MAFUNDISHO YA BIBLIA KUHUSU UBATIZO

3y ago
584 Views
22 Downloads
583.40 KB
121 Pages
Last View : 6d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Ciara Libby
Transcription

MAFUNDISHO YA BIBLIA KUHUSU UBATIZOBobby Jamieson1

Mafundisho Ya Biblia Kuhusu UbatizoHakimiliki 2018 Ekklesia AfrikaHaki zote zimehifadhiwaKilichapishwa mara ya kwanza kwa lugha ya Kiingerezamwaka wa 2016 na B&H Publishing Group Nashville,Tennessee.Kuchapishwa mara ya kwanza kwa lugha ya Kiswahili mwakawa 2018 na Ekklesia Afrika, Nairobi Kenya.Kutafsiriwa na: Ronald KogoKuhakikishwa na: Milton Isiye na Abel LugailaNukuu za Biblia zimetolewa katika Biblia Habari Njema kwawatu wote, ambayo imechapishwa na Bible Society ofTanzania na Kenya mwaka wa 20012

YaliyomoMaelekezo ya msululu wa vitabu hiviUtanguliziSura ya Kwanza: Ubatizo ni nini?Sura ya Pili: Je, ni nani anapaswa kubatizwa?Sura ya Tatu: Je, watoto wanapaswa kubatizwa?Sura ya Nne: Kwa nini ubatizo unahitajika ndipomtu awe mshirika wa kanisa?Sura ya Tano: Je, ni wakati gani mtu anawezakubatizwa, lakini awe kweli hajabatizwaSura ya Sita: Je, ubatizo unapaswa kufanywa kwanjia gani na makanisa?3

Maelekezo ya msululu wa vitabu hiviMaisha ya mkristo ni maisha anayoishi kwa ufahamukwamba yeye ni mshirika wa kanisa. Ufahamu huu, ndiyomwongozo wa msululu wa vitabu tunavyovichapisha.Kwa mfano, kulingana na Biblia, Meza ya Bwanahuadhimishwa katika jamii ya kanisa na wala si jukumu lamtu binafsi. Wito wa kusambaza habari njema si jukumula mtu binafsi, bali ni jukumu lililopewa kanisa kwajumla. Mamlaka ya kanisa hawajapewa tu viongozi, balipia washirika wanaitwa kutekeleza mamlaka katikakanisa. Pia, kulingana na Biblia, kila mshirika ana kazi yakufanya.Kila kitabu katika msululu wa vitabu vyetu, kimeandikwakikilenga mshirika wa kawaida. Ikiwa maisha ya mkristo,ni maisha ambayo anaishi akifahamu kwamba yeye nimshirika wa kanisa, yeye lazima awe amebatizwa nakuletwa katika ushirika wa kanisa. Kwa sababu hii,mshirika ana jukumu la kufahamu mafundisho ya vitabuhivi ambavyo tunavichapa.Kama tu vile Yesu anaamuru kanisa kueneza na kulindaujumbe wa injili, vivyo hivyo, anakuamuru ueneze naulinde watu wake ambao wamezaliwa kwa nguvu za4

ujumbe wa injili, yaani kanisa. Msululu wa vitabu hivivitakueleza wazi jinsi ya kufanya kazi hii.Wewe unafananishwa na mwekezaji katika huduma yainjili ya Yesu Kristo. Je, mwekezaji hufanya nini? Yeyeau wao hujifunza kuhusu biashara, soko na wapinzaniwao katika kazi ambayo wanaekeza ndani. Wao hufanyahivi kwa sababu wanataka kupata faida kubwa katikabiashara. Mkristo amewekeza maisha yake katika ujumbewa Injili. Kwa hivyo sababu ya msululu wa vitabu hivi nikwamba, uweze kuleta mazao mengi katika ufalme waMungu kupitia kwa kanisa lako.Je, uko tayari kuanza kazi yako?Jonathan Leeman,Mhariri wa msululu wa vitabu hivi5

