Muhtasari Tanzania Ripoti Ya Maendeleo Ya Binadamu 2014

2y ago
169 Views
2 Downloads
1.11 MB
26 Pages
Last View : 13d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Brady Himes
Transcription

MuhtasariTanzaniaRipoti ya Maendeleo yaBinadamu 2014United Republic of TanzaniaMageuzi ya Kiuchumi kwa Maendeleo ya Binadamu

MuhtasariTanzaniaRipoti ya Maendeleo ya Binadamu 2014Mageuzi ya Kiuchumi kwa Maendeleo ya BinadamuUnited Republic of TanzaniaImplementing PartnerMuhtasarii

Hati ya Kumiliki 2015Kimeandaliwa naEconomic and Social Research Foundation (ESRF)51 Uporoto Street (Barabara ya Ali Hassan Mwinyi),Ursino Estates S. L. P 31226, Dar Es Salaam, TanzaniaSimu: ( 255) 22 2926084, 2926085, 2926086, 2926087, 2926088, 2926089, 2926090Simu ya Mkononi: 255 754 780133, 255 655 780233Nukushi: 255 22 2926083Barua pepe: esrf@esrf.or.tz au info@esrf.or.tzTovuti: http://www.esrf.or.tz au http://www.thdr.or.tzShirika la Maendeleo la Umoja wa MataifaOfisi ya Tanzania182 Mzinga way, Barabara ya Msasani, OysterbayS.L.P 9182, Dar Es Salaam, TanzaniaSimu: ( 255) 22 2112576, 255 686 036 436Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa,Tanzania:Simu: 255 686 036 436, 255 686 036 436Ofisi ya Mkurugenzi wa UNDP nchini Tanzania:Simu: 255 686 036 475, 255 686 036 475Barua pepe: registry.tz@undp.orgTovuti: http://www.tz.undp.orgSerikali ya Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWizara ya Fedha,S.L.P 9111,Dar es salaam.Simu: 255 22 2111174 6Nukushi: 255 22 2110326Tovuti: http://www.mof.go.tzHaki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kutoa sehemu ya chapisho hili, kuhifadhali au kuwasilisha, katika umbo lolote au kwanamna yeyote ile, ki eletroniki, kwa kutumia mitambo, kunakili, kurekodi au vinginevyo, bila idhini ya awali.ISBN 978-9987-770-02-1Mchoro katika ukurasa wa mbele umebuniwa na ndugu Haji Chilonga waLa petitie Galerie, Oysterbay Shopping Centre, Barabara ya Toure, Masaki S.L.P 105160 Dar es Salaam, Tanzania.Kimesanifiwa na kuchapishwa na Jamana Printers, TanzaniaiiTANZANIA HUMAN DEVELOPMENT REPORT 2014

