MASWALI NA MAJIBU - Al Itrah

1y ago
70 Views
2 Downloads
2.65 MB
250 Pages
Last View : 12d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Sutton Moon
Transcription

MASWALI NA MAJIBU أسئلة و إجابات Fikira za kivitendo zinazotatua matatizo ya kijamiina mambo ya kiutamaduni katikamwangaza wa rejea za kisharia za kijamii أفكار عملية تعالج مشاكل اجتماعية وقضايا ثقافية على ضوء مصادر الشيعة اإلمامية Mwandaaji:Mahdi Ja’far SulailMtarjumi:Abdul Karim Juma Nkusui12 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 111/10/2017 6:51:31 PM

ترجمة أسئلة و إجابات أفكار عملية تعالج مشاكل اجتماعية وقضايا ثقافية على ضوء مصادر الشيعة اإلمامية إعداد : مهدي صليل من اللغة العربية إلى اللغة السواحلية 11/10/2017 6:51:31 PM 12 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 2

Haki ya kunakili imehifadhiwa na:AL-ITRAH FOUNDATIONISBN: 978 – 9987 – 17 – 011 –1Mwandaaji:Mahdi Ja’far SulailMtarjumi:Abdul Karim Juma NkusuiKimehaririwa na:Ustadh Hemedi LubumbaKimesomwa Prufu na:Al-Haji Ramadhani S. K. ShemahimboKimepitiwa na:Al Haji Mujahid RashidKimepangwa katika Kompyuta na:Al-Itrah FoundationTole la kwanza: Machi, 2018Nakala: 2,000Kimetolewa na kuchapishwa na:Al-Itrah FoundationS.L.P. 19701 Dar es Salaam, TanzaniaSimu: 255 22 2110640 / 2127555Barua Pepe: alitrah@yahoo.comTovuti: www.alitrah.infoVitabu mtandaoni: www.alitrah.info/ebooks/ILI KUSOMA QUR’ANI MUBASHARAKWA NJIA YA MTANDAO,TEMBELEA: www.somaquran.com12 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 311/10/2017 6:51:31 PM

YALIYOMOUtangulizi . 1Neno la Mchapishaji. 2Utangulizi wa Sheikh Hasan Saffar. 4Dibaji . 9Mas’ala ya Qur’ani. 161.Kupima kwa kutumia Qur’ani. 172.Mama wa waumini. 183.Hawaigusi ila wenye kutwaharika. 204. Aya ya utakaso. 225.Kupanga kwa Sura za Qur’ani. 236. Ambao amewaneemesha Mwenyezi Mungu. 257.Bismillah katika Surat Tauba. 268.  Kutajwa Nabii Isa pamoja na jinala mama yake 269.  Maana ya kauli ya Nabii waMwenyezi Mungu Isa : Tawafaytani(Uliponifisha) 2710.Mauti ya kwanza. 2812 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 411/10/2017 6:51:31 PM

11.Nini makusudio ya ‘Aali Yasin’. 29Mas’ala ya Kifikra. 301.Nini sababu ya kuumbwa?. 302.Kumuona Mwenyezi Mungu Mtukufu. 333.Moto na Jinni. 364.  Kuhifadhiwa Qur’ani kutokana nakupotoshwa. 375.Falsafa ya kuumba na taklifu. 386.Uimamu kwa Mashia. 407. Toba ya mwenye kuritadi. 418. Tofauti baina ya Uislamu na Imani. 439.Jini na athari yake kwa mwanadamu. 4410. Uchawi na kuondolewa taufiki. 48Mambo ya Kiutamaduni. 501.Rejea za hadithi sahihi. 512. Adabu ya dua na masharti ya kujibiwa. 523.Kuota usingizini. 554.Mazingira ya kuamrisha mema. 575.  Wanaoishi ugenini na uhusianobaina ya jinsia mbili. 5912 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 511/10/2017 6:51:31 PM

