MAANA ZA MAJINA YA WATU WA PEMBA KATIKA LUGHA

2y ago
348 Views
5 Downloads
859.26 KB
105 Pages
Last View : 6d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Aydin Oneil
Transcription

MAANA ZA MAJINA YA WATU WA PEMBAKATIKA LUGHA YA KISWAHILI: UCHUNGUZI KIFANIMOH’D HAJI ALITASNIFU ILIYOWASILISHWA IKIWA NI SEEMU YA MASHARTI YAKUPATIWA SHAHADA YA UZAMILI (M.A.) KISWAHILI YA CHUOKIKUU HURIA CHA TANZANIA2016

iiUTHIBITISHOAliyetia sahihi hapa chini anathibitisha kwamba ameisoma Tasnifu yenye mada“Maana za Majina ya Watu wa Pemba” na ameridhika kwamba imefikia kiwangokinachotakiwa na inafaa kuwasilishwa kwa ajili ya utahini wa shahada ya Uzamili(M.A Kiswahili) ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania. Dkt. Zelda Elisifa(Msimamizi) .Tarehe

iiiHAKI MILIKIHairuhusiwi kuiga au kunakilikwa namna yoyote ile tasnifu hii, kwa njia yakielektroniki, kurudufu nakala, kurekodi au njia yoyote nyengine, bilaya idhini yamwandishi au Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa niaba ya mwandishi.

ivTAMKOMimi Ali, Moh’d Haji, nathibitisha kuwa hii ni kazi yangu halisi na haijawahikuwasilishwa katika Chuo Kikuu kingine chochote kwa ajili ya kutunukiwa shahadahii au nyengine yoyote. .Sahihi Tarehe

vTABARUKUNaitabaruku kazi hii kwa mama yangu, Mauwa Haji Amani, kwa malezi yakemazuri na kunisisitiza kutafuta elimu. Aliniambia “Mwanangu kwa elimu na maliwatu hujenga familia zao. Familia hazijengwi kwa ujinga na unyonge”.

viSHUKURANIAwali ya yote sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu naardhi na vilivyomo vyote pia. Ni yeye aliyenipa nguvu, uwezo na afya, kuwezakukamilisha kazi hii. Baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu. Nawashukuru walewote walionisaidia kuandaa kazi hii. Nathamini mchango wao mkubwa kwangu nanakiri kuwa bila wao kazi hii ingekuwa ni ndoto tu. Kwa vile ni vigumu kuwatajawote walioshiriki kunisaidia kwa njia moja au nyingine kufanikisha utafiti huu.Natumia fursa hii kutaja wachache ambao katu siwezi kuwasahau kwa mchango waomkubwa walioutoa kuniwezesha kukamilisha kazi hii. Shukurani pekee zimwendeemsimamizi wangu, Dkt. Zelda Elisifa, ambaye alinipa muongozo katika kuwasilishawazo la utafiti, uandaaji wa pendekezo, kufanya utafiti hadi kuikamilisha tasnifu hii.Kwa busara na hekima zake aliniongoza, alinishauri na kunikosoa kila palipostahilibila kuchoka. Nakiri kuwa nimejifunza mengi kutoka kwake. Usimamizi na msaadawake kwangu katu haumithiliki. Pia napenda kumshukuru mwalimu wangu wa somola utafiti Dkt. Pembe Lipembe ambaye ndiye aliyenionesha njia na kuniwashia taahadi nimeweza kufikia kileleni mwa tasnifu hii. Sitakuwa mwizi wa fadhilakumsahau mke wangu mpenzi, aliyenipa ushirikiano mkubwa na kutoa muhangawakati wake wenye thamani ili niweze kufanikisha kazi hii. Shukurani nyengineziwaendee mwl. Bakari Kombo, Waziri Juma na Hamad Abdalla kwa kunishaurivizuri. Namalizia shukurani kwa wale wote walioshiriki katika kutoa taarifa zautafiti. Wote walioshiriki kufanikisha kazi hii, Mungu awape kila la kheri katikamaisha yao. Ameen.

