatia wao) Hadithi 1Na kauli yake (( Musiwatukane masahaba wangu, naapa nayule ambae nafsi yangu iko mikono mwake lau mmoja wenu atatoadhahabu mfano wa Uhud asingelifikia gao la mmoja wao wala nusuyake))2Na kauli yake (Allah Allah katika masahaba wangu,musijewafanya malengo ya matusi, aliewapenda basi ni kwasababu yamapenzi yangu na aliewachukia ni kwa sababu ya kunichukia mimi,na aliewaudhi basi ameniudhi mimi na alieniudhi mimi basiamemuudhi Allah na aliemuudhi Allah basi anakaribia kumnyakua)3Na pamoja na mapenzi ya Allah Taala kwao na kuridhiwa nao,na kutukuzwa kwao na Nabii (S.A.W) na kuwafanya wabora kulikowengine katika wana wa umma huu, lakini ndimi za bandiazimewatukana, na kalamu za mamluki, zimetilia nguvu juu ya idadi yamasahaba miongoni mwao waliotangulia mongoni mwao wa awali shiawasiyoyafanya, wakawasingizia kwa yale ambayo wao wametakasika1-Al Bukhary 35/3 Kitaabu Fadhw’aailus Swa’haaah, na Muslim 185/72Al Bukhary 21/7, Muslim 188/7 .3Ibn Maajah 189/88

nayo, bila ya kujali Aya za Qur’an zenye kuwatakasa na zenyekuwaridhia, na Hadithi sahihi za Mtume (S.A.W) zenye kunyanyuaubora wao, zikitegemea riwaya za kihistoria za kubuni, wanaojifanyawaislamu wakaupaka matope kwazo toka kwa maadui zake,matamanio ya nafsi yakafanyia kazi kulikuza mpaka zikawa niuhakika au kama zilivyowapitikia, pamoja na kwamba hayana asilikwenye, bali ni dhana mbovu na ubunifu tu, zilizochipuka tokakwenye fahamu mbovu na upelekeaji matokeo ya makosa.Na katika nyaraka hizi nitazungumzia kuhusiana na mmoja waMasahaba watukufu waliotafunwa na ndimi ovu na kuzushiwa uzushiwaliopenda, na madai batili yaliojazwa uongo na ubaguzi na uadui.Huyo ni sahaba wa Mtume (S.A.W)(Abu Hurairah-r.a-) Sahaba,mtumishi wake na hafidhi wa Sunna zake (SAW).Nitajitahidi kumuelezea, usuhuba wake na Mtume (S.A.W), najuhudi zake katika kuitumikia Sunna ya Nabii (S.A.W ), hivyonitaonyesha uongo na shubuha zilizoenezwa dhidi yake, kwa lugha yauwazi, na kuepusha kila ugumu, nitafanya ufupisho na kuwa mbali naurefushaji, ili kuweza kufahamika na kila mmoja kwa daraja yake, nanategemea msaada na tawfiqi ya kwa Allah kwa yote haya.Doktori Harith bin Sulaiman15 Muharram 1420H - 1/5/1999M9

