Kuzaliwa Mara Ya Pili

3y ago
329 Views
14 Downloads
489.90 KB
208 Pages
Last View : 12d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Esmeralda Toy
Transcription

Kuzaliwa Mara ya Pili

Kuzaliwa Maraya Pili

Kuzaliwa Mara ya PiliEditorial PeregrinoApartado 1913350 Moral de Calatrava (Ciudad Real)UispaniaKuandaliwa mara ya kwanza katika lugha ya Kiingereza na Christian FocusPublications Ltd mwaka wa 2009 na kuitwa Finally Alive. Desiring God Foundation 2009.Kuandaliwa mara ya kwanza katika lugha ya Kiswahili na Editorial Peregrino, mwakawa 2011.Publication under the auspices of Christian Books Worldwide 2011 Editorial Peregrino kwa Kiswahili.Mtafsiri: Sukesh Pabari.Kuhakikishwa na Ronald Kogo na Paul MusembiJalada imetayarishwa na Samuel Cabera Fernandez.Mistari ya Biblia imenuukuliwa kutoka Holy Bible in Kiswahili, 2010. Imechapishwana Biblica – Africa, P.O. Box 60595 – 00200, Nairobi, Kenya.Kimechapishwa katika nchi ya Uispania.ISBN: 978-84-96562-75-2Depósito legal:Kimechapishwa katika nchi ya UispaniaPrinted in Spain

YaliyomoUtangulizi11Sehemu ya Kwanza: Je, inamaanisha nini kuzaliwamara ya pili?Sura ya Kwanza, Jambo la kuzaliwa mara ya pilini jambo muhimu sana29Sura ya Pili, Kuzaliwa mara ya pili kunamaanishakupewa maisha mapya kutoka kwa Mungu34Sura ya Tatu, Kuzaliwa mara ya pili kunamaanishahaitoshi kujua kwamba Yesu Kristo ni Bwana,bali kupata maisha ya kiroho kutoka kwake37Sura ya Nne, Kuzaliwa mara ya pili kunamaanishakuwa kiumbe kipya42Sehemu ya Pili, Je ni kwa nini tunahitaji kuzaliwamara ya pili?Sura ya Tano, Tunahitaji kuzaliwa mara ya pili kwasababu tumekufa katika mambo ya kiroho55Sura ya Sita, Tunahitaji kuzaliwa mara ya pili kwasababu sisi ni watumwa wa dhambi na shetani67Sura ya Saba, Tunahitaji kuzaliwa mara ya pili kwasababu tutapata faida nyingi73

YaliyomoSura ya Nane, Tunahitaji kuzaliwa mara ya piliili tuweze kufahamu ni kwa nini Kristo alikujahapa ulimwenguni79Sura ya Tisa, Uhusiano kati ya kuja kwake Kristo nakuzaliwa kwetu mara ya pili84Sehemu ya Tatu, Je, ni namna gani mtu anazaliwamara ya pili?Sura ya Kumi, Ni nini Mungu anafanya ili tuwezekuzaliwa mara ya pili93Sura ya Kumi na Moja, Kuzaliwa upya kwa viumbevyote105Sura ya Kumi na Mbili, Mungu anatuzaa maraya pili kwa kutuosha na kwa kutufanya watu wapya109Sura ya Kumi na Tatu, Mungu anatuzaa mara ya pilikupitia kwa imani116Sura ya Kumi na Nne, Tunazaliwa mara ya pilikupitia kwa mahubiri ya ujumbe wa Biblia125Sehemu ya Nne, Je, matokeo ya kuzaliwa mara ya pilini gani?Sura ya Kumi na Tano, Yule ambaye amezaliwa maraya pili ataushinda ulimwengu133Sura ya Kumi na Sita, Kuzaliwa mara ya pili, imanina upendo144Sura ya Kumi na Saba, Uhuru kutoka kwa tabia yadhambi155

