UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 - Mwalimu Wa Kiswahili

3y ago
2.1K Views
123 Downloads
1.17 MB
55 Pages
Last View : 1d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Dani Mulvey
Transcription

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017UTUNGAJI/UANDISHIUtungaji ni neno linalotokana na kitenzi “tunga”. Kitenzi hiki kwa mujibu waKamusi ya Kiswahili Sanifu (2004:414) linamaanisha “toa mawazo kutokaubongoni na kuyakusanya, kisha kuyadhihirisha kwa maandishi, kwa kusimulia,kwa kuyaimba au kwa muziki.Kwa hiyo tunaweza kusema kuwa, utungaji ni kutoa mawazo binafsi kutoka akilinimwa mtu kuhusiana na mambo mbalimbali katika jamii, kisha kuyaweka wazi kwanjia ya mdomo au maandishi.Kile kilichotungwa na mtunzi kinawezakudhihirishwa kwa mitindo mbalimbali, kama vile riwaya, mashairi, tamthiliya,insha na barua.Dhima ya Utungaji Utungaji huwezesha watu kutoa maelezo, mawazo au maoni kwa njia yamaandishi au mazungumzo. Utungaji huwezesha utumiaji wa lugha fasaha, sanifu na uwezo wa kujielezakwa njia ya maandishi au mazungumzo. Utungaji huwezesha utumiaji wa mantiki, mpangilio mzuri wa mawazo,mtiririko na matumizi sahihi na fasaha ya lugha na kanuni za fasihi. Utungaji huwezesha kutoa taarifa mbalimbali zinazohusu maisha yetu yakila siku. Kupitia njia ya utungaji, watu hupata taarifa kuhusu vitumbalimbali vinavyozunguka maisha yao ya kila siku. Utungaji hutumika kuelimisha, kukosoa na hata kuonya. Maandishi aumazungumzo (masimulizi) yanayotokana na utungaji huweza kuakisi halihalisi ya maisha ya jamii, na hivyo ikawa ni kama kioo cha kujitazama nakujirekebisha. Utungaji, hususan unaotokana na kazi za fasihi hutumika kuburudishajamii. Hadithi na tanzu nyingine za fasihi zinazotokana na utungajihuburudisha, huliwaza na kufurahisha jamii. Utungaji hutumika kukuza lugha kwa njia ya mazungumzo au maandishi.Mzungumzaji na msikilizaji hupata ufundi wa kujieleza zaidi kupitiaMaeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 1

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017utungaji, hali kadhalika mwandishi na msomaji hupata ufundi wa kujielezazaidi kupitia njia ya utungaji.Kanuni za Utungaji boraUtungaji bora ni lazima uzingatie kanuni zifuatazo: Matumizi mazuri ya nyakati: mfano, wakati uliopo, ujao na uliopita au halitimilifu. Matumizi mazuri ya lugha fasaha (lugha inayoeleweka). Mpangilio mzuri wa mawazo na mantiki, yaani kutochanganya mawazo,kutorudiarudia mawazo au kutosahau mawazo. Matumizi bora ya vituo na alama za uandishi. Matumizi bora ya sarufi ya lugha inayohusika. Utungaji bora hugawanyika katika sehemu kuu zinazobainisha muundo wakazi yenyewe mf. Insha hugawanyika sehemu nne ambazo ni: Kichwa chainsha, Utangulizi, Kiini na Hitimisho Utungaji bora huwa na mifano ya kutosha.Uandishi wa InshaInsha ni utungo wenye sentensi nyingi zilizopangwa katika aya, zenyekuzungumzia mada moja. Kwa mfano, insha zinaweza kuwa zinazungumziamada zifuatazo: Umuhimu wa Chakula Bora, Tiba Kutokana na Vyakula;Ujamaa ni Imani au Jamii Inakwenda Kombo.Mambo ya kuzingatia katika uandishi wa Insha.Bila kujali aina ya insha inayoandikwa, yapo mambo kadhaa ya kuzingatiawakatiwa kuandika insha. Mambo hayo ni pamoja na:(a) Kubaini mada ya kuandikia insha na kuielewa vyema.(b) Kupanga mawazo katika mtiririko wenye mantiki(c) Kutumia mtindo unaoendana na kusudi la insha. Kwa mfano, mtindo wamasimulizi, unafaa kwa hadithi au insha zingine za kisanaa.(d) Kutumia lugha fasaha na inayoeleweka(e) Kufuata kanuni za uandishi. Kwa mfano, matumizi ya alama za uandishi,aya, herufi kubwa na ndogo, n.k(f) Kupanga insha katika muundo wake, yaani kichwa, utangulizi, kiini naMaeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 2

