HOTUBA YA BAJETI YA WAZIRI WA ELIMU YA JUU, SAYANSI

2y ago
644 Views
4 Downloads
293.80 KB
63 Pages
Last View : 1d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Julia Hutchens
Transcription

HOTUBA YA BAJETI YA WAZIRI WA ELIMU YA JUU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA,MHESHIMIWA PROF. PETER M. MSOLLA (MB), WAKATI WA KUWASILISHABUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2007/2008UTANGULIZI1. Mheshimiwa Spika, kutokana na taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni naMwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii inayohusuWizara yangu, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu sasa likae kamaKamati ili liweze kupokea, kujadili na kupitisha Makadirio ya Matumizi ya Wizara yaElimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Taasisi zake kwa mwaka wa fedha2007/2008.2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote, sina budi kuwapongeza Waheshimiwa Dkt.Asha-Rose Migiro kwa kuteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Dkt. Batilda Salha Burian (Mb) kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya WaziriMkuu-Bunge, Benard Membe (Mb) kuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje naUshirikiano wa Kimataifa, Gaudence Cassian Kayombo (Mb) kuwa Naibu Waziri waMipango, Uchumi na Uwezeshaji na William Mganga Ngeleja (Mb) kuwa NaibuWaziri wa Nishati na Madini. Vile vile niwapongeze Waheshimiwa Wabungewaliojiunga na Bunge hili kwa kuchaguliwa na kuteuliwa, Mheshimiwa MtuturaAbdallah Mtutura, Mbunge wa Tunduru na Mheshimiwa Florence Essa Kyendesa,Mbunge wa viti Maalum. Naomba pia niwapongeze waliochaguliwa kuwakilishanchi yetu ya Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki, ambao ni Mheshimiwa Dkt.Didas John Massaburi, Mheshimiwa Dkt Aman Walid Kabourou, Mheshimiwa Dkt.George Francis Nangale, Mheshimiwa Sylivia Kate Kamba na Mheshimiwa SeptuuNassoro, Mheshimiwa Dkt. Said Gharib Bilal, Mheshimiwa Dkt Janet Deo Mmari naMheshimiwa Dkt. Fortunatus Lwanyatika Masha.3. Mheshimiwa Spika, aidha napenda niungane na Waheshimiwa Wabunge, ndugujamaa na marafiki katika kuwafariji na kuwapa pole familia, ndugu, na wapigakura wa marehemu Mheshimiwa Juma Jamaldini Akukweti aliyekuwa Waziri1

wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Mbunge wa Tunduru na MheshimiwaAmina Chifupa Mpakanjia, Mbunge wa viti maalumu (CCM). Mungu aziwekeroho za marehemu mahali pema peponi, Amina.4. Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa wale wotewaliowezesha kutekeleza majukumu ya Wizara yangu kwa kipindi kilichopita, naambao wamewezesha kuandaa mipango ya mwaka 2007/2008 na kuboresha hojayangu ambayo naiwasilisha katika hotuba hii. Aidha, natoa shukrani kwa wananchiwote wa Tanzania kwa mchango wao katika kutekeleza majukumu ya Wizarayangu. Natoa shukrani zangu za pekee kwa Naibu Waziri wangu, MheshimiwaGaudentia Mugosi Kabaka (Mb); Katibu Mkuu Dkt. Naomi BakunziKatunzi, Watendaji katika Wizara yangu pamoja na taasisi zilizo chini ya Wizara,mashirika mbalimbali ya ndani na nje kwa misaada na ushauri wao. Kwa namnaya pekee natoa shukrani zangu kwa Waheshimiwa Wabunge wa Kamati yaKudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii chini ya Mwenyekiti wake MheshimiwaOmar Kwaang’w Mbunge wa Babati Mjini (CCM) kwa ushauri wao. Aidha,napenda kumshukuru Mheshimiwa Suzan Anselm Jerome Lyimo Mbunge waviti maalum (CHADEMA) ambaye ni msemaji mkuu wa kambi ya upinzani kuhusuWizara yangu na Waziri Kivuli kwa ushirikiano wake na mchango wake katikakuiboresha hoja hii.5. Mheshimiwa Spika, Wizara katika kipindi cha kuanzia Julai, 2006 imeendelea nautekelezaji wa majukumu na mipango yake kwa kuzingatia Ilani ya Uchaguzi yaCCM ya mwaka 2005 - 2010, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, Mkakati wa KukuzaUchumi na Kupunguza Umaskini, Sera ya Elimu ya Juu, Sera ya Elimu ya Ufundi naMafunzo, Sera ya Sayansi na Teknolojia, Mpango Kabambe wa Wizara, pamoja naahadi na maagizo mbalimbali ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniaalipoitembelea Wizara tarehe 1 Februari, 2006. Hivyo lengo la taarifa hii ni kuelezahali ya utekelezaji wa ahadi za Serikali kwa mwaka wa fedha 2006/2007 namalengo ya wizara pamoja na makisio ya bajeti kwa mwaka 2007/08.2

