KUCHUNGUZA MAUDHUI YA NYIMBO ZA KAMPENI ZA UCHAGUZI MKUU .

3y ago
232 Views
2 Downloads
1,004.55 KB
137 Pages
Last View : 11d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Maxton Kershaw
Transcription

KUCHUNGUZA MAUDHUI YA NYIMBO ZA KAMPENI ZA UCHAGUZIMKUU ZANZIBAR 2000-2010DAUD MOH’D ALITASNIFU ILIYOWASILISHWA IKIWA NI SEHEMU YA MASHARTI YAKUPATIWA SHAHADA YA UZAMILI (M.A. KISWAHILI) YA CHUOKIKUU HURIA CHA TANZANIA2017

iiUTHIBITISHIAliyetia saini hapa chini anathibitisha kwamba ameisoma kazi hii na anaidhinishaikubaliwe kwa utahini na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania tasnifu yenye mada:“Kuchunguza Maudhui ya Nyimbo za Kampeni za Uchaguzi Mkuu Zanzibar2000-2010" na kupendekeza ikubaliwe kwa ajili ya kukamilisha masharti yakutunukiwa Shahada ya Uzamili(M.A Kiswahili) ya Chuo Kikuu Huria -------Prof. Dkt. ----------------------Tarehe

iiiHAKIMILIKITasnifu hii au sehemu yake yoyote hairuhusiwi kukaririwa, kuhifadhiwa,kubadilishwa au kuhaulishwa kwa mbinu yoyote ile: kielektroniki, kunakilishwa,kurudufiwa, kupigwa picha, au kurekodiwa kwa utaratibu wowote ule katika haliyoyote ile bila ya idhini ya maandishi kutoka kwa mwandishi wake au kutoka ChuoKikuu Huria cha Tanzania, kwa niaba yake.

ivIKIRARIMimi, Daud Moh’d Ali, ninathibitisha kwamba, tasnifu hii ni kazi yangumwenyewe na haijawahi kuwasilishwa katika Chuo Kikuu kingine chochote, kwaajili ya kutunukiwa Digrii yoyote.Saini.Tarehe

vTABARUKUNinaitabaruku kazi hii kwa watu muhimu kwangu, kwanza, wazazi wanguwapendwa marehemu baba yangu bwana Moh‟d Ali Shamata na mama yangu bibiMkasi Khamis Khatib (Mungu awalaze mahali pema peponi, amin), ambao kwapamoja wamejitolea kwa hali na mali kufanikisha matarajio yangu ya kielimuyaliyoniwezesha kufikia hatua hii. Pili, mke wangu mpenzi Zakia Iddi Ali, watotowangu wapendwa, dada, ndugu na kaka zangu wote wa ukoo wa Shamata Mustafa,kwa pamoja ninawatunukia zawadi hii adhimu kwao.

viSHUKURANIAwali ya yote ninapenda nimshukuru Mwenteezi Mungu, Muumba mbingu na ardhikwa kunijaalia nguvu, uhai, uzima, uwezo na jitihada kukamilisha utafiti huu. Utafitihuu umekamilika kutokana na msaada wa watu tafauti. Si rahisi kuwataja wote. Hatahivyo, nitawatataja baadhi kwa niaba yao. Kwanza ninamshukuru kwa dhatimsimamizi wangu Prof. Dkt. Sheikh T.S.Y.M Sengo kwa kuniongoza katikakukamilisha kazi hii. Pili, ninawashukuru wazazi wangu wapendwa kwa kujitoleakwa hali na mali kunipeleka skuli na kunisimamia hadi kupata akili zilizoniwezeshakufikia kiwango cha uzamili huu.Tatu, ninatoa shukurani zangu za dhati kwa mke wangu mpendwa Zakia Iddi Ali,kwa ustahamilivu na ushirikiano wake kwa kipindi chote cha masomo yangu. Nne,mwalimu Mmanga Mjengo Mjawiri wa Chuo Kikuu Cha Taifa cha Zanzibar (SUZA)kwa ushirikiano wake hadi nikapata data zilizokamilisha utafiti huu. Ninamshukurukaka yangu Issa Khamis Issa kwa kunikutanisha na wana kikundi cha sanaa, mila nautamaduni cha Zanzibar. Pia wanafunzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwakushirikiana nami katika harakati za masomo.Shukrani za pekee zimwendee Dkt. Maulid Haji Omar, kwa kunipa maelekezo namsaada wa kutosha hadi kukamilika kwa utafiti huu. Walimu na wanafunzi wote waChuo Kikuu cha Suza. Baraza la Sanaa na Muziki Zanzibar. Mwisho, viongozi wotewa vikundi vya Ngoma na Taarab, kwa kushirikiana nami hadi kukamilika kwautafiti huu.