10

MLANGO WA KWANZAMAELEZO YANAYOMUHUSU NA SIRA YAKEJina na Nasabu Yake4Watu wametofautiana katika jina la Abu Huraira (r.a) kabla yakusilimu kwake kwenye kauli kadha imesemwa: Abdu Shams binSakhar, kasemwa Abdi Amr bin Abd Ghunum. Ikasemwa zaidi yahiyo; kama walivyo tofautiana kwenye jina lake baada ya kusilimukuna kauli mbali mbali, mashuhuri yao ni Abdurahman bin Sakhar.Imesimuliwa toka kwake kwamba amesema "Jina langu lilikuwaAbdu Shams, katika zama za ujahili, Mtume (S.A.W) akaniitaAbdurahman5 . Na lolote liwalo jina lake ni kwamba kun-ya yake AbuHuraira ndio limezidi jina lake, akawa hajulikani ila kwalo na siojengine.Imesimuliwa sababu ya kuitwa kun-ya hiyo, ni kwambaamesema: "Nilikuwa nikichunga kondoo wetu, na nilikuwa na kipakakidogo, basi nikawa usiku nakiweka kwenye mti, ukifika mchanakinanifuata na kucheza nacho hivyo nikaitwa Abu Huraira.Ama nasabu yake wanahistoria wanasema anatoka katikakabila la Azdy la Kiyemen, alifariki Abu Huraira 57 au 58 au 59Baada ya Hijra akiwa na umri wa miaka sabini na nane, na kauli yamwisho ameidhoofisha AIhafidh Adhahabiy, na Ibn Hajar yeye piakwa kutegemea kauli ya mwanzo, kifo chake kilikuwa MadinatuMunawara, na inasemekana Aqiiq, akabebwa mpaka Madina na4At Tirmidhiy katika As Sunan 350/5 na Al Hakim katika Mustadrak 506/35Al Hakim katika Mustadrak 507/3,Ibn Hajar katika Iswaba 202/4 na lbn Abdil Barr katika Al Istiia’ab ,Hamish ya Iswaba.205/4 na baada ya hapo.11

kuzikwa Baqii na katika wasindikizaji wake walikuwa Abdullahi binOmar, na Abu Said Alkhudriy(R.A).6Kusilimu na Usahaba WakeAbu Huraira alisilimu mwaka wa Khaibar katika mwezi waMuharram mwaka wa saba Hijriya, na kushuhudia vita hivyo pamojana Mtume (S.A.W). Kutoka kwa Said ibn Musayyib, toka kwa AbuHuraira amesema (Tulishuhudia pamoja na Mtume siku yaKhaibar )7 Toka kwa Abuilghaith, toka kwa Abu Huraira, amesema(Tulitoka pamoja na Nabii (S.A.W) kuelekea Khaibar Allahakatufungulia) Hadithi8Kama alivyoshuhudia vita vyengine katika vita vilivyokujabaadae,na kwa hivyo akajipatia fadhila za Jihadi katika njia ya Allahzaidi ya ile hadhi ya usahaba wa Mtume (S.A.W), kwa vilealisuhubiana nae tokea siku hiyo mpaka kifo chake (S.A.W), na nimuda usiozidi miaka minne9,alikamatana nae katika muda huomkamatano uliokamilika alihama kwao kwa ajili ya kuchukua tokakwake na kusoma, hivyo mkono wake upo pamoja na mkono waMtume (S.A.W), anazunguka pamoja nae popote alipozunguka,anakwenda pamoja wala haachani nae popote nyumbani wala safarini,kwani hakushughulishwa na kuuza, kununua wala kuchunga mali.Imesihi kwamba amesema "Hakika nyie mnadai kwamba AbuHuraira kazidi kwa mapokezi ya hadithi toka kwa Mtume (S.W.A)Wallahi ni ahadi, hakika mimi nilikuwa masikini aliyesuhubiana naMtume (S.A.W) kwa kujaza tumbo langu, na Muhajirina walikuwa6 Al Hakim katika Mustadrak 508/3 na Adh Dhahabiy kwenye Siyar Aa’laam An Nubalaa 262-267,A Ibn Hajar katika Iswaaba 210/4, lbn Abdil Barrkatika Al Istiiaab ,Hamish ya Iswaba.209-210/4. na A’qiiq ni umbali wa Meli kumi toka Madina,7 AlBukhariy 74/5.8 AlBukhariy katika Fat-h 225/6, Muslim Sherhun Nawawiy 42-43/1,na Ahmad 225/19 Muslim Sherhun Nawawiy128/212

