HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA

2y ago
165 Views
3 Downloads
441.45 KB
106 Pages
Last View : 1d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Angela Sonnier
Transcription

HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI,TEKNOLOJIA NA UFUNDI MHESHIMIWA PROF.JOYCELAZARONDALICHAKO(MB.)AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YAMATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2016/17DODOMAMEI, 2016i

ii

“Natambua juhudi kubwa zimefanyika katika upanuzi waelimu ya awali, msingi, sekondari na vyuo vikuu.Serikali ya awamu ya tano, itajielekeza katika kuongezaubora wa elimu inayotolewa ikiwa ni pamoja nakuongeza mkazo katika masomo ya sayansi.”Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais waJamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakatiakifungua rasmi Bunge la 11, tarehe 22 Novemba2015.

YALIYOMOYALIYOMO.VIFUPISHO .iiii1.0 UTANGULIZI .12.0 DIRA, DHIMA NA MAJUKUMU YA WIZARA YAELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI.4DIRA NA DHIMA YA WIZARA .4MAJUKUMU YA WIZARA .43.0 VIPAUMBELE VYA WIZARA YA ELIMU,SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI .64.0 MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI KWAMWAKA 2015/16 .85.0 MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMUKWA MWAKA 2015/16 NA MPANGO NABAJETI KWA MWAKA 2016/17 . 105.1 UTUNGAJI NA UTEKELEZAJI WA SERAYA ELIMU .105.2 UPATIKANAJI WA FURSA ZA ELIMUNA MAFUNZO .145.3 KUINUA UBORA WA ELIMU NAMAFUNZO .165.4 TAFITI NA HUDUMA KWA JAMII .365.5 SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UBUNIFU .405.6 URATIBU WA TAASISI NA WAKALA .49i

5.7USIMAMIZI WA UTEKELEZAJI WAPROGRAMU NA MIRADI .676.0 SHUKRANI . 837.0 MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2016/17 86VIAMBATISHO . 88ii

AMISEMIOVCSIDASLADSSTHEPDeutscher Akademischer AustauschDienstDepartment for InternationalDevelopmentEuropean UnionFolk Development CollegesInformation and CommunicationTechnologyKusoma, Kuandika na KuhesabuLiteracy and Numeracy EducationSupportMpango wa Maendeleo ya Elimu yaSekondariNational Council for TechnicalEducationNational Examination Council ofTanzaniaOfisi ya Rais, Tawala za Mikoa naSerikali za MitaaOrphans and Vulnerable ChildrenSwedish International DevelopmentAgencySchool of Library Archives andDocumen- tation StudiesScience, Technology and HigherEducation Projectiii

SWASHTEHAMATETUDSMUNESCOUNICEFVETAVVUSchools Water Sanitation and HygieneTeknolojia ya Habari na MawasilianoTaasisi ya Elimu TanzaniaUniversity of Dar es SalaamUnited Nations Educational Scientificand Cultural OrganizationUnited Nations Children’s FundVocational Education and TrainingAuthorityVirusi Vya Ukimwiiv

1.0UTANGULIZI1.Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwana Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge yaHuduma na Maendeleo ya Jamii ndani ya Bunge lakoTukufu, ambayo imechambua Bajeti ya Wizara yaElimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, naomba kutoahoja kwamba sasa Bunge lako likubali kupokea nakujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Kazi za Wizara kwamwaka 2015/16 na Mpango wa Utekelezaji wa Bajetikwa mwaka 2016/17. Aidha, naliomba Bunge lakoTukufu likubali kupitisha Makadirio ya Mapato naMatumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia naUfundi kwa mwaka wa fedha 2016/17.2.Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee kabisana kwa heshima kubwa napenda kutoa shukranizangu za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muunganowa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe JosephMagufuli kwa imani kubwa aliyoonesha kwangu kwakuniteua kuwa Mbunge na Waziri wa Elimu, Sayansi,Teknolojia na Ufundi. Ninatambua ukubwa wadhamana aliyonipa na changamoto zilizopo katikaSekta hii. Napenda kumhakikishia Mheshimiwa Raisna wananchi wote kwa ujumla kuwa nitafanya kazihii kwa uadilifu na umahiri wa hali ya juu, ilikuhakikisha kuwa tunakidhi matarajio ya Watanzaniakatika sekta hii ya elimu ambayo ndiyo uti wamgongo wa maendeleo ya taifa letu.1

