Maarifa Ya Jamii - Necta

1y ago
26 Views
2 Downloads
1.35 MB
73 Pages
Last View : 12d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Gia Hauser
Transcription

BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIATAARIFA YA UCHAMBUZI WA MAJIBU YAWATAHINIWA KATIKA MASWALI YA MTIHANIWA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI MWAKA2019MAARIFA YA JAMII

BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIATAARIFA YA UCHAMBUZI WA MAJIBU YAWATAHINIWA KATIKA MASWALI YA MTIHANI WAKUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2019MAARIFA YA JAMIIi

Kimechapwa naBaraza la Mitihani la Tanzania,S. L. P. 2624,Dar es Salaam, Tanzania. Baraza la Mitihani la Tanzania, 2019Haki zote zimehifadhiwa.ii

YALIYOMODIBAJI . iii1.0UTANGULIZI . 12.0UCHAMBUZI WA MAJIBU YA WATAHINIWA KATIKA KILA SWALI. 22.1. Sehemu A . 22.1.1. Kipengele I: Uraia . 22.1.2. Kipengele II: Historia .192.1.3. Kipengele III: Jiografia .352.2. Sehemu B . 503.0UCHAMBUZI WA KUFAULU KWA WATAHINIWA KATIKA KILAMADA . 584.0HITIMISHO . 615.0MAPENDEKEZO . 62KIAMBATISHO . 64iii

DIBAJITaarifa hii ya uchambuzi wa majibu ya maswali ya Mtihani wa Kumaliza Elimuya Msingi mwaka 2019 kwa somo la Maarifa ya Jamii imeandaliwa kwa lengola kutoa mrejesho kwa watahiniwa, walimu, watunga sera, watunga mitaalana wadau wengine wa elimu. Majibu ya watahiniwa katika mtihani ni kiashiriakimojawapo kinachoonesha maarifa, stadi na mielekeo ambayo watahiniwawaliweza kupata au kutopata katika kipindi cha miaka saba ya Elimu yaMsingi.Katika taarifa hii, sababu mbalimbali zilizosababisha watahiniwa kuweza aukushindwa kujibu maswali kwa usahihi zimeainishwa. Uchambuzi unaoneshakuwa watahiniwa waliopata alama za juu walikuwa na maarifayaliyowawezesha kubaini matakwa ya maswali au kuhawilisha maarifa ilihaliwatahiniwa waliokuwa na uelewa mdogo hawakuweza kubaini matakwa yamaswali au kuhawilisha maarifa. Kimsingi, watahiniwa wengi waliopata alamaza chini waliandika majibu yasiyo sahihi ilhali wengine hawakujibu baadhi yamaswali au walichagua jibu zaidi ya moja kinyume na maelekezo ya mtihani.Uchambuzi wa kila swali umefanyika ambapo dosari mbalimbali walizooneshawatahiniwa wakati wa kujibu maswali zimeainishwa. Aidha, ulinganifu wakiwango cha kufaulu kati ya mwaka 2018 na 2019 kwa kila mada umefanyikaili kuonesha kupanda au kushuka kwa kiwango cha kufaulu katika kila mada.Baraza la Mitihani la Tanzania lina imani kuwa mrejesho huu utawawezeshawadau mbalimbali wa elimu kuchukua hatua madhubuti ili kuboreshaufundishaji na ujifunzaji. Ni matumaini ya Baraza la Mitihani kuwa mamlakahusika zitahakikisha kuwa dosari zilizoainishwa katika taarifa hii zinapatiwaufumbuzi ili kuongeza ujuzi na maarifa kwa watahiniwa wanaotarajiwakuhitimu elimu ya msingi miaka ijayo. Mwisho, Baraza la Mitihani linapendakutoa shukrani za dhati kwa Maafisa Mitihani, na wengine wote waliohusikakatika kuandaa taarifa hii.Dkt. Charles E. MsondeKATIBU MTENDAJIiv