UtanguliziMsomaji wangu, tujifunze kuhusu ubatizo. Kitabu hikiambacho ni kidogo, kina mambo mengi ambayo ni yamuhimu sana kwako haswa ikiwa wewe ni Mkristo.Ikiwa wewe umeokoka, ni furaha yangu kwambaunasoma kitabu hiki. Pia kuna vitabu vingi vingineambavyo ningekuhimiza usome vitabu vinne vya injili nakitabu cha Greg Gilbert ambacho kinaitwa, “Yesu ninani?” Pia ninakuhimiza kwamba wewe na rafiki wakomchukue muda msome Biblia kwa pamoja, na mjadilikuhusu inamaanisha nini kumfuata Yesu.Ningependa kuzungmza na mtu ambaye ameokoka lakinihajabatizwa. Huenda hujui ubatizo inamaanisha nini. Piahuenda unajua maana ya ubatizo, lakini unajiuliza kwanini unapaswa kubatizwa. Labda unajiuliza kama kweliubatizo ambao ulibatizwa nao, ulikuwa wa kweli! Labdaulibatizwa ukiwa mdogo, na hukumbuki kama kweliulikuwa umeokoka au la. Kitabu hiki kinashughulikiamambo haya yote.6

Kusudi langu ni kwamba, ikiwa wewe ni mkristo lakinihujabatizwa, ninaomba kwamba mafundisho ya kitabuhiki yatakushawishi ubatizwe.Kikundi cha pili ambacho ninalenga, ni wale wakristoambao wanataka kujifunza zaidi kuhusu ubatizo. Huendaumebatizwa, lakini unataka kufahamu zaid kuhusu amrihii ya Yesu Kristo kwa kanisa lake. Huenda unatakakuelewa ili uweze kumweleza mwenzako kuhusu jambohili la ubatizo. Ni ombi langu kwamba kitabu hikikitaweza kuyajibu maswali yako yote.Ningependa kikundi kingine kisome kitabu hiki niwachungaji. Mara kwa mara wachungaji ndiyo huwawanafanya kazi hii ya kuwabatiza washirika wao.Wachungaji huwa wanawasaidia sana washirika waokufahamu ubatizo ni nini na unapaswa kufanywa kwa njiagani. Pia wachungaji huwa wanadhihirisha kama kwelimtu kuwa mshirika wa kanisa anahitaji kubatizwa au la.Ninajua kwamba hatutakubaliana katika mambo yote yakitabu hiki. Kuhusu ubatizo kuna mambo kadhaa ambayowakristo huwa hawakubaliani nayo. Lakini ninaombakwamba kitabu hiki kitakufaidi sana, hata katika yaleambayo hukubaliani nayo.7

Katika kitabu hiki, tunauliza maswali, je, ubatizo ni nini?ni nani ambaye anapaswa kubatizwa?, Tutazingatia swalihili, je, watoto wachanga wanahitaji kubatizwa? Piatunaona ubatizo ambao si wa kweli. Halafu tutatazamajinsi makanisa yanapaswa kuendesha mambo ya ubatizo.Asante sana kwa kuchukua muda wako na kusoma kitabuhiki. Ninaomba kwamba kitakusaidia katika mwenendowako na Yesu, na katika kuwasaidia wengine.8

Sura ya KwanzaUbatizo ni nini?Je, utafanya nini ikiwa ulikuwa kando ya bwawa lakuongelea, kisha rafiki yako akuingize katika bwawahilo? Je, utafanya nini? Utapuuza kitendo chake?Mfano wa pili, utafanya nini ikiwa rafiki yako atakuja naakuingize ndani ya maji, halafu aseme, “sasaumebatizwa!” Hata kama haujui mengi kuhusu ubatizo,nadhani utakuwa na shauku ya kwamba, ijapokuwakitendo hicho ni cha nadra sana, rafiki yako atakuwaamekosea. Haujabatizwa; kile ambacho kimefanyika nikuwa umeingizwa ndani ya maji.Je, nini kinapaswa kufanyika ndipo ubatizo uwe wakweli? Ukweli ni kwamba, ubatizo wa kweli si jambo lakushangaza, bali ni jambo ambalo litafanyika ukiwaunajua na ukiwa umejitolea mwenyewe. Je, kunamakanisa ambayo yanawabatiza watoto wachanga?Ukweli ni kwamba watoto huwa hawajitoi kubatizwa,wao hubatizwa bila idhini yao. Je, yule ambaye anabatiza,anapaswa kuwa mchungaji au mtu yeyote? Je, mahali pa9

