Kuchambua Maudhui Yanayopatikana Katika Hadithi Za Watoto Katika Jamii .

1y ago
13 Views
3 Downloads
588.07 KB
107 Pages
Last View : 17d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Harley Spears
Transcription

KUCHAMBUA MAUDHUI YANAYOPATIKANA KATIKA HADITHI ZAWATOTO KATIKA JAMII YA WAPEMBAMWANAIKA MADI MZEETASNIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SEHEMU YA LAPEKEE LA KUTUNUKIWA DIGRII YA UZAMILI (M.A. KISWAHILI) YACHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA2015

iiUTHIBITISHOAlietajwa hapo chini anathibitisha kuwa amesoma tasnifu hii iitwayo KuchambuwaMaudhui ya Hadithi za Watoto Katika Jamii ya Wapemba. Na nimependekezaikubaliwe na chuo kikuu huria cha Tanzania kwa ajili ya kutimiza sehemu ya sharti lakutunukiwa Digirii ya M.A ya Kiswahili ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.Sheikh, Professa, Daktari, T. S. Y. Sengo(Msimamizi)Tarehe

iiiHAKI MILIKIHairuhusiwi kuigwa au kunakili kwa namna yoyote ile ya tasnifu hii kwa ajili yoyotekama vile kieletroniki, kurudufu nakala, kurikodi au njia yoyote nyingine bila ya idhiniya mwandishi au Chuo Kikuu Huria kwa niaba.

ivTAMKOMimi, Mwanaika Madi Mzee nathibitisha kuwa hiini kazi yangu mwenyewe nahaijawahi kuwasilishwa katika Chuo Kikuu chengine chochote kwa ajili ya kutunukiwashahada hii au nyengine yoyote.SainiTarehe

vTABARUKUTasnifu hii naitabarukia mama yangu mpendwa Asha Maalim Hassan pamoja na babayangu mpenzi Madi Mzee Omar kwa kunilea na kunipeleka shule. Mwenyeezi Munguawabariki na kuwapa kila la kheri.

viSHUKURANIKwanza namshukuru Allah (s.w.) kwa kunijaalia siha njema na kuniwezesha kufikakiwango hiki cha elimu. Namshukuru Mungu kunijaalia misaada ya kitaaluma kutokakwa wataalamu ambao sitoweza kuwataja wote.Nawashukuru wahadhiri wote wa Kiswahili wa OUT na SUZA kwa ushauri waowalionipa wakati wote nilipokuwa nikiandika tasnifu hii, waliniwezesha kuimarikakitaalimu, Mungu awabariki. Siwezi kuwasahau wahadhiri wetu wote walioshirikikatika kozi hii kama Professa Tigiti Sengo, Professa Emmanuel Mbogo, Professa JamesMdee, muhadhiri Mohd Omary na wale wote waaliotusaidia katika kukamilisha kozihii.Shukurani za pekee zimwendee mshauri wa M.A.Kiswahili, tawi la Pemba MaalimuBakari Kombo ambaye katowa mchango mkubwa tokea kuanza hadi kukamilika kwakozi hii. Mungu amlipe kila la kheri kwawema huu usiopimika wala kulipika. Pianamshukuru mume wangu Ali Rajab Alikwakunivumilia hadi nikaikamilisha kuiandikatasnifu hii.