viiIKISIRIUtafiti huu umechunguza maudhui ya nyimbo za kampeni za uchaguzi mkuu,Zanzibar (2000-2010). Mtafiti aliongozwa na madhumuni mahsusi matatu, lakwanza, kuchunguza na kuainisha nyimbo za kampeni za uchaguzi mkuu, Zanzibar2000-2010, la pili, Kutathmini mchango wa nyimbo za kampeni za uchaguzi mkuuZanzibar, katika kustawisha jamii ya Wazanzibari, na la tatu, Kutafuta mbinu zakufanya nyimbo hizo ziwe zinaleta umoja badala ya utengano katika jamii yaWazanzibari. Katika kufanikisha madhumuni hayo, mtafiti alifuata njia zilizostahikikwenda kwenye vikundi vya ngoma na kukutana na malenga ili kupata dataalizozihitaji kwa watafitiwa. Watafitiwa hao waligawanyika katika makundi yavijana, watu wazima wenye maarifa na kumbukumbu za mambo ya kihistoria,walimu, wasanii, wataalamu wa lugha ya Kiswahili na utamaduni, na waandishi wahabari. Mtafiti aliongozwa na nadharia ya mtu na Utamaduni, nadharia ya Fasihi inakwao, nadharia ya Tabia na nadharia ya Uhalisia katika ukusanyaji na uchambuzi wadata za utafiti. Aidha, utafiti umetaja kipengele cha lugha, wahusika na mandhari ilikuibulia maudhui yaliyokusudiwa. Utafiti umeonesha dhamira ya kuhamasisha, ajirakwa vijana, na mmomonyoko mkubwa wa maadili ya jamii. Mwisho, utafiti umetoamapendekezo kwa watafiti wa usoni.

viiiYALIYOMOUTHIBITISHI . iiHAKIMILIKI . iiiIKIRARI . ivTABARUKU . vSHUKURANI . viIKISIRI . viiYALIYOMO . viiiORODHA YA MAJEDWALI . xiiiORODHA YA VIAMBATISHO . xivSURA YA KWANZA . 1UTANGULIZI WA JUMLA . 11.1Utangulizi . 11.2Usuli wa Mada . 11.3Usuli wa Tatizo . 31.4Tamko la Tatizo la Utafiti . 81.5Lengo la Utafiti . 81.6Madhumuni Maalumu . 81.7Maswali ya Utafiti . 81.8Umuhimu wa Utafiti. 91.9Mipaka ya Utafiti . 101.10Matatizo ya Utafiti na Utatuzi Wake . 101.10.1 Kiutawala . 10

ix1.10.2 Kuwapata Wahojiwa . 111.10.3 Kuwapata Wasanii. 111.10.4 Matatizo ya Kijamii . 111.10.5 Matatizo ya Kitaalimu . 111.11Mpangilio wa Tasnifu . 121.12Hitimishi . 12SURA YA PILI . 13UTALII WA KAZI TANGULIZI NA MKABALA WA KINADHARIA . 132.1Utangulizi . 132.2Maana ya Fasihi Simulizi . 132.3Maana ya Nyimbo . 142.4Histori ya Nyimbo . 162.5Sifa za Nyimbo . 192.6Aina za Nyimbo . 202.6.1 Nyimbo za Tumbuizo . 202.6.2 Kongozi . 212.6.3 Nyimbo za Uganga . 212.6.4 Nyimbo za Dini . 222.6.5 Wawe . 232.6.6 Tenzi . 232.6.7 Tendi. 232.6.8 Mbolezi. 232.6.9 Kimai . 232.6.10 Nyiso . 24

x2.6.11 Nyimbo za Vita . 242.6.12 Nyimbo za Kazi . 252.6.13 Nyimbo za Uwindaji . 252.6.14 Nyimbo za Watoto . 252.6.15 Nyimbo za Taifa . 272.6.16 Nyimbo za Siasa . 272.7Fani Katika Nyimbo . 282.7.1 Utangulizi . 282.7.2 Vipengele vya Fani. 292.8Mapitio ya Maandishi. 312.9Mkabala wa Nadharia. 382.10Maelezo ya Dhana Muhimu . 382.10.1 Nadharia ya Mtu na Utamaduni . 382.10.2 Nadharia ya Fasihi ina Kwao . 392.10.3 Nadhariya ya Tabia . 402.10.4 Nadharia ya Uhalisia . 412.11Hitimishi . 44SURA YA TATU . 45MBINU ZA UTAFITI . 453.1Utangulizi . 453.2Mkabala wa Utafiti . 453.3Eneo la Utafiti . 453.4Mbinu za Utafiti . 463.4.1 Mbinu ya Maktabani . 46

