KIONGOZI CHA MWALIMU KWA SHULE INAYOJALI

2y ago
696 Views
17 Downloads
2.00 MB
44 Pages
Last View : 9d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Ophelia Arruda
Transcription

Step 4: development of school action planECO-SCHOOLS PROGRAMME - TANZANIAKIONGOZI CHA MWALIMUKWASHULE INAYOJALI MAZINGIRA NA ELIMUKWA MAENDELEO ENDELEVUKwa Shule za Msingi TanzaniaStep 5: curriculum localizationKimetayarishwa kwa ushirikiano waShirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili, Tanzania naDanish Outdoor Council1

Step 4: development of school action planECO-SCHOOLS PROGRAMME - TANZANIAKIONGOZI CHA MWALIMUKWASHULE INAYOJALI MAZINGIRA NA ELIMUKWA MAENDELEO ENDELEVUKwa Shule za Msingi TanzaniaStep 5: curriculum localizationKimetayarishwa kwa ushirikiano waShirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili, Tanzania naDanish Outdoor Councili

Kimeandikwa: Elisa Pallangyo kwa niaba ya TFCG Tanzania Forest Conservation GroupChapa ya Kwanza March 2017Kimepigwa chapa: DTPHaki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kutafsiri, kupiga chapa au kukitoakitabu hiki kwa jinsi yoyote ile bila ya idhini ya maandishi toka kwa TFCGShirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania- Tanzania Forest Conservation Group (TFCG)S.L.P 23410, Dar es Salaam-Tanzania.Simu: 022 2669007,Barua pepe:tfcg@tfcg.or.tzTovuti: www.tfcg.orgKuhusu the Tanzania Forest Conservation GroupKitabu hiki kimetengenezwa na Shirika la Kuhifadhi misitu ya Asili Tanzania (TFCG). TFCG nishirika lisilo la kiserikali ambalo ujumbe wake ni kuhifadhi na kurudisha bioanuwai ya misitumuhimu kidunia ya Tanzania kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijayo.ii

YALIYOMOSHUKURANI.1. Utangulizi.2. Elimu kwa Maendeleo Endelevu na muundo wa shuleinayojali mazingira (eco-school).Elimu kwa Maendeleo Endelevu (EME).Dhana ya Shule inayojali Mazingira (Eco-school).Mtazamo wa Uchunguzi, Maono, Matendo na Mabadiliko (UMMM), IVAC.Mbinu za kufundishia Elimu ya Mazingira.MATUMIZI YA ZANA ZA ELIMU YA MAZINGIRA .3.23336131520Uboreshaji mtaala.Uingizaji wa Elimu ya Mazingira katika mtaala.Mtazamo wa Haki Sawa na Shule inayojali Mazingira(Rights-Based Approach and Eco-Schools).Uingizaji Miradi Midogo katika mtaala.2222Ushirikiano kati ya jamii na shule.Kufahamisha/pasha habari na kuhusisha.Kuhamasisha ukusanyaji / uwekaji pamoja rasilimali.292931Kuchangisha Fedha (Fundraising) .Utafiti unaohusu uchangishaji fedha.Rasilimali/mali za jamii.Watu wa kujitolea.Uongozi na majukumu katika uhamasishaji wa rasilimali .Miradi ya kuongeza li 1: Mbinu na taratibu za kufundishia na kujifunzia.Jedwali 2: Uchambuzi wa taratibu za ufundishaji za Elimu ya Mazingira.Jedwali 3: Taratibu/mbinu za ufundishaji na ujifunzaji, thamani namatumizi yake.Jedwali 4: Njia za kuifahamisha jamii juu ya elimu ya mazingira.1517Jedwali 5: Mpangilio wa kuomba ufadhili.3511930

SHUKURANIShirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania (TFCG) linapenda kuwashukuru wote waliosaidiakatika utayarishaji wa Kiongozi hiki:· izara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kuunga mkono kazi hii, kwa majadilianoWna mapendekezo yao wakati ya maandalizi, hasa kwa Bwana Robert Lwikolela,Mratibu Elimu ya Mazingira;·DOC (Danish Outdoor Council) kwa ushirikano wao katika kutengeneza Kiongozi hiki;· ANIDA (Danish International Development Agency) kwa ufadhili wa kutengenezaDKiongozi hiki;· alimu katika shule za msingi zilizopo katika tarafa za Mvomero na Turiani, WilayaniWMvomero, kwa kutoa maoni;· aratibu Elimu wa kata za tarafa za Mvomero na Turiani kwa maoni wakati waWkuandika hiki kiongozi;· atumishi wa mradi wa AVA kwa kusaidia katika maandalizi ya kiongozi hiki hasa kwaWBwana Hassan Chikira, Meneja wa Mradi, Raymond Nlelwa, Hamisi Masinde, EmanuelLyimo, Daniel Mwaifunga na Gerald Alphonce;· atumishi wa Ofisi ya Elimu wilayani Mvomero kwa majadiliano na ushauri waoWmuhimu wakati wa maandalizi ya Kiongozi hiki;·Athman Mgumia kwa kuandaa michoro iliyopo katika kiongozi hiki;·Elisa Pallangyo, Mratibu wa Programu kwa kuandaa Kiongozi hiki;·Nike Doggart, Mshauri, TFCG kwa kusimamia uandaaji wa Kiongozi hiki;· harles Meshack, Mkurugenzi Mtendaji wa TFCG kwa kuunga mkono wakati waCmaandalizi ya kiongozi hiki;2