viiIKISIRIKazi hii ilihusika na hadithi za Paukwa . Pakawa. Imechunguza maudhuiyanazopatikana katika hadithi za watoto katika jimbo la Mkanyageni Mkoa wa kusiniPemba. Ili kufikia lengokuu lililokusudiwa mbinu mbalimbali za utafiti zilihusika.Mbinu hizo ni za mahojiano pamoja na uchunguzi wa kimaktaba. Nadharia tatu zautafiti zilitumika. Nadhariza hizo ni mwitiko wa msomaji, nadharia ya simiotiki nanadharia ya sosholojia (kijamii).Kwa upande wa matokeo ya utafiti, mtafitiamegunduwa dhamira kadha wa kadha zilizoibuka kutokana na utafiti na uchambuzialioufanya. Dhamira hizo ni ugumu wa upatikanaji wa elimu, umoja na mshikamanomiongoni mwa wanajamii. mapenzi na ndoa, kuonya,nafasi ya mwanamke, ukarimu,uzembe na uvunjaji wa kanuni pamoja na utawala bora. Kifani, mtafiti amegunduakwamba, baadhi ya vipengele vya fani vilivyosaidia kuibua dhamira katika hadithi zawatoto za Kipemba ni kipengele kinachohusu wahusika, matumizi ya lugha, muundo,mtindo na mandhari.Ujumbe uliojitokeza katika hadithi za watoto ni pamoja na wazeekuwaasa watoto juu ya kufuata ushauri wa wazazi wao kwa kila wanalotaka kulifanya,kujitenga na mambo mbalimbali ambayo yanaweza kukuletea vikwazo au matatizo,wanataalimu wawe wavumilivu, wasiwe na ufedhuli na lugha chafu kwa wanafunziwao. Ujumbe mwengine uliopatikana ni kuwa na juhudi ya kazi na kuwacha kujigambapasipo sababu, kutokuwa na imani na kila mtu,kuepuka ubinafsi na ujanja katika kazi,kutii kanuni na utii wa wake na waume zao na kuepuka ushawishi wa mashoga na watuwengine.

viiiYALIYOMOUTHIBITISHO . iiHAKI MILIKI . iiiTAMKO . ivTABARUKU . vSHUKURANI . viIKISIRI . viiYALIYOMO . viiiVIFUPISHO . . .xivSURA YA KWANZA. 11.0UTANGULIZI WA JUMLA . 11.1Kitangulizi cha Kisiwa cha Pemba. 11.2Utangulizi wa Sura . 21.3Usuli wa Tatizo la Utafiti. 21.4Tamko la Tatizo la Utafiti . 61.5Madhumuni ya Utafiti . 71.5.1 Madhumuni Mahususi . 81.5.2 Maswali ya Utafiti . 81.6Umuhimu wa Utafiti . 81.7Mipaka ya Utafiti. 91.8Vikwazo vya Utafiti . 91.8.1 Utatuzi wa Vikwazo vya Utafiti . 101.9Hitimisho . 10SURA YA PILI . 102.0UTALII WA KAZI TANGULIZI NA MKABALA WA KINADHARIA . 102.1Utangulizi wa Sura . 10

ix2.2Dhana Mbalimbali Zihusuzo Mada . 112.2.1 Hadithi au Simulizi . 112.2.2 Fasili ya Ngano . 132.2.3 Dhana ya Fasihi ya Watoto. . 132.2.4 Aina za Hadithi . 162.2.5 Ngano . 172.2.6 Tarihi . 172.2.7 Visasili . 182.2.8 Vigano. 182.2.9 Soga . 182.3Dhana ya Dhamira . 192.4Uchambuzi wa Vipengele vya Fani. 202.4.1 Wahusika . 202.4.2 Mazingira . 202.4.3 Lugha . 212.5Baadhi ya Vipengele vya Maudhui . 212.5.1 Ujumbeni . 212.6Utalii wa Kazi Tangulizi . 212.7Mwega wa Nadharia . 272.7.1 Maana ya Nadharia . 272.7.2 Sababu za Kuchaguwa Nadharia Hizo . 272.7.3 Nadharia ya Kijamii . 272.7.4 Nadharia ya Simiotoki . 282.7.5 Nadharia ya Mwitiko wa Msomaji . 282.8Hitimishoa . 29SURA YA TATU. 30

x3.0MBINU ZA UTAFITI . 303.1Utangulizi wa Sura . 303.2Maana ya Mahojiano . 303.2.1 Sababu za Kuchagua Mbinu ya Mahojiano . 303.2.2 Faida za Mahojiano . 303.2.3 Hasara za Njia ya Mahojiano . 313.2.4 Uteuzi wa Watafitiwa . 313.2.5 Jedweli la Watafitiwa . 313.3Muundo waUtafiti . 323.4Hitimisho . 32SURA YA NNE . 334.0 UCHAMBUZI NA UCHANGANUZI WA DATA . 334.1Utangulizi wa Sura . 334.2Uchambuzi wa Data . 334.3Dhamira Zilizopatikana Katika Hadithi Zilizokusanywa Katika Jamii yaWapemba. . 334.3.1 Dhamira ya Ukaidi . 334.3.2 Dhamira ya Ujasiri . 344.3.3 Dhamira ya Malezi . 354.3.4 Dhamira ya Ushujaa . 354.3.5 Dhamira ya Uongozi Mbaya . 364.3.6 Dhamira ya Kusaidiana. 364.3.7 Dhamira ya Uchoyo . 374.3.8 Dhamira ya Kiburi . 374.3.9 Dhamira ya Kufanya Kazi . 384.3.10 Dhamira ya Subira . 39