xi3.4.2 Mbinu ya Masikanini (Makaazini) . 473.4.3 Mbinu ya Usaili . 473.4.4 Mbinu ya Hojaji . 483.4.5 Watafiti Wasaidizi . 493.5Uteuzi wa Watafitiwa . 503.5.1 Vijana . 513.5.2 Watu Wazima . 513.5.3 Walimu . 523.5.4 Wasanii . 523.5.5 Wasomi. 523.5.6 Wataalamu wa Lugha ya Kiswahili. 533.5.7 Waandishi wa Habari . 533.6Ukusanyaji wa Data . 543.7Zana za Kukusanyia Data . 543.8Hitimishi . 55SURA YA NNE . 56UWASILISHAJI NA UCHAMBUZI WA DATA . 564.1Utangulizi . 564.2Kukusanya na Kuainisha Nyimbo za Kampeni za Uchaguzi Mkuu,Zanzibar 2000-2010 . 574.3Kutathmini Michango ya Nyimbo za Kampeni za Uchaguzi Mkuu,Zanzibar Katika Kustawisha Jamii ya Wazanzibar . 644.3.1 Kuburudisha . 644.3.2 Kuhamasisha . 65

xii4.3.3 Ajira kwa Vijana . 674.3.4 Kujenga Maadili . 674.4Kutafuta Mbinu za Kufanya Nyimbo za Kampeni za Uchaguzi Ziwe.Zinaleta Umoja Badala ya Utengano Katika Jamii ya Wazanzibari . 684.5Uchambuzi wa Maudhui ya Nyimbo za Kampeni . 694.5.1 Umoja wa Jamii ya Wazanzibari . 714.5.2 Maadili . 724.5.3 Mila na Utamaduni . 734.5.4 Migogoro . 774.6Hitimishi . 80SURA YA TANO. 81MUHTASARI, HITIMISHI NA MAPENDEKEZO . 815.1Utangulizi . 815.2Muhutasari wa Tasnifu . 815.3Matokeo ya Utafiti . 825.4Mapendekezo ya Utafiti . 835.5Mapendekezo Juu ya Utafiti Fuatishi . 84MAREJELEO . 85VIAMBATANISHI . 90

xiiiORODHA YA MAJEDWALIJedwali Namba 3.1: Jumla ya Watafitiwa 31 . 53

xivORODHA YA VIAMBATISHOKiambatanishi 1: Nyimbo za Kampeni . 90Kiambatanishi 2: Hojaji kwa Walimu na Wasomi . 117Kiambatanishi 3: Muongozo wa Mahojiano na Wadau Mbalimbali wa Nyimboza Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar WakiwemoWasanii, Vijana, Walimu, Wataalamu wa Lugha yaKiswahili, Wasomi na Waandishi wa Habari . 122

1SURA YA KWANZAUTANGULIZI WA JUMLA1.1UtanguliziKatika sura hii, mtafiti amezungumzia kwa kina kuhusu chimbuko na tatizo la utafitihuu. Utafiti huu unahusu maudhui ya nyimbo za kampeni za uchaguzi mkuuZanzibar: (2000-2010). Mtafiti amekusudia kubainisha usuli wa mada ya utafiti kwakufafanua fasili za nyimbo na umuhimu wa nyimbo. Mtafiti amezungumzia usuli watatizo kwa kuonesha sababu za mivutano na uhasama uliyotokea wakati wa kampeniza chaguzi zilizopita Visiwani, na kuonesha mivutano,ubaguzi na uhasamaunaozagaa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu Zanzibar.Utafiti huu umefanywakatika Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.1.2Usuli wa MadaHistoria ya Zanzibar ni pana na ni yakale sana. Historia ya Visiwa hivi imeanzamiaka na karne nyingi zilizopita. Visiwa hivi ni sehemu ya kumbukubu ya historia yaulimwengu, Waajemi wafanyabiashara, walivigundua na kuvifanya makao makuukwa safari kati ya Mashariki ya Kati, India na Afrika. Kabla ya wafanyabiashara haokuingia Zanzibar, watu wa asili walikuwa ni wavuvi, wakulima na wafugaji. Mila nadasturi zao, ni za kupendana, kuishi pamoja, kufanyakazi zao pamoja kwa ujimauliodumisha mafahamiano ya pamoja.Watu hao wa Zanzibar, walikuwa na tawalazao za jadi.Sheriff (1995) anasema, utawala wa jadi wa watu wa Zanzibar ulikuwa ni wawakuu wa vijiji. Kila kijiji kilikuwa kikiongozwa na mtu ambaye aliheshimiwa