1.0 UTANGULIZIMtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE 2019) ulifanyika tarehe 11na 12 ya mwezi Septemba, 2019. Katika mtihani huo, somo la Maarifa yaJamii lilifanyika tarehe 11/09/2019. Jumla ya watahiniwa 947,077walisajiliwa kufanya mtihani huo ambapo watahiniwa 933,335 sawa naasilimia 98.6 walifanya mtihani wa somo la Maarifa ya Jamii. Uchambuziwa majibu ya mtihani wa Maarifa ya Jamii unaonesha kuwa watahiniwa714,341 sawa na asilimia 76.63% walifaulu.Somo la Maarifa ya Jamii katika mtihani wa PSLE 2019 lilikuwa na jumlaya maswali 40 ya kuchagua na 5 ya majibu mafupi yaliyokuwayamegawanyika katika sehemu kuu mbili A na B. Sehemu A ilikuwa namaswali 40 ya kuchagua ambayo yalikuwa yamegawanyika katikavipengele vitatu. Kipengele cha I: Uraia – kilichokuwa na maswali 12,kipengele cha II: Historia – kilichokuwa na maswali 14 na kipengele chaIII: Jiografia kilichokuwa na maswali 14. Sehemu B ilikuwa na maswali 5ya majibu mafupi ambayo ni swali 1 la Uraia, maswali 2 ya Historia namaswali ya mwisho 2 ya somo la Jiografia.Watahiniwa walitakiwa kujibu maswali yote kutoka katika sehemu zotembili. Aidha, katika swali la 1 - 40 watahiniwa walipewa machaguomatano katika kila swali, ambayo kati yake kulikuwa na jibu sahihi.Watahiniwa walitakiwa kuchagua jibu sahihi na kisha kuweka kivuli katikaherufi ya jibu sahihi katika fomu maalum ya kujibia (OMR). Katika kujibuswali la 41 – 45 watahiniwa walielekezwa kuandika majibu yao katikanafasi zilizoachwa wazi kwa kutumia kalamu ya wino wa bluu au mweusi.Katika taarifa hii, herufi ya jibu sahihi imewekewa alama ya nyota (*)katika majedwali na chati. Zaidi ya hayo, asilimia ya watahiniwa ambaohawakufuata maelekezo ya namna ya kujibu swali iliwekwa katikauchambuzi na kupewa jina “Mengine” ikimaanisha watahiniwa ambaohawakujibu kabisa swali husika au walichagua jibu zaidi ya moja kamainavyoonekana katika majedwali na chati.Katika uchambuzi huu, idadi yawatahiniwa na asilimia yao katika kila chaguo umeoneshwa. Ubora wakiwango cha kufaulu kwa watahiniwa katika kila swali utategemea idadiya watahiniwa waliochagua jibu sahihi. Katika uchambuzi huu pia, sababuza watahiniwa kuchagua jibu, vipotoshi zimebainishwa.Katika uchambuzi huu, ukokotoaji wa kiwango cha kufaulu utategemeaidadi ya watahiniwa waliochagua au kuandika jibu sahihi kama ifuatavyo;1

endapo watahiniwa asilimia 0 hadi 39 ndio watakaokuwa wamechagua aukuandika jibu sahihi, ufaulu katika swali au mada hiyo utaelezwa kuwa nihafifu. Kwa upande mwingine, endapo watahiniwa kati ya asilimia 40 hadi59 watakuwa wamechagua au kuandika jibu sahihi, ufaulu katika swalihilo utaelezwa kuwa ni wa wastani. Aidha, ufaulu katika swali au madautaelezwa kuwa mzuri endapo watahiniwa asilimia 60 au zaidi watakuwawamechagua au kuandika jibu sahihi.2.0 UCHAMBUZI WA MAJIBU YA WATAHINIWA KATIKA KILA SWALI2.1.Sehemu A2.1.1. Kipengele I: UraiaSwali la 1: Kwa nini ni muhimu kuwa na wimbo wa shule?A Ni utambulisho wa shuleB Huendeleza utamaduni wa taifaC Huunganisha taifaD Huhamasisha uzalendoE Huwaenzi walimuSwali hili lilitoka katika mada ya Alama za Shule na za Taifa na lililengakupima uelewa wa watahiniwa kuhusu umuhimu wa kuwa na wimbowa shule. Kiwango cha kufaulu katika swali hili kilikuwa kizuri ambapowatahiniwa 697,707 (74.75%) waliweza kuchagua jibu sahihi A, Niutambulisho wa shule. Ni wazi kuwa watahiniwa walikuwa na uelewawa kutosha kuhusu umuhimu wa wimbo wa shule kwani kila shule inawimbo wake ambao mara nyingi huimbwa katika shule husika. Kwamisingi hiyo watahiniwa waliweza kuhamisha uzoefu wa maisha yao yakila siku na kubaini jibu sahihi. Alama nyingine zinazotambulisha shuleni nembo ya shule, kauli mbiu ya shule na mipaka ya shule. Chati Na.1inaonesha ufaulu wa watahiniwa katika swali la 1.2

Chati Na. 1 Asilimia ya watahiniwa katika kila chaguo katika swali la 1.Chati Na. 1 inaonyesha kiwango kizuri cha kufaulu kwa watahiniwakwani asilimia 74.75 walichagua jibu sahihi.Kwa upande mwingine, watahiniwa wengine walichagua majibu yasiyosahihi kama ifuatavyo: watahiniwa 115,426 (12.37%) walichaguakipotoshi B Huendeleza utamaduni wa taifa; walichagua kipotoshi hikiwalifikiri kuwa wimbo wa shule ni kielelezo cha utamaduni wa potoshiC,Huunganisha taifa. Watahiniwa hao walishindwa kutofautisha kati yamchango wa wimbo wa shule na wa Taifa. Wimbo wa taifa unawezakuunganisha taifa mfano ubeti wa “Mungu ibariki Tanzania”; nakwamba wimbo wa shule ni maalumu kwa ajili ya mazingira ya shulehusika na sio kwa taifa zima. Watahiniwa 65,339 (7.00%) walichaguakipotoshi D Huhamasisha uzalendo; hawakuwa na ufahamu kuwawimbo wa shule hutambulisha shule na hauhamasishi uzalendo.Uzalendo ni hali ya mtu kuipenda nchi yake na kuwa tayari kuilinda.Mwisho, watahiniwa 18,338 (1.96%) walichagua jibu lisilo sahihi E,Huwaenzi walimu. Watahiniwa hao wanaonesha kuwa walikuwa nauelewa mdogo kuhusu umuhimu wa wimbo wa shule na kwambawimbo wa shule hauenzi walimu waliopo shuleni bali husaidiakuitofautisha shule moja na nyingine.3