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017hitimisho.Muundo Wa InshaInsha hugawanyika katika sehemu kuu tatu ambazo ni: Kichwa cha InshaKichwa cha insha huandikwa kwa herufi kubwa, katikati, juu yainsha. Hakipaswi kuzidi maneno matano na hupigiwa mstari. Utangulizi (Mwanzo)Katika sehemu hii inampasa mwandishi atoe maelezo mafupi namaana ya habari aliyopewa. Kiini cha insha oishughulikia huku akitoa mifano hai inayoendana na hali halisi. Hitimisho (Mwisho)Inampasa mwandishi kutoa mapendekezo (maoni) ya msingi aukusisitiza kwa ufupi yale aliyoyaelezea katika habari yenyewe.NB: Hitimisho sio ufupisho wa hoja zilizojadiliwa katika sehemu ya inshayenyewe.Aina za InshaAina ya insha au jina la insha hujulikana kutokana na mawazo yamwandishi. Kuna aina nyingi za insha lakini tunaweza kuziweka aina hizokatika makundi makuu mawili ya insha za hoja na insha za wasifu. Kilakundi kati ya makundi haya mawili kuna insha za kisanaa na insha zisizo zakisanaa.Zingatia kielelezo kifuatachoInsha za KisanaaHojaInsha zisizo za KisanaaInshaInsha za KisanaaWasifuInsha zisizo za KisanaaMaeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 3

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017Insha za kisanaa hutumia vipengele mbalimbali vya fasihi katika kuwasilishaujumbe - mfano nahau, methali, ,misemo au tamathali za semi huwezakutumika. Insha zisizo za kisanaa hazitumii lugha ya kifasihi katikakufikisha ujumbe.Insha za wasifu huelezea sifa (uzuri au ubaya) za kitu, hali au mtu fulani.Insha za hoja ni insha ambazo hutetea mawazo ya aina fulani na kupingamengine kwa uthibitisho uliodhahiri. Mfano wa insha za wasifu ni Uzuri wabahari ya Hindi, Fahari ya Mlima Kilimanjaro, n.k. mfano wa insha za hojani: Ukimwi ni Ugonjwa Hatari, Uhuru wa Bendera, n.k.Mfano wa Insha ya WasifuAtukuzwe Nyerere wa TanzaniaNyerere wa Tanzania, kiongozi shujaa wa dunia – amepata kutukuka pande zote zadunia. Alizaliwa katika kijiji cha Butiama, Wilaya ya Musoma Vijijini mkoaniMara. Alisoma elimu ya msingi katika shule ya Mwisenge – mojawapo ya shule zazamani sana hapa nchini. Alipata elimu ya sekondari huko Tabora. Alijiunga naChuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda kabla ya kwenda huko Uingerezakusomea shahada ya M.A.Baada ya uhuru toka Uingereza, Mwalimu Nyerere alishughulika sana na suala laukombozi wa Tanganyika na Afrika kwa ujumla. Alionesha jitihada za wazikupambana na mabeberu wa Kiingereza hadi uhuru wa Tanganyika ukapatikanatarehe 9/12/1961. Tanganyika ikawa ya kwanza kupata uhuru wake ukilinganishana nchi zote za Afrika ya Mashariki na kati – sifa kuu kwa Nyerere waTanganyika.Nyerere alishirikiana na Karume kuziunganisha nchi hizo na kuzaa Tanzania – jinalililotumika na kuheshimiwa kote ulimwenguni. Wakati Nyerere akichanganyaudongo wa Tanganyika na Zanzibar alitamka maneno ya hekima yafuatayo:“Tumeamua kuziunganisha nchi zetu ili kuimarisha umoja wa Afrika. Naaminikuwa maadui wetu watachukia na kuhuzunika kwa kitendo hiki cha kishujaaMaeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 4