1.UtanguliziElimu ina uwezo wa kumpa binadamu maarifa na baadaye kumbadilisha mwelekeo na tabiayake kuendena na mabadiliko ya dunia.Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania pamoja na serikali ya Tanzania wamejitahidikufanya kazi ya kujenga uwezo na welewa wa mazingira kwa shule, jumuiya na wananchi kwaujumla ili waweze kutoa michango yao ya kuhifadhi na kulinda mazingira na rasilimali zao kwaajili ya maendeleo endelevu.Mojawapo wa mbinu za kupata maendeleo endelevu ni pamoja na kutumia na kuendelezaElimu ya Mazingira shuleni na katika jamii. Serikali imekuwa inaingiza Elimu ya Mazingira katikamitaala ya shule za msingi, sekondari na vyuo. Uingizaji wa Elimu ya Mazingira katika mitaalaitasaidia kwa kiasi kubwa kulinda na kuhifadhi mazingira yetu na hivyo kupata maendeleoendelevu.Kiongozi hiki cha Mwalimu kinakusudia kuwapatia welewa, stadi na kuwajengea uwezo walimuwa kuingiza Elimu ya Mazingira na Elimu kwa Maendeleo Endelevu katika mtaala wa shule zamsingi Tanzania. Kiongozi hiki pia kinamjengea mwalimu uwezo wa kutumia taratibu / mbinuza ufundishaji na ujifunzaji zinazounga mkono Uchunguzi, Maono, Matendo na Mabadiliko(UMMM), IVAC. Mfumo wa UMMM unasisitiza kutumia njia za ufundishaji na ujifunzaji wavitendo, kufikiri kwa makini, uhuru wa kujieleza/kulezea mawazo yako na kutumia mazingirayako kama zana za kufundishia na kujifunzia. Mbinu zote hizi zinaendeleza haki za binadamuna elimu bora kwa mwanafunzi.Ni matumaini kuwa Kiongozi hiki kitamwezesha mwalimu aweze kuingiza Elimu ya Mazingira/Elimu kwa Maendeleo Endelevu katika mtaala na wanafunzi waweze kupata maarifa, stadiza maisha na njia sahihi za kubadilisha mwelekeo na tabia zao katika kufikia MaendeleoEndelevu.2. Maendeleo Endelevu na muundo wa shuleinayojali mazingira (eco-school)MatokeoMwalimu aweze kuelewa maana ya Elimu kwa Maendeleo Endelevu, kuiingiza katika ufundishaji kwa kutumia mbinu za Shule inayojali Mazingira (Eco-schools) na kuzitumia vema kanuniza maendeleo ya uchumi, usawa kijamii na mazingira endelevu katika maishaElimu kwa Maendeleo Endelevu (EME)Elimu ni utaratibu wa mafunzo ambao unamwezesha mtu kujijenga kiakili na kitabia. Kila Taifalina mfumo wake wa elimu ambao unaweza kubadilika kutokana na malengo na mahitaji yawakati uliopo. Elimu ni njia ya kusaidia na kuiwezesha jamii kukabiliana na changamoto zamaisha sasa na baadaye. Elimu kwa Maendeleo Endelevu ni neno linalotumika zaidi kimataifana lilianza kutumika katika waraka wa umoja wa mataifa uitwao Agenda 21. EME inawahimizabinadamu kujenga stadi, maarifa thamani na tabia ili waweze kutoa maamuzi ya jinsi ya kuishikiendelevu.Mwaka 2002 Umoja wa Mataifa uliamua 2005 hadi 2014 iwe karne ya Elimu kwa Maendeleo3