wakishughulishwa na kofi za sokoni, na Ansari nao wakishughulishwakusimamia mali zao, mimi –siku moja-nilihudhuria majlisi ya Mtume(S.A.W) akasema ((Ni nani atakaetandika mtandio wake mpakanimalize maneno yangu, halafu alikamate, asisahau kamwe alichosikiatoka kwangu?. mimi nikatandika burda mpaka akamalizamazungumzo yake kisha akalikamata kunipa, basi naapa na YuleAmbaye nafsi yangu iko kwenye Mikono yake sikusahau chochotenilichokisikia toka kwake baada ya hapo.)10Na kwa hili, kwamba Abu Huraira (r.a) aligubikwa na barakaza usuhuba wake na Mtume (S.A.W), kukamatana nae,kumuhudumikia, na ndio akapata baraka ya usuhuba, Allah (S.W)akamruzuku hifadhi ya aliyoyasikia toka kwa Mtume (S.A.W) nakutosahau .Mapenzi Yake Kwa Mtume (S.A.W) na Huduma Zake KwakeAbu Huraira (r.a) alikua mwingi wa mapenzi kwa Mtume(S.A.W), aliitilia nguvu imani kwake, akajikurubisha kwake kwa lilelinalomridhisha, hufurahi kwa furaha zake, akihuzunika kwa huzunizake, akiumizwa na kutukanwa Mtume (S.A.W), hata yakiwa matusiyanatoka kwa mtu wa karibu zaidi kwake, imesihi toka kwakekwamba amesema: "Nilikua nikimlingania mama yangu kwenyeuislamu akiwa mshirikina, basi siku moja nikamlingania, akasemakuhusu Mtume (S.A.W) ninayoyachukia, hivyo nikamwendea Mtume(S.A.W) huku nalia, nikamwambia Ewe Mtume wa Allah nilikuwanikimlingania mama yangu kwenye uislamu, lakini anakataa, leonimemlingania akasema kuhusiana nawe yanayonikera, hebuimuombe Allah amuongoe mama wa Abu Huraira”Akasema Mtume (S.A.W) "Ewe Allah muongoe mama wa AbuHuraira”.10 AlBukhariy 248/4-Al Buyuu’u,Muslim Sherhun Nawawiy 52-56/16 Fadhwaailus Swahaabah, na matamshi ni ya Bukhaariy.13

Nikatoka nikiwa na furaha kwa dua ya Nabii (S.A.W.)nikenda mpaka mlangoni akawa mkali, akasikia sauti ya miguu yangu,akasema :hapo hapo Ewe Abu Huraira na nikasikia, mchuruziko wamaji, akakoga na kuvaa nguo yake na kujitanda mtandio wake, harakaharaka akafungua mlango, na akasema Laa ilaaha illa Allahnashuhudia kwamba Muhammad ni Mtumwa wa Allah na Mtumewake.Akasema;’Hapo nikarejea kwa Mtume (S.A.W), nikamjianikilia kwa furaha, akasema nikamwambia Ewe Mtume wa Allahfurahi, hakika Allah ametakabalia dua yako na amemuongoa mamawa Abu Huraira, amkashukuru Allah, na kumsifu, akasemakheri".Hadithi11Hadithi hii inatuonesha hali ya mapenzi ya Abu Huraira (r.a)kwa Mtume (S.A.W) na kilio chake anapotukanwa,kwa kumtukuzaMtume (S.A.W) Aba Hurairah(r.a)kwa kumtekelezea ombi lake kwadua ya kuongolewa mama yake alieongolewa na Allah kwa baraka yadua,kitu ambacho kiliongeza furaha za Abu Huraira (r.a),na kufurahina kulia kwake kwa hilo.Alikua akiwasilisha mapenzi yake kwa Mtume (S.A.W) kwamfano wa kauli yake ’Ameniusia kipenzi changu (S.A.W) juu yamambo matatu, nisiyawache mpaka nitakapokufa: kufunga siku tatukatika mwezi, sala ya dhuha na kulala baada ya witri’12Na kauli yake nimemsika kipenzi changu akisema: "Pambo lamuislam litafikia pale udhu unapofikia’.1311Muslim Sherhun Nawawiy 51-92/16,Fadhwaailus Swahaabah,na Ibn H’ibbaan 142/8, na lafdhi ni ya Muslim.12 AlBukhariy 54/2na Muslim 158/2 na matamshi ni ya Bukhaariy13 Ahmad;Al Musnad 27/17,na muradi wa pambo ni nuru.14