xi4.3.11 Dhamira ya Makaazi. 394.3.12 Dhamira ya Ubinafsi. 404.3.13 Dhamira ya Urafiki . 414.3.14 Dhamira ya Uchoyo . 414.3.15 Dhamira ya Ujanja . 424.3.16 Dhamira ya Wizi naUbadhirifu wa Mali. . 434.3.17 Nafasi ya Mwanamke . 434.3.18 Dhamira ya Uzembe . 444.3.19 Dhamira ya Uvunjaji waSheria . 454.3.20 Dhamira ya Unyonyaji. 464.3.21 Dhamira ya Utawala Bora. 464.3.22 Dhamira ya Umoja na Mshikamano . 474.3.23 Dhamira ya Mapenzi na Ndoa. 474.3.24 Dhamira ya Uhalifu . 484.4Ujumbe Uliopatikana Katika Hadithi Zilizokusanywa Katika Jamii yaWapemba . 494.5Vipengele vya Fani Vilivyosaidia Kuibuwa Dhamira Katika Hadithi zaWatoto Katika Jamii ya Wapemba . . .524.5.1 Wahusika . 534.5.1.1 Mhusika Pate. . 534.5.1.2 Mhusika Mize . 534.5.1.3 Mhusika Mwengine ni Zimwi . 534.6Katika Hadithi ya 2ya Chura na Jingoo Kuna Wahusika Wafuatao . 544.6.1 Chura . 544.6.2 Jongoo . 544.7Katika Hadithi ya 3 ya Makame wa Makame Kuna Wahusika Wafuatao . 55

xii4.7.1 Makame wa Makame. 554.8Katika Hadithi ya 4 ya Paka na Panya Kuna Wahusika Wafuatao . 554.8.1 Panya . 554.8.2 Paka . 554.9Hadithi ya 5 ya Sungura ina Wahusika Wafuatao. 564.9.1 Nfaki . 564.9.2 Sungura . 564.10Katika Hadithi ya 6 ya Fisi na Simba Tumewaona Wahusika HawaWafuatao . 574.10.1 Simba . 574.10.2 Fisi . 574.11Katika Hadithi ya 7 ya Kungu Mauwa kuna Wahusika Wafuatao . 574.11.1 Mwau . 574.11.2 Lau . 584.12Hadithi ya 15 ya Muhamedi ina Wahusika Hawa: . 584.12.1 Muhamedi . 584.13Katika Hadithi ya 9 ya Yamuimui inaWahusika Hawa Wafuatao: . 594.13.1 Yamuimui . 594.13Hadithi ya 12 ya Babu Dii Imetupatia Wahusika Hawa Wafuatao: . 594.13.1 Babu Dii. . 594.13.2 Mke wa Babu Dii. . 594.13.1 Bibi Kizee. . 604.14Katika Hadithi ya 13 ya Kijoka Kuna Wahusika Hawa . 604.14.1 Mama Yake Kijoka. 604.15Hadithi ya 14 ya mtu na ndugu yake wahusika Waliomo ni . 614.15.1 Binadamu . 61

xiii4.15.2 Simba . 614.16Hadithi ya 10 ya Bunuasi na Wafuatao . 614.16.1 Bunuwasi . 614.7Matumizi ya Lugha Katika Hadithi Teule za Wapemba. . 624.7.1 Tamathali za Usemi . 634.7.4 Takriri . 644.7.5 Tanakali Sauti. 644.7.6 Taswira . 644.7.7 Methali . 654.8Mandhari . 65SURA YA TANO . . . . . 675.0HITIMISHI, MUHTASARI NA MAPENDEKEZO . 675.1Utangulizi wa Sura . 675.2Hitimishi . 675.3Muhutasari wa Utafiti . 685.3.1 Matokeo ya Utafiti. 685.4Mapendekezo . 69MAREJELEO . . . 70

xivVIFUPISHOOUT:The Open University of TanzaniaSUZA:The University of ZanzibarTUKI:Taasisi ya Ukuzzaji KiswahiliTALILUKI:Taasisi ya Kiwahili na Ligha za KigeniS.W:Subhanna WataalaM.A.:Master of Kiswahili