2kutokana na kuhamia eneo hilokabla ya wengine na kuonekana kuwa ni muasisi wakijiji. Kiongozi huyo ndiye aliyekuwa na uwezo kamili wa kuamua na kuagiza.Pamoja na uwezo alionao kiongozi huyo, alikuwa akiteuwa wasaidizi wake kutokakatika koo mbalimbali ili maoni na fikra zao ziweze kusaidia kufikia uamuzi wabusara na wa pamoja.Viongozi hao wateuliwa walikuwa na maarifa ya mambomengi yaliyohusu jamii zao na yaliyoaminika mbele ya wen

kwenda kwenye vikundi vya ngoma na kukutana na malenga ili kupata data alizozihitaji kwa watafitiwa. Watafitiwa hao waligawanyika katika makundi ya vijana, watu wazima wenye maarifa na kumbukumbu za mambo ya kihistoria, walimu, wasanii, wataalamu wa lugha ya Kiswahili na utamaduni, na waandishi wa habari.

Related Documents:

mawazo ya wanamsambao hususani katika ugawaji wa ngano bila kuchunguza kwa umakini sifa ya kila kundi. Propp anaamini kuwa ili kuchunguza asili ya ngano ni vema kuanza kuchunguza aina za ngano kwa kuangalia maumbo ya ngano. Hivyo mtazamo huu unaangalia asili ya ngano kwa kuchunguza maumbo ya ngano husika. Ubora wa nadhairia hii, nadharia hii inasaidia kujua aina za ngano kutokana na dhima zake .

Ephraim hajui Kiswahili fasaha lakini nyimbo zake hizo alifundishwa kuziimba kwa lugha ya Kiswahili na mchungaji ambaye pia ni muimbaji wa nyimbo za Injili kutoka Tanzania, Ency Mwalukasa. Muimbaji huyo amesema ataendelea kuimba nyimbo za injili kwa sababu zime

kuchambua maudhui yanayopatikana katika hadithi za watoto katika jamii ya wapemba mwanaika madi mzee tasnifu iliyowasilishwa kwa ajili ya kutimiza sehemu ya la pekee la kutunukiwa digrii ya uzamili (m.a. kiswahili) ya chuo kikuu huria cha tanzania 2015

Kiswahili, Kidato cha 3 Maazimio ya Kazi Muhula wa Kwanza 4-5 6 1 2 3-4 Hadithi fupi Fasihi teule Kusikiliza na kuzungumza Utunzi Hadithi fupi Siku ya Mganga Maudhui katika riwaya Lugha ya dini Umbo la barua rasmi Pwaguzi Kufikia mwisho wa somo, mwanafunzi aweze: kujadili dhamira ya mwandishi. kuchambua maudhui na tamathali za lugha .

Wapemba. Surahii pia inatoa taarifa za awali kuhusu mada ya utafiti ambapo mtafiti ataelezea kuhusu usuli wa mada,tatizo la utafiti,malengo ya utafiti yakiambatana na mswali ya utafiti ,umuhuimu wa utafiti mipaka ya utafiti hatimae hitimisho , haya yote yameelezewa juu ya kuchunguza matumizi ya tafsida katika lahaja

Kikoloni, za Kidini na kibinafsi. Chuki si tabia ya Wasomi. Ushairi wa Kiswahili una kwao (Sengo, 2009). Hii inadhibitishwa na utafiti uliofanywa na Mulokozi na Sengo (1995) ambao nao walihitimisha kwamba, Ushairi wa Kiswahili unatokana na nyimbo za Kiafrika ingawa na wao wanakiri kuwa fasihi ya Kiarabu na Dini ya

ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2020 utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015. Vilevile, maudhui ya Ilani hii yamezingatia Mwelekeo wa Sera za Chama Cha Mapinduzi wa 2020-2030, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2020-2050. Aidha, Ilani hii imezingatia fursa na changamoto

and STM32F103xx advanced ARM-based 32-bit MCUs Introduction This reference manual targets application developers. It provides complete information on how to use the low-, medium- and high-density STM32F101xx, STM32F102xx and STM32F103xx microcontroller memory and peripherals. The low-, medium- and high-density STM32F101xx, STM32F102xx and STM32F103xx will be referred to as STM32F10xxx .