3.Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hiikumpongeza sana Mhe. Dkt. John Pombe Magufulikwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania wa Awamu ya Tano. Aidhanampongeza kwa uongozi wake wenye kuzingatiauwajibikaji na utendaji wenye tija kwa kazi kubwaanayoifanya ya kuwatumikia kwa moyo wa dhatiwananchi wote.4.Mheshimiwa Spika, Napenda pia kumpongeza kwadhati Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwakuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania na kwa kuandika historiamuhimu sana ya kuwa Makamu wa kwanzamwanamke tangu nchi yetu ilipopata uhuru. Vilevile,nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa MajaliwaKassim Majaliwa, kwa kuteuliwa na Rais na baadayekuthibitishwa na Bunge lako kuwa Waziri Mkuu waJamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha,nawapongeza Mheshimiwa Job Ndugai (Mb) naMheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mb) kwakuchaguliwa kuwa Spika na Naibu Spika wa Bungehili la 11 pamoja na Wenyeviti wote wa Bunge.5.Mheshimiwa Spika, napenda pia kuwapongezaMheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein kwakuchaguliwa kuwa Rais wa Serikali ya Mapinduziya Zanzibar kwa kipindi cha Pili na MheshimiwaBalozi Seif Ali Iddi kuwa Makamu wa Pili wa Rais.2

6.Mheshimiwa Spika, ninapenda kuishukuru Kamatiya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleoya Jamii chini ya Mwenyekiti wake MheshimiwaPeter Serukamba, kwa ushauri mzuri waliotupatiawakati wa maandalizi ya Bajeti hii. Wizara yanguimezingatia na itaendelea kuzingatia ushauri namaelekezo ya Kamati kwa lengo la kuleta ufanisikatika utendaji wa Sekta ya Elimu, Sayansi, naTeknolojia. Aidha, napenda kumshukuru Waziri kivuliwa Wizara hii, Mheshimiwa Susan Lyimo, kwaushirikiano wake.7.Mheshimiwa Spika, Hotuba yangu imegawanyikakatika sehemu kuu Saba: Sehemu ya Kwanza niUtangulizi; Sehemu ya Pili ni Dira, Dhima naMajukumu ya Wizara; Sehemu ya Tatu ni Vipaumbelevya Wizara kwa mwaka 2016/17; Sehemu ya Nne niMapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwaMwaka 2015/16; Sehemu ya Tano ni Mapitio yaUtekelezaji kwa mwaka 2015/16 na Mpango na Bajetikwa Mwaka 2016/17; Sehemu ya Sita ni Shukrani;na sehemu ya Saba ni Maombi ya Fedha.3

2.0DIRA, DHIMA NA MAJUKUMU YA WIZARAYA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NAUFUNDIDIRA NA DHIMA YA WIZARA8.Mheshimiwa Spika, Dira ya Wizara ni kuwa naMtanzania aliyeelimika na mwenye maarifa, stadi,umahiri, uwezo na mitazamo chanya ili kuwezakuchangia katika kuleta maendeleo ya Taifa. Aidha,Dhima ya Wizara ni kuinua ubora wa elimu namafunzo na kuweka mifumo na taratibuzitakazowezesha kupata idadi kubwa ya Watanzaniawalioelimika na wanaopenda kujielimisha zaidi iliwaweze kuchangia katika kufikia malengo yamaendeleo ya Taifa letu.MAJUKUMU YA WIZARA9.Mheshimiwa Spika, Majukumu ya Wizara ya Elimu,Sayansi, Teknolojia na Ufundi ni kama ifuatavyo:(i) kutunga na kutekeleza Sera za Elimu, Utafiti,Huduma za Maktaba, Sayansi, Teknolojia,Ubunifu na Uendelezaji wa Mafunzo yaUfundi;(ii)kuendeleza Elimumsingi kwa Kutoa Ithibatiya Mafunzo ya Ualimu na Maendeleo yaKitaalamu ya Walimu;(iii)kubainisha Vipaji na Kuviendeleza;4