Swali la 2: Ipi ni kazi ya Afisa Mtendaji wa kijiji?A Kuongoza vikao vyote vya serikali ya kijijiB Kuteua wajumbe wa kamati mbalimbaliC Kusimamia uchaguzi wa serikali ya kijijiD Kukusanya mapato kutoka vyanzo mbalimbali katikakijijiE Kutoa adhabu kwa wahalifu katika kijijiSwali lilitungwa kutoka mada ya Serikali za Mitaa na liliwatakawatahiniwa kubaini jukumu la Afisa Mtendaji wa kijiji. Kufaulu kwawatahiniwa katika swali hili kulikuwa hafifu ambapo watahiniwa107,120 (11.48%) waliweza kuchagua jibu sahihi C, Kusimamiauchaguzi wa serikali ya kijiji. Pamoja na kazi hiyo, Afisa Mtendaji waKijiji ana majukumu ya kusimamia mkutano mkuu wa kijiji kwakushirikiana na mwenyekiti wa serikali ya kijiji, kusimamia upatikanajiwa huduma za kijamii katika eneo lake la utawala na kuongoza kamatimbalimbali za serikali ya kijiji. Chati Na.2 inaonesha kiwango hafifu chaufaulu wa watahiniwa katika swali la 2.Chati Na. 2: Asilimia ya watahiniwa katika kila chaguo katika swali la 2.Aidha, watahiniwa 403,924 (43.28%) waliochagua kipotoshi A,Kuongoza vikao vyote vya kijiji; hawakujua kuwa Mwenyekiti waSerikali ya kijiji ndiye huongoza mikutano ya serikali ya kijiji. Vilevile,watahiniwa 103,323 (11.07%) walichagua kipotoshi B, Kuteuawajumbe wa kamati mbalimbali. Watahiniwa hawakuelewa kuwa4

Wajumbe wa kamati mbalimbali ya kijiji huteuliwa na halmashauri yakijiji, na siyo Afisa Mtendaji wa kijiji. Watahiniwa 258,246 (27.67%)walichagua kipotoshi D, Kukusanya mapato kutoka vyanzo mbalimbalikatika kijiji. Vyanzo vya mapato ya kijiji husimamiwa na serikali ya kijijina siyo Afisa Mtendaji wa Kijiji. Mwisho, watahiniwa 54,778 (5.87%)walivutiwa na kipotoshi E, Kutoa adhabu kwa wahalifu katikakijiji.Watahiniwa hawa hawakujua kuwa ulinzi na usalama katika kijijihusimamiwa na kamati ya ulinzi ya kijiji na wala siyo Afisa Mtendaji wakijiji.Swali la 3: Kipi ni kiashiria cha utawala bora katika jamii?A Idadi kubwa ya wanasheria B Idadi kubwa ya magerezaC Idadi kubwa ya wafungwa D Idadi ndogo ya wafungwaE Uongozi unaofuata sheriaSwali hili lilitungwa kutoka katika mada ya Misingi ya Demokrasia nalililenga kupima maarifa ya watahiniwa kuhusu viashiria vya utawalabora. Kiwango cha ufaulu katika swali hili kilikuwa kizuri ambapowatahiniwa 785,918 (84.20%) walichagua jibu sahihi E,Uongoziunaofuata sheria. watahiniwa ambao walichagua jibu sahihi walikuwana uelewa mzuri juu ya misingi ya utawala bora. Baadhi ya viashiriavingine vya utawala bora ni kuzingatia haki za binadamu, katiba yakidemokrasia, ushirikishwaji wa wananchi, uhuru wa vyombo vyahabari na uwazi. Chati Na.3 inaonesha kiwango kizuri cha ufaulu wawatahiniwa katika swali la 3.Chati Na. 3: Asilimia ya watahiniwa katika kila chaguo katika swali la 35

Chati Na. 3 inaonyesha kiwango kizuri cha ufaulu wa watahiniwa kwaniasilimia 84.20 waliweza kuchagua jibu sahihi.Chaguo A, Idadi kubwa ya wanasheria, lilivutia watahiniwa 53,946(5.78%) ambao hawakujua kuwa, kuwa na idadi kubwa ya wanasheriahakuhakikishi uwepo wa utawala bora. Pia, watahiniwa 26,014 (2.79%)walichagua kipotoshi B, Idadi kubwa ya magereza, Watahiniwa 33,787(3.62%) walichagua kipotoshi C, Idadi kubwa ya wafungwa na mwishowatahiniwa 28,604 (3.06%) walichagua kipotoshi D, Idadi ndogo yawafungwa. Watahiniwa wote hawa walichagua vipotoshi kutokana nakutoelewa kuwa magereza ni sehemu ambayo watu waliopatikana namakosa hutunzwa, na uwepo wa idadi kubwa au ndogo ya wafungwasio kiashiria cha utawala bora. Aidha, serikali duniani kote zina hudumaza magereza bila kujali uwepo au kutokuwepo kwa utawala bora.Swali la 4: Yupi kati ya wafuatao ni kiongozi wa sekretariati ya Bungela Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?A Naibu spikaB Waziri MkuuC Katibu wa BungeD SpikaE Mwenyekiti wa BungeSwali hili lilitungwa kutoka kwenye mada ya Katiba ya Jamhuri yaMuungano wa Tanzania na liliwataka watahiniwa kubaini kiongozi waSekretarieti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kiwangocha ufaulu wa watahiniwa kilikuwa hafifu, ambapo watahiniwa 132,381(14.18%) tu ndio walichagua jibu sahihi C, Katibu wa Bunge. Katibu waBunge ndiye mtendaji mkuu katika ofisi ya Bunge la Jamhuri yaMuungano wa Tanzania, mshauri wa Spika katika mambo yote yautawala na ndiye kiongozi wa Sekretarieti ya Bunge la Jamhuri yaMuungano wa Tanzania. Jukumu la Sekretarieti ya Bunge la Jamhuriya Muungano wa Tanzania ni kuhakikisha kuna ufanisi katikautekelezaji wa shughuli za Bunge. Chati Na.4 inaonesha kiwango chaufaulu wa watahiniwa katika swali la 4.6