viiIKISIRIUtafiti huu ulichunguza maana za majina ya watu wa Pemba. Utafiti huu ulifanyikakatika kisiwa cha Pemba mkoa wa kusini, Wilaya ya Chake-Chake. Mtafitialiongozwa na malengo mahususi matatu. Kwanza, kubainisha maana za majina yawatu katika jamii ya Wapemba, pili kueleza mazingira yanayosababisha watukupewa majina hayo katika jamii ya Wapemba na tatu kufafanua vigezovinavyowaongoza watoa majina kwa wanaume na wanawake. Ili kufikia lengo kuulililokusudiwa mbinu mbalimbali za utafiti zilihusika. Mbinu hizo ni pamoja namahojiano na hojaji. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya semiotiki ambayo msingiwake mkubwa ni ishara na maana zake katika lugha. Nadharia ya pili iliyotumika ninadharia jumuishi ya Giles ambayo msingi wake mkubwa ni kuchunguza vibainishivya jamii mbalimbali. Nadharia hizi ziliakisi data za utafiti huu kutokana na maoniyaliyotolewa na watafitiwa. Utafiti umebaini kuwa majina yanayotolewa kwa watuyanabeba maana zifuatazo: Maana za majina yatokanayo na miezi ya kiislamu,matukio mbalimbali, maeneo matukufu, siku za wiki, miongo na hali mbalimbaliwalizozaliwa watoto. Mazingira yanayosababisha watu kutoa majina katika jamii yaWapemba ni Siku wanazozaliwa watoto, wakati wanamozaliwa, miezi wanayozaliwana migongano katika jamii. Utafiti umebaini vigezo vinavyowaongoza watoa majinakwa wanaume na wanawake kuwa ni Itikadi za kidini, urithi, umashuhuri,kuondokana na majina ya zamani na kuvutiwa na herufi fulani mwanzoni mwa jinana kuvutiwa na silabi fulani mwishoni mwa jina.

viiiYALIYOMOUTHIBITISHO. iiHAKI MILIKI . iiiTAMKO . ivTABARUKU . vSHUKURANI . viIKISIRI . viiORODHA YA JEDWALI . xiiORODHA YA MICHORO . xivORODHA YA VIFUPISHO . xvSURA YA KWANZA . 11.0USULI WA MADA . 11.1Dhana ya Nomino au Jina katika Historia ya Uchambuzi wa Lugha . 11.1.1 Wanafalsafa Awali . 11.1.2 Majina Katika Lugha ya Kiingereza . 31.1.3 Majina Katika Lugha ya Kiswahili . 41.1.4 Majina Katika Jamii ya Wapemba . 91.1.5 Asili ya Majina ya Wapemba . 101.2Tatizo la Utafiti . 101.3Malengo ya Utafiti . 121.3.1 Lengo Kuu la Utafiti . 121.3.2 Malengo Mahususi . 121.4Maswali ya Utafiti . 121.5Mipaka ya Utafiti . 12

ix1.6Umuhimu wa Utafiti. 131.7Vikwazo vya Utafiti . 131.8Muhtasari wa Sura . 14SURA YA PILI . 152.0MAPITIO YA KAZI TANGULIZI NA KIUNZI CHA NADHARIA . 152.1Utangulizi . 152.2Kazi Tangulizi Kuhusu Majina kwa Ujumla . 152.3Kazi Tangulizi Kuhusu Majina ya Watu na Mazingira Yake . 182.4Majina Katika Bara la Asia . 182.4.1 Majina Katika Bara la Ulaya . 182.4.2 Majina Katika Bara la Afrika . 192.4.3 Majina Katika Tanzania . 202.5Maana za Majina . 242.6Kiunzi cha Nadharia . 252.6.1 Nadharia ya Semiotiki . 262.6.2 Nadharia Jumuishi ya Giles. 322.7Ombo la Kiutafiti . 342.8Muhtasari . 34SURA YA TATU . 353.0MBINU ZA UTAFITI . 353.1Utangulizi . 353.2Mkabala wa Utafiti . 353.3Eneo la Utafiti . 363.4Sampuli Lengwa ya Watafitiwa . 37