MAFANIKIO YALIYOPATIKANA KATIKA MWAKA WA FEDHA 2006/20076. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/07 wizara yangu kupitia Idarana Taasisi zake imefanikiwa kutekeleza ahadi nyingi ilizozitoa Bungeni mwaka jana.Naomba niwasilishe utekelezaji na mafanikio kama ifuatavyo:IDARA YA ELIMU YA JUU7. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/07 Idara ya Elimu ya Juuimetekeleza yafuatayo:Imeongeza idadi ya wanafunzi katika Elimu ya Juu kutoka wanafunzi 52,108 hadi68,029 ambalo ni ongezeko la asilimia 30.6 ukilinganisha na udahili wa mwaka2005/06.Imehakikisha mitaala ya elimu ya juu inakidhi mahitaji ya soko la ajira na kujiajiri. Imedhamini wanafunzi 1,422 wa shahada ya kwanza ya Udaktari (MD) katikavyuo vikuu nchini.Imedhamini wanafunzi 90 raia wa Uganda, ikiwa ni utekelezaji wa mkataba wakubadilishana wanafunzi wa shahada ya kwanza katika Vyuo vikuu vya Afrikaya Mashariki.Imeendelea na udhamini wa mafunzo ya wanafunzi watano, raia wa China ikiwa niutekelezaji wa mkataba wa ushirikiano kati ya Tanzania na China.Imeelimisha umma kuhusu Sera ya uchangiaji wa elimu ya juu.Imepitia rasimu ya Sera ya Elimu ya Juu ya mwaka 1999 iliyohuishwa na ambayoimejadiliwa na wadau mwezi Juni, 2007.Imekamilisha mchakato wa kuwapata viongozi wa vyuo vikuu vya Ardhi na ChuoKikuu cha Tiba na Sayansi za Afya Muhimbili.3

Imeendelea na udhamini wa mafunzo ya wanataaluma themanini (80) katika vyuovikuu vya umma.IDARA YA ELIMU YA UFUNDI8. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Idara ya Elimu yaUfundi ilitekeleza yafuatayo:Ilidhamini mafunzo kwa wanafunzi 1,754 katika ngazi ya Ufundi Sanifu katika Vyuona Taasisi za Ufundi zilizo chini ya Wizara.Iligharimia mafunzo ya watumishi kumi na wawili (12) wa Chuo cha Ufundi Arushana Makao Makuu katika ngazi ya udaktari wa falsafa (4) na Shahada ya Uzamili(8).Iliratibu na kugharamia mafunzo maalumu ya ualimu (Pedagogical Skills) kwawahandisi 23 walioajiriwa katika Chuo cha Ufundi Arusha.IDARA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA9. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Idara ya Sayansi naTeknolojia ilitekeleza yafuatayo: Iliandaa rasimu ya Sera ya Taifa ya Utafiti na kujadiliwa na Sekretariati yaBaraza la Mawaziri. Iliendeleza mchakato wa urejeaji wa Sera ya Taifa ya Sayansi na Teknolojiakwa madhumuni ya kutunga Sera mpya ya Taifa ya Sayansi, Teknolojia naUbunifu. Iliendeleza taratibu za uanzishwaji wa Taasisi ya Nelson Mandela, katika eneola kudumu lililoko Karangai katika Halmashauri ya Wilaya ya Arumeru, Arusha.4