MASWALI NA MAJIBU6.Uendeshaji wa Taasisi za kidini. 617. Tamko la Istighifari. 638.Kuamiliana na historia. 649.Sababu za kupotoka vijana. 6610.Maana ya upendo na kuelemea kihisia. 6811. Tofauti baina ya dhambi na kosa. 7112.Dhana ya nchi na uraia. 7113.Kujiunga na Seminari za Masomo ya dini. 7614.  Kupima nguo kwa dhiraa nasababu za kuchelewa kuolewa. 8215.Hatua za kutunga. 8416.Kutoa jarida la Utamaduni la kidini. 8517.Maana ya uchamungu. 8618.Uhusiano baina ya wafuasi wa madhehebu. 87Mambo ya Kifamilia. 901.Mume anamtukana mke wake. 912.  Kati ya wajibu wa kutoa matumizina hisia za upendo. 93vi12 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 611/10/2017 6:51:31 PM

MASWALI NA MAJIBU3.Mume wangu ana mahusiano kupitia intaneti. 954. alalamikia hali yangu kwaNmwanaume ajnabi. 995.Naogopa dada yangu kupotea. 1026.Mke wangu hajui mambo ya dini yake. 1047.D ada yangu sio mwenye kulazimianana dini . vipi nitamrekebisha?. 1078.Mama yangu hafanyi uadilifu kati yetu. 1109.Baba yangu ananidhulumu. 11310. Vipi nitambadilisha mume wangu?. 11511.Siwavumilii watoto wangu, nawapiga!!. 11712.Mtoto wangu anapuuza swala yake. . 12013.Naogopa kuandikwa miongoni mwa waasi. 12314.Mimi nina hasira kwa mke na watoto. 12615.Kutibu ukaidi kwa watoto. 12816.Mume wangu ananipiga. 13017.Mama yangu amenigombeza. 13218.Msingi ya kuwalea watoto. 134vii12 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 711/10/2017 6:51:31 PM

MASWALI NA MAJIBU19.Mume wangu ananiambia maneno yenye kujeruhi. 13620.Baina ya upole na kutetea haki. 13721.Mke wangu wakati mwingine haswali. 139Matatizo na Utatuzi.1431.Nimempenda lakini yeye anakataa. 1442.Nimezama katika kuangalia filamu. 1463.Najaribu kuilea nafsi yangu bila ya mafanikio. 1494.Nakabiliwa na uzembe katika kutekeleza Swala. . 1515.Nataka toba. 1546. Vipi nitajinasua na dhambi?. 1577.Nakabiliwa na usahaulifu. 1618. Toba kutokana na kuwasiliana (kwenye mitandao). 1639. Wasiwasi utaniuwa. 16510.Kufikiria, Je kunawajibisha kuoga?. 16911. Vipi nitahisi raha na furaha. 17112.Nakabiliwa na dharau kutoka kwenye familia yanju. 17213.Nakabiliwa na wasiwasi katika twahara. 177viii12 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 811/10/2017 6:51:31 PM

MASWALI NA MAJIBU14.Kuchombezana wakati wa uchumba. . 17915.Nimemwasi Mola Wangu, ni namna gani nitatubia?. 18116.  Naogopa mauti na ninahisi kuzembeambele ya Mwenyezi Mungu. 18617.Nataka kurejea kwa Mola Wangu hali ya kutubia. 18918.Namna gani nitajinasua na fikra za kutawaliwa. 193Mambo ya Kijamii.1951. Vitendo vya vijana vya kimakosa. 1962.Mshikamano wenye mpasuko. 1983.Michezo katika vilabu. 1994.Uombezi katika kisasi. 2005.Kuzidisha mahari. 2026. Anatishia kusambaza picha yangu. 2037.Istikhara katika kuvunja uchumba. 2058.Kukata uhusiano na mwanaume aliyeoa. 2079.Mume wangu yuko chini ya kiwango changu kijamii. 21010.Ulazima wa kujituma kutatua matatizo ya kijamii. 213ix12 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 911/10/2017 6:51:31 PM