Endelevu. Lengo hasa la UN ni kuweka mkazo katika juhudi za kukuza maendeleo endelevuduniani kwa kutumia elimu na ujifunzaji.Maana ya MaendeleoMaendeleo maana yake ni maendeleo ya watu. Mabarabara, majumba, kuongeza mazao, navitu vingine vya aina hii, siyo maendeleo; ni vyombo vya maendeleo. Maendeleo yasiyokuwamaendeleo ya watu hayana maana kwani hayahusiani na maisha ya kesho tunayojenga(Nyerere Octoba, 1968).Maendeleo ni mabadiliko chanya ya hali ya maisha ya jamii kutoka hali duni kwenda hali njemazaidi kwa kujitosheleza kwa mahitaji muhimu ya maisha ikiwemo chakula, malazi, mavazi nahuduma bora za jamii zinazofanya jamii ipate maisha bora na ya furaha. Kwa mtu binafsi,maendeleo ni kuongezeka kwa ujuzi na uwezo, uhuru zaidi, ubunifu, nidhamu binafsi, wajibuna kujitosheleza kwa vitu (Rodney, 1972:9). Kwa ufupi maendeleo ni ustawi wa maisha yawatu. Kwa maana kwamba, watu wapate mahitaji muhimu ya kuishi kama chakula bora, maji,huduma bora za afya, malazi, elimu na huduma nyingine za kijamii. Mtu anayetembelea garila kifahari wakati huohuo amekula chakula kisicho bora na kulala maeneo duni huku afya yakeikiterereka huyo hana maendeleo.Maana ya Maendeleo EndelevuIli jamii iwe na maendeleo endelevu inahitaji kukidhi mahitaji ya sasa bila kuharibu au kuzuiavizazi vijavyo kupata na kukidhi mahitaji yao muhimu. Ni falsafa ya namna tunavyowezakutumia raslimali zinazotuzunguka na kuhakikisha tunawarithisha watoto wetu rasilimali hizobila kuzimaliza ili nao waweze kuendeleza maisha yaoMaana ya Elimu kwa Maendeleo EndelevuElimu kwa maendeleo endelevu ni mfumo wa ufundishaji na ujifunzaji unaojikita katika mawazona kanuni zinazoleta uendelevu. Mawazo hayo ni pamoja na haki za binadamu, kupunguzaumaskini, maisha endelevu, amani, ulinzi wa mazingira, demokrasia, afya, bioanuwai,mabadiliko ya tabia nchi, usawa kijinsia, na ulinzi wa mila na tamaduni zetu. Katika shule zetuhatutaona njia za kujifunza na ufundishaji katika mitaala kwa ajili ya kuleta maendeleo tu lakinitutaona mifumo endelevu kama vile utawala, uhusishwaji wa wadau na jamii, mipango yamuda mrefu, ufuatiliaji na upimaji.Kuhusisha mtizamo wa shule nzima, itamaanisha shule yote ikiwa ni pamoja na wanafunzi,walimu na watawala watafanya kazi kujenga shule endelevu ambazo Elimu kwa maendeleoendelevu itaingizwa katika mitaala.Uingizwaji wa elimu kwa maendeleo endelevu katika shule haitaongeza tu uhifadhi wamazingira vizuri pekee lakini ukitekelezwa vizuri utaongeza ubora wa elimu na njia endelevuza kuishi.Kwa nini maendeleo endelevu ni muhimu?Watu zaidi ya bilioni moja duniani wanaishi katika maisha ya ufukara. Watu chini ya asilimia 20ya idadi ya watu duniani hutumia zaidi ya asilimia 80 ya rasilimali za dunia.Malengo makuu ya Elimu kwa Maendeleo EndelevuElimu kwa maendeleo endelevu ina lengo ya kusaidia watu kujenga mwelekeo, stadi namaarifa ili kujenga maamuzi kwa ajili ya wao wenyewe na wengine kwa sasa na baadaye na4

kutenda kutokana na maamuzi waliyoyafanya. Inamaanisha siyo tu kuwapa watu habari balikuhakikisha kuwa shule zinaelekezwa kubadilisha jamii kuelekea matendo endelevu.Malengo ya Elimu kwa Maendeleo Endelevu·Kujenga welewa wa maana ya maendeleo endelevu.·Kuhakikisha kuwa maarifa ya Elimu kwa maendeleo endelevu yanatolewa na kutumiwakwa vitendo katika ngazi zote za elimu (formal education).·Kuimarisha maarifa, welewa na uhusishwaji wa walimu na wakufunzi katika maana nadhana ya maendeleo endelevu ambapo kwa pamoja huhusisha uhusiano wa uchumi,mila, siasa na tamaduni.·Kuchanganua na kuchambua thamani ya maana mbalimbali za maendeleo endelevu.·Kutengeneza kivyako maana ya maendeleo endelevu.·Kutengeneza ubia kati ya wadau ikiwa ni pamoja na sekta binafsi.·Kuunda mfumo ambapo Elimu kwa maendeleo endelevu inaweza kukuzwa nakuendelezwa.Wajibu wa Elimu katika Maendeleo EndelevuElimu ni muhimu katika kukuza thamani, tabia na mienendo ya maisha inayohitajika katikamaisha endelevu. Elimu inahitajika katika kukuza welewa, kuisaidia jamii, watu binafsi naserikali ili kuweza kutoa maamuzi sahihi. Elimu haitoi tu habari lakini inawajenga watu katikamatendo endelevu.Uhusiano kati ya elimu na maendeleo endelevuElimu ni ufunguo wa uwezo wa kufikia matarajio endelevu kwa taifa loloteElimu inaweza:·Kuongeza mazao ya kilimo.·Kupunguza idadi ya vifo.·Kuwafanya wanawake kutoa maamuzi sahihi.Kusudi la elimu kwa maendeleo endelevuKufundisha na kujifunza kwa ajili ya maisha endelevu ya baadaye itakuwezesha mwalimukupanga uzoefu wa ujifunzaji ambao utawafanya wanafunzi kujenga na kutathmini njiambadala kwa ajili ya maisha ya baadaye ambayo ni endelevu na kushirikiana na wenzao ilikujenga ndoto zao za dunia nzuri kufikiwa.Ngazi za maendeleo endelevu· Mazingira: Welewa wa utajiri wa maliasili zetu na udhaifu na uendelevu wa mazingirayetu.· Uchumi: Unyeti na umuhimu wa ukuaji wa uchumi na athari/matokeo yake kwa jamiina mazingira.· Jamii: Welewa wa taasisi za kijamii na wajibu wao katika mabadiliko na maendeleo yatamaduni zao.5