Chati Na.4: Asilimia ya watahiniwa katika kila chaguo katika swali la 4Chati Na. 4 inaonesha kiwango hafifu cha kufaulu kwa watahiniwakatika swali la 4 kwani ni asilimia 14.18 tu walioweza kuchagua jibusahihi.Kwa upande mwingine, chaguo A, Naibu Spika, liliwavutia watahiniwa165,292 (17.71%) ambao hawakuwa na ufahamu wa jukumu la NaibuSpika. Naibu spika huendesha vikao vya Bunge wakati Spika hayupo.Watahiniwa 323,487 (34.66%) walichagua kipotoshi B, Waziri Mkuubila kujua kuwa Waziri Mkuu ni kiongozi mkuu wa shughuli zote zaserikali Bungeni. Vilevile chaguo D, Spika lilivutia watahiniwa 243,511(26.09%). Watahiniwa waliochagua jibu hili hawakuwa na uelewa kuwaSpika wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ndiye kiongozi mkuu washughuli zote za Bunge. Pia huwakilisha wabunge katika vikao vinginevyote nje ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mwishowatahiniwa 62,300 (6.67%) ambao walichagua kipotoshi E Mwenyekitiwa Bunge hawakufahamu kuwa Mwenyekiti wa Bunge huongoza vikaovya Bunge endapo Spika na Naibu Spika hawapo. Kwa ujumlawatahiniwa waliochagua vipotoshi hawakufahamu muundo wa uongoziwa sekretarieti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.7

Swali la 5: Ipi kati ya zifuatazo ni sifa za uchaguzi huru na wa haki?A Kuwepo na waangalizi wa uchaguzi kutoka nchinyingineB Uhuru wa wapiga kura kushangilia barabaraniC Askari polisi kupewa mamlaka kuhesabu kuraD Watu kupiga kura kupitia sanduku la siriE Watu kupiga kura kwa kunyosha mkonoJedwali Na. 1: Idadi na asilimia ya watahiniwa kwa kila chaguoMachaguoIdadi yawatahiniwaAsilimia 2103,1336,84816.509.4010.3651.9511.050.73Katika jedwali la 1 kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa ni cha wastanikwani asilimia 51.95 walichagua jibu sahihi.Swali lilitungwa kutoka katika mada ya Demokrasia na lilipima maarifaya watahiniwa kuhusu sifa za uchaguzi huru na wa haki. Kama JedwaliNa. 1 linavyoonesha kufaulu katika swali hili kulikuwa kwa wastaniambapo watahiniwa 484,852 (51.95%) waliweza kuchagua jibu sahihiD, watu kupiga kura kupitia sanduku la siri. Sanduku la siri la kupigiakura ni mojawapo ya sifa za uchaguzi huru na wa haki. Sanduku la sirila kura humwezesha mpiga kura kutumia haki yake ya kidemokrasiakuchagua viongozi wake anaowapenda bila hofu au vitisho. Sifanyingine za uchaguzi ulio huru na haki ni haki sawa kwa vyama vyasiasa na wagombea, kampeni huru kwa vyama vyote vya siasa,kupewa nafasi sawa wakati wa kampeni ili kuwafikia wapiga kura nchinzima, kuwepo kwa chombo huru cha kusimamia uchaguzi, uchaguziusiobagua chama cha siasa au mgombea, kampeni huru kwa vyamavyote vya siasa na haki sawa kutumia vyombo vya habari ili kunadisera za vyama wakati wa kampeni za uchaguzi.Hata hivyo, watahiniwa wengine 154,036 (16.50%) walichaguakipotoshi A, Kuwepo kwa waangalizi kutoka nje. Watahiniwahawakutambua kwamba waangalizi kutoka nje ya nchi hawahusikikatika usimamizi wa uchaguzi. Hivyo, uwepo wao hauhakikishi uwepowa uchaguzi ulio huru na haki. Watahiniwa 103,133 (11.05%)walichagua jibu lisilo sahihi E, Watu kupiga kura kwa kunyosha mkono,8