1SURA YA KWANZA1.0 UTANGULIZI WA JUMLA1.1Kitangulizi cha Kisiwa cha PembaKisiwa cha Pembakina mapisi marefu.Kwa upande wa jina la kisiwa inasemekana kuwalinatokana na neno la Kiswahili “kupemba”kwa maana ya kuongoza chombo kwaumakini. Fasili hii inatokana na hali ya kisiwa cha Pemba kuzungukwa na mkondomkubwa na wenye hatari.Pemba ikiitwa Al-jaziratul hadhara “kwa maana ya kisiwa chakijani kutokana na rutuba ya ardhi yake na kukifanya kisiwa kuwa bustani nzuri (Krain1998).Maulid (2011) anadai kwamba “Msumbiji kuna Pemba,hivyo Wapemba waliletwa kwawingi kisiwani Pemba na hao hasa ndio walioleta jina hilo na herufi “n”katika Kiswahilichakisiwani Pemba, badala ya “m,” kwa mfano neno “nkate”badala “mkate”.Sengo(1985), anasema kwamba Pemba ni kizushi cha volkano, kilizushwa kutoka chini yabahari.Kijiografia:katika mwelekeo wa kaskazini na kusini mwa dunia kisiwa cha Pembakipo upande wa kusini mwa mstari wa ikweta.Na mwelekeo wa magharibi na masharikikimepakana baina ya kilomita 30-50 nje ya ufukwe wa Tanganyika katika mwambao waAfrika ya mashriki.Kisiwa cha Pemba kina eneo la ukubwa wa kilomita 863 za mraba.(Omar 2011).Kwa hiyo, mtafiti anaona, kutokana na udogo wa kisiwa cha Pemba, hapo kale jamii yaWapemba iliweza kushirikiana katika suala la malezi ya watoto wao, na malezi hayoyaliweza kufikishwa kwa watoto kwa njia mbalimbali, ikiwemo kuwakusanya watoto nakuwasimuliya hadithi za paukwa pakawa. Dhamira zilizokuwemo katika hadithihizo,ziliwafunza watoto mambo mengi, ikiwa ni pamoja na jinsi ya kuishi katika jamii

2zao, kuwatii wazee wote na kujifunza amali za jamii zao, ili waweze kufuata mila nadesturi za jamii zao.1.2Utangulizi wa SuraKatika kipengele hiki tunazungumzia kitangulizi cha kisiwa cha Pemba,tatizo la utafiti,usuliwa tatizo la utafiti, madhumuni ya utafiti na maswali ya utafiti. Pia mtafitiameelezea umuhimu wa utafiti, eneo la utafiti, mipaka ya utafiti, vikwazo vya utafiti,tamko la tatizo la utafiti, sababu za kuchaguwa mada na utatuzi wa vikwazo vya utafiti.1.3Usuli wa Tatizo la UtafitiKatika utafiti huu,mtafiti amekusudia kuainisha maudhi katika vipegele vya dhamiranaujumbe wa hadithi za watoto katika jamii ya wapemba. Masimulizi ya hadithi za watotoni moja miongoni mwa vijipera vya fasihi simulizi. Kuhusiana na mada ya fasihisimulizi,Mulokozi (1996) anaeleza kuwa fasihi simulizi imekuwa na umuhimu mkubwakatika jamii,ikiwemo haja ya kuelimisha jamii juu ya masuala yanayofaa kufuatwa nayale yasiyofaa kufuatwa, ili jamii iweze kuwa katika mwenendo bora wa kimaisha. Kwakuwa hadithi za watoto ni kijitanzu kidogo cha fasihi simulizi, mtafiti ameona ipo haja yakuidokeza dhana ya fasihi simulizi, ingawa kwa ufupi.wataalamu waliotowa maonikuhusu maana ya fasihi simulizi miongoni mwao ni Finnegan(1970), Metteru (1989),Balisidya (1983), Sengo (1985), naOkpwho (1992).Matteru (1989), anasema kwamba fasihi simulizini fasihi inayotegemea mdomo, njiamojawapo ya kutolea na kuenezea elimu. Balisidya (1983), fasihi simulizi ni elimu yakifasihi ambayo hutumia mdomo au njia nyengine katika kuwasilisha na kusambazaelimu kwa wasikilizaji na watumiaji wake. Kama anavyoainisha Okopwho (1992), fasihisimulizi ni elimu itolewayo kwa neno la mdomo. Mawazo hayo yote yanawezakuhitimishwakwa kauli ya Mulokozi(1996), fasihi simulizi ni maneno ya sanaa tendezi,