Sehemu za elimu kwa maendeleo endelevu·Maarifa·Stadi / ujuzi·Taswira·ThamaniElimu kwa Maendeleo Endelevu hutetea yafuatayo:······ Kujifunza kwa kutumia njia na mbinu anuwai kwa pamoja ambazo huingizwa katikamtaala na sio somo moja tu kwa ajili ya kuleta Elimu kwa Maendeleo Endelevu.Kushirikisha thamani na kanuni zinazozungumzia maendeleo endelevu. Fikira yakinifu na utatuzi wa matatizo ambazo huongeza kujiamini katika kutatuamatatizo na changamoto za maendeleo endelevu.Ufundishaji anuwai.Wanafunzi kushiriki katika maamuzi ya jinsi ya kujifunza. Kutatua matatizo ya taifa na kimataifa na kutumia lugha ambazo wanafunzi hutumiazaidi.Dhana ya Shule inayojali Mazingira (Eco-school)Utangulizi: Dhana ya Shule inayojali Mazingira ilibuniwa nchini Denmark mwaka 1994. Nimojawapo ya programu ambazo zinaendelezwa na Foundation for Environmental Education(FEE) ambayo imeenea katika nchi nyingi duniani.Maana ya Shule inayojali MazingiraNi shule ambayo inazingatia sera ya mazingira katika kuongoza shughuli zake ambazozinafuata ngazi saba ambazo huruhusu shule ijulikane kama shule inayojali mazingira nahivyo kuitwa Shule inayojali Mazingira (Eco-school).Dhana ya Eco-school imejengwa kutokana na kuweka mazingira katika kitovu cha ujifunzajishuleni. Mazingira yamepewa kipaumbele katika mtaala na katika shughuli za kila siku.Mambo yahusiyo mazingira huweza kuchukuliwa katika mtaala na kufanyiwa kazi katikashughuli na changamoto za kila siku shuleni na nyumbani pia. Dhana hii hukazia matendo nauwezo, uhamishaji wa maarifa, ujuzi na thamani kwa kutumia ushirikiano wa shule na jamii.Shule inayojali Mazingira (Eco-school) na maendeleo endelevuShughuli ya Shule inayojali Mazingira (Eco-school) sio tu kufanya shule ipendeza kimazingirabali zaidi inatakiwa kuwajengea walimu, wanafunzi na jamii inayoizunguka shule uwezo,maarifa ya matumizi endelevu ya maliasili ili waweze kuongeza ubora wa maisha yao.Shule inayojali Mazingira (Eco-school) ni zaidi ya usimamizi wa mazingira shuleni. Niprogram ya kukuza welewa wa mazingira unaohusishwa na masomo yote yaliyoko katikamtaala. Zaidi ya hapo, masuala mtambuka kama vile; elimu kwa maendeleo endelevu,kupunguza umaskini, ujasiriamali, haki katika mazingira na jamii, elimu ya afya yote hayayanaweza kutatuliwa kwa kuhusisha Eco-schools.Shule inayojali Mazingira (Eco-school) ni mkakati wa demokrasia na ushiriki unaotoa fursakwa wajifunzaji (shuleni na wanajamii) ili waweze kujizoesha uraia wao katika maeneo yao.6

Shule inayojali Mazingira (Eco-school) ni mchakato wa ujumla unaofanya kazi kwa kuhusishashule nzima pamoja na jamii inyoizunguka shule na vyombo vya habari. Inahamasisha kazikwa pamoja (teamwork), na hujaribu kushirikisha welewa anuwai katika kuendesha shulekatika mbinu za kuendeleza na kukuza usimamizi wa mazingira, maendeleo na uendelevu.Eco-schools na Elimu kwa Maendeleo EndelevuMfumo wa Shule inayojali Mazingira (Eco-schools) unaonyesha vichocheo muhimu vya elimukwa maendeleo endelevu (ESD) ambavyo ni:(a)Kukuza na kuongeza ubora wa elimu.(b) Kuelekeza mfumo wa elimu uliopo katika ngazi zote ili uweze kushughulikiamaendeleo endelevu. Kutoa elimu inayofaa ambayo inajumuisha kanuni, ujuzi,taswira na thamani endelevu.(c) Kukuza welewa wa jamii juu ya uendelevu kwa kutumia shughuli hisishi (sensitizationactivities).(d) Kuwafunza wafundishaji wa ESD kama vile kufundisha juu ya uanzishwaji wa miradimidogo, uingizwaji wa mazingira katika mitaala n.k.(e) Kuwahusisha wadau mbalimbali katika shughuli za elimu, ambao ni pamoja naserikali ya Tanzania, sekta binafsi na asasi zisizo za kijamii katika uanzishwaji wamiradi midogo (micro projects).Programu ya Eco-schools nchini Tanzania:Programu ya Shule inayojali Mazingira hapa nchini inakusudia: kukuza kanuni za elimu kwamaendeleo endelevu nchini Tanzania kupitia shule za msingi na kukuza ushirikiano wa shulena jamii katika matumizi endelevu ya maliasili kwa kuongeza faida kwa wanafunzi wanaotokakatika shule maskini na jamii zinazoizunguka shule.Eco-schools na uwezo wa wanafunziShule inayojali Mazingira (Eco-school) huongeza uwezo wa:· awasiliano kwa ajili ya kukuza majadiliano kati ya walimu na wanafunzi na kati yaMwanafunzi wenyewe·Kutengeneza maono, kuona mbali (vision)·Kufikiri kwa makini·Kutengeneza taswira mpya·Kutoa maamuzi·Kufanya matendo sahihi7