MASWALI NA MAJIBU11.Baina ya kufariki mzani wangu na hafla ya Maulidi. 21512.Ndoa imechelewa kwa sababu ya istikhara. 21713.Kuvunja uchumba bila ya sababu. 21814. Wanawake wanazungumza dhidi yangubila ya sababu. 21915.Je, nifanye mawasiliano pamoja na asiyenipenda?. 22216.Usimamizi wa msikiti na vipindi vya kidini. 22417. Talaka kwa ajili ya kujali watoto wangu. 22518.  Jamaa yangu wa karibu anafanya mahusianoyenye mashaka. 22619.Heshima wakati wa uchumba. 227x12 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1011/10/2017 6:51:31 PM

MASWALI NA MAJIBUَّ بِس ِْم ه َّح ِيم ِ للاِ الرَّحْ ٰ َم ِن الر UtanguliziKitabu hiki ni toleo la Kiswahili la taasisi ya Al ItrahFoundation. Chapisho lake limelenga kukidhi mahitaji ya kiroho ya zama hizi pamoja na Ubongo na fikrazinazokuwa za Muislam. Jitihada kubwa zimefanywa naTaasisi kuweka chapisho hili la Kiswahili katika msingiwa haki na wenye kukubalika katika Uislam.Unaombwa kwa Taadhima ukisome kitabu hiki katika malengo yaliyokusudiwa. Pia Unaombwa kuwasilisha kwetu maoni yako huru juu ya chapisho letu hili,jambo ambalo tutashukuru sana.Kutangaza ujumbe wa Uislam ni kazi ambayo inahitaji ushirikiano wetu sote. Taasisi inakuomba kuungana na kushirikiana kama ilivyoagizwa katika aya yaQur’an: (Surat Saba’ 34:46).Na rehma za Allah ziwe juu yako.Wako katika UislamAl Itrah FoundationBarua Pepe: alitrah@yahoo.comSMS: 255 778 300 140112 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 111/10/2017 6:51:31 PM

MASWALI NA MAJIBUَّ بِس ِْم ه َّح ِيم ِ للاِ الرَّحْ ٰ َم ِن الر NENO LA MCHAPISHAJIMaswali na Majibu ni kitabu kinachotoa mwongozo kwa njia ya maswali na majibu. Kitabu hiki nimkusanyiko wa maswali aliyoulizwa Sheikh Hasan alSaffar katika programu yake ya maswali na majibu iliyoandaliwa katika tovuti yake. Sheikh wetu huyu amechukua fursa hii ili kujua ni kitu gani watu wanatakakujua na ambacho hawakijui, hususan kwa wale ambaohawakupata fursa ya kusoma katika vyuo vya kidiniSisi kama wachapishaji tunakiwasilisha kitabu hikikama kilivyo kwa wasomaji wetu na kuwashauri wasome yaliyomo humo, wayafanyie kazi na kuyazingatiana kufaidika na hazina iliyoko ndani yake.Hivyo, ni matumaini yetu kwamba wasomaji wetuwatanufaika vya kutosha kutokana na kitabu hiki,kwani tumekiona ni chenye manufaa sana, hususanwakati huu wa maendeleo makubwa ya elimu katikanyanja zote ambapo uwongo, ngano za kale na upotoshaji wa historia ni vitu ambavyo havina nafasi tenakatika akili za watu.212 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 211/10/2017 6:51:31 PM