DibajiKutolewa kwa Ripoti ya kwanza ya Dunia ya Maendeleo ya Binadamu mwaka 1990, kuliashiria mabadiliko ya fikrakuhusu dhana ya maendeleo. Ripoti hii na zile zilizofuatia, zinazotolewa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifakwa zaidi ya miaka 20 iliyopita, zimebadili namna nchi nyingi zinavyoshughulikia changamoto za maendeleo. Hivisasa, nchi nyingi zinatumia utaratibu wa kushughulikia changamoto za maendeleo kwa kuwaona watu kama kiini chamaendeleo hayo. Kuanzia wakati huo, nchi nyingi zimekuwa zikiandaa ripoti za maendeleo ya binadamu za nchi aukanda zao kila baada ya kipindi fulani. Kwa jumla, zaidi ya ripoti 600 za mendeleo ya binadamu za kanda, au nchi,zimezinduliwa na zaidi ya nchi 143. Ripoti hizi ni zana za kimkakati, za ushawishi, zinazoandaliwa kupitia mchakatoshirikishi ndani ya nchi na kanda husika katika kushughulikia masuala muhimu na kufafanua vipaumbele vya watu.Ripoti hizi ni chanzo muhimu cha ugunduzi na utungaji wa sera za maendeleo na utekelezaji wake.Toleo hili la Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya Tanzania ya 2014 ni toleo la kwanza, ambalo mada yake kuu niMageuzi ya Kiuchumi kwa Maendeleo ya Binadamu. Katika muongo uliopita, kumekuwapo na mabadiliko yakimtazamo kuhusu sera za maendeleo kwa kutozingatia kiwango cha matokeo ya mabadiliko pekee bali mabadiliko yaubora katika ukuaji wa kiuchumi kama yanavyoelezwa katika dhana ya mageuzi ya kiuchumi. Mageuzi ya kiuchumi,kwa namna ya pekee, ni muhimu kwa Tanzania kwa kuwa, wakati Tanzania inashuhudia kiwango cha Ukuaji waPato la Taifa kinachovutia, cha zaidi ya asilimia 7 tangu mwaka 2000, ukuaji huu hauendi sambamba na kupunguakwa umasikini wa kipato. Serikali ya Tanzania imedhamiria kupunguza umasikini, kwa kiasi kikubwa, na kuwanchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Dhamira hii haihitaji ukuaji wa uchumi endelevu pekee, bali mageuzimakubwa ya kiuchumi yanayohusisha mabadiliko ya msingi ya muundo wa uchumi. Ripoti hii inachambua mageuziya kiuchumi ambayo ni muhimu ili kuiwezesha Tanzania kufikia lengo la kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo2025, kama inavyolengwa na dira ya taifa ya maendeleo mpaka 2025. Ripoti hii ina sura nne na viambatisho vyatakwimu. Sura ya kwanza inatoa, kwa ufupi, hali ilivyo ya ukuaji wa maendeleo ya binadamu nchini Tanzania. Suraya pili inajadili maana ya mageuzi ya kiuchumi na inaonyesha chanzo cha mchakato endelevu wa mageuzi ya ukuajiwa kiuchumi nchini Tanzania. Sura ya tatu inajadili aina ya mageuzi ya kiuchumi tunayohitaji, wakati sura ya nneinatoa hitimisho pamoja na maoni ya namna ya kuyafanya mageuzi ya kiuchumi ili yalete maendeleo ya binadamu.Viambatisho vya takwimu vinatoa picha halisi ya viashiria muhimu vya kijamii na kiuchumi vya maendeleo yabinadamu.Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu nchini Tanzania ya mwaka 2014 imeandaliwa kwa msaada wa mradi wa Maendeleoya Binadamu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa ambao unajumuisha mtandao wa ripoti za dunia, kandana nchi. Ripoti hii iliandaliwa kwa kuwatumia wataalamu na washauri wa ndani na kupata mrejesho kutoka kwawadau mbalimbali. Wadau hao walikuwa ni wataalamu na watekelezaji wa sera za maendeleo ikiwa ni pamoja navyombo mbalimbali vya serikali. Uandaaji wa ripoti hii umehusisha mtandao wa wasomi kutoka katika taasisi zakitaifa za utafiti na vyuo vikuu kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa. Asasi ya tafiti za Kiuchumina Kijamii (ESRF) ilikuwa mshiriki mkuu katika utekelezaji, ikifanya kazi kwa karibu na taasisi muhimu kama Ofisiya Taifa ya Takwimu, Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Zanzibar, na Idara ya Uchumi ya Chuo Kikuu chaDar es Salaam. Meneja wa mradi na sekretarieti ya uandaaji wa ripoti hii walifanya kazi za kila siku za uandaaji kwaushirikiano wa karibu na timu ya wataalamu kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Asasi ya tafiti zaKiuchumi na Kijamii, na Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Vile vile, kikosi kazi kikubwazaidi, kilichojumuisha wataalamu 35 kutoka katika taasisi mbalimbali za taifa na wakala za maendeleo, walitoa msaadamkubwa, mrejesho na mwongozo katika kipindi chote cha uandaaji wa ripoti hii. Mchakato wa uandaaji ulihusishakuwapa wataalamu kazi ya kuandika makala kumi, ambazo zilitoa maudhui muhimu kwa ajili ya uandishi wa ripotihii. Sambamba na hilo, uandaaji wa ripoti ulihusisha ukusanyaji wa kiwango kikubwa wa taarifa mbalimbali kuhusumaendeleo ya kiuchumi na kijamii, na kutengeneza majedwali yanayoonyesha viashiria vikuu vya maendeleo yabinadamu, kama ilivyowasilishwa kwenye viambatisho vya kitakwimu.Tumependa kumshukuru Dkt. Hoseana Lunogelo, Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, kwa kutoa fursa kwa asasi yakekusimamia uandaaji wa ripoti hii. Shukurani maalumu zimwendee Dkt. Tausi Kida, Mkurugenzi wa Programu waMuhtasariiii