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017tulichokifanya, lakini daima hatutaogopa chochote. Muungano wetu utadumumilele na milele. Mungu ibariki Tanzania. Mungu ibariki Afrika. Amina!”Sifa ya pekee inayomtofautisha Mwalimu Nyerere unapomlinganisha nawanafalsafa wengine duniani kama vile Karl Marx na Mao ni kwamba yeyealiwapigania wanyonge wote kote ulimwenguni bila kujali ubaguzi wa rangi,kabila, taifa au bara. Aliwatetea wanyonge wa Afrika. Aliwapigania wanyonge waUlaya na Mashariki. Aliwapigania wanyonge wa bara la Asia. Hali kadhalikaaliwapigania na kuwatetea wanyonge wa bara la Amerika ya Kusini. Hivyo ni sifaya pekee inayofaa kumtofautisha na wanafalsafa wengine waliomtangulia.Nyerere atatukuzwa daima kwa ushujaa wake. Alikuwa si kiongozi wakujikombakomba kwa mataifa mengine ya kibeberu. Alipotishiwa au kuwekewavikwazo/vitisho, alivunja mara moja uhusiano wa kidiplomasia na taifalinalohusika. Kwa mfano mwaka 1965 alivunja uhusiano wa kidiplomasia na nchiya Uingereza baada ya nchi hiyo kuitangaza nchi ya Zimbabwe kama koloni lakela kudumu la Walowezi. Kitendo hiki kilimpatia sifa na heshima kubwa hapaAfrika na duniani kote – kwa wapenda amani.Ingawa ni vigumu kuzitaja sifa zake mpaka mwisho, lakini sifa ya kupiga makelelekatika majukwaa ya kimataifa haitaweza kusahaulika. Hakuwa msomi mkimyakama wasomi wa enzi hizi. Alitumia elimu yake ipasavyo kuitetea falsafa yake yaHaki na Usawa kwa Binadamu Wote katika majukwaa ya kimataifa.Wananchi wa Uganda daima humkumbuka na kumtukuza kwa jinsi alivyotumianguvu za kijeshi kuung‟oa utawala wa kidikteta wa Nduli Idd Amini Dada.Wakikumbuka mateso waliyoyapata enzi za utawala huo, humtukuza na kumuenziNyerere usiku na mchana.Nyerere hataweza kusahaulika kwa jinsi alivyopinga kitendo cha viongoziwachache wenye hila kuendelea kung‟ang‟ania kwenye madaraka. Alikuwakiongozi wa kwanza hapa Afrika na pengine duniani kote kung‟atuka kwenye kiticha Urais. Alifanya hivyo kwa hiyari ili kutoa nafasi kwa wananchi wenginewashike wadhifa huu nyeti hapa nchini kwetu.Mwalimu Nyerere ni mwenzetu, ni rafiki yetu, ni mtu wa watu, ni baba wa taifaletu, ni babu yetu mwenye hekima na busara. Paji lake la uso lilijaa hekima naMaeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 5

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017busara. Kinywa chake daima kilinena maneno ya hekima na busara. Fikra zakezitadumu milele kwenye vichwa vya wakulima, wasomi, wanafalsafa, mapadri,masheikh, wachungaji, watawa na hata kwenye bongo za waovu wa Tanzaniadaima watamkumbuka.Kifo cha Mwalimu Nyerere kimeleta pengo kubwa kwa jamii yote ya wapendaamani kote ulimwenguni. Ingekuwa mbegu ya mmea tungeipanda sote tuendeleekuhekimika kutokana na hekima na busara zake.Kifo cha Mwalimu Nyerere ni kama mwindaji asiye na silaha kwenye mwitu wenyewanyama wakali kama fisi, simba, ngiri, tembo, nyoka, nyati, n.k. Je, mwindajiatafanya nini?Daima sifa na hekima za Mwalimu Nyerere zitukuzwe Tanzania, Afrika naulimwenguni kote.Mfano wa insha ya hojaKijana wa leo nina balaa!!Kilio, kilio, kilio kwa kijana wa leo, Afrika! Wakati vijana wengine wanapoombwakujiunga na jeshi ili kujenga na kulinda nchi yao, siyo kwangu. Kwangunaburutwa msituni, kujiunga na jeshi kuendeleza vita ya wenyewe kwa wenyewe.Napigana na ndugu zangu ndani ya taifa moja ili matumbo machache yafaidialmasi, dhahabu, mafuta na maliasili nyingine. Naingizwa katika vita isiyo namaana yoyote kwangu.Nikitaka kutafuta elimu, hakuna madarasa. Upepo umeezua paa la nyasi la shuleyetu! Nikibahatika kupata kaelimu kadogo; chini ya mti, nazuiwa kufikiri zaidi.Naambiwa kuwa, Afrika hakuna kufikiri! Mtu mweusi hana fikra ila mtu mweupendiye mwenye fikra. Natakiwa nifuate fikra zake!Nikitaka ajira, naambiwa uzoefu miaka mitano au kumi na zaidi. Uzoefu nitaupatawapi? Nikitamani kujiajiri mazingira hayaniruhusu: Umasikini, umasikini tenaumasikini umenikumbatia!Nikijiunga na siasa, wimbo maarufu kote ulimwenguni ni demokrasia. Demokrasiaina mizengwe, umajimbo, ukabila, udini, ubabe, rushwa, ubabaishaji, utapeli naMaeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 6