(iv) kusimamia Uendelezaji wa Mafunzo katikaVyuo vya Maendeleo ya Wananchi;(v)kusimamia Mfumo wa Tuzo wa Taifa;(vi) kuainisha Mahitaji ya Nchi katika Ujuzi naKuuendeleza;(vii) kuweka Viwango vya Taaluma ya Ualimu;(viii) kusimamia Ithibati na Uthibiti wa Shule;(ix) kusimamia Huduma za Machapisho yaKielimu;(x)kutegemeza/kuimarisha utumiaji wa Sayansi,Uhandisi, Teknolojia na Hisabati;(xi) kuendeleza Wataalamu wa ndani katikaSayansi, Teknolojia na Ubunifu;(xii) kuratibu utafiti katika Sayansi na Teknolojia;(xiii) uendelezaji wa Rasilimaliwatu na UongezajiTija ya Watumishi walio chini ya Wizara; na(xiv) kuratibu Shughuli za Idara, Mashirika,Wakala, Programu na Miradi iliyo chini yaWizara.5

3.0VIPAUMBELE VYA WIZARA YA ELIMU,SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI10.Mheshimiwa Spika, Dira ya Maendeleo ya Taifa(2025) imelenga kuifanya Tanzania kuwa nchi yakipato cha kati ifikapo mwaka 2025. Katika juhudiza kufikia lengo hili, Wizara ya Elimu, Sayansi,Teknolojia na Ufundi ina jukumu la kuandaawataalamu wenye ujuzi na maarifa watakaotoamchango wenye tija kwa maendeleo ya nchi yetu.Wizara yangu inatambua kuwa utekelezaji wa azmaya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuwa na uchumiwa viwanda inategemea kwa kiasi kikubwa ufanisikatika Sekta ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Uborawa rasilimali watu ni jambo la msingi sana katikakuhakikisha kuwa tija na ufanisi vinakuwepo katikaSekta zote muhimu ili kuchochea kasi ya ukuajiuchumi na hatimaye kuiwezesha nchi yetu kufikiauchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.11.Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia mwelekeo huo,katika mwaka 2016/17, vipaumbele vya Sekta yaElimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi ni kamaifuatavyo:(i)kuinua ubora wa elimu na mafunzo katikangazi zote za elimu na mafunzo nchini;(ii)kuimarisha mifumo na usimamizi wa Ithibatina Uthibiti wa Ubora wa Elimu na mafunzo;6

(iii) kuongeza upatikanaji na ushiriki katika fursaza elimu na mafunzo; na(iv) kuimarisha tafiti na matumizi ya Sayansi,Teknolojia na Ufundi kwa lengo la kuongezachachu ya maendeleo.7

4.012.MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETIKWA MWAKA 2015/16Mheshimiwa Spika, naomba nianze kutoa tathminiya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa mwaka wafedha 2015/16 kuanzia tarehe 1 Julai, 2015 haditarehe 30 Aprili, 2016.Ukusanyaji wa Maduhuli Kwa Mwaka 2015/1613.Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015/16, 1,684.47ambapoShilingi9,268,457,100.00 zilitarajiwa kukusanywa na Idarawakati Shilingi 276,806,114,584.47 zilitakiwakukusanywa na Taasisi zilizo chini ya Wizara.Makusanyo ya maduhuli hadi kufikia tarehe 30 9.12 ambayo ni sawa na asilimia69.7 ya makadirio. Kati ya fedha hizo, Shilingi5,723,343,678.36 zilikusanywa na Idara na Shilingi193,698,889,670.76 zilikusanywa na Taasisi zilizochini ya Wizara.Matumizi ya Kawaida na Maendeleo kwa Mwaka2015/1614.Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha2015/16 bajeti ya Wizara ilikuwa ni Shilingi1,094,195,824,888.49(Matumiziyakawaida8