YaliyomoSura ya Kumi na Nane, Kuwapenda wengine naupendo wa Mungu165Sehemu ya Tano, Je, ni namna gani tunawezakuwasaidia wengine ili wazaliwe mara ya pili?Sura ya Kumi na Tisa, Waambieni wote habari njemaya Yesu Kristo177Sura ya Ishirini, “Ninawatuma kufungua macho yao”187Sura ya Ishirini na Moja, Kuzaliwa Upya na nchi mpya198

“Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budikuzaliwa mara ya pili. Upepo huvuma po poteupendapo. Mvumo wake unausikia lakini huweziukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwakila mtu aliyezaliwa na Roho”.Yohana 3:7-8

UTANGULIZIYesu Kristo alisema, “Huna budi kuzaliwa mara ya pili”(Yohana 3:7). Hii inamaanisha kwamba jambo hili la kuzaliwamara ya pili ni jambo kuu sana, na kwa hivyo kila mmoja wetuanapaswa kulifahamu vizuri sana jambo hili. Katika kitabu chaYohana sura ya tatu, Yesu Kristo anafundisha kuhusu kuzaliwamara ya pili, na wakati tunasoma sura hii, tunaona kwamba sisiwanadamu ni wenye dhambi, na hatuwezi kufanya chochotekujiokoa: “Upepo huvuma po pote upendapo. Mvumo wakeunausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako.Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho” (Yohana 3:8).Yesu Kristo hapa anaongea kuhusu kazi ya Roho Mtakatifu, naanasema kwamba kazi ya kuokoa watu wa Mungu ni kazi yakeRoho Mtakatifu.Kuna watu wawili katika historia ya dunia ambao maisha yaoyanaonyesha wazi kabisa kwamba wokovu ni kazi ya MunguRoho Mtakatifu mwenyewe. Kwanza, tunasoma kumhusu mtummoja ambaye aliitwa Augastine ambaye aliokoka mwaka wa386, na pili tunasoma kumhusu mtu mwingine ambaye aliitwaC.S. Lewis ambaye aliokoka mwaka wa 1931. Wote wawiliwalikaa miaka mingi bila wokovu na walipiga vita dhidi ya Mungumiaka mingi kabla ya kuokoka. Lakini Mungu Roho Mtakatifualitumia njia tofauti kabisa kumwokoa kila mmoja wao.Hadithi ya AugustineAugustine alikuwa na dhambi moja ambayo alipenda sana, na hiiilikuwa dhambi ya uasherati. Kwa miaka 16, yeye alifuata dhambihii kwa moyo wake wote. Wakati alikuwa miaka 16 aliondokanyumbani mwake na kuanza kuishi maisha ya dhambi. Lakinimamake Monika alikuwa ameokoka, na yeye alivumiliakumwombea kijana wake. Wakati Augustine alikuwa miaka 32,alianza kuwaza juu ya wokovu. Aliandika, “Nilitafuta njia yaKuzaliwa Mara ya Pili 11