kufanyia ubatizo, panapaswa kuwa wapi, kanisani aumahali pa popote?Ubatizo ni Sura hii itajibu swali hili, “Ubatizo ni nini?” Nitaanzakwa kueleza ni nini Biblia inafundisha kuhusu ubatizo,halafu pia nitaeleza mambo machache kuhusu kileambacho si ubatizo. Kama hajabatizwa kwa sababuhaukuwa na uhakika ya ubatizo ni nini, ni tumaini langukwamba hii sura itakusaidia kufahamu ubatizo na kuwezakutii amri ya Yesu kuhusu ubatizo.Ubatizo ni kitendo cha kanisa kuthibithisha na kuonyeshaushirika wa mkristo na Krsito kwa kumzamisha kwenyemaji, na pia ni kitendo cha mkristo kudhihirishahadharani kujitolea kwake kwa Kristo na watu wake, nakwa hivyo kuunganisha mkristo na kanisa nakumtofautisha na dunia.Kutokana na maneo haya, tutazame kila mstari jinsiunaambatana na maandiko.10

Kanisa ndilo linabatizaUbatizo ni kitendo cha kanisa. Ubatizo ni jambo ambalomtu humfanyia mwingine. Mtu awezi kujibatizamwenyewe, lazima kuwe na vikundi viwili ambavyovinahusika. Na kila kikundi husema kitu kwa mwinginena kwa dunia.Watu siku hizi hufikiria ya kwamba ubatizo ni jamboambalo wanaweza amua kujifanyia, kama kuamuakununua shati kwa dukani. Unaponunua shati dukani,haijalishi nanai anayekuuzia au duka analo nunua shatihiyo. Katika ubatizo, anayebatizwa ndiye huwa tunatiliimkazo sana. Yule anayebatizwa, anapaswa kufanyamwenyewe uamuzi wa kubatizwa, kwa sababu ni yeyeambaye anataka kufanya tangazo kwamba wako pamojana Yesu. Mfano wa Filipo na Towashi wa Kushi katikaMatendo ya Mitume 8, kwa wengi wanaweza kuwazakwamba ubatizo ni jambo dogo.Agano Jipya linapeana picha kamili ya ubatizo. Kileambacho tunakipata katika Matendo ya Mitume 8, siyojambo ambalo limezingatia sana katika maandiko yaBiblia yote. Haufai kuanza katika Matendo ya mitumekuhusu jambo la ubatizo, bali katika injili ya Matayo 1611

na 18. Katika vifungu hivi, Yesu amekabidhi funguo vyaufalme kwanza kwa mitume halafu kwa kanisa. Funguovya Ufalme ni vya kufungu duniani kilicho fungwambinguni, na kufungua dunia kile kilicho funguliwambiguni. Hii inamanisha ya kwamba, mitume walikuwana mamlaka kutoka kwa Yesu kuamua kwa niaba yaYesu. Leo mamlaka hayo yamekabidhiwa kanisa. Wazaya hakimu anapokuwa anatoa uamuzi wake. Yeye huwaanatoa uamuzi huu kulingana na sheria ya nchi. Yeye nimwakilisha wa nchi kutekeleza sheria ya nchi.Mamlaka ya kufanya tangazo maalumu kwa niaba yambinguni, ni jambo ambalo Yesu amelikabidhi kanisa,siyo mtu binafsi. Matayo 18:20: “Kwa maanawanapokutana watu wawili au watatu katika jina langu,hapo mimi nipo pamoja nao.” Hapa, Yesu haongeleikikundi cha watu wachache, ambao kuwepo kwake Yesumiongoni mwao ni jambo ambalo halieleweki. Kanisa nimukutano wa mara kwa mara wa watu wawili au watatuwanaokiri jina la Kristo. Kristo yuko pamoja nakusanyiko hilo na amewapea mamlaka ya kuzungumzakwa jina lake.Tunahitaji kuelewa haya yote, ndipo tuelewe kazi yetu yakuyafanya mataifa kuwa wanafunzi wa Yesu katika12