Shilingi 511,525,227,000.00 na Matumizi yamaendeleo Shilingi 582,670,597,888.49). Hadikufikia tarehe 30 Aprili, 2016 fedha ambazozimekwishatolewa na Hazina zilikuwa Shilingi789,460,338,381.61 (Matumizi ya kawaida Shilingi351,284,829,898.00 na Matumizi ya MaendeleoShilingi 438,175,508,483.61) sawa na asilimia72.15 ya bajeti ya Wizara. Aidha, fedha zilizotumikahadi kufikia tarehe 30 Aprili 2016 zilikuwa ni Shilingi694,148,943,065.89 (Matumizi ya kawaida Shilingi313,796,049,657.61 na Matumizi ya maendeleoShilingi 380,352,893,408.28) sawa na asilimia 87.9ya fedha zilizotolewa.9

5.015.MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMUKWA MWAKA 2015/16 NA MPANGO NABAJETI KWA MWAKA 2016/17Mheshimiwa Spika, mwaka 2015/16, Wizara ililengakusimamia utekelezaji wa mambo makuu yafuatayo:(i)utungaji na utekelezaji wa Sera za Elimu;(ii)upatikanaji wa fursa za elimu na mafunzo;(iii)ithibati ya Shule;(iv) uthibiti ubora wa elimu;(v)mafunzo ya Ualimu, hususan wa Sayansi,Hesabu, Ufundi (ikiwemo ufundi sanifumaabara), Lugha na KKK;(vi) uratibu wa shughuli za Taasisi na Wakala; na(vii) usimamizi wa utekelezaji wa programu namiradi mbalimbali.5.1 UTUNGAJI NA UTEKELEZAJI WA SERA YAELIMU16.Mheshimiwa Spika, mojawapo kati ya majukumuya msingi ya Wizara yangu ni kubuni na kutungaSera mbalimbali za kusimamia Elimu, Mafunzo yaUfundi, Sayansi, Teknolojia, Ubunifu, Huduma zaMaktaba na Utafiti.10

Utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo (2014)17.Mheshimiwa Spika, katika mwaka2015/16, yafuatayo yalifanyika:wafedha(i)kutafsiri Sera ya Elimu na Mafunzo (2014) kwalugha ya Kiingereza na kukamilisha maandaliziya Mkakati wa Utekelezaji wa Sera ya Elimu;(ii)kufanya uchambuzi wa mahitaji ya mabadilikoya sheria ili kutekeleza Sera ya Elimu naMafunzo (2014);(iii)kuhuisha mitaala ya elimu ya awali, elimu yamsingi na elimu ya sekondari. Aidha, vitabu vyakiada vya Darasa la Kwanza vinavyoendana naMtaala uliohuishwa vinasambazwa kwenyeMikoa na Halmashauri zote nchini; na(iv) ufuatiliaji na tathmini yamajukumu ya Wizara.utekelezajiwaUtekelezaji wa Elimumsingi bila Malipo18.Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza azma yaSerikali ya kutoa Elimumsingi bila Malipo, Wizarayangu ilitoa Waraka wa Elimu Namba 6 wa mwaka2015 kwa lengo la kutoa mwongozo wa namna yakutekeleza Elimumsingi bila malipo. Waraka waElimu Na. 6 umeweka bayana majukumu ya wadauwote muhimu katika utoaji wa Elimumsingi bilaMalipo ambapo imeainishwa kuwawazazi11