Iliendelea kuelimisha jamii kupitia vipindi 52 vya Radio na maonyesho kuhusuelimu ya juu, Sayansi na Teknolojia. Ilitoa jumla ya tuzo 119 kwa wanafunzi wa kike kutoka shule 20 zilizofanyavizuri katika masomo ya Sayansi na Hisabati katika mitihani ya kumaliza kidatocha nne mwaka 2006 (18); kidato cha sita mwaka 2006 na 2007 (25); vyuovikuu, taasisi za serikali na binafsi za Elimu ya Juu na Ufundi (43). Aidha wizarapia ilitoa tuzo 33 kwa shule za sekondari zilizowezesha wanafunzi hao kufanyavizuri katika masomo hayo.IDARA YA SERA NA MIPANGO:10.Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa fedha 2006/2007 Idara ya Sera naMipango ilitekeleza yafuatayo: Iliratibu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi yamwaka 2005-2010, na kuandaa taarifa ya utekelezaji. Iliratibu utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo 21, katika Taasisi na MakaoMakuu. Kati ya miradi hiyo, 18 ni miradi inayogharamiwa na fedha za ndanina 3 inagharamiwa na fedha za nje. Iliratibu uanzishwaji wa Chuo Kikuu cha Dodoma, ambapo upembuziyakinifu umekamilika na kujadiliwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge yaHuduma za Jamii, Kamati ya Makatibu Wakuu na Baraza la Mawaziri. Iliratibu shughuli za ushirikiano wa Kimataifa, ikiwa ni pamoja nakuhudhuria Vikao vya EAC, SADC na kuingiaMikataba ya Maridhiano(MOU) na nchi marafiki. Iliratibu maandalizi ya mpango maalum (Quickwin Programme) kwa ajili yakuendeleza Elimu ya Juu na Ufundi utakaofadhiliwa na Benki ya Dunia.5

Iliratibu maandalizi ya mkakati wa kuendeleza Elimu Juu na Ufundi (Higherand Technical Education Development Programme) ili kukabiliana naongezeko la wanafunzi linalotokana na mafanikio ya Mpango wa Elimu yaMsingi (MEM) na Sekondari (MES).IDARA YA UTAWALA NA UTUMISHI11. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007, Idara ya Utawala naUtumishi ilitekeleza yafuatayo: Iliratibu mafunzo mbalimbali ndani na nje ya nchi kwa watumishi arobainina saba (47) ili kuwaongezea ujuzi maarifa na ufanisi katika utendaji waokazi. Iliendelea kushirikisha sekta binafsi katika utoaji wa huduma zisizo rasmi(non-core services) Makao Makuu pamoja na Chuo cha Ufundi Arusha,hususani huduma za ulinzi, usafi na chakula.Iliratibu upatikanaji wa vibali vya ajira 1,528 katika vyuo vikuu na Taasisi zakekwa lengo la kupunguza uhaba wa wafanyakazi.Iliadhimisha siku ya UKIMWI ya Wizara kwa kufanya shughuli mbalimbalizinazohusu upimaji UKIMWI kwa hiari, matumizi ya dawa za kurefushamaisha kwa waishio na virusi vya UKIMWI na kupunguza maambukizo yaUKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Pia iliandaa mwongozo wakushughulikia taratibu za kutoa lishe na matibabu kwa watumishi waishio navirusi ya UKIMWI.Iliajiri watumishi kumi na nne (14) kati ya hao wawili (2) Makao Makuu na kuminambili(12)ChuochaUfundiArusha.wamepandishwa vyeo na 3 kuthibitishwa kazini.6Aidha,watumishi22