Utangulizikupata furaha katika Mungu, na niliona kwamba siwezi kupatafuraha katika Mungu bila kumwamini Yesu Kristo.”Siku moja, katika mwaka wa 386, Augustine alikuwa akitembelearafiki yake mmoja, Alypius. Hawa wawili walikuwa wakiongeakumhusu mtu mmoja ambaye alikuwa mtakatifu sana na aliitwaAntony. Augustine alijua kwamba yeye mwenyewe alikuwamtumishi wa dhambi na kwamba wale ambao walikuwawameokoka walikuwa huru katika Kristo. Augustine aliandika,“Nilikuwa katika bustani la nyumba moja wakati niliongea narafiki yangu. Nilijua kwamba mimi ni mwenye dhambi mkuumbele za Mungu na nilikuwa na wasiwasi sana moyoni mwangukwa sababu ya dhambi zangu. Nilijua kwamba katika moyowangu nilikuwa na vita, na kwa sababu ya vita hivi karibu niwewazimu! Nilijua kwamba Mungu ananiita niende kwake ili nipatemsamaha wa dhambi zangu, na nilitaka sana kwenda kwake. Hiindiyo sababu nilikuwa na vita moyoni mwangu.”Wakati Augustine alikuwa katika bustani hili alianza kuonakwamba maisha ya dhambi yatamharibu kabisa, na maisha yawokovu katika Kristo yatamletea faida kubwa sana. Kwa hivyoalikuwa na vita hivi ndani yake: kuendelea kufuata maisha yadhambi na kujiharibu au kufuata maisha matakatifu katika Kristona kupata furaha nyingi kwa kuokoka. Augustine aliandika,“Vita hivi viliendelea ndani yangu hadi nililia sana. Baada yamuda kidogo, nilisikia sauti ya mtoto mdogo ambaye alichezamchezo fulani karibu na lile bustani. Mtoto huyu alikuwaakiimba, ‘Chukua na usome, chukua na usome!’ Kwa hivyonilichukua Biblia ambayo ilikuwa karibu nami na nilianzakuisoma. Nilifungua Biblia na nilisoma maneno haya: ‘Basi natuenende kwa adabu kama inavyopasa wakati wa mchana, si kwakufanya karamu za ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, sikwa ugomvi na wivu. Bali jivikeni Bwana Yesu Kristo, walamsifikiri jinsi mtakavyotimiza tamaa za miili yenu yenye asili ya12 Kuzaliwa Mara ya Pili

Utangulizidhambi’ (Warumi 13:13-14). Wakati nilimaliza kusoma manenohaya, nuru ya Mungu iliingia moyoni mwangu na giza la dhambililiondoka.”Hapa tunasoma ni namna gani Augustine aliokoka. Baada ya sikuhiyo, yeye hakurudi kwa dhambi zake. Tunaona hapa ni namnagani Roho Mtakatifu alimwokoa. Roho Mtakatifu alitumia sautiya mtoto mdogo ambaye alicheza katika bustani fulani karibu naAugustine, na pia Roho Mtakatifu alitumia neno la Mungukuondoa giza kutoka moyoni wake na kuleta nuru ndani yake.Hadithi ya C.S. LewisMwaka wa 1925, Lewis alianza kufundisha lugha ya kiingerezakatika chuo kikuu katika nchi ya Uingereza. Wakati huo yeyealikuwa hajaokoka. Leo yeye anajulikana sana katika nchi yakekwa sababu yeye ameandika vitabu vingi sana.Siku moja katika mwezi wa Septemba mwaka wa 1931, Lewisalizungumza na rafiki wawili kuhusu dini ya Ukristo. Tunawezakuona kwamba Mungu Roho Mtakatifu alianza kazi yake ndani yaLewis siku hiyo.Kesho yake, Lewis aliokoka, lakini jambo hili lilikuwa tofautikabisa na lile la Augustine. Lewis alikuwa ndani ya gari akiendasafari fulani. Baada ya kuokoka aliandika hivi:“Nilikuwa safarini ndani ya gari wakati niliokoka. Wakati garililianza safari yake mimi sikuamini kwamba Yesu Kristo niMwana wa Mungu, lakini wakati gari lilimaliza safari yake baadaya masaa machache tu, mimi nilimwamini Kristo. Lakini wakatiwa safari hii sikuwa na mawazo kuhusu wokovu au sikuhisimambo mengi moyoni mwangu. Nilikuwa kama mtu ambayeanazinzia kitandani. Hivi ndivyo ilikuwa wakati mimi niliokonikiwa safarini siku hiyo.”Kuzaliwa Mara ya Pili 13