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017kushindana bila kukubali kushindwa. Siasa barani kwetu ni kiini macho namatokeo yake ni „demoghasia‟ isababishayo vifo. Ubinafsi umejaa! Kujipitishiamarupurupu kibao! Ubaguzi! Majigambo! Dharau .!Nikitaka kusema, naambiwa mjinga, Nikidai haki, naambiwa madai yangu ni yakijinga. Nalazimishwa kuandika barua ya kuomba msamaha na kuahidi kuwasitadai haki tena! Nalazimishwa kuwa bubu. Kijana msomi nanyimwa uhuru wakutoa mawazo yangu mbele ya jumuiya yangu. Kijana msomi nafungwa mdomo.Kijana msomi kukaa na kunyamaza kimya ni usaliti. Usaliti kwa jamii ya walipakodi ambao pesa zao zimenisomesha hadi kuitwa msomi. Kijana msomi, kutofikirini dhambi nyekundu pyuuu!- isiyosameheka. Msomi kutofikiri ni kifo cha kifikrakwangu mimi kijana wa Kiafrika.Chochote ninachotaka kufanya kinanikatisha tamaa. Nikiwa „deiwaka‟ mpigadebe, kila siku nitaamkia korokoroni! Nikitaka kujiburudisha na gongo au viroba ni kifo cha ajabu. Nikibugia unga – kwangu ni kifo cha mende wekundu!Nikijiingiza kwenye ukahaba, natozwa kodi ya maendeleo! Nikitaka kuwa“changudoa”, UKIMWI unaniwinda kama mamba awindavyo viumbe baharini!Sasa nifanye nini? Balaa kubwa kwangu!Nikiamua kuokoka, wokovu hauonekani. Nimebaki njia panda. Mchungajiamekuwa mwongo, katu hasemi ukweli. Ananilaghai kuwa wokovu upo karibukuingia badala ya kuniambia kweli wokovu umekwishatoweka. Naambiwa kuwanijiwekee hazina mbinguni ambako kutu na wadudu hawataharibu maliyangu Huu ni utapeli.Ingekuwa vizuri kama ningeelezwa wazi jiwekee akiba tumboni mwa sheikh autumboni mwa mchungaji au tumboni mwa padre! Naambiwa kuwa toeniulichonacho utabarikiwa badala ya kuambiwa kuwa kitayabariki matumbo yawachache!Nakumbuka wakati mama yangu alipokuwa mwalimu katika shule ya msingi yaMabonde Kuinama, aliniambia kwamba, urithi wa utamaduni wetu ni mila nadesturi za Afrika. Lakini siku hizi sivyo. Siku hizi naambiwa kuwa urithi wa kizazikipya ni bia aina ya “Safari Larger”.Maeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 7