VYUO VIKUU:CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (KAMPASI YA MLIMANI)12. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Chuo Kikuu cha Dar esSalaam (Kampasi ya mlimani) kilitekeleza yafuatayo: Kilidahili jumla ya wanafunzi 6,027, kati yao wanafunzi wa Shahada ya kwanzani 3,890 wanafunzi wa kike ni 1,400 sawa na 36% na Shahada ya Uzamili ni2,137 wanafunzi wa kike ni 577 sawa na 27%. Kiliendeleza juhudi za kutumia teknolojia ya mawasiliano (ICT) katikakufundisha na kujifunza kwa kutumia Kituo cha Elimu Endelevu (Centre forContinuing Education), kuwafundisha wahadhiri mbinu mpya na bora zakufundishia pamoja na kuimarisha mtandao wa ndani (Local Area Network) Kiliajiri watumishi 281 wanataaluma 185 na waendeshaji 96 katika ngazimbalimbali kwenye idara 17 zenye upungufu mkubwa wa wafanyakazi. Kiliendelea kushirikiana na taasisi za ndani na nje ya nchi kugharamia utafitikulingana na sera ya utafiti ya chuo. Kiliendelea kutumia mikakati mbalimbali pamoja na kutoa mafunzo maalumkwa wasichana wanaotaka kujiunga na programu za sayansi, uhandisi nateknolojia, uchumi na takwimu, ili kuinua uwiano wa wavulana kwa wasichana. Kiliendeleza ujenzi wa madarasa mawili yenye uwezo wa kutumiwa nawanafunzi 1,000 kila moja kwa wakati mmoja. Ujenzi umefikia asilimia 70.7

Kilikamilisha ujenzi wa msingi wa jengo la Utawala la Taasisi ya Sayansi zaBahari iliyopo Buyu Zanzibar. Kilikamilisha ujenzi wa kitengo kitakachotumiwa na kituo cha ujasiriamali. Kilikamilisha ujenzi wa awamu ya kwanza ya mradi wa Mlimani City. Kilikabidhiwa majengo yaliyokuwa ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL)yaliyoko Kijitonyama, kwa ajili ya Kitivo cha Uhandisi Umeme na Mifumo yaKompyuta cha Kampasi ya Uhandisi (COET). Kiliendelea na ukarabati wa Mabweni ya wanafunzi husasan bweni Na. 2 na Na.5.CHUO KIKUU CHA SOKOINE CHA KILIMO13. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 ChuoKikuu chaSokoine cha Kilimo kilitekeleza yafuatayo: Kilidahili jumla ya wanafunzi 1,089 kati ya hao Shahada ya kwanza niwanafunzi 820 wanafunzi wa kike wakiwa ni 33% na Shahada Uzamili 269wanafunzi wa kike wakiwa 30%.Kiliimarisha tafiti zinazolenga kuboresha kilimo, mifugo na maliasili mfano kilimocha mboga na matunda katika vijiji vya Mvomero, Mgeta, Mkuyuni, Kiroka,Matombo na Bunduki mkoani Morogoro. Kilianzisha majaribio ya kutumia panya buku kutambua kuwepo kwa vimeleavya ugonjwa wa kifua kikuu (TB) pamoja na panya hao kuendelea kutumikakatika kufichua mabomu. Matokeo ya awali yameonyesha kwamba panya bukuwana uwezo mkubwa wa kutambua TB kwa kunusa makohozi ya wagonjwakwa kasi zaidi kuliko binadamu anapotumia darubini.8

washirikishawanataaluma na wadau ndani na nje ya nchi. Kiliendesha kozi fupi, semina na kutoa huduma za ushauri wa kilimo, utunzajina usimamizi wa mali ya asili, misitu, na ufugaji kwa wakulima na wafanyakazi. Kilikamilisha ujenzi wa maktaba iliyopo Kampasi ya Solomon Mahlangu najengo la Ujasiriamali na Biashara. Kilikarabati madarasa 3, mabweni 12, maabara 1 na nyumba za wafanyakazi 4.CHUO KIKUU MZUMBE14. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Chuo Kikuu Mzumbekilitekeleza yafuatayo: Kilidahili wanafunzi 816 wa Shahada ya kwanza, kati ya hao wanafunzi wa kikeni 358 sawa na 44% na wa kiume ni 458. Aidha Chuo kilidahili wanafunzi 282wa Shahada ya Uzamili kati yao wanafunzi 133 ni wa kike sawa na 47%. Kiliendelea na ujenzi wa ukumbi wa mihadhara wenye uwezo wa kutumiwa nawanafunzi 300 katika kampasi ya Mbeya. Ujenzi huu utakamilika mweziSeptemba, 2007. Kilisomesha Wahadhiri watano (5) shahada ya uzamili na tisa (9) masomo yaShahada ya Uzamivu. Kilikamilisha tafiti ishirini na moja (21) katika maeneo ya Sayansi ya Jamii,maeneo hayo ni;-“Public Private �Financial Management”-“Administration”9