hawakujua kuwa, kunyosha mikono wakati wa kupiga kura hakutoi hakikwa watu kupiga kura kwa viongozi wanaowataka bila hofu au vitisho.Ukweli ni kwamba zoezi la kupiga kura kwa kunyosha mkono nisehemu ya demokrasia ya moja kwa moja ambayo inafaa katika eneodogo la kijiografia au idadi ndogo ya watu. Pia, watahiniwa 96,702(10.36%) walichagua kipotoshi C, Askali polisi kupewa mamlaka yakuhesabu kura. Katika uchaguzi huru na wa haki Jeshi la Polisilinawajibu wa kutoa ulinzi kwa wagombea wa vyama vyote vya siasawakati wa mikutano ya kampeni za uchaguzi na siku ya kupiga kura.Mwisho,watahiniwa 87,772 (9.40%) walichagua kipotoshi B, Uhuru wawapiga kura kushangilia barabarani. Watahiniwa hao hawakutambuakuwa kushangilia barabarani/ mitaani siyo sifa ya uchaguzi huru na wahaki. Kitu cha muhimu ni taratibu za uchaguzi zinazozingatia maadili yauchaguzi yaliyokubalika na wadau wote wa uchaguzi wakati wauchaguzi.Swali la 6: Ipi kati ya zifuatazo ni tahadhari ya kuchukua kabla yakuvuka barabara sehemu ambayo hakuna alamamilia autaa za barabarani?AKuangalia kushoto na kulia kabla ya kuvukabarabaraBKuangalia kulia, kushoto na kulia tena kabla yakuvuka barabaraCKuangalia nyuma, kulia, mbele na kushoto kabla yakuvuka barabaraDKuangalia mbele na nyuma kabla ya kuvukabarabaraEKuangalia kulia, kushoto na kukimbia kuvukabarabaraSwali lilitungwa kutoka mada ya Ulinzi na usalama katika ngazi yaShule/Taifa. Swali hili lililenga kupima uelewa wa watahiniwa juu yatahadhari za usalama barabarani. Kiwango cha ufaulu wa watahiniwakilikuwa hafifu ambapo watahiniwa 357,640 (38.32%) tu ndio waliwezakuchagua jibu sahihi B, kuangalia kulia, kushoto na kulia tena kabla yakuvuka barabara. Watahiniwa waliobaini jibu sahihi walikuwa naufahamu wa tahadhari za usalama barabarani zinazoweza kuchukuliwawakati wa kuvuka barabara upande wa pili. Tahadhari nyingine nipamoja na waenda kwa miguu kutembea upande wa kulia wa9

barabara. Katika maeneo ya mijini sehemu zenye barabara za lamiwaenda kwa miguu wanashauriwa kuvuka sehemu zenye alamamilia.Chati Na.5 inaonesha ufaulu wa watahiniwa katika swali la 6.Chati Na.5: Ufaulu kwa watahiniwa katika swali la 6Kwa upande mwingine, watahiniwa 326,017 (34.93%) walichagua jibulisilo sahihi A, Kuangalia kushoto na kulia kabla ya kuvuka barabara.Pia watahiniwa 133,666 (14.32%) walichagua kipotoshi C, Kuangalianyuma, kulia, mbele na kushoto kabla ya kuvuka barabara. Watahiniwa61,239 (6.56%) walivutiwa na jibu lisilo sahihi E, Kuangalia kulia,kushoto na kukimbia kuvuka barabara na mwisho watahiniwa 50,098(5.37%) walichagua kipotoshi D, Kuangalia mbele na nyuma kabla yakuvuka barabara. Watahiniwa waliochagua vipotoshi A, C, D na Ehawakuwa na ufahamu kuhusu tahadhari ya kuchukua wakati wakuvuka barabarani. Watu wanapaswa kuwa waangalifu wanapopitabarabarani Kwa miguu. Pia matumizi sahihi ya alama za onyo Kwawatumiaji wa barabara ili kuepusha ajali za barabarani ambazohusababisha ulemavu, uharibufu wa mali pamoja na vifo.10

Swali la 7: Ipi kati ya zifuatazo ni sababu ya kuvunjika kwa iliyokuwaJumuiya ya Kwanza ya Afrika Mashariki mwaka 1977?ANchi wanachama kuwa na makabila mengiBTofauti ya ukubwa wa nchi wanachamaCTofauti za lughaDTofauti za kiitikadi kati ya nchi wanachamaETofauti za sarafuJedwali Na. 2: Idadi na asilimia ya watahiniwa kwa kila chaguoMachaguoIdadi yawatahiniwaAsilimia 37672,5247,62112.5211.3818.9448.587.770.82Katika jedwali la 2 kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa ni cha wastanikwani asilimia 48.58 walichagua jibu sahihi.Swali lilitungwa kutoka mada ya Ushirikiano baina ya Tanzania naMataifa Mengine na lililenga kupima uelewa wa watahiniwa kuhususababu ya kuvunjika kwa jumuiya ya kwanza ya Afrika Masharikimwaka 1977. Kama Jedwali Na. 2 linavyoonesha ufaulu wa watahiniwaulikuwa wa wastani ambapo watahiniwa 453,376 (48.58%) waliwezakuchagua jibu sahihi D, Tofauti za kiitikadi kati ya nchi wanachama,watahiniwa walikuwa na maarifa ya kutosha kuhusu tofauti za kiitikadizilivyo sababisha kuvunjika kwa jumuiya hiyo. Tanzania ilikuwainafuata itikadi ya Ujamaa na Kujitegemea wakati Kenya na Ugandazilifuata itikadi za kibepari. Ikumbukwe kwamba dunia pia ilikuwaimegawanyika katika kambi mbili zilizokuwa zinapingana kiitikadi.Kambi ya kijamaa ikiongozwa na Urusi na kambi ya kibepariikiongozwa na Marekani huku kila kambi ikijaribu kupanua wigo waushawishi wake duniani. Vita baridi kati ya kambi hizo mbili ilisababishauhasama baina ya nchi na kutengeneza mazingira ya kutoaminianayaliyokuwa na athari kubwa katika uhusiano wa kimataifa. Aidha,Uganda chini ya utawala wa dikteta Idd Amin ilikuwa na mgogoro wampaka na Tanzania baada ya Uganda kujaribu kutwaa sehemu yaardhi ya Tanzania.Kipotoshi C, Tofauti za lugha kiliwavutia watahiniwa 176,795 (18.94%).Watahiniwa hao hawakuwa na ufahamu wa lugha maarufu11