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017Kijana wa sasa naangalia wizi wanaofanyiwa watu maskini lakini sisemi chochote.Najinyamazia kimya. Wizi umo makanisani, misikitini, Ikulu, mahakamani na hatabungeni. Lengo ni kuwanyanyasa, kuwadhulumu, kuwaonea, kuwanyonya nakuwadhalilisha wanyonge. Hakika kunyamaza kwangu ni usaliti. Nimeitambuanafasi yangu. Naahidi kupambana hadi kufa na kupona.Uandishi wa barua na kadi za mialikoKuna aina mbalimbali za barua. Aina hizo hugawanywa katika makundimakuu mawili ambayo ni Barua za kirafiki/kindugu na Barua rasmi.(a) Barua za Kirafiki/KinduguHizi ni barua zinazoandikwa kwenda kwa ndugu, jamaa na marafiki kwamadhumuni mbalimbali kama vile:- Kusalimiana- Kujulishana maisha yetu ya kila siku- Kuomba msaada au kutoa shukrani kwa kutimiziwa maombi yetu.- Kutoa hongera, rambirambi, pongezi, n.k.Sehemu za Barua za Kirafiki/Kindugu Anuani ya MwandishiHuandikwa kwenye pembe ya kulia ya karatasi. Anuani hii ndiyohutumiwa na mwandikiwa wakati wa kujibu barua aliyoipokea na piahutambulisha maskani ya mwandishi wa barua kwa wakati huo. Kwahiyo, ni wajibu wa mwandishi kuandika anuani yake vizuri. Ni lazimaiandikwe waziwazi. TareheHii huandikwa mara baada ya anuani ya mwandishi. Huandikwa ilikumjulisha mwandikiwa barua imeandikwa lini na kama imefika kwawakati au imechelewa. Zipo njia mbalimbali za kuandika tarehe, nazo ni:- 20.9.2017- 20/9/2017- 20-9-2017- 20 Septemba, 2017- Septemba 20, 2017Maeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 8

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017 Mwanzo wa baruaBarua za kirafiki/kindugu huanza kama ifuatavyo:- Baba mpendwa,- Mpendwa baba,- Mwanangu mpendwa,- Mama mpenzi, n.k. Barua yenyeweHii ni sehemu muhimu sana. Sehemu hii ndiyo inayomfanyamwandikiwa aelewe kusudi la mwandishi. Sehemu hii iandikwe vizuri ilibarua ieleweke kwa urahisi. Mwisho wa baruaMwisho wa barua ni sehemu inayostahili kuandikwa vizuri. Njiazifuatazo ni baadhi ya zile zitumikazo kumalizia barua ya kindugu.- Mwanao akupendaye.- Wako wa moyoni.- Rafiki yako akupendaye.- Wako akupendaye.- Wasalaam, baba yako, n.k. Jina la MwandishiNi vizuri kuandika jina lako mwishoni mwa barua ili yuleunayempelekea afahamu barua imetoka kwa nani.Maeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 9

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017Mfano wa barua ya kirafikiShule ya Sekondari Mbezi Beach,S.L.P 60213,Dar Es Salaam.03/07/2017.Mpendwa,Salaam sana. Natumai u mzima pamoja na jamaa na marafiki wa haponyumbani. Nami ni mzima na ninaendelea na masomo yangu vizuri hapashuleni. Napenda kukujulisha kuwa maendeleo yangu kimasomo hapashuleni ni mazuri sana. Katika mtihani wa kumaliza mwaka wa pilinimeshika nafasi ya pili kati ya wanafunzi 195 wa kidato cha tano.Nimeamua kusomea mchepuo wa biashara ili hatimaye niwe mchumi wanchi yetu hivyo naomba tuzidi kuombeana heri.Pamoja na mafanikio hayo yote, kuna tatizo kubwa sana ambalo linazidikuniandama hapa shuleni. Tatizo hili linanikosesha kabisa raha, kilawakati huwa ninahuzunika. Tatizo hili huwa ni la umasikini. Sina hatashilingi tano ya kununulia kipande cha muhogo. Hivyo, naomba uuzeyule jogoo mkubwa unitumie pesa haraka iwezekanavyo.Wasalimie wote wanaonifahamu hapo kijijini. Msalimie sana shangaziwangu Lilian Joackim.Wako akupendaye,Haidari Hamisi.(b) Barua RasmiKwa kawaida barua rasmi huandikwa kwa makusudi mbalimbali kamavile, kutoa taarifa za tukio fulani, kuomba kazi, kuagiza vifaa au vitu,kumwalika kiongozi katika shughuli maalumu, kutoa taarifa yakushindwa kufika mkutanoni, n.k.Barua rasmi zipo za aina nyingi, lakini zinaweza kugawanywa katikamakundi matatu makubwa yafuatayo:Maeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 10