UtanguliziTunaona hapa kwamba hawa watu wawili waliokoka, lakini njiaambayo Mungu alitumia kuwaokoa ilikuwa tofauti kabisa.Augustine alikuwa na vita vikubwa sana ndani yake wakatialiokoka, lakini Lewis alikuwa tu safarini na Mungu alimwokoa.Wote wawili baada ya kuokoka waliweza kusema, “Sisi tunajua yakwamba tumepita kutoka kwa mautini kuingia uzimani” (1 Yohana3:14). Kitabu hiki kimeandikwa kufundisha kuzaliwa mara ya pilini nini.Kuchanganyikiwa kuhusu kuzaliwa mara ya piliKuna watu wengi leo ulimwenguni ambao hawafahamu vizurikuzaliwa mara ya pili kunamaanisha nini. Wakati tunaona mambohapa ulimwenguni, tunaona kwamba kuna wengi leo ambaowanadai wamezaliwa mara ya pili. Lakini wakati tunachunguzamaisha yao, tunaona kwamba hakuna tofauti kamwe kati yamaisha yao na maisha ya wale ambao hawajazaliwa mara ya pili.Wakati unachunguza maisha yao kwa nje, wanaonekana kwambakweli wao wamezaliwa mara ya pili na ni watu wa Mungu. Waowanasema wamezaliwa mara ya pili, na kila wiki wanaendakanisani. Pia wao wanadai wanamhudumia Mungu katikamakanisa yao: wengine ni waimbaji, na wengine wanahubiri nenola Mungu. Wote wanadai kwamba wanaishi maisha matakatifu yakumpendeza Mungu.Lakini wakati tunachunguza maisha yao kwa makini sana, tunaonakwamba ukristo wao ni wa nje tu, ni ukristo wa kuwaonyeshawengine tu, si ukristo wa ukweli. Mioyoni mwao, wao wanapendapesa na vitu vya dunia na anasa za dunia kama tu wale ambaohawajazaliwa mara ya pili. Wengi wao wanafanya kazi ya kanisasi kwa sababu wanapenda Mungu, bali wanawaza kwambawatapata faida ya pesa na vitu vya dunia. Pia, wakatitunachunguza maisha yao ya siri, tunaona kwamba wao ni wenyedhambi kama tu wale ambao hawadai kwamba wamezaliwa maraya pili. Kwa nje, wanaonyesha kwamba wao ni watu wa Mungu14 Kuzaliwa Mara ya Pili

Utangulizina watu watakatifu, lakini mbele za rafiki wao wa karibu sana waowanaishi maisha ya dhambi na wanapenda dhambi kama tu watuwa dunia.Makosa makuuSasa, kuna jambo moja kuu sana ambalo sisi sote tunapaswakufahamu vizuri sana. Tunapaswa kufahamu kwamba, fahamu yawatu wengi kuhusu kuzaliwa mara ya pili ni fahamu ya uongo.Tunapaswa kufahamu kwamba watu wengi sana wanafanyamakosa makuu wakati wanawaza juu ya kuzaliwa mara ya pili.Wengi wanawaza kwamba wao wanajua kuzaliwa mara ya pili ninini na ni namna gani mtu anazaliwa mara ya pili, lakini kwaukweli wamechanganyikiwa kabisa. Fahamu yao kuhusukuzaliwa mara ya pili ni tofauti kabisa na yale Biblia inafundishakuhusu jambo hili.Leo, mtu akisema, “Nimezaliwa mara ya pili,” watu wengi wadunia wanamwamini. Wao watasema, “Huyu amesema kwambayeye amezaliwa mara ya pili na ameokoka, basi, hii ni kweli. Yeyekweli amezaliwa mara ya pili, yeye kweli ameokoka.” Halafubaada ya muda wanaona kwamba mtu huyu anaishi maisha yakekama tu watu wa dunia wanaishi maisha yao. Wanaona kwambahuyu mtu anafanya mambo mabaya mabaya na anapenda sanadunia. Wakati watu wa dunia wanaona hii, wanasema, “Kwelihata wale ambao wamezaliwa mara ya pili wanaishi maisha yaokama tu watu wa dunia!” Kwa kusema hivi wao wanamaanishakwamba mtu anaweza kuwa amezaliwa mara ya pili lakini maishayake yawe hayana mabadiliko hata kidogo. Watasema, “Yeyeanaishi maisha yake tu kama watu wa dunia, ingawa amezaliwamara ya pili. Kwa hivyo kuzaliwa mara ya pili na kuokokahaimaanishi kwamba mtu atakuwa tofauti na wengine. Hata waleambao wamezaliwa mara ya pili na kuokoka wanaishi tu maishaya dhambi.”Kuzaliwa Mara ya Pili 15