x3.5Usampulishaji . 373.6Mbinu za Kuikusanya Data . 393.6.1 Hojaji (Dodoso) . 403.6.2 Mahojiano. 423.7Maadili ya Utafiti . 433.8Mchakato wa Kukusanya na Kuchambua Data . 443.9Muhtasari . 45SURA YA NNE . 464.0WASILISHO NA UCHAMBUZI WA DATA . 464.1Utangulizi . 464.2Uwasilishaji wa Data . 464.3Maana ya Msingi ya Majina ya Watu wa Pemba . 464.3.1 Majina Yatokanayo na Miezi ya Kiislamu . 474.3.2 Majina Yatokanayo na Matukio Mbalimbali . 484.3.3 Majina Yatokanayo na Maeneo Matukufu . 504.3.4 Majina Yatokanayo na Siku za Wiki. 514.3.5 Majina Yatokanayo na Misimu . 534.3.6 Majina Yatokanayo na Nyakati Mbalimbali . 544.3.7 Majina Yenye Maana Dokezi . 554.3.8 Majina Yanayobeba Maana Husishi . 584.3.9 Muhtasari . 614.4Mazingira Yanayotumiwa Kwenye Kuwapa Watu Majina . 614.4.1 Matukio . 624.4.2 Siku Waliyozaliwa . 63

xi4.4.3 Wakati Waliozaliwa . 644.4.4 Miezi Waliozaliwa . 644.4.5 Migongano Katika Jamii . 654.4.6 Muhtasari . 664.5Vigezo Vinavyowaongoza Watoa Majina kwa Wanawake na Wanaume . 674.5.1 Itikadi za Kidini . 684.5.2 Kigezo cha Kuondokana na Majina ya Zamani . 694.5.3 Kigezo cha Urithi . 734.5.4 Kigezo cha Umashuhuri . 744.5.5 Kuvutiwa na Herufi au Silabi Fulani. 744.5.6 Muhutasari wa Sura . 76SURA YA TANO . 775.0MUHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO . 775.1Utangulizi . 775.1.1 Muhtasari wa Utafiti. 775.1.2 Muhtasari wa Matokeo ya Utafiti . 785.2Hitimisho . 795.3Mapendekezo ya Tafiti Fuatishi . 79MAREJEO . 81VIAMBATISHO . 86

xiiORODHA YA JEDWALIJedwali Na.2.1:Mifano ya Maana ya Majina ya Kigogo . 23Jedwali Na. 3.1:Idadi ya Watafitiwa kwa Kila Shehia . 38Jedwali Na. 3.2:Idadi ya Watafitiwa Waliopewa Dodoso . 39Jedwali Na. 4.1:Maana za Majina Yanayotokana na Miezi ya Kiislamu . 47Jedwali Na. 4.2:Maana za Majina Yanayotokana na Matukio ya Kidini . 49Jedwali Na. 4.3:Majina Yanayotokana na Maeneo Matukufu Katika Historiaya Uislamu . 51Jedwali Na. 4.4: Maana za Majina Yenye Asili ya Kibantu yanayotokana na Sikuza Wiki . 52Jedwali Na. 4.5: Maana za Majina Yanayotokana na Misimu Mbali Mbali KatikaMwaka . 53Jedwali Na. 4.6:Maana za Majina Yanayotokana na Wakati wa Kuzaliwa . 55Jedwali Na. 4.7:Majina Yenye Maana Dokezi . 56Jedwali Na. 4.8:Majina Yenye Maana Husishi . 59Jedwali Na. 4.9:Mazingira Yanayotumiwa Kwenye Kuwapa Watu wa PembaMajina . 62Jedwali Na. 4.10: Majina Wanayopewa Watu Kulingana na Siku Waliyozaliwa . 63Jedwali Na. 4.11: Majina Wanayopewa Watu wa Pemba Kulingana na MieziWaliyozaliwa . 65Jedwali Na. 4.12: Vigezo Vinavyowaongoza Watoa Majina ya Wanawake naWanaume . 67Jedwali Na. 4.13: Baadhi ya Majina Mapya na Tafsiri Zake . 70Jedwali Na. 4.14: Baadhi ya Majina Yenye Viambishi vya kike . 70