Kilinunua kompyuta 130 kwa ajili ya kuboresha ufundishaji. Kilikamilisha upanuzi wa maktaba ya Chuo, kampasi ya Mzumbe. Kiliendelea na ujenzi wa mabweni ya wanafunzi na ofisiCHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA15. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Chuo Kikuu HuriachaTanzania kilitekeleza yafuatayo: Kilidahili wanafunzi 3,868 kati ya hao Shahada ya kwanza ni wanafunzi 3,354wanafunzi wa kike wakiwa 987 sawa na 29% na Shahada ya uzamili 514 katiya hao wanafunzi wa kike wakiwa 58 sawa na 11%. Kilikarabati ofisi za wafanyakazi makao makuu na katikamikoa ya Iringa,Dodoma na kuzindua rasmi majengo ya mkoa wa Singida. Kiliongeza idadi ya wanataaluma na waendeshaji ili kuimarisha utendaji. Idadiya wanataaluma imefikia 181, waendeshaji 166 na mafundi wa TEKNOHAMA10. Kilianzisha vituo vipya katika wilaya tatu (3) za mkoa wa Dar es salaam, ilikukabiliana na idadi kubwa ya wanafunzi. Kiliimarisha huduma za maktaba kwa kuongeza majengona muda wamatumizi katika mkoa wa Dar es salaam.CHUO KIKUU CHA DODOMA ( THE UNIVERSITY OF DODOMA)16. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/07 nilitoa taarifakuhusu niaya Serikali ya kuanzisha Chuo Kikuu kipya hapa Dodoma. Napenda kuliarifu Bungelako tukufu kwamba Serikali imeanzisha Chuo Kikuu hicho kinachoitwa Chuo Kikuucha Dodoma (The University of Dodoma).10

Chuo hiki kipo katika eneo la Chimwaga ambapo jumla ya hekta 6,000 zimetolewana Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) kwa ajili ya ujenzi wachuo. Kwa sasa chuo kinaendesha shughuli zake katika jengo la Chimwaga.Katika miezi takribani 7 ya uhai wake, Chuo Kikuu cha Dodoma kimewezakutekeleza yafuatayo: Kimerekebisha jengo la Chimwaga (Remodeling), ili kupata vyumba 31 katiya hivyo vyumba 15 ni ofisi na 16 ni madarasa. Kati ya madarasa hayo 3yana uwezo wa kuchukua jumla ya wanafunzi 360, madarasa 5 yana uwezowa kuchukua wanafunzi 400 na madarasa 8 yana uwezo wa kuchukuawanafunzi 360. Kimenunua samani kwa ajili ya ofisi, vyumba vya mihadhara na kwa ajili yamalazi ya wanafunzi. Kimekarabati nyumba moja itakayotumika kama Zahanati. Kimepata watendaji wakuu wakiwemo; Mkuu wa Chuo, Mwenyekiti waBaraza, Makamu Mkuu wa Chuo na Makamu Wakuu wa Chuo wawili. Kimetangaza nafasi za kazi kwa ajili ya wanataaluma 80 na waendeshaji134. Kimetangaza nafasi za masomo katika fani za Elimu, Sayansi ya Jamii naSayansi za Kompyuta.VYUO VIKUU VISHIRIKICHUO KIKUU KISHIRIKI CHA SAYANSI ZA AFYA MUHIMBILI17. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Chuo Kikuu Kishirikicha Sayansi za Afya Muhimbili kilitekeleza yafuatayo: Kilidahili jumla ya wanafunzi 331 kati ya hao wanafunzi wa kiume ni 230 nawa kike ni 101 sawa na 31%.11