3ambayo huwasilishwa kwa njia ya mdomo na kuhifadhiwa kwa maandishi, flash, CD,sahani za santuri, kanda za kurikodi na njia nyengine za kuhifadhi elimu hiyo.Mulokozi, ameainisha tanzu za fasihi simulizi katika makundi sita, ambayo nimazungumzo, ushairi, semi maigizo na masimulizi (1989). Hadithi kama moja ya kitanzucha tutumbi au nathari, kinaelezwa kwa uainishaji wake kwa kuwa ni cha muda mrefu,Kwa mujibu wa Okpewho (1982), kuna vigezo au njia nne, na katika hizo ndizo mpakasasa zimetumika kuainisha hadithi. Kwavile mtafiti data zake alizipata moja kwa mojakutoka kwa watafitiwa wake, aliona ni bora kuvianisha vigezo hivyo kama vifuatavyo:Kigezo cha kwanza ni kigezo cha unguli, katika kigezo hicho kunajitokeza nganozihusuzo mwanadamu na ngano za Miungu. Pili ni kigezo cha lengo la nganoinayohusika, katika kigezo hichi ngano zinaainishwa kwa kuzingatia lengo la usimulizi,kama vile ngano za kimaadili na ngano za kuhimiza kazi, kundi kubwa la ngano ni zileza kimaadili.Tatu ni kigezo cha sifa na ubora wa ngano, kigezo ambacho ndichokinachoonekana kubeba kundi kubwa la ngano. Katika kigezo hiki kuna ngano ambazohuambatana na uerevu au ulaghai wa wahusika.Ngano za kihistoria ambazo huhusu vita, vizazi, mashujaa, usuli wa kitu au jambo fulaniNne ni kigezo cha muktadha wa utendaji wa ngano, katika kigezo hichi kinachoangaliwazaidi ni ngano inatendwa wakati gani na katika mazingira gani. Kwa mfano, kwa kutumiakigezo hiki, tunaweza kupata hadithi zinazotendwa wakati wa mbalamwezi, nganozinazitendwa wakati wa ibada, wakati wa misiba na hata wakati wa mavuno, kama ilivyokatika jamii za kipemba wakati wa mavuno ya karafuu watu husimuliana hadithi wakatiwakiwa wanachambuwa karafuu kwa lengo la kuwa wachambuzi wasichoke walawasisinzie.

4Utanzu wa fasihi ambao umekuwa ukipewa umuhimu mmojawapo ni huo wa hadithi,katika kitanzu cha hadithi za watoto, matendo yanayooneshwa na wahusuka hujengamtiririko wa vituko vinavyokamilisha hadithi hiyo. Wahusika katika hadithi wanawezakuwa ni binadamu na viumbevyengine vyovyote, ambavyo vimepewa sifa zakibinadamu. Viumbe hivyo, hujenga zaidi, dhamira iliyokusudiwa na kuchaguliwakutokana na tabia za viumbe hivyo. Kwa mfano, mnyamakama Simba, huwakilishadhanna ya ukali, Sungura huwakilisha ujanja,fisi huwakilisha woga na tamaa, pia zimwina shetani huwakilisha dhanna ya viumbe vinavyotisha Hamad (1981).Hamad(keshatajwa) anaendelea kusema, hadithi hizo aghalabu huwa ni fupifupi, hivyo hutumiamuundo wa moja kwa moja ili zieleweke kwa urahisi. Katika hadithi hizo za jadi, fananipia,ana nafasi katika kufikisha ujumbe, kwani hupata fursa ya kushiriki katika utambajiwa hadithi.Pia hadithi za aina hiyo, hutumia nyimbo ambazo husaidia sana kufikisha ujmbe kwahadhira, vilevile nyimbo hutumika kuwaburudisha wasikilizajiHamad(ameshatajwa).Hamad anaendelea kwa kusema,hadithi chanzo chake katika jamii ni makuzi na walezikuishi pamoja katika miji na vitongoji kutokea asili, watu walipoanza kutumia lugha yafasihi kama ni chombo cha mawasiliano .Nivigumukwa mtafiti yoyote kuweza kuthibitisha kama aliweza kumpatamzeealiyeweza kukumbuka tarehe maalumu na pahala pamojawapo palipoanza sanaahii.Wengi walisema, fani hii ni moja kati ya jumla ya mazungumzo ya maana ambayomara nyingi huwa ni mchanganyiko wa wazee nawatoto kukutana na kutambiana hadithikwa shabaha yakutahadharishana,kushauriana,kuonyana na kuelezana mambo muhimuyanayohusu maisha yao. Kutokana na mfumo wa jadi hadithi mara zote, zilitolewanyakati za jioni, aghalabu baada ya sala za magharibi na isha. Zama hizo, ilikuwa nimarufuku au ni mwiko kutambiana hadithi mchana kwa sababu ya harakati za kimaisha.