Kama ambavyo akielezea pupa la kukamatana na Mtume(S.A.W), na utumishi wake kiasi kwamba hawachii fursa yakumuhudumikia Mtume (S.A.W) ila akiichukua, katika hayo ni:kwamba yeye alikuwa akimbebea Mtume (S.A.W) kiriba cha ngozichenye maji kwa ajili ya udhu wake na haja yake, basi mara mojaalipokuwa akimfuata na kiriba hicho, akasema nini huyu?Akamwambia Abu Huraira, akamwambia niletee mawe nistanjie,usiniletee mfupa, wala kinyesi cha mnyama, basi nikamletea mawenabeba kwa ncha ya nguo yangu, mpaka nikayaweka pembeni mwake,kisha nikaondoka).Hadithi. 14 Katika hayo ni yaliyosimuliwa na AbuZuraa bin Amr bin Jariir toka kwa Abu Huraira, amesema “Mtume(SAW), aliingia chooni nikampelekea kitungi cha maji, basi akastanji,na akapangusa mkono wake ardhini, na nikampelekea kitungichengine, akatawadhia’ 15Katika hayo vilevile ni aliyosimulia Mujahid toka kwa AbuHuraira (r.a) amesema Alinipita Mtume wa Allah (S.A.W) akaitambuanjaa kwenye uso wangu, akanita Ewe Abu Huraira? Nikamuitikialabaika ya rasulallahi nikaingia pamoja nae nyumbani akaona maziwakwenye chombo, akasema ‘Mumeyapata wapi haya? Akaambiwa"amekuletea Fulani", akasema ”Ewe Abu Huraira nenda kwa watu waSuffa ukawaite” Watu wa Suffa ni wageni wa uislamu, wasio najamaa wala mali. Mtume wa Allah (S.A.W) akiletewa sadakaakiwapelekea, wala hachukui chochote, na akiletewa zawadi akitumia,na kuwashirikisha wao, basi nikachukizwa kunipeleka kwao,nikasema nilitarajia nipate maziwa haya yanitie nguvu, na ni maziwakiasi gani haya kwa watu wa Suffa, na utiifu kwa Allah na Mtumewake ni lazima, basi nikawaendea wakaja na kuitikia wito,walipokwishakaa, akiniambia "Yachukue Abu Huraira uwape” basinikawa nawapa, mtu-anakunywa mpaka kumtosha mpaka14 Bukhariy 240/,15 Ahmad : Al Musnad 239 /1515