zinazozungumzwa katika nchi wanachama wa Afrika ya Mashariki.Lugha ya Kiswahili inayozungumzwa na watu wengi katika nchi zote zaAfrika ya Mashariki. Aidha, nchi zote wanachama ziliwahi kuwamakoloni ya waingereza hivyo lugha ya kiingereza ilizungumzwa pia nawatu wengi katika eneo hili. Kutokana na hilo tofauti za lugha haikuwahoja ya msingi ya kuvunjika kwa jumuiya ya Afrika Mashariki. ChaguoA, Nchi wanachama kuwa na makabila mengi liliwavutia watahiniwa116,834 (12.52%). Watahiniwa hao hawakuwa na ufahamu kuwauwepo wa makabila mengi hakikuwa chanzo cha kuvunjika jumuiya yaAfrika Mashariki. Chaguo B, Tofauti ya ukubwa wa nchi wanachamaliliwavutia watahiniwa 106,193 (11.38%) ambao hawakujua kuwatofauti ya ukubwa wa nchi miongoni mwa wanachama haikusababishakuvunjika kwa jumuiya kwani makubaliano ya ushirikiano baina ya nchiwanachama yanajengwa kwa kuzingatia maslahi ya kila mwanachama.Vilevile, watahiniwa 72,524 (7.77%) walichagua kipotoshi E, Tofauti zasarafu bila kujua kuwa nchi wanachama walitumia sarafu mojainayoitwa shilingi. Hivyo, haikuwa sababu ya kuvunjika Jumuiya yaAfrika Mashariki.Swali la 8: Ni katika eneo lipi Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF)limekuwa mstari wa mbele?AKujenga uchumi wa kijamaa katika nchizinazoendeleaBKupiga vita usafirishaji wa bidhaa kutoka nchi tajirikwenda nchi maskiniCKuimarisha mfumo wa chama kimoja katika nchimaskiniDKusaidia wakimbizi katika nchi za AfrikaEKueneza utandawazi dunianiSwali lilitungwa kutoka mada ya Utamaduni wa Tanzania na TamaduniNyingine na lilipima maarifa ya watahiniwa kuhusu taasisi za kibenki zakimataifa ambazo ziko mstari wa mbele katika harakati za kuenezamfumo wa utandawazi. Kiwango cha ufaulu wa watahiniwa kilikuwahafifu kwani watahiniwa wachache tu 168,354 (18.04%) waliwezakubaini jibu sahihi E, Kueneza utandawazi duniani. Watahiniwa hawawalikuwa na maarifa ya kutosha kuhusu shughuli za taasisi kubwa zakibenki za kimataifa mfano Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF). Shirikala Fedha la Kimataifa limeshiriki kwa karibu sana katika juhudi za12

kufufua uchumi wa nchi nyingi za Afrika kwa kutoa mikopo yenyemasharti yanayolenga kuimarisha mfumo wa utandawazi katika nyanjazote za kisiasa na kiuchumi. Chati Na.6 inaonesha ufaulu wawatahiniwa katika swali la 8.Chati Na. 6: Kufaulu kwa watahiniwa katika swali la 8.Kipotoshi A, Kujenga uchumi wa kijamaa katika nchi zinazoendeleakiliwavutia watahiniwa 392,133 (42.10%) kutokana na historia yaTanzania ya kufuata itikadi ya Ujamaa. Hivyo, kuamini kuwa maslahiya taasisi ya fedha ya kimataifa yanafanana na ya nchi zinazoendeleaikiwemo Tanzania. Kipotoshi B, Kupiga vita usafirishaji wa bidhaakutoka nchi tajiri kwenda nchi maskini, kiliwavutia watahiniwa 109,076(11.69%) ambao hawakuwa na ufahamu kuwa lengo la taasisi za fedhaza kimataifa ni kulinda maslahi ya makampuni makubwa ya kimataifaikiwa ni pamoja na soko la bidhaa kutoka nchi tajiri. Watahiniwa 102,625 (11.00%) walichagua kipotoshi C, Kuimarisha mfumo wa chamakimoja katika nchi maskini hawakujua kuwa ushawishi wa mfumo wachama kimoja ulipotea duniani baada ya kusambaratika kwa kambi yamashariki iliyokuwa ikiongozwa na Urusi. Kwa upande mwingine, nchiza magharibi na taasisi zake za kimataifa zimekuwa zikiweka shinikizokwa nchi zinazoendelea kuruhusu demokrasia ya vyama vingi.Vilevile, chaguo D, Kusaidia wakimbizi katika nchi za Afrika, lilivutiawatahiniwa 151,164 (16.20%) ambao hawakuwa na ufahamu kuwakazi ya taasisi za kibenki za kimataifa au za ndani ni kutoa mikopo kwamasharti nafuu kwa nchi, taasisi au mtu binafsi. Jukumu la kusaidiawakimbizi liko mikononi mwa Shirika la Umoja wa Mataifalinalishughulikia wakimbizi UNHCR kwa kushirikiana na jumuiya yakimataifa na taasisi nyingine zisizo za kiserikali.13