ESRF na Meneja wa Mradi wa kuandaa ripoti hii, kwa uratibu na msaada wa kiufundi wakati wa mchakato wotewa kuandaa na kutoa ripoti hii. Shukurani za pekee ni kwa Profesa Marc Wuyts wa Taasisi ya Mafunzo ya Kijamiiya Uholanzi1 kwa mwongozo wake wa kitaaluma alioutoa katika mchakato wote. Zaidi ya hayo, shukurani za pekeeziwafikie timu iliyoandaa ripoti hii kwa umakini wao. Timu hiyo inawajumuisha Dkt. Rodgers Dhliwayo (UNDP),Bwn. Amon Manyama (UNDP), Dkt. Tausi Kida (ESRF), Dkt. Jehovaness Aikaeli (UDSM), Dkt. Kenneth Mdadila(UDSM), Bwn. Ahmed Markbel (NBS), Bwn. Sango Simba (NBS), Bwn Deogratias Mutalemwa (ESRF), Bi.Monica Githaiga (UNESCO) na Prof. Marc Wuyts (ISS). Pia, tungependa kumshukuru Dkt. Amarakoon Bandara –Mshauri wa uchumi wa zamani wa UNDP nchini Tanzania – ambaye amefanya kazi muhimu katika hatua za awaliza maandalizi ya ripoti hii kabla ya kuhamishiwa katika ofisi za UNDP nchini Zimbabwe.Shukurani zetu pia ziwafikie timu ya waandaji wa mswada wa ripoti iliyojumuisha wataalamu wafuatao: Dkt. TausiKida na Prof. Haidari Amani (sura ya 1); Dkt. Hazel Gray (sura ya 2); Prof. Gelase Mutahaba, Prof. Ernest Mallyana Dkt. Jehovaness Aikaeli (sura ya 3); Prof. Gelase Mutahaba, Prof. Ernest Mallya na Prof. Haidari Amani (suraya 4), and Dkt. Kenneth Mdadila na Dkt. John Mduma (viambatisho vya takwimu). Uandaaji wa viambatisho vyatakwimu ulifanikiwa sana kutokana na msaada mkubwa kutoka katika Ofisi za Taifa za Takwimu za Tanzania Barana Zanzibar. Kwa msingi huo, tunalazimika kuwashukuru Dkt. Albina Chuwa – Mkurugenzi Mkuu NBS – na Bwn.Mohamed Hafidh – Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar – kwa msada wao katika uandaaji waripoti hii ya mwaka 2014. Tunamshukuru Dkt. Richard Whitehead – Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Uhariri naUchapishaji iliyopo Bergen Norway – kwa kuhariri mswada wa mwisho wa ripoti hii. Tungependa kutoa shukuranizetu kwa Bwn. Nicolai Schulz kwa mchango wake katika uandaaji wa muhtasari wa ripoti na Bwn. Rashid Chuachuakwa kutafsiri muhtasari wa ripoti katika lugha ya Kiswahili. Shukurani maalumu zimfikie msanii wa Kitazania,Bwn. Haji Chilonga, kwa usanifu wa jalada la ripoti hii. Pia, tungependa kumshukuru Bi. Margareth Nzuki na timunzima ya Idara ya Mawasiliano na Maarifa ya ESRF kwa msada wao wakati wa usambazaji wa ripoti hii. Mwisho,tunamshukuru Bwn. Danford Sango (ESRF) na Bwn. Yasser Manu (ESRF) kwa mchango wao katika uandaaji waripoti hii; watu hawa ambao wanaunda sekretarieti ya mradi wa THDR, wametoa mchango mkubwa katika kuratibushughuli za siku hadi siku katika kipindi chote cha uandaaji wa ripoti hii.Tungependa kuwashukuru waandishi wafuatao wa makala za utangulizi wa ripoti hii:(i) Dkt. Tausi Kida na Prof. Haidari Amani – waandishi wa makala ya utangulizi # 1, “Hali na ukuaji wa maendeleoya binadamu nchini Tanzania”;(ii) Prof. Marc Wuyts na Dkt. Blandina Kilama – waandishi wa makala ya utangulizi # 2, “Mageuzi ya Kiuchuminchini Tanzania: Suala la manufaa au matatizo?”;(iii) Prof. Marc Wuyts na Dkt. Blandina Kilama – waandishi wa makala ya utangulizi # 3, “Mabadiliko ya Uchumiwa Tanzania: mitindo ya ulimbikizaji na mabadiliko ya kimuundo”;(iv) Dkt. Amarakoon Bandara, Prof. Rajeev Dehejia na Bwn. Shaheen Lavie-Rouse – waandishi wa makala yautangulizi # 4, “Kiungo kati ya ukuaji wa uchumi na maendeleo ya binadamu”;(v) Prof. Longinus Rutasitara na Dkt. Jehovaness Aikaeli – waandishi wa makala ya utangulizi # 5, “Utaratibu upiunahitajika ili kufikia lengo la Dira ya Maendeleo ya Tanzania la 2025?”(vi) Dkt. Razack Lokina na Prof. Anthony Leiman – waandishi wa makala ya utangulizi # 6, “Usimamizi wa maliasiliza madini na gesi kwa ajili ya ukuaji endelevu na maendeleo ya binadamu nchini Tanzania”;(vii) Prof. Alfred Agwanda na Prof. Haidari Amani – waandishi wa makala ya utangulizi # 7, “Ongezeko la idadi yawatu, muundo na mwenendo wake nchini Tanzania”;(viii) Prof. Phares Mujinja na Dkt. Tausi Kida – waandishi wa makala ya utangulizi # 8, “Matokeo ya mabadilikoya sekta ya afya nchini Tanzania: sera, viashiria na upatikanaji wa huduma za afya”;(ix) Prof. Suleman Sumra and Dkt. Joviter Katabaro – waandishi wa makala ya utangulizi # 9, “Kushuka kwa ubora1ivISS—Institute of Social StudiesTANZANIA HUMAN DEVELOPMENT REPORT 2014