Hatua 7 za Kuunda Shule inayojali MazingiraHatua saba za kuunda shule inayojali mazingira (Eco-School) zinatambuliwa kimataifa, hatahivyo mpangilio na jinsi ya kuzitumia hutegemea na eneo lenyewe.1.Kuunda kamati ya Eco- School. Kamati hii inaundwa na:§§§§§2. wakilishi 1 kutokaMKamati ya ShuleWawakilishi 2 wa wazaziWalimu 2Wanafunzi 4Mwalimu mkuuTathmini ya mazingira ya shule§§§8 ngalia changamotoAzilizoko shuleni kutokana naidadi, ubora, na upatikanajiwa rasilimali na athari zauharibifu wa mazingirashuleni na katika jamiiTabia na matendo ya watuNjia za kupatia kipato, uwekaji akiba/dunduiza namatumizi

3.Kutengeneza maono na malengoMaandiko malumu yanayoelezea shule itakavyoshughulikiachangamoto zilizogundulika wakati wa ukaguzi wa mazingira4.Kutengeneza Mpango Kazi§ O rodhesha shughuli, hatua zakuchukua, nani mhusika na mudawa kufanya shughuli.§ H uongoza utekelezaji wa shughulizilizopangwa.§ Huwezesha kutekeleza malengo.§ N i zana/kifaa cha kupimiauwajibikaji.5.Kuhusisha mtaala (localize curriculum) kwa:§§§9 utumia taratibu mahsusiKza ufundishajiKutumia zana zinazopatikana katikamzingira yetuKuwepo kwa tathmini ya kila wakati (continousassessment)

6.Ufuatiliaji na upimaji shughuli za Eco-school itia/angalia maendeleo yaPprogramAndika maendeleo yaliyofikiwa na changamoto za programTembelea mara kwa mara shughuli za programChanganua/chunguza mpango kazi, shughuli baada yashughuliTathmini matokeo ya program kwa walengwaHusisha matokeo ya tathmini katika shughuli§§§§§§7.Kujulisha na kuhusisha jamii kubwa kwa kutumia:§§§§§§§§§10Barua pepeMbao za matangazoRedioMabarazaMikutanoRipoti za shuleMuzikiDramaSiku za wazazi (open days)

Shughuli za kufanyaWanawarsha wafanye yafuatayo:Shughuli ya 1: Kueleza maana ya Maendeleo EndelevuSwali la 1: Taja changamoto 3 za maendeleo endelevu katika wilaya yako1. 2. 3. Swali la 2: Taja matatizo ya maendeleo endelevu katika wilaya yako na taifa na uoanisheyanayofanana na yaliyo tofautiYanayofanana:Yaliyotofauti:1. .1. .2. .2. .3. .3. .Swali la 3: Ni wapi katika mtaala wanafunzi hujifunza mambo ya dunia kuhusu:Jambo sehemu katika mtaala1.Idadi ya watu .2.Usalama wa chakula .3.Makazi mijini .4.Nishati .5.Viwanda .6.Spishi .7.Mabadiliko ya tabianchi .Shughuli namba 2 - vipimo vya Maendeleo EndelevuSwali la 1: Kwa nini kipimo cha siasa kwa maendeleo endelevu ni kipengele muhimu?Shughuli namba 3 – TafakariSwali la 1: Andika vitu 5 ambavyo vinatakiwa viwepo katika maana ya Elimu kwa MaendeleoEndelevu1. 2. .3. .4. 5. 11

Swali la 2(a) Kwa kutumia hivyo vitu 5 andika kivyako maana ya Elimu kwa MaendeleoEndelevu. Swali la 2(b) Kwa fikra zako mwenyewe je nini maana ya elimu kwa maendeleo endelevu? Swali la 2 (c) Unawezaje kutumia maliasili zilizoko katika eneo lako kufundisha na kujifunziajuu ya maendeleo endelevu ya binadamu?Shughuli namba 4Swali la 1: Je ni shughuli gani unaweza kuzifanya kuongeza welewa wa jumiya ya shulenzima kuhusu umuhimu wa elimu kwa maendeleo endelevu katika shule yako?12