nikawaendea wote, na nikampa Mtume wa Allah (S.A.W) basiakanyanyua uso wake kwa tabasamu, akasema: ”Nimebakia mimi nawewe” nikawambia kweli Ewe Mtume wa Allah (S.A.W),Akaniambia "kunywa" basi nikanywa akaniambia "kunywa”nikanywa, basi hakuacha kuendelea anasema "kunywa" nakunywampaka nikasema "Naapa kwa yule ambae amekutuma kwa haki sinanafasi ya kuyaweka hivyo akayachukua akanywa yaliyobaki.” 16Riwaya hizi na kabla ya hizi zinatuonesha pupa la AbuHuraira juu ya kumhudumia Mtume wa Allah (S.A.W) utii wake,kama zinavyotuonesha upeo wa kumtegemea kwake Mtume wa Allah(S.A.W) na kuwapendelea wao kuliko nafsi yake, kiasi kwambahakunywa maziwa aliyopewa zawadi pamoja na kuyahitajia Mtumewa Allah (S.A.W) ila baada ya kunywa wao wote, na wakashiba kwabaraka za Mtume wa Allah (S.A.W) na hilo sio geni kutoka kiongozi,mwenye tabia adhimu.Elimu na Ubora WakeAbu Huraira alikuwa katika maulamaa wa Masahaba nawabora wao, hilo linashuhudiwa na riwaya za wengi miongni mwaowaliosimulia toka kwake, na kwenda kwake katika Fatwa, kwaniMasahaba waliosimulia toka kwake miongoni mwao ni, Zaid binThabit, Abu Ayoub Al- ansari, Abdullah bin Abbas, Abdullah binZubeir, Ubayya bin Kaab, Jabir bin Abdillaah, Aisha, Musawir binMakhramah, Abu Musal Ash-ariy, Anas bin Malik, Abu Raafiimuachwa huru wa Mtume wa Allah (S.A.W) na wengineo katikaMasahaba (r,a); katika matabiina ni Qabiswa bin Dhuaib, Sai’d bin AlMusayyib,Urwa ibn Az ubair, Salim bin Abdillahi bin Omar, AbuSalamah bin Abdir Rahman, Abu Saleh Asamman, Ataa bin AbiiRabaah, Ataa bin Yasaar, Mujahid, Ashaabiy, Ibn Siryn Ikrimah,Naafii maula wa Ibn Omar, Abu Idris Al Khawlaniy. na wengineo16 Adhdhahabiy As Siyar Aa’laam An Nubalaa 591-592/2, asili ya riwaya hii imo kwenye Bukhary 179-180/7. Kitaab:Ar Riqaaq , na As Suffa ni pahalaalipopaandaaMtume wa Allah (S.A.W)kwa ajili ya mafukara wa Kihajirina.16

katika Matabiina (r.a)17 Amesema Bukhariy (r.a);’Wamesimulia tokakwake watu mia nane au zaidi.18Kama walivyosimulia toka kwake, walikuwa wakimwendeakuuliza masuali na fatwa, na wengine wapo waliomtanguliza katikamasuala hayo na kumuafiki katika aliyoyasema.Amesema Al-shaafii (r.a) "Ametupa habari Maalik, toka kwaMaalik, toka kwa Yahya bin Saiid toka kwa Bukair bin Al Ashaji,toka kwa Muawiyah bin Iyaash Al Answari" Kwamba yeye alikuwaamekaa pamoja na Ibn Azubair, akaja Muhammad bin Al Bukair,akauliza kuhusu mtu aliewacha talaka tatu kabla ya kuingia ndani basiakampeleka kwa Abu Huraira (r.a) na Ibn Abbas nasi tulikua kwaAisha, akaenda akamuuliza ibn Abbas akamwambia Abu Huraira"Mpe fatwa Ewe Abu Huraira, amekujia akiwa na shida, akasema"Moja inamtenganisha nae na tatu zinamuharamishia, mpaka aolewena mume asiekuwa yeye, na akasema Ibn Abbas mfano wa hayo19. Natoka kwa Azzuhriy, toka kwa Salim, kwamba amemsika Abu Huraira(r.a) 20akisema "Kaumu wenye kuhirimia waliniuliza kuhusiana nawasiohirimia waliowapa zawadi kiwindwa, nikawaamrisha wakile.’Na toka kwa Ziyaad bin Maynaa, amesema "Walikua IbnAbbas Ibn Omar, Abu Said, Abu Huraira na Jabir pamoja mfano wao,wakitoa Fatwa Madina toka kwa Mtume wa Allah (S.A.W) Tokeaalipokufa Othman mpaka walipokufa, na watano hao Fatwaziliendelea.2117 na Al Haakim :Al Mustadrakm 513/3, Adhdhahabiy: As Siyar Aa’laam An Nubalaa 580 -585/218 Adh Dhahabiy:Tadhkirat ul Huffaadh’36/1,na Ibn Hajar :Al Isw’aabah205/419 Maalik :Al Muwattw’a na As Shaafi’i: AL Musnad36/3.20 Maalik :Al Muwattw’a 351-352/121Adhdhahabiy AsSiyar Aalaam An Nubalaa 606-60717