Matayo 28. Kwanza Kristo anatukumbusha kuwa Yeyendiye aliye na mamlaka mbiguni na duniani (mstari wa18). Baadaye ya hayo maneno, anawamuru wanafunziwake kufanya watu wengine kuwa wanafunzi wake nakuwabatiza kwa Jina la baba, Mwana na Roho Mtakatifu.Halafu anawaambia wafundishe kila kitu ambachoamewamuru, kazi hii hii inaendeleshwa na kukamilishwakatika kanisa. Mwisho anawahakikishia kwamba atakuwapamoja nao wakati wanapokuwa wanafanya kazi hii: “Nami nipo pamoja nanyi siku zote; naam, mpaka mwishowa nyakati. Mafundisho ya Mathayo 16, 18 msingi wakeuko katika mafundisho ya Mathayo 28.Ni nani anayo mamlaka ya kubatiza? Je, mkristo yeyote?Ikiwa uko kwa kazi ya kuhubiri injili mahali ambapohakuna wakristo wengine, itabidi ufanye kazi hiyo yaubatizo kwa wale ambao wanaokoka. Utafanya hivyo kwasababu mahali hapo hakuna kanisa. Matendo ya Mitume 8inatoa mfano kwako kama utawahi kuwa katika hali hiyo.Wakati huo huo, kumbuka kwamba Yesu amehusishawazi wazi uwepo wa mamlaka kwa makanisa na watuwawili au watatu wanaokusanyika kwa jina lake. Kwakawaida ni kanisa ambalo lina mamlaka ya kubatiza.Ubatizo hufanywa na mtu mmoja, kwa niaba ya kanisa.Kanisa hubatiaza kupitia kwa mwakilisha wake ambaye13

anaeze kuwalitamchangua.mchungajiaumtuambayekanisaKanisa halina mamlaka ya kukataa kumbatiza mtuambaye anakiri kuokoka na anaonekana kuishi kulinganana kukiri kwake (Matendo Ya mitume 11:17-18). Lakinipia ni vyema kufahamu kwamba, kanisa linahusika kwasababu tangaza la ubatizo wa mtu, pia ni ushuhudamkubwa wa kanisa kwa wale ambao hawajaokoka.Kanisa linaakilisha mbingu hapa duniani.Ubatizo huthibitisha na kuonyesha kwamba mwenyekubatizwa, ameungana na KristoJe, ushuhuda wa kanisa katika kubatiza ni wa aina gani?Kwa kuwa ubatizo wa kanisa huthibitisha imani ya yaYule ambaye anabatizwa, kwamba yeye yuko ndani yaKristo. Huthibitisha ya kuwa yule ambaye anasema yakwamba umeunganika na Kristo katika ufufuo wake, nimkristo. Kanisa huweka muhuri unaoonekana kwa wote.Imani hutuunganisha kwa Kristo ndipo tuweze kuonamanufaa ya kifo na ufufuo wake. Ubatizo ni ishara yamuungano huo.14