Mtazamo wa Uchunguzi, Maono, Matendo na Mabadiliko(UMMM), IVACKusudi: Kuwawezesha/kuweka wazi mtazamo wa dhana ya (UMMM) IVAC kwa walimuMatokeo ya ujifunzaji: Baada ya mafunzo ya eneo hili walimu wataweza·Kuelezea mtazamo wa UMMM kwa wanafunzi.·Kutumia mtazamo wa UMMM katika kujifunzia na kufundishia.·Kuanzisha miradi midogo kwa kutumia mtazamo wa UMMM.Uwezo wa ujifunzaji:Baada ya eneo hili walimu wataweza:·Kuulizia na kugundua matatizo ya mazingira·Kuwa na mtazamo wa matatizo ya mazingira na shida zilizoko·Kujenga maamuzi sahihi juu ya masuala ya mazingira na miradi midogo·Kutenda matendo sahihi·Kufanya tafiti zinazohusu mazingiraMtazamo wa UMMM ni mtazamo muhimu sana katika kufundishia na kujifunzia unaotumikana Eco-schools katika kutekeleza elimu ya mazingira kwa ajili ya uendelevu.Ni mtazamo wa kujifunzia/kufundishia ambao unajumuisha mitazamo shirikishi mingine.Mtazamo wa UMMMNi mtazamo shirikishi na ambao unamlenga zaidi mwanafunzi katika kufundishia na kujifunzia.Mtazamo huu (UMMM) unasisitiza njia za kufundishia na kujifunzia ziwe za matendo nakutumia mazingira ya asili. Mtazamo huu unasisitiza wanafunzi kufikiri kwa makini na kuelezeamawazo na mitizamo yao katika uhalisia wa maisha kwa kuongozwa na mwalimu. UMMMhupelekea kuendeleza ujuzi wa maisha na thamani za watu binafsi ambazo ni muhimu kwamaisha na maendeleo ya jamii. Katika elimu ya mazingira, wanafunzi huchunguza, huelezeamaono yao, huelekeza jinsi ya kutenda na mabadiliko kutokana na jinsi walivyoelewa namahitaji ya mazingira yanayogusa maisha yao.Faida za mtazamo wa UMMM· ushawishi wanafunzi kila wakati kuchunguzaHdhana wanayofundishiwa na kujifunzia.· anafunzi wanauliza maswali muhimu kilaWwanapofundishwa dhana na vipengele.· anafunzi wanajibidisha kutafuta majibu yaWmaswali wanayoulizwa/kukutana nayo.· ila wakati wanafunzi hutafuta faida na hasaraKza majibu wanayopewa.· anafunzi hutafuta maono na kupataWmapendekezo.·Wanafunzi hujifunza jinsi ya kujieleza wenyewe.·Mtazamo huu hutumainisha wanafunzi kujifunza13

wenyewe katika matukio na ugunduzi.·Huusisha mafunzo darasani na mazingira yahusiyo jamii zinazozunguka shule.·Inatumainisha wanafunzi kufikiri kwa makini.·Inatumainisha wanafunzi kushiriki katika mchakato wa kufundishia na kujifunzia.·Mtazamo huu huwafanya wanafunzi kutambua vyema mazingira na maliasili zake.·Husaidia wanafunzi kutambua matatizo ya mazingira na mbinu za kuyakabili.· Hutumainisha wanafunzi kupendekeza njia za kutatua matatizo ya mazingira namchakato wa mabadiliko.Mbinu za kuuliza maswali ya kuongeza / zidisha UMMMUchunguzi: Uchunguzi unaelekezwa na maswali yafuatayoNi kwa nini ni muhimu kwetu?Je aina ya maisha na hali tunayoishi hutengeneza ushawishi?Je zamani ilikuwaje na kuna mabadilko yoyote?Je itakuwaje mbeleni kama hakuna lolote litakalofanyika kubadili huu mwenendo?Maono:Kuna njia gani mbadala ambazo tunafikiria?Je kuna hali gani katika nchi na tamaduni nyingine?Tunapendelea nini na kwa nini?Matendo:Kuna uwezekano wa matendo gani ya kuweza kufikia mabadiliko?Je ni matendo gani ya kufanya?Mabadiliko:Mabadiliko gani yatatuleta karibu na maono?Mabadiliko katika maisha yetu, darasani na katika jamii?Matumizi ya mtazamo wa UMMMMatumizi ya mtazamo wa UMMM yanaweza kuelezewa kwa kufikiria dhamira ya elimu yamazingira kama vile MAJI, USIMAMIZI WA TAKA, MISITU, NISHATI na mengineyo.Maswali elekezi:Je kuna vyanzo vipi vya maji katika mazingira yako?Vyanzo vya mito vinapatikana wapi katika jamii yako?Ubora wa maji ulikuwaje miaka kumi iliyopita na ukoje sasa?Ni kwa nini ni muhimu kulinda vyanzo vya maji katika jamii?Ni muhimu kila baada ya uchunguzi wa chochote katika mazingira au dhana, ifuatiwe naripoti ya yaliyogundulika na majumuisho.Sehemu nyingine ya UMMM ni maono ambapo maswali elekezi yanaweza kuwa:Kama mwanafunzi ninataka mchakato wa usimamizi wa taka uwe wa namna gani katikajamii?Sisi kama watoto tunawezaje kusimamia takataka tofauti na watu wazima?Usimamizi hafifu wa taka utatuathiri vipi sisi watoto?Matendo na mabadiliko kama sehemu ya elimu ya mazingira yanaweza kutumiwa nawalengwa kwa kushawishi matendo yatokanayo na wadau kutoka shule na jamii.14