xiiiJedwali Na. 4.15: Majina na Namna Yanavyogeuza Jinsia Kutokana naKubadilika Irabu Mwishoni. 71Jedwali Na. 4.16: Ubadilishanaji wa Irabu /u/ Kuwa Irabu/a/ UnaosababishaUbadilikaji wa Jinsia Katika Jina . 72Jedwali Na. 4.17: Majina Yanayofanana Herufi za Mwanzo. 70Jedweli Na: 4.18: Majina Yanayofanana Silabi za Mwisho. 71

xivORODHA YA MICHOROMchoro 2.1: Ishara, Kiashiriwa na Kiashiria . 27Mchoro 2.2: Piramidi ya Peirce ya Kufasiri Ishara . 28Mchoro 2.3: Mihusianisho ya Kufasiri Ishara. 30

xvORODHA YA VIFUPISHOBAKIZA -Baraza la Kiswahili la walimuNa-NambaProf-ProfesaTUKI-Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili

1SURA YA KWANZA1.0 USULI WA MADA1.1Dhana ya Nomino au Jina katika Historia ya Uchambuzi wa LughaKapinga (1983:36) anasema: “Jina ni neno linalotaja kitu fulani kusudi kutofautishana kukipambanisha miongoni mwa vitu vingine”.Habwe na Karanja (2004:8) wanasema:“Nomino ni maneno ambayo hutaja majinaya watu, vitu, hali, mahali, vyeo, dhana, na hata vitendo”.Wanaendelea kusema ndio maana baadhi ya wanaisimu huita nomino majina kwasifa hii ya kutaja vitu.Bakiza (2010:133) Wanasema: “Jina ni neno linalotumika kutambulisha mtu,mnyama, kitu, jambo, mahali au kitu”.1.1.1 Wanafalsafa AwaliDhana hii ilianzishwa na wanaisimu waliochunguza lugha ya kigiriki na kilatini.Wanaisimu hawa ni kama vile Plato,Aristotle, Protagoras, Dionisious Thrax,Priscian na Apollonius. Hapa chini ni maelezo mafupi ya wanaisimu hao.a) Plato: Huyu ni mwanafalsafa mkongwe alizaliwa Ugiriki mwaka 348 kablaya Kristo.Yeye alibainisha kuwepo kwa kategoria ya nomino katika uchambuziwake wa sentensi, ambapo aliigawa sentensi katika sehemu mbili yaaninomino na kitenzi. Kama inavyobainishwa katika mchoro huu

2S SentensiSN KAmbapo;S SentensiN NominoK KitenziKanuni hii inafafanua uchambuzi wa sentensi kama ulivyofanywa na Plato kwakunesha kwamba sentensi imeundwa kutokana na nomino na kitenzi.b) Aristotle, ambaye alizaliwa mwaka 328 kabla ya Kristo na alibainisha uwepowa kategoria ya nomino katika sentensi za lugha ya Kigiriki na Kilatini. Piaalibainishakuwa katika lugha kuna nomino na kitenzi pia kiunganinishiambacho huunganisha tungo na tungo.c) Protagoras, huyu ni mwanafalsafa wa Kilatini aliyebainisha kuwepo kwakategoria ya nomino katika lugha ya Kilatini.d) Dionisious Thrax ni mwanamapokeo wa kwanza kubainisha aina za manenokatika lugha ya kilatini na alibainisha aina nane za maneno. Nazo ni nomino aujina, kitenzi, kibainishi, kibadala (kiwakilishi), kiungo (kiunganishi), kielezi,faridi peke na kihusishi.Baada ya kuangalia kwa ufupi michango ya wanaisimu wa kale waliobainishakuwepo kwa kategoria ya majina (nomino) katika lugha ya Kigiriki na Kilatini,