“Maana , mnajua kwamba sisi tuliobatizwa tukaungana naKristo Yesu, Tulibatizwa na kuungana na kifo chake.Tulipobatizwa tuliungana na kifo chake, tukazikwapamoja naye, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutokawafu kwa kitendo kitukufu cha baba, sisi pia tuwezekuishi maisha mapya.” (Warumi 6:3-4)“Tangu kufika kwa hiyo imani, sheria si mlezi wetu tena.Kwa njia ya imani, ninyi nyote mmekuwa watoto wamungu katika kuungana na Kristo. Ninyi nyotemliobatizwa mkaungana na Kristo ni kama vile mmemvaaKristo.” (Wagalatia 3:25-27)Ubatizo ni ishara ya kazi ya injili katika maisha ya mtu.Ni ishara ya kwamba umeacha dhambi na akaunganikakwa Kristo kwa imani. Ubatizo haudhihirishi kukiri tu,bali pia kazi ya Mungu katika maisha ya mtu. Waza juuya kifo, kuzikwa na kufufuka kwa Yesu. Ubatizohudhibitishia wale ambao wanashuhudia muangano wamtu na kifo, kuzikwa, na ufufuo Yesu Kristo. Mtuhuingizwa kimwili kwa maji na kuinuliwa kutoka kwamaji. Ishara ya kufa kwa dhambi na kufufuka kwa maishamapya ndani ya Yesu Kristo.15

Ubatizo huonyesha kuungana kwetu na Kristo, namanufaa ya hiyo muungano. Kupitia kwa Kristo dhambizetu zinasamehewa na Kuoshwa. Ubatizo unaonyeshamambo haya yote. Petero aliuambia umati siku yapentecoste, “Tubuni na kila mmoja wenu abatizwe kwajina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi zenu nakupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu (Matendo yaMitume 2:38). Anania alimwambia Paulo, “Sasa basi, yanini kukawia zaidi? Simama ubatizwe na uondolewedhambi zako kwa kuliungama jina lake” (Matendo yaMitume 22:16). Katika Kristo tunapata maisha mapyaambayo yamejazwa na nguvu za Roho Mtakatifu. Mfanowa kutolewa ndani ya maji wakati wa ubatizo, inaashiriahaya maisha. (Warumi 6:4; Wakolosai 2:11-12). Katikaubatizo kanisa linathibitisha ya kwamba yule mtu ambayeanakiri imani katika Kristo ameunganika na Kristo, nainaonyesha huo muungano na manufaa yake.Wakati wa ubatizo, mtu huzamishwa ndani ya majiJe, kanisa hudhihirishiaje mtu kwamba amefufuka kutokakwa dhambi na yuko hai katika Kristo? Jibu ni kwamba,kwa kumuzamisha kwa maji. Neno la kigiriki “baptize”,ambalo neno letu “ubatizo” hutoka, linamanisha kuingizaau kurusha kitu ndani ya maji, kwa kawaida kusababisha16

kuzama kabisa. Biblia katika Agano Jipya inafundisha nakuonyesha kwamba ubatizo ni kuzamishwa. Yohanambatizaji alibatiza “huko Ainoni karibu na Salimu kwasababu huko kulikuwa na maji mengi” (Yohana 3:23), nahakuna ishara ya kwamba ubatizo uliyofanywa nawanafunzi wa Yesu ulihataji maji kidogo.Zaidi, wakati Towashi wa Kushi aliweka imani yakekatika Kristo, alimwabia Filipo, “Tazama, hapa kunamaji! Kuna kitu gani cha kunizuia mimi nisibatizwe?”(Matendo ya Mitume 8:36). Na tunasoma, “Akaamurugari lisimamishwe. Wakateremka, yule Towashi naFilipo, wakaenda pale kwenye maji. Filipo akambatiza.Walipotoka katika yale maji, Roho wa Bwanaakamchukua Filipo na yule Towashi hakumwona tena.Kwa hiyo akaendelea na safari yake akiwa amejawa nafuraha” (Matendo ya Mitume 8:38-39). Inaonekana yakwamba ubatizo ulihitaji maji mengi kushida yalewalikuwa nayo kwenye gari, kwa hivyo iliwabidiwashuke ndipo wafanye ubatizo.Hatimaye, maelezo ya Paulo ya kwamba ubatizo huashiriakifo, kuzikwa na kufufuliwa na Kristo, kwa yule anayebatizwa. Katika Warumi 6:1-4, ni wazi kwambakubatizwa ni kuzamisha. Kuzamishwa kimwili huonyesha17