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017- Barua za kuomba kazi- Barua za kutoa taarifa- Barua za kuagiza au kupokea bidhaa/vitu.Sehemu za barua rasmi(i) Anuani ya mwandishiAnuani hii huandikwa pembe ya juu kulia ili kutambulisha maskani yamwandishi na pia hutumiwa na mwandikiwa wakati wa kuijibu barua husikainapobidi.(ii) TareheHuandikwa chini ya anuani ya mwandishi ili kumjulisha mwandikiwa kamabarua hiyo imefika mapema au imechelewa.(iii) Kumbukumbu nambaBarua rasmi huwa na kumbukumbu namba. Huu ni utambulisho maalumuwa barua husika. Kumbukumbu namba aghalabu huwa ni kifupi cha jina lataasisi inakotoka barua hiyo, kule inakokwenda, hiyo ni barua ya ngapi namwaka husika. Mf: Mbss/crdb/02/17(iv) Anuani ya mwandikiwaAnuani hii hutanguliwa na cheo cha mwandikiwa na huwekwa upande wakushoto chini ya kumbukumbu namba. Nafasi ya mstari mmoja au zaidihuweza kurukwa baina ya kumbukumbu namba na anuani ya mwandikiwa.(v) Mwanzo wa baruaSehemu hii huandikwa chini ya anuani ya mwandikiwa. Ni heshima kutajacheo cha mwandikiwa mwanzoni mwa barua ya namna hii, kwa mfanoNdugu Katibu, Ndugu Ofisa Mifugo, n.k.(vi) Kichwa cha baruaKichwa cha barua hutaja kwa ufupi jambo linalohusu barua hiyo. Kichwacha barua huandikwa waziwazi katikati ya barua mara baada ya mwanzo wabarua. Ni muhimu kiwe kifupi na chenye kueleweka waziwazi. Hufaa zaidiMaeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 11

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017kikiandikwa kwa herufi kubwa na kupigiwa mstari. Hakipaswi kuzidimaneno matano.(vii) Barua yenyeweSehemu hii huandikwa mambo yote muhimu kuhusu barua yenyewe. Baruayenyewe iwe fupi na yenye taarifa za lazima tu. Uanzaji wa barua yenyeweumrejeshe msomaji kwenye mada ili kufupisha maelezo mengi kama vilekwa kusema:- Mada tajwa hapo juu inahusika- Rejea barua yako ya tarehe .yenye Kumb. Na .- Husiana na mada tajwa hapo juu, n.k.(viii) Mwisho wa baruaMwisho wa barua huwa ni tamko la heshima la kumalizia barua. Maranyingi mwisho unaotumika katika barua rasmi ni kama vile:- Wako mtiifu,- Wako katika ujenzi wa taifa,- Wako katika kazi, n.k.(ix) Saini na jina la mwandishiMwisho wa barua mwandishi hupaswa kutia saini na jina lake kamautambulisho wake juu ya kilichoandikwa. Saini hupaswa kutiwa kwamkono.(x) Cheo cha mwandishiBaada ya jina mwandishi hupaswa kuandika cheo chake. Cheo kinawezakuwa:- Mwanakijiji- Muombaji- Mwalimu Mkuu- Afisa Mtendaji, n.kMaeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 12

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017Aina za Barua Rasmi1. Barua ya Kuomba KaziBarua ya kuomba kazi inahitaji uangalifu sana katika sehemu ya baruayenyewe. Barua hii inatakiwa iandikwe kwa umakini na ujuzi mwingi.Katika barua hii kuna mambo makuu manne ambayo ni: kutaja kaziunayoomba, jinsi ulivyopata taarifa, elimu, ujuzi na uzoefu, maelezo binafsina wadhamini.Mfano wa barua ya kuomba kazi:Kijiji cha Mto wa Mbu,S.L.P 4507,Arusha.04/7/2017Meneja wa Kiwanda,Kiwanda cha Kusindika Matunda,S.L.P 0717,Iringa.Ndugu,YAH : OMBI LA KAZI YA UKARANIHusika na kichwa tajwa hapo juu. Ninayo heshima kuomba kazi ya ukarani katikakiwanda chako kama ilivyotangazwa kupitia gazeti la “Sanifu” Uk. 3 la tarehe20/6/2017.Mimi nilisoma katika kituo cha Elimu ya Watu Wazima huko Mufindi. Baadayenilijiunga na masomo kwa njia ya posta na kuhitimu kwa ufaulu wa masomo yaKiswahili, Siasa na Kiingereza.Nina umri wa miaka 45, nimeoa na nina watoto wanne. Mimi ni mwanakijiji wakijiji cha Magadini. Napendelea michezo na kazi za mikono. Ninaweza kusoma nakuandika vizuri na ninayo hati nzuri.Maeda, T.S0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tzUk 13