wa elimu nchini Tanzania: mapendekezo ya kukabiliana na mwenendo huu”;(x) Prof. Flora Kessy na Bi. Mashavu Omar – waandishi wa makala ya utangulizi # 10, “Hali halisi ya maendeleo yabinadamu na matarajio ya Zanzibar kuifikia Dira ya Maendeleo 2020”.Maandalizi ya Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya mwaka 2014 yamenufaika kwa kiasi kikubwa kutokana namrejesho na mwongozo uliotolewa na wajumbe wa kikosi kazi cha kuandaa ripoti, chini ya uenyekiti wa Dkt. ServaciusLikwelile – Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Wajumbe wengine walitokeakatika ofisi zifuatazo: Wizara ya Fedha, ESRF, NBS, Tume ya Mipango, Ofisi ya Rais, Wizara ya Afya na Ustawi waJamii, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Mtakwimu Mkuuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (OCGS), UDSM, REPOA, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), Taasisiya UONGOZI, Hakielimu, UNDP, Shirika la Kazi Duniani, Benki ya Dunia, Shirika la Afya la Dunia, UNICEF,Bunge la Tanzania, Jukwaa la Utu wa Watoto2 na Shirika la Kimataifa la Kusaidia Wazee.3 Tungependa kuwashukuruwajumbe wa kikosi kazi cha uandaaji wa ripoti kwa msaada wao usio na kikomo katika kipindi chote cha uandaajiwa ripoti hii.Uzinduzi rasmi wa mradi wa kuandaa Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya Tanzania ulifanyika bungeni tarehe31 Agosti, 2013 na ulihudhuriwa na wabunge zaidi ya 200. Tukio hilo lilitumika kama fursa ya kuomba ushaurikwa wabunge kuhusu mada kuu ya ripoti ya mwaka 2014. Kwa heshima kubwa, tunamshukuru Mh. Shamsi VuaiNahodha, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa wa wakati huo, ambaye alizindua tukio hili kwa niaba yaMh. Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Serikali ya Tanzania. Tunaishukuru Ofisi ya Bunge, inayoongozwana Mh. Spika Anne Makinda, kwa ukarimu wake katika kufanikisha mradi wa uandaaji wa ripoti na Mh. Job Ndungai,Naibu wa Spika, kwa kuongoza shughuli ya uzinduzi wa mradi wa THDR. Shukurani maalumu ziwafikie wabungewote walioshiriki katika sherehe za uzinduzi na kwa michango yao kuhusu mada kuu ya ripoti ya mwaka 2014.Hatimaye, tunashukuru kwa busara na mwongozo uliotolewa na Mh. Prof. Jakaya Mrisho Kikwete wakati waKongamano la Kitaifa lililoandaliwa na ESRF kuhusu “Kufungua Fursa za Kukuza Uchumi: Mageuzi ya Kiuchumikwa Maendeleo ya Binadamu, lililofanyika tarehe 11 Septemba, 2014. Mada kuu ya kongamano hilo la kitaifailitokana na Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya mwaka 2014, na kongamano lilihusisha uwasilishaji wa mada namajadiliano kuhusu makala kumi za utangulizi. Ni matumaini yetu kuwa ripoti hii itatoa uelewa mpana kuhusuuhusiano kati ya mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya binadamu nchini Tanzania — changamoto zake, fursa zakena vikwazo vyake. Zaidi ya hayo, pia tuna matumaini kuwa ripoti itatumika kama zana ya kuchochea uchaguzi mzuriwa sera, kufanya maamuzi sahihi, na hivyo kuleta mabadiliko nchini.Dkt. Servacius LikwelileKatibu Mkuu,Wizara ya Fedha,Tanzania23Bwn. Alvaro RodriguezMratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa naMwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleola Umoja wa Mataifa,TanzaniaChildren’s Dignity ForumHelp Age InternationalMuhtasariv