UtanguliziHivyo ndivyo watu wa ulimwengu wanawaza wakati wanaonakwamba yule ambaye anadai amezaliwa mara ya pili anaishimaisha ya dhambi. Lakini haya ni makosa makubwa.Mafundisho ya Agano Jipya.Wakati tunasoma Agano Jipya, tunapata mafundisho ambayo nitofauti kabisa na yale ambayo wengi leo wanafundishwa. Leowengi wanafundishwa kwamba mtu akisema kwamba yeyeamezaliwa mara ya pili na kuokoka, wote watamwamini nakusema, “Kweli amezaliwa mara ya pili.” Halafu wakati mtuambaye anadai amezaliwa mara ya pili anaishi maisha ya dhambi,wengi wanasema kwamba hakuna tofauti yoyote kati ya waleambao wameokoka, na watu wa dunia. Wengi leo wanafundishwahaya. Lakini wakati tunasoma Agano Jipya tunapata mafundishoambayo ni tofauti kabisa na haya.Agano Jipya linasema kwamba kuzaliwa mara ya pili si kazi yamwanadamu, bali ni kazi ya Mungu mwenyewe. Pia, Agano Jipyalinasema kwamba ikiwa mtu anadai amezaliwa mara ya pili, lakinianaishi maisha ya dhambi kila siku, basi yeye hajazaliwa mara yapili. Agano Jipya linafundisha kwamba mtu huyu amejidanganya,au yeye anajua kwamba yeye hajazaliwa mara ya pili lakinianataka kuwadanganya wengine ili apate faida fulani, na kwahivyo anaonyesha kwamba yeye amezaliwa mara ya pili. AganoJipya linatufundisha kwamba ikiwa mtu amezaliwa mara ya pili,basi maisha yake yatabadilika kabisa na yeye ataanza kuishimaisha matakatifu, na ikiwa maisha yake hayajabadilika, basi yeyehajazaliwa mara ya pili, hata kama anasema kwa mdomo wakekwamba amezaliwa mara ya pili.Kwa mfano, wakati tunasoma waraka wa 1 Yohana, tunasomamambo haya wazi kabisa.16 Kuzaliwa Mara ya Pili

Utangulizi·····“Kama mkijua kuwa Yeye ni mwenye haki, mwajuakwamba kila atendaye haki amezaliwa na Yeye” (1 Yohana2:29).“Ye yote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababuuzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutendadhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu” (1 Yohana 3:9).“Wapenzi na tupendane, kwa kuwa upendo watoka kwaMungu. Kila apendaye amezaliwa na Mungu naye anamjuaMungu” (1 Yohana 4:7).“Kwa maana kila aliyezaliwa na Mungu huushindaulimwengu.Huku ndiko kuushinda kuushindakoulimwengu, yaani, hiyo imani yetu” (1 Yohana 5:4).“Tunajua ya kuwa yeye aliyezaliwa na Mungu hatendidhambi, bali aliyezaliwa na Mungu hujilinda wala yulemwovu hawezi kumdhuru” (1 Yohana 5:18).Katika kitabu hiki tutajifunza mistari mingi kama hii ili tuone ninini Biblia inafundisha kuhusu kuzaliwa mara ya pili. Tunajuakwamba hakuna yeyote ambaye amekamilika na kwamba hakunayeyote ambaye hatendi dhambi. Hii tunajua. Lakini pia tunajuakwamba ikiwa mtu anadai amezaliwa mara ya pili, lazima aanzekuacha dhambi zake na kufuata njia ya utakatifu. Mistari kama ikiwa kuhusu wokovu. Wengi wanadai kwambawamezaliwa mara ya pili, lakini kwa ukweli hawajazaliwa mara yapili. Wengi wanaonekana kwamba wamezaliwa mara ya pili,lakini kwa ukweli wanawadanganya wengine, na hawajazaliwamara ya pili kamwe. Mungu anajua mambo haya yote, na hiindiyo sababu waraka wa 1 Yohana uliandikwa.Bibliainatufundisha kwamba wengi ambao hawajazaliwa mara ya piliwameingia kanisani na wameleta kuchanganyikiwa kwingi.Kuzaliwa Mara ya Pili 17