Mfumo wa matendo unaweza kutekelezwa kwa kutumia mtu mmoja mmoja, vikundi, au jamiikwa kutumia uongozi mbalimbali kupitia meseji, drama, majadiliano. Wanafunzi wanawezakuhusika kwa kuwapelekea ujumbe jamii kupitia redio, maandiko, video na mikutano yawazazi.Shughuli ya kufanya:Jiweke kwamba unafundisha darasa la sita juu ya vitendo na shughuli zinazohatarisha misitukatika mazingira yao (Jiografia drs la 6 Mada kuu/mada ndogo: 2.4 Misitu; Tumia mtazamowa IVAC katika kufundisha kipindi kwa vitendo)Mbinu za kufundishia Elimu ya MazingiraMatokeo ya mafunzoHadi mwisho wa kitengo hiki ninategemea· Kukubali (adopt), kutafiti, kuimarisha na kutumia njia sahihi mbalimbali kufundishiaelimu ya mazingira· Elezea kwa ufasaha taratibu tofauti, mazingira na stadi za kuwapatia wanafunzi moyowa kuhifadhi mazingiraUwezo·Kutambua mbinu anuwai ambazo zinaweza kutumika kufundishia elimu ya mazingira·Elezea njia sahihi kwa kila utaratibu iliyotambuliwa·Kuoanisha yaliyomo katika taratibu sahihiMada: Mbinu za kufundishia elimuJedwali 1: Mbinu na taratibu za kufundishia na kujifunziaUtaratibuJinsi ya kufanya/ShughuliMajadilianoMaswali na majibu, mjadala,kuelezea hadithi, mahojiano,safari za mafunzo (field visit), bungua bongoDramaMichezo ya kuigiza, drama, mazungumzo, mjadalaMaonyesho (exhibition)Maonyesho, maelezo kwa kutumia picha, chora ramani juuya ardhini, ramani ukutani, vitu halisiUwakilishiMichoro,chati, picha, mabangoUtaratibu wa vikundiKuripoti, kukaa katika vikundi, bungua bongo (brainstorming)Utatuaji matatizoUshindanishaji, uchambuzi, mafumboKudadisi na uvumbuziKazi za miradi, utafiti, safari za mafunzo, maswali, kudadisina uvumbuzi, mahojianoUjifunzaji wa ushirikaMajdiliano, kurekodi, maswali na majibu, kuripotiUtaratibu wa miradiKutumia vikundi,Michezo ya uigizaji (roleDhihirisha, elezea, kuhusianisha, dhaniaplay)Kutafsiri pichaKuangalia, husianisha,CinemaKuonyesha, kuoanishaJaribioKutoa maagizo, kuangalia, kurekodi, kuripoti, kuandikaUgunduzi wenye mwongozo Kutoa maelezo, kuelezea, kusoma, safari za mafunzo, utafitiKatika eneo hili mwalimu atawezeshwa kuelewa mbinu sahihi za ufundishaji ambazo15

zitawawezesha wanafunzi kupata uwezo wa kiutendaji ambao utachangia katika utunzaji nauhifadhi wa mazingira.Eneo hili litawawezesha kuelewa maana ya:Mazingira: Mazingira ni vitu vyote vihusivyo mazingira katika mazingira na kwa ajili yamazingiraTaratibu / mbinu za elimu ya mazingira: Ni mikakati na vitendo vya namna ya kutatuamatatizo na changamoto zitokanazo na shughuli za binadamuUtambuzi wa mikakati utakufanya kupata maarifa, ujuzi, maono, mtizamo na kubadilika kwatabia na kuchukua hatua juu ya matumizi, ulinzi, na matumizi endelevu ya maliasili.Maswali ya tafakari·Neno mazingira lina maana gani kwako?·Kwa nini umehusishwa katika kipengele hiki?·Ni utaratibu gani wa ufundishaji katika kitengo hiki ambao umeshawahi kuutumia?·Ni taratibu zipi ambazo haziwezi kutumika katika elimu ya mazingira?16