kuzikwa,kutolewahuonyeshakufufuliwanakuunganishwa na Yesu Kristo. Kwa hivyo kanisalinathibitisha na kuonyesha kuungana kwa aliyeaminipamoja na Kristo.Ni tendo la mkristoLakini ubatizo siyo tendo la kanisa pekee, pia ni tendo lamkristo. Kanisa hubatiza, Mkristo anabatizwa. Fikiriajinsi wale waliomsikiliza Petero wakati wa pentencostewalifanya.Watu waliposikia maneno haya yaliwachoma moyoni,wakawauliza Petro na wale mitume wengine, “Tufanyenini ndugu zetu?” Petro aliwajibu, “Tubuni, muachedhambi na kila mmoja wenu abatizwe katika jina la YesuKristo, ili msamehewe dhambi zenu; nanyi mtapokeazawadi ya Roho Mtakatifu. Kwa maana ahadi hiiilitolewa na Mungu kwa ajili yenu na watoto wenu, nawale wote walio nchi za mbali, na kila mtu ambayeBwana Mungu wetu anamwita kwake.”.Wotewaliopokea ujumbe wa Petro walibatizwa na zaidi yawatu elfu tatu wakaongezeka katika kundi la waaminisiku hiyo.18

Wale waliotubu dhambi zao na kumuamini Yesu Kristowalibatizwa.Ubatizo ndiyo tendo la kwanza la hadharanilinalodhihirisha imani ya kumpokea Yesu kama Bwana namwokozi wa maisha yetu. Kama wewe ni Mkristo, Yesuanakuamru ubatizwe. Ni kitu ambacho ni lazima ufanye;hakuna mtu yeyote anaweza kukufanyia.Wale ambao hawajaokoka, hawafai kubatizwa. Ubatizounathibitisha na kuonyesha muungano wa mkristo naKrsito, kwa hivyo ni wale tu ambao wameunganika naKristo kwa imani wanastahili kubatizwa.Ubatizo ni kitendo ya Yule aliyeokoka kujitoleahadharani kwa KristoMkristo hufanya nini katika suala la ubatizo? Huwaanajitolea hadharani kwa Kristo. Ubatizo ni njia yakuonyesha hadharani kuwa umekuwa Mkristo. Ni jinsiunavyokiri imani yako, kwa kunyenyekea kwa BwanaYesu Kristo.Kwa ajili ya kuitikia wito wa injili, tumeamuriwakumfuata Yesu kwa matendo ya nje na ndani. Matendo yanje hutangaza kile tulichonacho ndani yetu. Ubatizohufanywa wazi, mbele ya mashhaidi. Waza juu ya wale19

waliotubu na wakabatizwa wakati wa pentecoste. Walewote walijitokeza kutoka kwa umati wa watu wabatizwewalikuwa wanaashiria kuwa wamekuwa wafuasi waYesu.Wafuasi wa Kristo wanapaswa kuwa watu ambaowanaonekana na kila mtu. “Kila mtu atakayenikiri mbeleya watu, mimi pia nitamkiri mbele ya Baba yangu aliyembinguni. Lakini yeyote atakayenikana mbele ya watu,mimi pia nitamkana mbele ya Baba yangu aliyembinguni” (Mathayo 10:32-33). Hakuna wanafunzi waYesu wa kisiri. Njia ya pekee ya kumfuata Yesu nikufanya hivyo hadharani, mahali ambapo kila mtuanaweza kukuona. Na ubatizo ndiyo njia ambayotunatangaza mbele ya kanisa na dunia yote kuwa sisi niwatu wa Kristo. Yesu anataka wanafunzi wake waangazendipo ulimwengu umwone kupitia kwao. Ubatizo ndiyonjia ya kuingia katika hiyo mwanga.Kama uko na wasiwasi juu ya kutangaza imani yakohadharani, angalia ubatizo kama usaidizi na siyo kiziizi.Yesu ajaacha utegemee ujasiri wako ama ubunifu wakokujua jinsi utakavyojitangaza umekuwa mkristo;amekuonyesha njinsi ya kufanya hivyo. Ameifanya iwe20