UtanguliziNi kwa nini nimeandika kitabu hiki.Kitabu hiki kinahusu kuzaliwa mara ya pili. Nina sababu tatu nikwa nini nimeandika kuhusu kuzaliwa mara ya pili katika kitabuhiki.1. Kwanza, nimeandika kuhusu kuzaliwa mara ya pili kwa sababukuna kuchanganyikiwa kwingi duniani leo kuhusu jambo hili lakuzaliwa mara ya pili. Je, ni nini Biblia inatufundisha kuhusukuzaliwa mara ya pili? Wengi katika dunia leo wamesikia kuhusukuzaliwa mara ya pili lakini hawajui hata kidogo jambo hililinamaanisha nini. Pia, kuna wengi ambao wanadai kwamba waowenyewe wamezaliwa mara ya pili, lakini hata hawa hawajuijambo hili linamaanisha nini.Katika Biblia, jambo hili la kuzaliwa mara ya pili ni jambo kuusana. Kwa hivyo ni lazima sana tufahamu jambo hili la kuzaliwamara ya pili linamaanisha nini. Ni lazima tufahamu jambo hili ilituweze kujua kama kweli sisi tumezaliwa mara ya pili, na pia sisituweze kuwasaidia wengine kuzaliwa mara ya pili.2. Pili, nimeandika kitabu hiki kuhusu kuzaliwa mara ya pili kwasababu ninataka wale ambao wamezaliwa mara ya pili wafahamuni nini Mungu amefanya ndani yao. Vile tumeona, kuna wengiambao wamezaliwa mara ya pili lakini hawafahamu hiiinamaanisha nini. Mungu Roho Mtakatifu amefanya kazi kuusana ndani yao, lakini wao hawaelewi ni nini Mungu amefanya.Kuzaliwa mara ya pili ni jambo kuu sana, na sisi hatuwezi kuelewakila kitu kuhusu kuzaliwa mara ya pili kwa sababu hii ni kazikubwa sana ya Mungu. Lakini Biblia inatufundisha mengi kuhusukuzaliwa mara ya pili na wengi ambao wamezaliwa mara ya pilihawajui ni nini Biblia inafundisha. Hata baada ya kufahamumengi katika Biblia kuhusu kuzaliwa mara ya pili tunawezakusema tu, “Tunaona taswira kama ya kwenye kioo” (1Wakorintho 13:12). Kwa hivyo ni maombi yangu kwamba baada18 Kuzaliwa Mara ya Pili