5Japo kuwa mwiko ulikuwa na siri za kimsingi,hapo kale,mpaka leo unaumuhimu,pamojana maendeleo ya kisasa. Katika madrasa hasa ya msingi, ipo dharura yakuwatolea watoto hadithi na wao kutambiana hadithi zao mchana. Hii ni njia, miongonimwa njia za kuendeleza mafunzo kwa jumla. Maelezo hayo yanaonyesha chimbuko lahaditi katika jamii za kale. Hadithi katika misingi yake ya maana ni hisia za jamii katikakulea na kuadilisha jamii. Mtoto katika jamiiyake alijengwa kuamini kuwa mzee(mtumzima) hakosei na iwapo baba wa mtoto kakosea mtoto hamwambii baba yakehivyo waziwazi atatumia mbinu inayostahiki, kama kusema alimsia babu fulani akisemakufanya jambo fulani ni vibaya na halifai katika jamii yetu. Huku akiwa na lengo lakumkosoa baba yake na haya ni mafunzo yaliyotokana na hadithi za watoto katika jamiiya Wapemba.Ndungo na wenzake (1991), wanaeleza kuwa utanzu huo ulikuwa na madhumuni yakusimulia hadithi au kutamba hadithi.Lengo mahsusi la kusimulia hadithi ni kuburudishaau kutumbuiza wasikilizaji.Utanzu huo ulipitishwa kutoka kizazi hadi kizazi kwa njiyaya mdomo. Utunzi wake, kinyumena hadithi za kileo, haujuilikani, yaani hakuna mtualiyeweza kusemwa ni hadithi ya mtunzi huyu au yule. Ni masimulizi ambayo nimali yajamii nzima na kwa hivyo hazikumilikiwa na mtunzi yeyote.Umuhimu wa hadithi za paukwa .pakawa, ulikuwa katika kuendeleza na kuhifadhimaadili na mienendo ya jamii. Hadithi ilipotungwa kila mtu alikuwa huru kuisimuliakwawengine. Hakuna hadithi iliyotungwa mara mbili tatu ikabakia ilivyo, kilailipotambwa ilkuwa ngeni naya kipekee.WWW.gafkosft.com/ walisema kuwa hadithi huwa na mianzo maalumu yaani huwanzakwa;Paukwa .pakawa au hadithi .hadithi,hadithi njoo ,hapo zamani za kale

6Pia, wamesema hadithi huwa na miishio maalumu. Mfano,hadithi yangu yaishiapapo .,wakaishi raha mustarehe. Hadithi hizo zilikuwa na umuhimu wake,mfanokuhifadhi au kurithisha amali za jamii. Kuelimisha au kutoa mafunzo kuhusu jambomaalumukupitisha muda, hasakwa watoto waliposubiri chakula kiive. Kwa mujibu waMuhamed na wenzake (1981), hadithi za watoto ni utanzu wa karne na karne,ambaomwanadamu na wataalamu kadhaa, wamewahi kufanya utafiti juu ya ngano.Kwa mfano,Finnegan (1970), Sengo (1985), Mulokozi (1986),Senkoro (1997), Okpewhonimiongoni mwa wataalamu waliowahi kutafiti hadithi simulizi na kufafanua vipengelekama vile, ngano, tendina visasili katika maudhui na fani. Hata hivyo, baada ya kutaliimaandishi imegundulikana kuwa hakuna uchunguzi wa dhamira za hadithi za watotokatika jamii ya Wapemba, uliowahi kuandikiwa. Kwa muktadha huo mtafiti wa kazi hiiameamuwa kulitupia macho eneo hili ili kuziba pengo hilo la utafiti ambalo nikuchambuwa maudhui katika vipengele vya dhamira na ujumbe za hadi