YaliyomoDibajiYaliyomoOrodha ya ramaniOrodha ya vielelezoVifupisho vya manenoUtanguliziiiiviviviviiviiiSura ya 1Hali ya maendeleo ya binadamu nchini TanzaniaMambo muhimu ya Maendeleo ya BinadamuIdadi ya Watu na Maendeleo ya Binadamu nchini Tanzania134Sura ya 2Mageuzi ya kiuchumi yanayoendelea: Kuangalia zaidi ya Ukuaji wa uchumiMwanzo wa Mageuzi ya KimuundoAjira na Mageuzi ya kiuchumi568Sura ya 3Ukuaji wa uchumi na maendeleo ya binadamu: Msisitizo katika mabadiliko ya sera za uchumiHistoria ya Sera za Uchumi za Tanzania tangu 1961Masuala muhimu na Vikwazo kwa Mustakabali wa Sera za Uchumi101011Sura ya 4Kuyafanya mageuzi ya kiuchumi yalete maendeleo ya binadamu nchini TanzaniaMageuzi Muhimu ya KiuchumiMambo Muhimu katika Kuhakikisha Uhusiano Wenye Manufaa kati ya Mageuzi ya Kiuchumi na Maendeleo ya BinadamuUjumbe Mahususi13131516Orodha ya ramaniRamani ya 1: Mgawanyo wa mikoa ya Tanzania Bara kulingana na kipimo cha Maendeleo ya Binadamu (HDI) kitaifa1Ramani ya 2: Mikoa ya Tanzania Bara ikioanishwa na kipimo cha HDI cha kimataifa 2Orodha ya vielelezoKielelezo cha 1: Hali ya Umasikini kwa mujibu wa Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya (HBS) na Kipimo cha Umasikinikwa kutumia Vigezo mbalimbali (MPI), Tanzania Bara3Kielelezo cha 2: Mabadiliko ya pato halisi la Taifa kwa mwaka (kwa silimia)5Kielelezo cha 3: Mchango wa kisekta kwenye Pato la Taifa (%) 1998-20126Kielelezo cha 4: Viwango vya ukuaji wa kisekta 1999-20126Kielelezo cha 5: Viwango vya ukuaji wa sekta ndogo za huduma7Kielelezo cha 6: Mgawanyo wa ajira katika sekta kuu (%)8Kielelezo cha 7: Kiwango cha ongezeko la watu wanaofanya na wasiofanya kazi14viTANZANIA HUMAN DEVELOPMENT REPORT 2014