Swali la 9: Nyimbo, maigizo na mashairi vinawakilisha nini?AItikadiBMatambikoCSanaa za ufundiDSanaa za maonyeshoEJando na unyagoSwali hili lilitoka katika mada ya Utamaduni Wetu. Lengo la swalililikuwa ni kupima uelewa wa watahiniwa kuhusu vielelezo mbalimbalivya utamaduni wetu. Kiwango cha ufaulu wa watahiniwa kilikuwa kizuriambapo watahiniwa 741,919 (79.49%) waliweza kuchagua jibu sahihiD, Sanaa za maonyesho. watahiniwa walikuwa na maarifa ya kutoshakuhusu vielelezo vya utamaduni ambapo waliweza kutofautisha Sanaaza ufundi na Sanaa za maonesho. Hivyo, kutovutiwa na majibumengine. Chati Na. 7 inaonesha ufaulu wa watahiniwa katika swali la9.Chati Na.7 Kufaulu kwa watahiniwa katika swali la 9.Chaguo A, Itikadi, liliwavutia watahiniwa 29,066 (3.11%) ambaohawakujua kuwa dhana ya itikadi ni msimamo wa kiuchumi, kisiasaama kijamii unaokubaliwa na jamii fulani, hivyo, chaguo hilo halikuwajibu sahihi. Kipotoshi B, Matambiko kilivutia watahiniwa 45,230 (4.85%)ambao pia hawakujua kuwa matambiko ni ibada inayofanywa na mtukwa mizimu yake akiomba baraka. Kipotoshi C, Sanaa za ufundi,kiliwavutia watahiniwa 65,096 (6.97%) ambao walishindwa kutofautishaSanaa za ufundi na Sanaa za maonesho. Hivyo, kuamini kuwa nyimbo,maigizo na mashairi vinawakilisha Sanaa za ufundi. Vilevile, kipotoshi14

E, Jando na unyago, kilivutia watahiniwa wengi 47,405 (5.08%) ambaohawakubaini tofauti ya sanaa za maonesho na dhana ya jando naunyago. Jando na unyago ni mila ya kuwafunza vijana wa kike nakiume maadili na desturi ya jamii husika. Kwa ujumla, watahiniwawalioshindwa kuchagua jibu sahihi walikosa maarifa ya kutosha yavielelezo mbalimbali vya utamaduni.Swali la 10: Ni sekta ipi inatoa nafasi za ajira kwa watanzania waliowengi?A MadiniB KilimoC ViwandaD BiasharaE UtaliiSwali lilitungwa kutoka katika mada ya Uchumi wetu na lilipima uwezowa watahiniwa kubaini sekta inayotoa ajira kwa watanzania waliowengi. Kiwango cha ufaulu wa watahiniwa kilikuwa kizuri ambapowatahiniwa 564,419 (60.47%) waliweza kuchagua jibu sahihi B, Kilimo.Idadi kubwa ya watahiniwa kubaini jibu sahihi inaonesha kuwawatahiniwa walio wengi wana maarifa ya kutosha kuhusu sektainayotoa ajira kwa watanzania walio wengi. Ikumbukwe kwamba zaidiya asilimia 80 ya Watanzania wanategemea kilimo kuendesha maishayao. Chati Na. 8 inaonesha ufaulu wa watahiniwa katika swali la 10.Chati Na. 8: Kufaulu kwa watahiniwa katika swali la 10.15

Chaguo A, Madini, lilivutia watahiniwa 40,967 (4.39%) kutokana najuhudi za serikali za kuboresha mazingira ya uwekezaji katika sekta hiina kulinda maslahi ya wachimbaji wadogo wa madini. watahiniwawalitumia uzoefu huo kuchagua kipotoshi hiki. Kipotoshi C, Viwanda,kimevutia watahiniwa 156,459 (16.76%) kutokana na juhudi za sasa zaserikali za kujenga uchumi wa viwanda. Kipotoshi D, Biashara, kilivutiawatahiniwa 128,265 (13.74%) kutokana na juhudi za serikalikuhamasisha ujasiriamali. Aidha, uwepo wa wafanyabiasharawadogowadogo katika sehemu za miji nchini umeshawishi baadhi yawatahiniwa kuamini kuwa biashara ni sekta inayotoa ajira kwawatanzania wengi. Vilevile, kipotoshi E, Utalii, kimevutia watahiniwa38,353 (4.11%). Sekta ya utalii ni chanzo cha fedha nyingi za kigenikwa taifa lakini haitoi ajira kwa kiwango sawa na sekta ya kilimo.Isitoshe, shughuli za utalii hufanyika katika maeneo machache tuyenye vivutio vya utalii wakati shughuli za kilimo hufanyika nchi nzima.Swali la 11: Chombo kilichoanzishwa mwaka 1964 ili kulinda uhuru namipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania niA Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.B Jeshi la Magereza la Tanzania.C Idara ya Uhamiaji Tanzania.D Jeshi la Polisi la Tanzania.E Jeshi la Mgambo la Tanzania.Swali hili lilitungwa kutoka mada ya Ulinzi na Usalama wa Taifa narasilimali zake na lilipima ufahamu wa watahiniwa kuhusu chombokilichoanzishwa mwaka 1964 ili kulinda uhuru na mipaka ya Jamhuri yaMuungano wa Tanzania. Kiwango cha ufaulu wa watahiniwa katikaswali hili kilikuwa kizuri ambapo watahiniwa 640,082 (68.58%)walichagua jibu sahihi A, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.Watahiniwa walikuwa na ufahamu wa kutosha wa chombokilichoanzishwa mwaka 1964 hivyo kutovutiwa na machaguo mengineyaliyokuwepo. Chati Na. 9 inaonesha ufaulu wa watahiniwa katikaswali la 11.16