Kilikamilisha maandalizi ya kukifanya Chuo Kikuu kamili cha Tiba na Sayansiza Afya (Muhimbili University of Health and Allied Sciences-MUHAS) Kilikamilisha ukarabati wa Mabweni ya wanafunzi yaliyopo barabara yaChole Dar es salaam. Kiliendelea na ujenzi wa kumbi mbili (2) za kufundishia zenye uwezo wakuchukua wanafunzi 350 kila moja kwa wakati mmoja na vyumba 40 vyaofisi. Kiliendelea na uendelezaji wa miundombinu ya Chuo huko Mloganzila Mkoawa Pwani kwa kushirikiana na TANROADS Kiliendelea na utafiti wa magonjwa ya binadamu hususan UKIMWI (chanjo),Kifua kikuu, Malaria na magonjwa ya wanawake. Kilikamilisha upanuzi wa maktaba ya Chuo.CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ARDHI NA USANIFU MAJENGO18. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Chuo Kikuu Kishiriki chaArdhi na Usanifu Majengo kilitekeleza yafuatayo: Kilidahili wanafunzi 466 wa shahada ya kwanza kati ya hao 375 ni wa kiume na91 ni wa kike sawa na 20% . Kilikamilisha maandalizi ya kukifanya kuwa Chuo Kikuu kamili cha Ardhi (ArdhiUniversity). Kilitayarisha mitaala itakayowezesha uanzishwaji wa idara mpya 16 badala ya 6za sasa, na hivyo kufanya idadi kuwa 22.Kiliimarisha matumizi ya teknolojia ya mawasiliano katika ufundishaji kwa kununuakompyuta sitini (60).12

Kiliajiri wahadhiri na watafiti ishirini na saba (27) na wafanyakazi waendeshajikumi na moja (11). Kilikamilisha ukarabati wa awali wa baadhi ya mabweni, ofisi, madarasa nanyumba za wafanyakazi. Kilikamilisha ukarabati wa jengo la zamani la utawala kuwa maktaba namadarasa.CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU CHA DAR ES SALAAM19. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Chuo Kikuu Kishiriki chaElimu cha Dar es Salaam kilitekeleza yafuatayo:Kilidahili wanafunzi 1,479 kati ya hao wa kiume ni 833 na wa kike 646, sawa na44%.Kiliajiri walimu 103 kati yao 3 wana Shahada ya Udaktari wa Falsafa, 39 Shahadaya Uzamili na 61 Shahada ya kwanza. Pia Chuo kiliajiri wafanyakaziwaendeshaji 191 kati yao 66 ni walimu wa Shule za Awali, Msingi na Sekondari,shule hizo zinamilikiwa na kuendeshwa kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo kwawalimu wanafunzi. Kilipanua maktaba na kununua vitabu 316 vya kufundishia na kujifunzia.Kilinunua vifaa vya maabara.13

CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA USHIRIKA NA STADI ZA BIASHARA MOSHI20. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Chuo Kikuu Kishiriki chaUshirika na Stadi za Biashara – Moshi kilitekeleza yafuatayo: Kilidahili wanafunzi 403 kati ya hao 69 ni kwa ajili ya Diploma ya Uzamili na334 ni kwa ajili ya Shahada ya kwanza. Kiliimarisha mtandao wa kompyuta kwenye maktaba. Kiliendeleza mafunzo ya wafanyakazi wanataaluma kumi (10) kufikiakiwango cha Udaktari wa Falsafa. Kiliboresha shughuli za utafiti na uchapishaji. Kiliendelea kuboresha kiwango cha huduma za uelekezi na ushauri.CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU CHA MKWAWA21. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Chuo KikuuKishirikicha Elimu cha Mkwawa kilitekeleza yafuatayo:Kilidahili wanafunzi 917 kati ya hao, wanafunzi wa kiume ni 656 na wa kike 301sawa na 33%.Kiliendelea na ukarabati wa mabweni, madarasa na kuweka samani.Kilikarabati na kupanua jengo la maktaba. Kiliendelea na ukarabati wa zahanati. Kilikarabati barabara, miundombinu ya maji safi na maji taka.Kiliweka samani katika mabweni ya wanafunzi yenye uwezo wa kuchukuawanafunzi 889.14