Utanguliziya kusoma kitabu hiki wewe utafahamu mengi kuhusu kuzaliwamara ya pili.Kuna sababu tatu ni kwa nini ninataka wale ambao wamezaliwamara ya pili wafahamu ni nini imefanyika ndani yao.(i)Kwanza, ninataka ufahamu ni nini imefanyika ndani mwakokwa sababu wakati unazaliwa mara ya pili na unapoendeleakukua katika imani yako, utakuwa na uhusiano na Munguambao ni mtamu sana, na utakuwa na hakika kwamba kweliMungu anakupenda na amekuokoa.(ii)Pili, ikiwa utafahamu vizuri inamaanisha nini kuzaliwamara ya pili, utaona utukufu wa Mungu na wa Yesu Kristona wa Roho Mtakatifu na wa neno la Mungu. Utapendazaidi sana Mungu na neno lake ukifahamu vizuri ni niniMungu alifanya wakati wewe ulizaliwa mara ya pili.(iii)Tatu, ikiwa utafahamu ni nini Mungu alifanya ndani mwakowakati wewe ulizaliwa mara ya pili, utaona kwamba hiiilikuwa kazi kuu sana ya Mungu. Wengi leo ambaowamezaliwa mara ya pili hawaelewi kwamba Munguamefanya kazi kuu sana na kwa hivyo hawa hawaishimaisha ya kufuata utakatifu. Lakini wakati utafahamukwamba Mungu amefanya kazi kuu sana ndani mwakowakati wewe ulizaliwa mara ya pili, basi utaanza kufuatautakatifu kwa moyo wako wote kwa sababu utafahamuvizuri kazi ya Mungu. Ni maombi yangu kwamba wakristowote wataishi yale maisha ambayo yanamtukuza Mungu iliwatu wa dunia wafahamu vizuri maisha ya ukristo ni ya ainagani.3. Tatu, nimeandika kitabu hiki kwa sababu kuna mamilioni yawatu hapa ulimwenguni ambao hawajaokoka. Wao hawajazaliwaKuzaliwa Mara ya Pili 19

Utangulizimara ya pili na kwa hivyo hawamfuati Bwana wetu Yesu Kristo nakumhudumia. Ni maombi yangu kwamba Mungu atatumia kitabuhiki kuwaonyesha watu hawa njia ya kuokoka, na kwamba Yeyeatawaokoa. Kuna wengi ambao wanahudhuria kanisa kila wikilakini hawajaokoka, na pia kuna wale ambao ni viongozi wamakanisa ambao hawajaokoka. Wao wanawaza kwambawameokoka kwa sababu walizaliwa katika jamii za ukristo nawamehudhuria kanisa tangu utotoni mwao, lakini haya yotehayamaanishi kwamba wameokoka. Ukristo wao ni wa nje tu, niwa kuwaonyesha wengine tu kwamba wao ni watu wa Mungu,lakini kwa ukweli hawa hawajaokoka.Ninataka kuwahudumia watu hawa kwa kuwaeleza ni niniinapaswa kufanywa ndani mwaao ili waokoke. Ninaombakwamba Mungu Roho Mtakatifu atatumia neno la Mungukuwaokoa wakati watasoma kitabu hiki. Kuzaliwa mara ya pili sikazi ya mwanadamu. Hakuna yeyote ambaye anaweza kuzaliwamara ya pili kwa uwezo wake. Hakuna mhubiri yeyote ambayeanaweza kumwezesha mwingine azaliwe mara ya pili. Hii ni kaziya Mungu pekee, ni Yeye anafanya kazi ndani yetu ili tuzaliwemara ya pili.Kila wakati Mungu anafanya kazi yake ili mtu fulani azaliwe maraya pili, anatumia neno lake. Petro anasema, “Kwa maanammezaliwa upya, si kwa mbegu ile iharibikayo, bali kwa ileisiyoharibika, kwa neno la Mungu lililo hai.Hili nenolililohubiriwa kwenu” (1 Petro 1:23-25). Kwa hivyo Biblia hapainatufundisha kwamba ni Mungu mwenyewe anafanya kazi ndaniya mtu ili mtu huyu azaliwe mara ya pili, na kwamba wakatiMungu anafanya kazi hii, anatumia neno lake, yaani injili ambayosisi tunahubiri. Kwa hivyo ni maombi yangu kwamba Munguatatumia mafundisho ya kitabu hiki kuwaokoka wale ambaohawajaokoka. Ninataka kufundisha wazi kabisa kuzaliwa mara yapili inamaanisha nini, ili wote waelewe.20 Kuzaliwa Mara ya Pili