Chati Na.9: Kufaulu kwa watahiniwa katika swali la 11.Chaguo B, Jeshi la Magereza la Tanzania, liliwavutia watahiniwa45,704 (4.90%) ambao hawakuwa na ufahamu kuwa jukumu la msingila Jeshi la Magereza ni kulinda na kuwahifadhi wafungwawaliopatikana na makosa mbalimbali hivyo, halikuwa jibu sahihi.Kipotoshi C, Idara ya Uhamiaji Tanzania,kilivutia watahiniwa 69,463(7.44%) ambao hawakuwa na ufahamu kwamba Idara ya uhamiaji ipochini ya Wizara ya Mambo ya ndani yenye jukumu la kuratibu shughulizote za uhamiaji nchini. Vilevile, kwa nafasi yake idara inashirikiana navyombo vingine vya ulinzi na usalama kuhakikisha kuwa nchi iposalama. Kipotoshi D, Jeshi la Polisi la Tanzania, kilivutia watahiniwa129,344 (13.86%) ambao hawakujua kuwa jeshi la Polisi lipo chini yaWizara ya Mambo ya Ndani lenye majukumu ya kila siku ya kulindausalama wa raia na mali zao. Jukumu lingine ni kusimamia usalamabarabarani. Vilevile, kipotoshi E, Jeshi la Mgambo la Tanzania,kilichaguliwa na watahiniwa 43,

maswali au walichagua jibu zaidi ya moja kinyume na maelekezo ya mtihani. Uchambuzi wa kila swali umefanyika ambapo dosari mbalimbali walizoonesha watahiniwa wakati wa kujibu maswali zimeainishwa. Aidha, ulinganifu wa kiwango cha kufaulu kati ya mwaka 2018 na 2019 kwa kila mada umefanyika ili kuonesha kupanda au kushuka kwa kiwango cha kufaulu .

Related Documents:

inayojadiliwa hapa ni: Fasihi ni Hisi, Fasihi ni Kioo cha Jamii, Fasihi ni Mwavuli wa Jamii, na Fasihi ni Zao la Jamii husika na Mielekeo yake ya maisha. 3. Mitazamo inayofafanua Uhusiano wa Fasihi na Jamii Kama lilivyo lengo la makala haya kwamba mchango wake ni kuongeza mchango katika kufafanua uhusiano uliopo baina ya fasihi na jamii.

coffee groups 1192043 infusion chamber with plug for coffee assembly for necta vending astro-astrop-brio250-brio3-brioc colibri-granmattino-kikko-kikkomax-kikkory-oblo spazio-venezia-zenith for lavazza lb3400zenith necta vending 0v17

WAZEE NA WATOTO KWA MIAKA 60 YA UHURU WA TANZANIA BARA. Ndugu Wananchi, Disemba 2021 nchi yetu inaadhimisha miaka 60 ya Uhuru tangu tarehe 09 Desemba, 1961 tulipoanza kujitawala hivyo, . Kufikia mwaka 2016 Wizara mbili ziliunganishwa ambazo ni Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, hivyo kutengeneza Idara Kuu ya

(2019). Muhtasari wa Somo la Maarifa ya Jamii Elimu ya Msingi Darasa la III-VII. Dar es Salaam: Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kunakili, kurudufu, kuchapisha wala kufasiri andiko hili kwa namna yoyote ile bila idhini ya maandishi ya Kamishna wa Elimu,

VII. Masomo hayo ni Kiswahili, English Language, Hisabati, Sayansi na Teknolojia, Uraia na Maadili, Maarifa ya Jamii na Stadi za Kazi. Mabadiliko katika mtaala, yalisababisha maboresho ya mihtasari ya masomo ya Darasa la III hadi la VII. Hiv

(c) Jaji kiongozi (d) Waziri wa sheria na katiba (e) Hakimu mkazi 9. Nini lilikuwa kusudio la maboresho ya katiba ya Tanzania yaliyofanyika mwaka 1992? (a) kuruhusu mfumo wa chama kimoja [ ] (b) kuruhusu uchaguzi

wahusika wakuu wa kazi ya fasihi na wahusika wadogo. Wahusika hao ndio wanaoipamba kazi fasihi na kuifanya iweze kuakisi mambo ya yaliyomo katika jamii (Msokile, 1992). Kwa muktadha huo tabia za wahusika wa kazi ya fasihi ndio ambao husawiri matukio na mambo mbalimbali yanayofanywa katika jamii inayohusika.

Modules which are part of Biology (Human) specifications only. * Only part of this chapter is required in the module: the sections needed are indicated in the te xt. The content you need for your AS exam. MICROSCOPES AND CELLS (1) 1 Cells are the basic units of organisms. In many organisms, cells are organised into tissues and tissues into organs. Several organs often link into an organ system .