Nae Adhahabiy amesema "Na ikutoshe kwamba mfano waIbn Abbas anamuekea adabu na kumwambia "Ewe Abu Huraira toaFatwa” 22Ibada na Taqwa YakeAbu Huraira (r.a) alikua maarufu kwa ibada, taqwa, na kilalililomkaribisha kwa Allah (S.W), Vipi isiwe hivyo, wakatiamesuhubiana na Kigezo Chema katika ibada, na kumuonyeshanamna afanyavyo Jihadi nafsi yake kwenye ibada mpaka miguu yakeikavimba (S.A.W), hivyo alikua akifanya ibada kwa wingi miongonimwa Sala, Saumu kusoma Qur’ani, na Sala za usiku. Toka kwaHammaad toka kwa Abbaas Al Jaryriy amesema "Nimemsikia AbaUthmaan An Nahdy Abu Huraira aliwaalika ugeni watu saba, basiakawa yeye, mkewe na mtumishi wao wanapokezana usiku sehemutatu, huyu anasali na anamuasha huyu, halafu analala huyu, akasema,nikasema “Ewe Mtume wa Allah (S.A.W) wewe unafungaje? akasemaama mimi nafunga siku tatu katika mwanzo wa mwezi, iwaponitatokewa na jambo huwa mwisho wa mwezi”23Na toka kwa Ibn Jarir amesema: amesema Abu Huraira (r.a)"Hakika mimi huugawa usiku wangu sehemu tatu, sehemu ya Quran,sehemu ya kulala na sehemu ya kukumbukia hadithi za Mtume waAllah (S.A.W) 24Na imesihi kwamba amesema:”Ameniusia kipenzi changu juuya mambo matatu; Saumu siku tatu katika kila mwezi, rakaa mbili zadhuha na nasali witri kabla sijalala” 2522 Adhdhahabiy AsSiyar Aalaam An Nubalaa 609/223 Ahmmad :Al Musnad 260/ 1624 Ibni Kathiir:Al Bidaayah wa An Nihaaya 133/825 Adhdhahabiy AsSiyar Aalaam An Nubalaa 611/2 na Ibni Kathiir:Al Bidaayah wa An Nihaaya 113/218

Na kutoka kwa Hamaad bin Salamah, toka kwa Hisham binSaid bin Zaid Al Answariy, toka kwa Shurahbil kwamba Abu Huraira(r.a) alikuwa akifunga Jumatatu na Al Khamis.26 Na zaidi ya hayoalikua mwingi wa Tasbiih na Alhamdu Lillahi Taala juu neema yaUislamu na nyenginezo katika neema alizomneemesha Allah Taala,kama alivyokua mwingi kumuogopa Allah (S.W) mwingi wakutahadharisha Moto –Allah atukinge nao-.Toka kwa Maimun bin Maisarah amesema “ Kila siku AbuHuraira (r.a) alikuwa daima akipaza sauti mara mbili kwa kusema"Usiku umekwenda, na mchana umekuja, na jamaa wa Firaunwametiwa motoni basi hakuna atamsikie akisema hivyo ila atajikingakwa Allah na moto".27 Na imesimuliwa toka kwa IbnMubarak:”Hakika Abu Huraira alilia katika maradhi yake, akaambiwaunalizwa na nini? Akasema "Silii juu ya dunia yenu hii, lakini juu yayatakayokua baada ya yangu, na uchache wa zawadi zangu, nakwamba mimi nimeingiliwa na jioni katika kupanda juu, namaangukio yake ima ni juu ya Pepo au Moto, basi sielewi ni kwa ipiya hizo nitachukuliwa , ”2