wanatakiwa kufanya yafuatayo:(i)kununua sare za shule na michezo, vifaa vyakujifunzia, chakula kwa wanafunzi wa kutwana kugharamia matibabu kwa watoto wao.(ii)kulipia nauli ya kwenda shule na kurudi kwawanafunzi wa kutwa.(iii) kulipa nauli za wanafunzi wakati wa likizo;kununua vifaa kwa ajili ya malazi shuleni navifaa vya kujifunzia.19.Mheshimiwa Spika, natoa wito kwa wazazi nawalezi kuunga mkono juhudi za Serikali zakuhakikisha kuwa watoto wote wanapata elimu. Nimuhimu wazazi mkawawezesha watoto wenukupata mahitaji ya shule na muhimu zaidi mjengeutamaduni wa kukagua madaftari ya watoto wenu ilikujiridhisha kama wanafundishwa shuleni.20.Mheshimiwa Spika, serikali hutoa fedha ya chakulakwa wanafunzi wa bweni tu. Hivyo, kama kunashule za sekondari ambazo zimesajiliwa kama shuleza kutwa lakini wamejenga Hosteli na miundombinuinayokidhi vigezo vya kuwa shule za bweni, MaafisaElimu wazitambue na wawasilishe maombi kwenyeWizara yangu ya kuomba kuzibadilisha hadhi.Endapo zitakuwa zimekidhi vigezo muhimuzitabadilishwa na kuwa shule za bweni. Kwakufanya hivyo, wanafunzi wataweza kutengewa12

fedha ya chakula kama ilivyoainishwa kwenyeWaraka wa Elimu Na. 6 wa mwaka 2015.Mpango wa Utekelezaji wa Sera ya Elimu naMafunzo (2014) kwa mwaka 2016/1721.Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2016/17, Wizarayangu itaendelea na utekelezaji wa Sera ya Elimu naMafunzo (2014) na Mkakati wake. Wizara itafanyamabadiliko ya Sheria ya Elimu na kupitia Sheria,Kanuni na Taratibu za taasisi zilizo chini ya Wizara,hususan Baraza la Mitihani, Taasisi ya ElimuTanzania, Taasisi za Ithibati na Uthibiti, Bodi yaMikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu na Mamlakaya Elimu Tanzania kwa lengo la kuimarishautekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo (2014) kwaufanisi. Aidha, Wizara itakamilisha taratibu zauundwaji wa Bodi ya Kitaalamu ya Walimu.22.Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2016/17, Wizarayangu itaendelea kuimarisha Mpango wa matumiziya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji. Vilevile,Wizara itatoa mwongozo wa kuwatambua nakuwaendeleza wanafunzi wenye vipaji, vipawa namahitaji maalumu na wenye kasi kubwa ya kujifunzamasomo ya Sayansi na Hisabati ili kuwezakuwaendeleza katika fani mbalimbali za teknolojia.13

Sera yaUbunifu23.Sayansi,TeknolojianaMheshimiwa Spika, katika mwaka 2016/17, Wizarayangu imedhamiria kuimarisha na kuongeza kasiya ukuaji wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kwakukamilisha mapitio ya Sera zifuatazo:(i)Sera ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia yamwaka 1996 na kutunga sera mpya ya Taifa yaSayansi, Teknolojia na Ubunifu;(ii)Sheria Na. 7 ya mwaka 1986 iliyoanzisha Tumeya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH)na kutunga sheria mpya ya Maendeleo yaSayansi, Teknolojia na Ubunifu; na(iii) Sheria Na. 7 ya mwaka 2003 iliyoanzisha Tumeya Nguvu za Atomiki (Tanzania Atomic EnergyCommission - TAEC).5.2 UPATIKANAJI WA FURSA ZA ELIMU NAMAFUNZOUdahili wa wanafunzi vyuoni24.Mheshimiwa Spika, Serikali ina lengo la kuendeleakuongeza fursa za Elimu na Mafunzo ili kuandaarasilimali watu itakayochangia maendeleo ya taifa.Kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya UfundiStadi, Wizara iliendelea kuratibu udahili wawanafunzi ambapo kwa mwaka 2015 wanafunzi14