17MaonyeshoKazi za vikundi-maarifa yakitakachoonyeshwayanahitajika kabla yamaonyesho-weka maelezoyakutosha katika kilaunachoonyesha-Vitu vya kuonyesha-Utayarishe kazi ya/za kuwapavikundi-Uwe na maamuzi yajinsi ya kuunda kikundi-waongoze wanafunzikutengeneza watakachoonyesha-ainisha kinachotakiwakuonyeshwa-Fundisha maudhui (content) yalazima-waongoze-wape wanafunzi maelezo-waweke wanafunzi katika vikundi-Usome na uwe na welewa wakazi yenyewe-Karatasi za kuandikiaza kila kikundi-waongoze jinsi ya kuripoti najitahidi kuwahusisha ambaohawana uwezo mkubwa-andaa jinsi ya kutathminimchakato wa kipindi chako-uwe na uamuzi juu ya mbinu zakutumia-Uisome na uijue mada vizuriMahojianoUnahitaji kujua kamamahojiano yatakuwakatika vikundi au la,kati ya walimu nawanafunzi au katikajozi za wanafunziJinsi ya kufanyaTaratibu / mbinu UnachohitajiJedwali 2: Uchambuzi wa taratibu za ufundishaji za Elimu ya MazingiraHasara-uchaguzi wa madausipoangalia wanachofahamuwanafunzi, utaratibu huu hufeli- wanafunzi werevu zaidihuwafunika wenginewasionekaneWanafunzi wanashirikishwa-Kufanikiwa kwake hutegemeavitu vilivyoko vya kuonyesha-Kufanikiwa kwake hutegemeauwezo wa mwalimu-Ni mbinu/utaratibu shirikishi Kama hakuna maandalizi namwongozo mzuri wanafunzi-stadi kama vile uongoziwenye uwezo zaidi huwafunikahupatikanawasio na uwezo-wanafunzi wanapatauwezo wa kulinganishawalichokuwa nacho-huongeza kujiamini kwamwanafunzi zaidi-humwezesha mwalimukuongeza nukuu zake kwaninyingine hakuwa nazo-mwalimu huwezakuwaelewa wanafunzi wakekiwelewa na uwezo-wanafunzi

Kiongozi hiki cha Mwalimu kinakusudia kuwapatia welewa, stadi na kuwajengea uwezo walimu wa kuingiza Elimu ya Mazingira na Elimu kwa Maendeleo Endelevu katika mtaala wa shule za msingi Tanzania. Kiongozi hiki

Related Documents:

Kiongozi cha Mwalimu Toleo la Milima ya Tao la Mashariki. 1 Elimu ya Mazingira kwa Shule za Msingi Toleo la Milima ya Tao la . FORS (Friends of Ruaha Society) kwa kutupa kiongozi cha awali. FORS ni shirika dogo lililopo Iringa ambalo

3. Uongozi wa Shule wanahaki ya kumfukuza mwanafunzi ambaye hajafika wastani unaotakiwa kwa kiwango cha Shule au tabia yake haiendani na mwenendo wa shule. 4. Nafasi ya BWENI inatolewa kwa wavulana na wasichana. 5. Wanafunzi wa KUTWA wanakaribishwa, Ada ya Shule kwa wanafunzi wa kutwa wasiotumia usafiri ni shilingi 930,000/ kwa mwaka. 6.

Kielelezo cha muuundo wa uongozi na mgawanyo wa majukumu katika shule. Majukumu ya mwalimu mkuu Mwalimu mkuu ni kiongozi na msimamizi mkuu wa shughuli zote za manejimenti na utawala katika shule.Pamoja na mambo mengine majukumu ya mwli mkuu ni Kusimamia utekele

KIONGOZI MTUMISHI Wakati moja niliona kibonzo cha mtoto mvulana, aliyekuwa kiongozi wa skauti ambaye alipeleka kikundi chake cha wavulana kukwea mlima, ambapo alipotea na kuuliza kama yeyote kati yao alikuwa na dira (compass). Jambo la kwanza kwa kiongozi

ya Machipuko Si siku ya shule Aprili 04/12 na 04/13 Mtihani wa SAT & ACT WorkKeys Wanafunzi wa Vidato vya Chini pekee A.M. Wanafunzi Wote wa HS P.M. Shule ya Msingi ya Siku Nzima Mei 05/11 Hakuna Shule 05/20 Siku ya Mwisho ya Shule ya 1 Wanafunzi wa Vidato vya Juu 05/27 Siku Nusu (Shule ya Msingi) 05/30 Sikukuu ya Makumbusho - Hakuna Shule Juni

Kwa kila kipindi cha muda na kwa kila eneo, mwongozo unapendekeza hatua ambazo kiongozi wa shule anapaswa kuzichukua wakati shule zimefungwa na wakati zinafunguliwa tena. . huyu anaweza kuwa mmiliki, mwalimu

Maombi na mara kwa mara Kiongozi wa Masomo ya Biblia, Mwalimu wa Shule ya Jumapili nk. Kwa kipindi cha cha 1972 mpaka wakati wa sasa Kimehaririwa na Lois E. Gloyd 421 E. Jackson Street, Ripon, WI 54971 legloyd@gmail.com Associate Degree: Computer Techn

Nutrition and Food Science [CODE] SPECIMEN PAPER Assessment Unit A2 1 assessing. 21 Option A: Food Security and Sustainability or Option B: Food Safety and Quality. 22 Option A: Food Security and Sustainability Quality of written communication will be assessed in all questions. Section A Answer the one question in this section. 1 (a) Outline the arguments that could be used to convince .