UtanguliziMpangilio wa kitabu hiki.Kitabu hiki kina sehemu tano, na katika kila sehemu nitauliza nakujibu swa

kwamba maisha ya dhambi yatamharibu kabisa, na maisha ya wokovu katika Kristo yatamletea faida kubwa sana. Kwa hivyo alikuwa na vita hivi ndani yake: kuendelea kufuata maisha ya dhambi na kujiharibu au kufuata maisha matakatifu katika Kristo na kupata furaha nyingi kwa kuokoka. Augustine aliandika, “Vita hivi viliendelea ndani yangu hadi .

Related Documents:

MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO-SOMO LA KWANZA 7 Uamuzi wa muhimu Sana katika maisha yako, ni kumkubali Yesu Kristo awe bwana na mwokozi wa maisha yako. Yohana 3:3 inasema, mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuona ufalme wa mbinguni. Ulipomuamini Yesu awe mwokozi wako, ulizaliwa mara ya pili.Kuzaliwa kwako upya kwa roho wa Mungu, .

3. Enciende la l mpara. 4. Coloca la c mara oscura frente a la l mpara. 5. Observa a trav s de la bolsa blanca y t pate con la casaca. 6. Otro compa ero antepondr la ßecha apuntando hacia abajo , entre la l mpara y la c mara oscura. 7. Luego , otro compa ero preguntar , al observador de la c mara oscura, lo siguiente: ÀHacia

Kata kunci: Asbab al-Nuzul, Tafsir Mara h Labi d, Kualitas. Tafsir Mara h Labi d merupakan salah satu kitab tafsir karya ulama Nusantara yakni Syekh Muhammad Nawawi al-Bantani. Dalam upaya menafsirkan ayat al-Qur‟an bila terdapat riwayat asbab al-nuzul Syekh Nawawi al-Bantani hampir selalu mencantumkan riwayat asbab al-nuzul.

Grandma OTHER)Mara's RAMBLINGS MARA NORTHEAST NEWSLETTER JANUARY 2013 - PAGE 2 TECH STUFF (AND by VE1VQ I want you to know that Walter did himself proud, re-FIBERGLASS POLE ANTENNA - PART 3 garding my Christmas present! It was actually several

Birds of Kenya's Masai Mara Naturetrek Itinerary Naturetrek Mingledown Barn Wolf's Lane Chawton Alton Hampshire GU34 3HJ UK T: 44 (0)1962 733051 E: info@naturetrek.co.uk W: www.naturetrek.co.uk Outline itinerary Day 1 Fly Nairobi & overnight Day 2/3 Lake Naivasha Day 4/8 Masai Mara Day 9 Depart Nairobi Day 8 Arrive London. Departs

The Serengeti-Mara ecosystem climate is tropical with distinct wet and dry seasons. There is a rainfall gradient south to north and west to east. The northern and western parts receive more rainfall than the southern and eastern parts. The Serengeti-Mara ecosystem climate is tropical and usually warm and dry; with mean monthly

FASIHI Julai / Agosti 2018 Muda: Saa 2½ MTIHANI AW MWISHO AW MUHULA AW PILI Kidato cha Nne KISAW HILI Karatasi - 102/3 Julai / Agosti 2018 Muda : Saa 2½ MAAGIZO 1. Jibu maswali MANNE pekee. 2. Swali la KWANZA ni la LAZIMA. 3. Kisha chagua maswali mengine matatu kutoka sehemu zilizobakia; yaani Riwaya, Hadithi Fupi, na Ushairi 4.

lic perceptions of the criminal courts by focusing on a few basic topics. We begin by discussing where the courts fit in the criminal justice system and how the public perceives the courts. Next, attention shifts to the three activities that set the stage for the rest of the book: Finding the courthouse Identifying the actors Following the steps of the process As we will see .