Vifupisho vya DISUATHDRUDSMUNESCOUNICEFUNDPDepartment for International DevelopmentEconomic and Social Research FoundationGross Domestic ProductHousehold Budget SurveyHuman Development IndexHighly Indebted Poor CountriesIntergrated Labour Force SurveyInstitute of Social StudiesMkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini TanzaniaMulti Dimensional Poverty IndexNational Bureau of StatisticsOxford Poverty and Human Development InitiativeSokoine University of AgricultureTanzania Human Development ReportUniversity of Dar es SalaamUnited Nations Educational Scientific and Cultural OrganizationUnited Nations Children’s FundUnited Nations Development ProgrammeMuhtasarivii

UtanguliziKatika muongo ulipita, Tanzania imeshuhudia ukuaji mzuri wa Pato la Taifa wa kiwango cha wastani wa asilimia 7. Hatahivyo, kinyume cha matarajio ya wengi, ukuaji huu haukwenda sambamba na kupungua kwa umasikini, isipokuwakwa maeneo machache, kama vile, kupunguza kiwango cha vifo vya watoto na kuongezeka kwa uandikishwaji wawanafunzi. Kwa jumla kiwango cha maendeleo ya binadamu nchini Tanzania hakiridhishi. Nchi imeshuka kwa nafasisaba katika vigezo vya maendeleo ya binadamu vya Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) vya mwaka2014. Ukuaji wa kiuchumi umeshindwa kuongeza uwezo wa wananchi walio wengi kuishi maisha bora.Ripoti hii inaonyesha kuwa ukuaji wa uchumi, japo ni jambo muhimu na linalohitajika lakini halitoshi. Tanzaniahaipaswi kutilia mkazo matokeo ya jumla pekee katika ukuaji wa uchumi, bali msisitizo uwekwe kwenye mabadilikoya ubora wa uzalishaji unaokwenda sambamba na mchakato wa ukuaji wa uchumi. Nchi inahitaji mageuzi yakiuchumi yanayoleta maendeleo ya binadamu. Mageuzi ya kiuchumi maana yake ni mabadiliko ya muundo katikauchumi, yanayoambatana na mchango mdogo kutoka katika sekta ya kilimo na mchango mkubwa kutoka katikasekta ya viwanda na utoaji huduma, vinavyokwenda sambamba na mageuzi katika kupunguza viwango vya uzazina vifo. Ili mageuzi ya kiuchumi yalete maendeleo ya binadamu, ni muhimu mageuzi hayo yaende sambamba nakutengeneza fursa za ajira, kukuza kipato, pamoja na kuongeza huduma za jamii. Tukiieleza dhana hii kwa namnanyingine, mageuzi ya kiuchumi yenye tija, yanakwenda sambamba na kupungua kwa umasikini kwa kiasi kikubwa nakuboreshwa kwa viwango vya maisha ya binadamu. Utoaji wa huduma bora za jamii, kama vile, afya, elimu, na majisafi ni muhimu katika kuhakikisha ushiriki wa Watanzania katika shughuli za kiuchumi. Kwa mwongozo na uongoziimara wa serikali, pamoja na sekta binafsi, mageuzi ya kiuchumi yanaweza kuongeza uzalishaji, kutengeneza ajira, nakuhakikisha uwepo wa huduma za jamii, na hivyo kuleta maendeleo ya binadamu.Muhtasari huu unafuata muundo wa ripoti kuu ya Maendeleo ya Binadamu Tanzania ya 2014: Sehemu ya (I) inafanyauchambuzi kuhusu hali ya maendeleo ya binadamu nchini Tanzania na kutoa maelezo kuhusu mabadiliko mawiliya kidemografia ambayo ni muhimu ili kuelewa mageuzi ya kiuchumi. Sehemu ya (II) inatoa ufafanuzi wa kinakuhusu dhana ya mageuzi ya kiuchumi na kuchambua mageuzi ya kiuchumi yanayotokea hivi sasa nchini Tanzania.Inaeleza umuhimu wa sera za kiuchumi kwa mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya binadamu. Sehemu ya (III)inatoa muhtasari wa historia ya sera na mageuzi ya kiuchumi nchini Tanzania tangu uhuru hadi sasa. Sehemu ya (IV)inapendekeza hatua na sera zinazoweza kufanya mageuzi ya kiuchumi yalete maendeleo ya binadamu nchini Tanzania.Hitimisho linatoa muhtasari wa matokeo ya ripoti na kutoa mapendekezo kupitia maeneo muhimu saba.viiiTANZANIA HUMAN DEVELOPMENT REPORT 2014