Shukrani zote zimemthibitikia Allah Mola wa viumbe vyote, . bila ya kujali Aya za Qur’an zenye kuwatakasa na zenye kuwaridhia, na Hadithi sahihi za Mtume (S.A.W) zenye kunyanyua . uwazi, na kuepusha kila ugumu, nitafanya ufupisho na kuwa mbali na urefushaji, ili kuweza kufahamika na kila mmoja kwa daraja yake, na

Related Documents:

MLANGO WA KWANZA 7 MAELEZO YANAYOMUHUSU NA SIRA YAKE 7 Jina na Nasabu Yake 7 Kusilimu na Usahaba Wake 8 Mapenzi Yake Kwa Mtume(S.A.W) na Huduma Zake Kwake 9 Elimu na Ubora Wake 12 Ibada na Taqwa Yake 14 Wema wake kwa mama yake na Mapenzi ya Watu Kwake 17 Pupa lake Juu Ya Kumfuata Mtume wa Allah(S.A.W) 18 Kauli na Hekima zake 19 Riwaya na Hifadhi Yake 21 Uadilifu na Hifadhi Yake 25

69 PG18210S Abu Rahma Jeries 70 PG15112S Abu Rashed Nadim 71 PG15113S Abu Rmeileh Said Maher 72 PG17313S Abu Rumhin Yara 73 PG18211S Abu Rumhin Layan 74 PG16112S Abu Saada Raed 75 PG18212S Abu Said (Kabiyi) Erez . 87 PG19476S Abu-Taleb Abdel Rahman Ahmed 88 PG19477S

PERIWAYATAN ABU KHURAIRAH DALAM KITAB SHAHIH BUKHARI ( Aplikasi teori Tahammul wa ada al- Hadits) A. Pendahuluan Abū Hurairah adalah salah satu dari beberapa tokoh sahabat yang diberi gelar al-mukatsirūn fī al-hadīs, yaitu orang yang banyak meriwayatkan hadis. Posisi Abū Hurairah memang sangat kontroversial.

Al-Miṣri, Abu ‘Ammar Maḥmūd, Terj. Umar Mujtahid, Biografi 35 Sahabat Nabi Saw, Umm Al-Qurā, Jakarta, 2014. Al-Miṣri, Al-Allāmah Abū al-Faḍl Jamāluddīn Muḥammad ibn Mukram Ibn Manẓūr al-frīqī, Lisan Al-‘Arab, Dār al-Fikr, Beirut, 1990. Al-Qurṭubī, Abū Abdullāh Muḥammad bin Aḥmad bin Abu Bakr, Terj.

1. Busuk Lunak Bakteri (Bacterial Soft Rot) Ciri Kerusakan : bahan jadi lunak, lembek, bau masam Komoditi yg diserang : bwg. merah/putih, wortel Jenis : Erwinia carotovora, Pseudomonas marginalis, Clostridium, Bacillus spp. 2. Busuk Kapang Abu-Abu (Gray Mold Rot) Ciri Kerusakan : Miselium kapang abu-abu, kerusakan akibat kelembaban tinggi dan .

OMAA/AUH ABU DHABI, UAE ABU DHABI INTL JEPPESEN.AIRPORT.BRIEFING. 2.1. CAT II/III OPERATIONS RWYs 13L and 31R approved for CAT II and RWY 31L for CAT II/III operations, special aircrew and ACFT certification required. 2.2. RWY OPERATIONS To reduce RWY occupanc

OMAA/AUH :: JEPPESEN ABU DHABI, UAE ABU DHABI INTL &@&-CAT I1 VOR DME ILS Rwy 31 ATIS I ABU DHABi Radar (APP)

American Math Competition 8 Practice Test 8 89 American Mathematics Competitions Practice 8 AMC 8 (American Mathematics Contest 8) INSTRUCTIONS 1. DO NOT OPEN THIS BOOKLET UNTIL YOUR PROCTOR TELLS YOU. 2. This is a twenty-five question multiple choice test. Each question is followed by