MASWALI NA MAJIBUTunamshukuru mwandishi wa kitabu hiki SheikhHasan Musa al-Safar kwa kazi kubwa aliyofanya kwaajili ya Umma huu wa Waislamu, Allah Azza wa Jallaamlipe kila la kheri na amuingize Peponi kwa salamana amani Insha’Allah. Halikadhalika tunamshukurundugu yetu Abdul Karim Juma Nkusui kwa kukitarjumikwa Kiswahili kitabu hiki, Insha’Allah na yeye AllahAzza wa Jalla amlipe kila kheri hapa duniani na hukoAkhera pia, bila kuwasahau na wale wote waliochangia kwa namna moja au nyingine mpaka kufanikishakuchapishwa kwake, Allah Mwenye kujazi awalipewote malipo mema hapa duniani na huko Akhera pia.MchapishajiAl-Itrah Foundation312 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 311/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUَّ بِس ِْم ه َّح ِيم ِ للاِ الرَّحْ ٰ َم ِن الر UTANGULIZI WA SHEIKHHASAN SAFFARUelewa wa mwanadamu katika elimu na maarifa,na kutafuta kwake haki na usahihi, ni sababu yamsingi ya kuzalika maswali katika akili yake. Kamaambavyo hali inayomkabili ya vita ndani ya nafsi yamwanadamu baina ya uwepo wake na akili yake kwaupande mmoja, na raghaba zake kwa upande mwingine, mara nyingi humuweka katika nafasi ya tahayarina kuuliza.Na mwanadamu anaikuta nafsi yake mbele ya haliya msongamano na mgongano baina ya mielekeo yenyekutatiza, namna gani anaweka daraja la vipaumbelevyake? Na namna gani atapambanua kati ya kile chamuhimu zaidi na cha muhimu?Na katika upande wa raghba zake anaweza kukabiliana na msukumo baina ya mielekeo na ugumu,anaweza kusimama kwa tahayari na kujiuliza. Hakikamwanzo wa maswali katika akili ya mwanadamu ni412 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 411/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUmatokeo ya umahususi wake wa kiakili, na aliyopewana Mwenyezi Mungu Mtukufu katika matakwa yanayompa uhuru wa kuchagua.Na swali ni dalili ya kuamka na ni kiashirio cha ufahamu, nalo linaonesha hisia za mwanadamu alizonazombele ya majukumu anayoyaulizia na kuyatafakari.Wakati ambapo kukosekana kwa swali kunaashiriauzembe katika akili na uvivu wa kijinga wa kutoamiliana na matukio ya maisha.Hakika swali linamuongoza mwanadamu kwenyemaarifa, na linamfanya awe karibu zaidi na usahihi, nakwa hiyo zimekuja nususi za kidini nyingi zinazomhimiza mwanadamu kufikiri na kuuliza. Na zinamsukumakuuliza maulamaa na wabobezi katika nyanja mbalimbali. Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Waulizeniwenye elimu ikiwa nyinyi hamjui.” Na tamko hili limerudiwa mara mbili katika Qur’ani tukufu katika Surat Nahli Aya ya 43, na katika Surat Anbiyai Aya ya 7.Na imepokewa kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwamba amesema: “Swali ni nusu yaelimu.”1 Na kwa sababu swali ni utamaduni wa kijamii.Imepokewa kutoka kwake : “Elimu ni hazina nafunguo zake ni swali, hivyo ulizeni Mwenyezi Mungu1.Kanzul-Umaal, Juz. 10, uk. 237, hadithi ya 2926.512 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 511/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUawarehemu, hakika wanalipwa watu wanne: Muulizaji,mzungumzaji, yaani mwenye kujibu, msikilizaji namwenye kuwapenda.”2Imekuja kutoka kwa Amirul-Muuminina kauliisemayo: “Nyoyo ni kufuli na funguo zake ni kuuliza.”3Na kutoka kwake : “Uliza ambalo hakuna budi kwako kulijua na wala husamehewi katika kutolijua.”4Na katika zama hizi mambo yamekuwa rahisi nanyenzo zimeandaliwa, na njia za maarifa zimeenea, nakuna uwezekano wa mtu yeyote kuwasiliana