1.Halimaendeleoya binadamunchini TanzaniaHALIyaYAMAENDELEOYA BINADAMUNCHINITANZANIAMaendeleo ya binadamu ni dhana inayojulikana sana nchini Tanzania. Tangu mwaka 1973, Rais wa kwanza na Babawa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alikwishajenga uelewa kuhusu dhana hii sambamba nafikra za mwanafalsafa maarufu Amartya Sen pamoja na mtazamo wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifakuhusu namna ya kushughulikia maendeleo ya binadamu. Nyerere aliona kwamba kukua kwa uchumi ni moja tukati ya nyenzo za kuleta maendeleo kwa Watanzania. Baadaye, Sen alisema maendeleo ya binadamu ni mchakato wakuongeza uwezo wa watu kuishi maisha bo

wa elimu nchini Tanzania: mapendekezo ya kukabiliana na mwenendo huu”; (x) Prof. Flora Kessy na Bi. Mashavu Omar – waandishi wa makala ya utangulizi # 10, “Hali halisi ya maendeleo ya binadamu na matarajio ya Za

Related Documents:

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu na zile za awali ni kwamba ukuaji wa kiuchumi pekee hauchangii kiotomatiki ukuaji wa maendeleo ya binadamu. Sera zinazotetea maskini na uwekezaji wenye maana katika uwezo wa watu – kupitia kwa kusisitiza elimu, lishe na afya, na ujuzi wa

Mradi wa WOLTS Tanzania – Muhtasari wa Ripoti--Mundarara, Agosti 2017 – Kiswahili E. Daley, K. Lanz, A. Mhinda, Z. Driscoll, J. Ndakaru, J. Grabham na E. Kereri 3 kuwa ni mkuu wa kaya ya mke mwingine. Tulidhani kuwa inawezekana, hata hivyo, baadhi ya wakuu wa kaya wanawake walitengwa na w

RIPOTI YA DUNIA YA UFUATILIAJI WA ELIMU ilIcMUHTASARI Dibaji Ripoti yaDunia ya Ufuatiliaji wa Elimu ya mwaka wa 2019imeandaliwa kwa kuwashirikisha timu ya wahamiaji wa kimataifa. Wanne kati yao ni watoto wa wakimbizi. Ha

MUHTASARI WA RIPOTI YA KAMATI YA BAJETI YA BARAZA LA WAWAKILISHI- ZANZIBAR KWA MWAKA WA FEDHA 2017/2018 . kutoa elimu maskulini na michezo. . ambapo Serikali imemuekea sharti la kuanza kuendeleza eneo alilopat

Kufuatilia majibu ya hoja za ukaguzi yaliyotolewa katika ripoti ya ukaguzi ya awali ili kuweza kujiridhisha na majibu ya hoja hizo. Kutoa ripoti ya ukaguzi ya mwisho kwa taasisi zinazokaguliwa inayoonesha hoja za ukaguzi zilizotolewa katika ripoti ya ukaguzi ya awali ambazo hazikupa

WILAYA YA KIRINYAGA YA KATI 2015 102/1- KISWAHILI KARATASI YA 1 - MWONGOZO WA KUSAHIHISHA 1. SWALI LA LAZIMA SURA (i) Kichwa / Anwani ya ripoti. - Ripoti ni ya nini, nani, nani aliteua jopo na mwaka. (ii) Utangulizi - Nani alitaka ripoti iandikwe. - Muda waliopewa - Tatizo lenyewe - Wanajopo na vyeo vyao. (iii) Mbinu za uchunguzi

TARP Tanzania Agricultural Research Project TAWIRI Tanzania Wildlife Research Institute TAWLAE Tanzania Association of Women Leaders in Agriculture and Environment TBC Tanzania Broadcasting Cooperation TBS Tanzania Bureau of Standard TCC Tanzania Communications Commission TCCIA Tanzan

While opening an AutoCAD 2000 drawing, you can use the Partial Open option to work with only part of the drawing file. If you are working with a large drawing, you can partially open the drawing and select a specific view and layers to work with instead of loading the entire drawing. See “Using Par- tial Open and Partial Load” on page 311. To open a drawing 1 In the Startup dialog box .