kuchambua maudhui yanayopatikana katika hadithi za watoto katika jamii ya wapemba mwanaika madi mzee tasnifu iliyowasilishwa kwa ajili ya kutimiza sehemu ya la pekee la kutunukiwa digrii ya uzamili (m.a. kiswahili) ya chuo kikuu huria cha tanzania 2015

Related Documents:

Kiswahili, Kidato cha 3 Maazimio ya Kazi Muhula wa Kwanza 4-5 6 1 2 3-4 Hadithi fupi Fasihi teule Kusikiliza na kuzungumza Utunzi Hadithi fupi Siku ya Mganga Maudhui katika riwaya Lugha ya dini Umbo la barua rasmi Pwaguzi Kufikia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze: kujadili dhamira ya mwandishi. kuchambua maudhui na tamathali za lugha .

maswali yeye aliuliza ilikuwa, 'Biblia ina hadithi kuhusu mtu ambaye alimezwa na samaki mkubwa. Alikuwa nani? Asilimia themanini ya watu katika kundi hilo, kwa ushujaa wakasema, 'Pinocchio!' Marla aliniambia tukiwa bado katika ibaada kwamba swali hilo bado liliulizwa katika kanisa ambako alihundumu katika Kusini mwa California na

Mathalan, chimbuko la hadithi za fasihi ya Kiswahili linatokana na chimbuko la ngano za Kiswahili (Kenguru, 2013). Baada ya wageni wa Kimagharibi kuingia Afrka mashariki, hasa Wamishionari, ngano kadhaa wa kadhaa zilifasiriwa na kuwa ndio msingi wa hadithi ndefu za Kiswahili. Baina ya mwaka 1940 na kuendelea hadi miaka ya 1960, hadithi ndefu nyingi za Kiswahili zilifuata mkondo wa ngano za .

sayansi ya leo lakini haijakuwa bado mathalan roketi za kinuklia. Tunaweza kuamini kuwa ulimwengu unaorejelewa kwenye hadithi waweza kuwa katika siku zijazo. Kuna aina ya sayansi bunilizi iliyo burudani tupu. Katika utangulizi wa riwaya ya Isaac Asimor (1955), hadithi ya sayansi bun

kundi ,fanya jukumu la maana katika masomo yote.Umahiri wa maelezo maalum na wa baina ya mitaala yameshikanishwa pamoja katika muktadha wa maelezo. . baina ya mitaala katika muda wa mwaka wa shule. Kwa kufanya hivo wanaangazia kusoma kwao . na wanachukua jukumu la mchakato wao wa kimasomo. Tathmini ya kibinafsi hufanywa katika

"Mafunzo ya kwanza." au ya "msingi" yote yanayopatikana katika kifungu hiki cha Biblia yamepanuliwa. Mafunzo haya yameandaliwa yawasaidie zaidi wale wanaopitia mafunzo ya Kuweka Msingi wa Imani katika Kanisa la Cornerstone maana yake kwa ni Kiswahili Kanisa la Jiwe la Pembeni. Mafunzo haya yanawawezesha kulenga zaidi katika kile .

zozote nne katika diwani ya Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyingine (alama 20) 6. Eleza nafasi ya vijana katika jamii ukerejelea hadithi fupi zifuatazo. a) Mapenzi ya kifa urongo (alama 5) b

TABE 11 & 12 READING PRACTICE TEST LEVEL M. Read the passage. Then answer questions 1 through 7. Whale Watching. Across the blue, rolling waves, a dark hump rises from the sea. It slides out of sight as an enormous tail lifts and falls. As it does, another hump rises beside it and begins the same dance. Several people cheer from the pontoon boat. Some raise their cameras, while others lift .