rahisi! Kile unafaa kufanya ni kukiri tu imani yako kwaKristo.Ubatizo siyo tu kukiri kwamba umeokoka, ubatizo nikufanya uamuzi wa kujitolea kwa Yesu Kristo. Petroanaandika jinsi ambavyo Noa na familia yakewalivyookolewa kutoka kwa ghadhabu ya Mungu katikagharika. Petero anafananisha hili na “Maji hayo nikielelezo cha ubatizo ambao sasa unawaokoa ninyi, sikwa kuondoa uchafu kwenye miili yenu, bali kamadhamana ya kuwa na dhamiri njema kwa Mungu kwa ajiliya kufufuka kwa Yesu Kristo” (1 Petro 3:21). Wakatiambapo Petro anasema kuwa ubatizo “huokoa,”anafafanua kuwa kile inaokoa siyo kuoshwa mwili namaji, bali ni imani ambayo ubatizo inadhihirisha. Kwaimani tunampokea Kristo aliye fufuliwa, halafutunabatizwa.Maneno haya, “ahadi ya dhana mzuri” inaweza chukuliwakama maombi ama ahadi, ama zote. Nafikiri mambo hayayote yanapatikana katika ubatizo, hata kama mstari huuunasisitiza moja ama nyigine. Ubatizo ni maombi ambayohutoa sauti kwa ombi la imani “niokoe, Bwana Yesu!”Kwa kujitabulisha na kifo na ufufuo wa Yesu Kristokatika ubatizo, mkristo husema kwamba Kristo ni21

mwokozi wake. Yeye huwa anamlilia Mungu, kwambaawe mkristofu kwa ahadi zake.Kubatizwa ni kujitoa kabisa, na kunyenyekea kwa Kristokama Bwana. Kubatizwa kwa jina la Kristo (Mathayo28:19) ni kunyenyekea kwa uongozi wake. Ubatizo nikiapo ya kutii mfalme Yesu. Ni kuhapa kwamba tutakuwawaaaminifu kwake. Ubatizo ni ahadi ya kutii amri zote zaKristo. Kubatizwa ni alama ya kuti amri “Yashikenimambo yote niliyowaamuru ninyi” (Mathayo 28:20).Hauwezi kumpokea Yesu kama mwokozi na ukosekumheshimu kama Bwana. Katika ubatizo tunauchukuwamsalaba wa Yesu na kutembea katika njia zake.Ubatizo ni dhihirisho la hadharani la imani. Ni mahaliambapo tunavaa mavazi ambayo yanatutambulishapamoja na Yesu. Ubatizo kwa mkristo ni kusema kwambaYesu Kristo ni mwokozi wake na anajitoa kunyenyekeakwake kama Bwana.Ni tendo la kanisaKatika ubatizo mkristo hujitolea siyo tu kwa Kristo pekee,bali pia kwa watu wa Kristo. Kumbuka tenakilichofanyika wakati wa pentecoste: “Wale wote22

waliopokea ujumbe wa Petro kwa furaha wakabatizwa nasiku ile waliongezeka watu wapatao 3,000” (Matendo yeMitume 2:41). Hawa wapatao 3000 waliogezewa kwanani? Kwa kanisa la Yerusalemu, ambapo hapo awaliwalikuwa watu 120 (Matendo ya Mitume 1:15). Walewaliobatizwa wakati wa pentecoste walijitoa kutoka kwaulimwengu wakaingia ndani ya kanisa. Na hivyo ndivyoilivyo, au inafaa kukuwa kwa kila mtu anaye batizwa leo.Kumkristo Yesu ni kujiunga na kikundi cha wale ambaowanamkristo. Kumpokea Yesu ni kupokea watu wake.Injili haituleti kwa Mungu peke (Waefeso 2:1-10), baliinatuunganisha na kila mmoja ambaye ni wa Mungu(Waefeso 2:11-22). Kumwita Mungu baba ni kukubaliwale wote ambao pia wanamwita baba na kuwachukuwakama ndungu wa jamii moja. Kuunganishwa na Kristo nikukuwa mmoja wa mwili wake (1