189,687 walidahiliwa katika vyuo mbalimbali vyaufundi. Aidha, kwa kupitia Baraza la Elimu ya Ufundiwanafunzi 75,186 walidahiliwa kwenye vyuombalimbali kupitia mfumo wa pamoja wa udahili.25.Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Tume yaVyuo Vikuu imeendelea kuratibu udahili wawanafunzi wanaojiunga na Elimu ya Juu kupitiaMfumo wa Udahili wa Pamoja (Central AdmissionSystem) wa kudahili wanafunzi wa Digrii ya kwanza.Katika mwaka 2015/16 wanafunzi 65,064 wa Digriiya kwanza walidahiliwa wakiwemo wanawake22,225 sawa na asilimia 34.2 na kufanya jumla yawanafunzi wote wa elimu ya juu kufikia 210,000.Wanafunzi hao walidahiliwa katika vyuo vikuu na vyuovikuu vishiriki 49 na Taasisi zisizo vyuo vikuu 21 (kamailivyo kwenye kiambatisho Na. 1).Elimu Maalum26.Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia kwamba elimuni haki ya msingi ya kila Mtanzania, Wizara yanguimeendelea kupanua fursa za elimu na mafunzo kwakuimarisha elimu kwa wanafunzi wenye mahitajimaalum. Katika mwaka 2015/16, Wizara yanguiliendesha mafunzo kwa walimu 142 kuhusuufundishaji wa Sayansi na Hisabati kwa wanafunziwasioona. Aidha, kupitia Chuo Kikuu Huria chaTanzania wanafunzi 45 viziwi na wasioona walipewamafunzo ya kutumia TEHAMA katika kurahisisha15

kujifunza ili waweze pia kupata maarifa na taarifambalimbali zilizoko kwenye mtandao.27.Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2016/17 Wizarayangu itafanya yafuatayo:(i)kununua vifaa mbalimbali vya wanafunzi wenyemahitaji maalum. Vifaa hivyo ni pamoja namashine za nukta nundu, fimbo nyeupe, viti vyamagurudumu, visaidizi vya kusikia, na vifaa vyavituo maalum vya msaada wa kitabibu;(ii)kukarabati na kufanya matengenezo ya vifaavya wanafunzi walemavu; na(iii)kuwezesha upatikanaji wa vifaa vya maabarana vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwawanafunzi wenye mahitaji maalum wa shuleza msingi na Sekondari.5.3 KUINUA UBORA WA ELIMU NA MAFUNZO28.Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inatambuakwamba elimu bora ina nafasi ya pekee katikakufanikisha ujenzi wa msingi wa uchumi wa kisasawa taifa linalojitegemea. Ili kukidhi azma hii, Wizarayangu imeimarisha na kuboresha mfumo wa ithibatina uthibiti wa shule na vyuo, mafunzo ya ualimu,mazingira ya kufundishia na kujifunzia pamoja nahuduma za maktaba.16

Ithibati ya Shule za Msingi na Sekondari29.Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendeleakusimamia ithibati ya shule kwa lengo la kuzipatiashule idhini ya kufundisha masomo husika,kuthibitisha Wamiliki na Mameneja wa Shule nakutoa vibali vya ujenzi wa shule zisizo za Serikali.Hadi kufikia Aprili, 2016 shughuli zifuatazo zilifanyika:(i)shule 174 zikiwemo shule za awali 4, msingi115 na sekondari 55 zilisajiliwa;(ii)kutoa vibali kwa Wamiliki 151 na Mameneja154 wa shule na vibali vya ujenzi wa shule 201zisizo za Serikali;(iii) kufuta vibali vya ujenzi kwa shule 37 kwa kuwavilikuwa vimeombwa zaidi ya miaka kumiiliyopita, na hapakuwa na jitihada za kuendeleana ujenzi na kuanza taratibu za kusajili shulehizo; na(iv) Wamiliki na Mameneja wa shule 13 walifutiwauthibitisho kutokana na shule zao kubadiliumiliki.30.Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2016/17, Wizarayangu itafanya yafuatayo katika ithibati ya shule;(i)kuhuisha na kuandaa Mwongozo wa Usajili waShule za Serikali na zisizo za Serikali kulinganana mahitaji ya sasa;17