Kilitoa mafunzo maalum kwa wanafunzi wa kike katika masomo ya Sayansi ilikuinua uwiano wa wanafunzi wa kike kwa wa kiume. Kiliajiri wafanyakazi waendeshaji 65 na wahadhiri 56TAASISITAASISI YA UANDISHI WA HABARI NA MAWASILIANO YA UMMA22. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Taasisi ya Uandishi waHabari na Mawasiliano ya Umma ilitekeleza yafuatayo: Ilidahili wanafunzi 301, kati ya hao wavulana ni 187 na wasichana 114,sawa na 38%. Iliongeza madarasa mawili yenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi sitini(60) kila darasa. Iliendesha kituo cha Radio – Radio Mlimani FM kwa kutoa ushauri wakitaalam katika masuala ya habari, mawasiliano ya umma, matangazo nautangazaji.TAASISI YA TEKNOLOJIA DAR ES SALAAM23. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007 Taasisiya TeknolojiaDar es Salaam ilitekeleza yafuatayo: Ilidahili jumla ya wanafunzi 793 wa mwaka wa kwanza katika programu zaShahada ya Uhandisi 278, Stashahada ya Ufundi sanifu 411 na Cheti chaUfundi sanifu 104. Aidha, kati ya wanafunzi 411 wa stashahada ya UfundiSanifu waliodahiliwa, 23 ni wa fani ya Uhandisi Migodi.15 p

elimu ya juu, Sayansi na Teknolojia. Ilitoa jumla ya tuzo 119 kwa wanafunzi wa kike kutoka shule 20 zilizofanya vizuri katika masomo ya Sayansi na Hisabati katika mitihani ya kumaliza kidato cha nne mwaka 2006 (18); kidato cha sita mwaka 2006 na 2007 (25); vyuo vikuu, taasisi za serikal

Related Documents:

3.0 VIPAUMBELE VYA WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI 10. Mheshimiwa Spika, Dira ya Maendeleo ya Taifa (2 025) imelenga kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025. Katika juhudi za kufikia lengo hili, Wizara ya E

Lugha ya Kiswahili. Changamoto tuliyonayo ni kwa Viongozi wengine kuiga mfano huu na Watanzania wote kuendeleza kazi hii nzuri iliyoanzishwa na Viongozi hawa. Kukua kwa Lugha ya Kiswahili sio tu kutaitangaza Nchi yetu, lakini vilevile, kutatoa ajira kwa Walimu wa Kiswahili

10. Mheshimiwa Spika, Katiba yetu, chini ya Kifungu cha 9, imeweka bayana kuwa mamlaka ya kuendesha nchi ni ya wananchi wenyewe. Kwamba nguvu na uwezo wa Serikali kufuatana na Katiba unatoka kwa wananchi wenyewe. Ni dhahiri kuwa, pamoja na kutoa ridhaa yao kwa Chama na viongozi wa kuwaongoza, wananchi ndio

3 RASIMU YA BAJETI YA MWAKA WA FEDHA 2017/2018 UTANGULIZI Mhe. Mwenyekiti, Maandalizi ya Bajeti ya mwaka 2017/18 yameanza mwezi November 2016 kwa wakuu wa

MUHTASARI WA RIPOTI YA KAMATI YA BAJETI YA BARAZA LA WAWAKILISHI- ZANZIBAR KWA MWAKA WA FEDHA 2017/2018 . kutoa elimu maskulini na michezo. . ambapo Serikali imemuekea sharti la kuanza kuendeleza eneo alilopat

Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi. Kiasi hiki ni sawa na asilimia 22.1 ya jumla ya bajeti yote ya Taifa ambayo ni Shilingi Bilioni 29,539.6. Takwimu hizi hazijumuishi deni la taifa. Kutokana na takwimu

chozi la heri 27) Suala la ufisadi limeshughulikiwa katika Chozi la heri kwa njia mbalijnbali. Fafanua njia hizo 28) Fafanua matumizi ya mbinu ya Sadfa katika chozi la heri 29) Hotuba ni kipengele cha kimundo. Eleza j

Abrasive jet machining is a modern machining process in which the Metal Removal takes place due to the impact of High Pressure, High Velocity of Air and Abrasive particle (Al2O3, Sic etc.) on a .