Ishara ya kufa kwa dhambi na kufufuka kwa maisha mapya ndani ya Yesu Kristo. 16 Ubatizo huonyesha kuungana kwetu na Kristo, na manufaa ya hiyo muungano. Kupitia kwa Kristo dhambi zetu zinasamehewa na Kuoshwa. Ubatizo unaonyesha mambo haya yote. Petero aliuambia umati siku ya

Related Documents:

uwezo alio nao katika kuishi maisha mapya. Tutajifunza jinsi wokovu unavyomletea Mkristo maisha haya mapya. Lakini pia, kwa sababu watu wengine wameyachanganya mafundisho ya wokovu, tutayachunguza mafundisho ya uongo kuhusu wokovu pia. Kwa mfano hali ya kutegeme matendo mema a kwa wokovu au utegemezi katika kifo cha Yesu pamoja na ubatizo.

Ikiwa una wasiwasi kuhusu dalili zozote zisizo za kawaida ambazo unaweza kuwa nazo, au una maswali kuhusu mchanganyiko wa athari kutokana na kupata chanjo zaidi ya moja kwa wakati mmoja. Ikiwa una wasiwasi kuhusu athari zako au ikiwa athari haziishi baada ya siku chache.

Maisha Mapya ndani ya Kristo kama muongozo wako. Matokeo ya mafundisho haya yanaweza kusababisha matunda ya milele. 2. Ifanye Biblia kuwa mamlaka yako katika kujibu maswali. Wanafunzi wanapaswa kuangalia vi-fungu vya Biblia wenyewe na wajaribu kujibu maswali kulingana na kile Biblia inachosema. Baadhi ya waamini wapya wanahitaji msaada

Año Paulino-, se ha añadido el tema titulado El corpus paulino. TEMARIO 1. La Biblia o Sagrada Escritura. 2. La inspiración de la Biblia. 3. La verdad de la Biblia. 4. Formación de los libros del Antiguo Testamento y de los evangelios. 5. El canon bíblico. 6. Interpretación de la Biblia. 7. El corpus paulino. 8. Anexos:

5. Cómo estudiar mejor la Biblia 4-6 6. Estándares insuficientes de autoridad 6-7 7. Información general de la Biblia 7-8 8. La palabra “Testamento” 8 9. Divisiones de la Biblia 9-10 10. Idiomas de la Biblia 10 11. Inspiración de l

1)La Biblia en un año, una vez al día: sigue el plan. Lee cada día las lecturas durante tu tiempo de lectura diaria de la Biblia para finalizar toda la Biblia en un año. 2)La Biblia en un año, dos veces al día: lee las lecturas de cada día, pero en dos momentos. Lea el pasaje del Antiguo Testamento por la mañana, y los

Los autores de la Biblia escribieron inspirados por Dios. La autoría de la Biblia es humana y divina. Dios se sirve de los autores humanos de la Biblia, con sus peculiaridades, para comunicarnos su mensaje. Por eso, los libros de la Biblia no presentan contradicciones entre sí. Como Dios, la Biblia es una, santa y verdadera.

Informational Black Holes in Financial Markets Ulf Axelson Igor Makarov April 2020 ABSTRACT We study how well primary nancial markets allocate capital when information about in-vestment opportunities is dispersed across market participants. Paradoxically, the fact that information is valuable for real investment decisions destroys the e ciency of the market. To add to the paradox, as the .