UTUNGAJI/UANDISHI - KISWAHILI 1 2017Mwalimu Mkuu wa Kituo cha Elimu ya Watu Wazima cha Mufindi na msimamiziwa masomo kwa njia ya posta anaweza kutoa taarifa zaidi juu ya uwezo w

aya, herufi kubwa na ndogo, n.k (f) . Hitimisho sio ufupisho wa hoja zilizojadiliwa katika sehemu ya insha yenyewe. . Nyerere wa Tanzania, kiongozi shujaa wa dunia – amepata kutukuka pande zote za dunia. Alizaliwa katika kijiji cha Butiama, Wilaya ya Musoma Vijijini mkoani

Related Documents:

Kiswahili) na Shahada ya Umahiri/Uzamili ya Sanaa katika Kiswahili (MA. Kiswahili – akitamilikia Fasihi) zote kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania. Chuoni anafundisha kozi za Kiswahili - Lugha, Isimu na Fasihi ikiwemo kozi ya Uandishi wa Kubuni. Pia, hufundisha Kiswahili

Kiswahili dialects are endangered by, among other factors, the onslaught of standard Kiswahili, English, and Sheng, and so they are likely to be dying. The paper holds the position that the Kiswahili dialects are vital for the development of standard Kiswahili and, therefore, their endangerment is the endangerment of standard Kiswahili.

Introduction to Kiswahili Poetry KSX 2102 Kiswahili Oral Literature KSX 2104 (with Mr Innocent Yerindabo) Introduction to Kiswahili Novels KSX 2202 History and Development of Kiswahili KSX 3101 Kiswahili Teaching Methods KSX 3201 Drafts Reviewed: Advanced Proficiency in Kiswahili KSX 1102 by Boaz Mutungi.

Song as an aspect of Kiswahili poetry. Origin and development of modern Kiswahili classics such as taarab. Leading founders of Kiswahili popular song in East Africa, history and development of Kiswahili solo, choral and orchestra composition. Themes, style and language use in popular Kiswahili songs.

4.0 KISWAHILI (102) 4.1 MATOKEO YA MTIHANI WA SOMO LA KISWAHILI Jedwali hili linaonyesha matokeo ya mtihani wa somo la Kiswahili katika muda wa miaka minne (2005 hadi 2008). Jedwali 6: Matokeo ya mtihani wa Kiswahili (2005 - 2008) Mwaka Karatasi Watahiniwa Alama ya Juu Alama ya Wastani Alama ya Tanganisho 2005 1 2 3 Jumla 259,301 40 80

Kwa mantiki ya nadharia hii, wataalamu hawa hukiona Kiswahili kuwa kilianza kama Pijini kwani ni tokeo la mwingiliano baina ya wenyeji wa pwani ya Afrika Mash

Huu ni mkusanyiko wa insha zinazohitaka katika mtaala wa elimu nchini Kenya hasa kwa wanafunzi wanojiandaa kwa mtihani wa kitaifa wa KCSE. Insha hizi zinafaa kutumiwa na mwalimu katika kuwaelekeza wanafunzi wanapofanya kazi yao ya kudurusu na wakati mwingine wanaposoma vipindi vya uandishi katika somo la Kiswahili. Martin Otundo (PhD fellow-

language that is spoken in the environment which they live, since the ability to distinguish the phonemes of one’s language environment is crucial to language acquisition. It is this ability which allows French children adopted by Japanese parents to speak the language of their environment (Jackendoff). Language Development 3 Exposure to language thus influences infants’ acquisition of .