3inafuata mchango wa baadhi ya wanaisimu wa lugha ya Kiingereza, Kiarabu naKiswahili walivyobainisha uwepo wa kategoria ya nomino (majina) katika lughahizi.1.1.2 Majina Katika Lugha ya KiingerezaWataalamu mbalimbali wa lugha ya kiingereza wamebainisha kuwepo kwa kategoriaya majina katika lugha hiyo.Glencoe (1979) alibainisha kuwepo kwa kategoria ya nomino (jina) katika lughaya Kiingerza na kufasili jina kuwa ni neno linalotaja majina ya watu, vitu,mahali, au dhan

inafuata mchango wa baadhi ya wanaisimu wa lugha ya Kiingereza, Kiarabu na Kiswahili walivyobainisha uwepo wa kategoria ya nomino (majina) katika lugha hizi. 1.1.2 Majina Katika Lugha ya Kiingereza Wataalamu mbalimbali wa lugha ya kiingereza wamebainisha kuwepo kw

Related Documents:

Ngeli za Nomino Makundi ya nomino katika lugha ya Kiswahili yenye sifa zinazofanana kisarufi. A-WA Huwa na majina ya watu, vilema, viumbe, vyeo na viumbe vya kiroho, n.k. Huchukua miundo kama vile M-WA, M-MI, KI-VI, n.k. mtu-watu, mkulima-wakulima mtume-mitume mkizi-mikizi kiwete-viwete

Kikristo ya kwamba watu wanaokolewa kwa neema ya Mungu tu kwa njia ya imani katika Yesu Kristo—na hii huifanya familia yote ya Kikristo (Wayahudi na Mataifa pia) kuwa moja; (3) Kisha kinajadili ile maana hasa ya huu msimamo wa wokovu kwa ile jamii mpya: watu wanapaswa kuishi maisha mapya kwa imani inayotiririka

Katika nchi nyingi za Afrika, "hitaji lisilofikiwa" la upangaji uzazi liko juu. Kwa kweli, chunguzi zinaonyesha kwamba kuna watu zaidi ambao wanaweza kutumia mbinu za kupanga uzazi kama wanaweza kuzipata zaidi ya watu ambao wanazitumia tayari. Kwa maneno mengine, kama aina mbalimbali za mbinu za kupanga uzazi ambazo watu

(e) Ni vitu gani ambavyo hutengenezwa kwa ngozi za wanyama? 37 4. Sarufi: Ngeli ya A-WA Hii ni ngeli ya majina ya viumbe wenye uhai kama vile watu, wanyama , ndege, wadudu na kadhalika Wanyama wote wa nyumbani hupatikana katika ngeli ya "A-WA". Mifano: a) Ng'ombe ana kula nyasi. Ng'ombe wana kula nyasi b) Punda anampiga mtoto teke.

nomino za pekee.nomino hizi zinaweza kuwa na umoja na wingi, hata hivyo kuna baahdi ya nomino za kawaida ambazo zina umoja au wingi tu. Kwa mfano: mwalimu/ walimu kiti/viti mtu/watu redio (haina wingi) NOMINO ZA DHAHANIA Ni majina ambayo hufikiriwa tu , hayawezi kugusika , kuonekana, kunusika wala kusikika.

Kila moja ya maumbo haya ni mofimu huru kwani kila moja ina maana kamili. Mofimu huru huwa ni neno lisilokuwa na viambishi vyovyote. Kishazi huru na mofimu huru hufanana kisifa kwa sababu zote huweza kusimama pekee katika tungo na kutoa maana kamili. 4. Fafanua dhana ya neno kuu na kijalizo katika muundo wa kirai.

Kwa hivyo, chozi la heri ni chozi ambalo linatoka wakati mhusika fulani amepata amani, utulivu na usalama. Chozi kwisha kupata baraka na mafanikio. Maana nyingine nekana ni chozi (la) afadhaliboranafuu. Kwa kujikita katika maana mbalimbali yanayojitokeza wakatimanenohayomawili yame

Achieved a high qualification In Radiology such as American Board, ABRMI or equivalent. Has an experience of at least 3 years after the higher qualification. Of the rank of Consultant Radiologist. Is employed on a full time basis , in the selected training hospital/ center -6-4.2 - Responsibilities and Duties of the Trainer Responsible for the actual performance of the trainee. Look after the .