(ii)kusajili shule za Awali, Msingi na Sekondarikwa kutilia mkazo uanzishwaji wa shule zenyemwelekeo wa Sayansi, Kilimo, Teknolojia naUfundi; na(iii)kusajili vituo vinavyotoa Elimu Nje ya MfumoRasmi na Elimu Huria.Uthibiti wa Ubora wa Shule za Msingi na Sekondari31.Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inatambuakwamba, uthibiti ubora wa shule ni jambo muhimusana katika kuimarisha ubora wa elimu na mafunzoyanayotolewa katika shule za msingi na sekondari.Hadi kufikia Aprili, 2016, shule 7,882 kati ya 17,242ambayo ni sawa na asilimia 46 ya shule zilizolengwazilifanyiwa ukaguzi. Aidha, walimu 292 waliteuliwakuwa Wathibiti Ubora wa Shule na kupangwa katikaofisi za Kanda na Wilaya kwa lengo la kuimarishaukaguzi wa shule.32.Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inafuatilia kwakaribu na kuhakikisha kwamba watoto wotewanafundishwa vema na wanaweza kumudu stadiza kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) kuanziahatua za mwanzo. Katika kutimiza azma hii WathibitiUbora w

3.0 VIPAUMBELE VYA WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI 10. Mheshimiwa Spika, Dira ya Maendeleo ya Taifa (2 025) imelenga kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025. Katika juhudi za kufikia lengo hili, Wizara ya E

Related Documents:

elimu ya juu, Sayansi na Teknolojia. Ilitoa jumla ya tuzo 119 kwa wanafunzi wa kike kutoka shule 20 zilizofanya vizuri katika masomo ya Sayansi na Hisabati katika mitihani ya kumaliza kidato cha nne mwaka 2006 (18); kidato cha sita mwaka 2006 na 2007 (25); vyuo vikuu, taasisi za serikal

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imekuwa ikiboresha Mtaala wa Elimu ya Msingi kuhakikisha kwamba elimu inayotolewa ni bora na inayomwandaa mwanafunzi kumudu maisha katika mazingira yake. Muktadha huu umeifanya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia iboreshe mchakato wa kufundisha

4.3.1 Elimu ya malezi ya awali na makuzi (ECEC), utambuzi wa mapema na afua za mapema (EIEI) . ECC Mtaala wa Msingi Uliopanuliwa ECEC Elimu ya awali ya utotoni na Uangalizi . MUHTASARI Ripoti hii ya dunia juu ya elimu jumuishi ina

Ingawa Sera ya Elimu ya Awali ipo, mafanikio ya sera hii ni madogo sana. Elimu ya Awali ilijumuishwa moja kwa moja katika elimu ya msingi (2014) lakini shule nyingi hazina madarasa mazuri ya elimu ya awali. Sekta ya shule za awali hazina walimu wenye st

Hali ya Elimu Andika idadi halisi ya huduma zilizopo kijijini. Idadi V401. Idadi ya shule za msingi za serikali V402. Idadi ya shule za msingi za binafsi V403. Idadi ya vituo vya elimu ya awali V404. Idadi ya shule za sekondari V405. Idadi ya shule za ufundi V406. Kuna kamati ya elimu na hu

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Imefadhiliwa na Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza (DFID) Agosti, 2017 MPANGO WA UTAYARI WA KUJIUNGA NA ELIMU YA SEKONDARI (MUES) EQUIP-Tanzania. Mpango wa Utayari wa Kujiunga na Elimu ya Sekondari (MU

Lugha ya Kiswahili. Changamoto tuliyonayo ni kwa Viongozi wengine kuiga mfano huu na Watanzania wote kuendeleza kazi hii nzuri iliyoanzishwa na Viongozi hawa. Kukua kwa Lugha ya Kiswahili sio tu kutaitangaza Nchi yetu, lakini vilevile, kutatoa ajira kwa Walimu wa Kiswahili

Le fabricant et l’utilisateur d’un additif alimentaire sont tenus: a. de transmettre à l’OSAV toute nouvelle information scientifique ou techni-que susceptible d’influer sur l’évaluation de la sécurité de cet additif; et b. d’informer l’OSAV, sur demande, des usages de l’additif concerné. Art. 11 Modification des annexes L’OSAV adapte régulièrement les annexes de la .