na maulamaa wabobezi katika nyanja mbalimbali za elimuya maisha. Hivyo hakuna udhuru kwa mwanadamukuzembea katika kuchuma maarifa au kubakia katikatahayuri ya ujahili.Katika upande wa kidini wamejitolea idadi kubwaya maulamaa katika kukabiliana na kupokea maswaliambayo yanafungamana na mambo ya kisharia, na hiyoni kupitia vyombo vya mawasiliano vya kisasa, na njiazilizo dhahiri zaidi ni kufungua sehemu za mawasilianokatika tovuti.Na kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenifadhilisha2.3.4.Tuhful-Uquul an Aali Rasuli, uk. 34Ghurarul-Hikam wa Duraril-kalim al-Kaadhim.“‘’““.612 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 611/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUkujiunga na njia ya wanafunzi wa elimu ya dini namaarifa kwa kiwango changu kidogo na juhudi zangufinyu, nilianzisha tovuti kwa msaada wa baadhi yandugu watukufu ambapo niliifungua mwaka 1999. Naikawa zinanifikia kupitia baruapepe ya tovuti yangu,barua nyingi ambazo zinabeba maswali mbalimbali naushauri, baadhi yake yanahusiana na mas’ala ya kidinina nyingine zinaelezea matatizo ya kijamii.Na nilikuwa ninanufaika na mas’ala hayo katikakuangalia baadhi ya matatizo ya kidini na ya kijamii,kama ilivyokuwa baadhi ya mas’ala yanahitajia utafitina kurejea kwa ajili ya kuandaa majibu yanayofaa. Nakwa wingi wa barua zinazokuja, pamoja na shughulizangu mbalimbali nilimuomba ndugu yangu mtukufuUstadhi Mahdi Ja’far Sulail anisaidie katika kufanyakazi hii. Kwa imani yangu kuwa kwa uwezo wakena msimamo wake na ikhilasi yake hakika alikuwani msaada na msaidizi bora sana kwangu. MwenyeziMungu amlipe malipo mema, na amzidishie malipo.Na kitabu ambacho kiko mbele ya msomaji mtukufu, kinakusanya mkusanyiko uliochaguliwa kutokakatika maswali na majibu hayo. Nataraji kuwa katikakuyasambaza kwake kutakuwa na manufaa na faidakwa wasomaji watukufu.712 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 711/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUNa mwisho ninarudia shukrani zangu kwa nduguyangu Ustadhi Sulail kwa kazi yake ya kuandaa kitabuhiki, na kwa huduma yake yenye kuendelea katika dinina jamii. Mwenyezi Mungu amhifadhi na amlinde, naakithirishe katika jamii watu mfano wake.Na shukrani ni za Mwenyezi Mungu Mola Mleziwa walimwengu.Hasan Musa Saffar,20 Rabiul-Awwal 1433 Hijiria,12 Februari 2012.812 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 811/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUَّ بِس ِْم ه َّح ِيم ِ للاِ الرَّحْ ٰ َم ِن الر DIBAJIMwanadamu anakabiliwa katika maisha yake yakijamii na ya kifamilia na matatizo mbalimbali,na yanampata mas’ala ya kifikira na kiutamaduni nayanahitaji mtazamo wa wazi unaomwangazia njia, nakumfunulia uwezo wake uliofichikana ambao unamuwezesha kuvuka matatizo. Katika Qur’ani tukufu nahadithi tukufu kuna maelekezo ya kuhimiza kuuliza nakutafuta elimu na maarifa. Anasema Mwenyezi MunguMtukufu katika Surat Nahli: وحي إِلَ ْي ِه ْم ۚ فَاسْأَلُوا أَ ْه َل ال ِّذ ْك ِر َ ِ َو َما أَرْ َس ْلنَا ِم ْن قَ ْبل ِ ُ ك إِ اَّل ِر َج اًال ن َ إِ ْن ُك ْنتُ ْم اَل تَ ْعلَ ُمون “Na hatukutuma kabla yako ila wanaume tuliowapawahyi. Basi waulizeni wenye ukumbusho ikiwa nyinyihamjui.” (an-Nahl; 16:43).Na inarudiwa Aya hiyo hiyo kwa tofauti ndogokatika Surat Anbiyaa: 912 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 911/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBU وحي إِلَ ْي ِه ْم ۖ فَاسْأَلُوا أَ ْه َل ال ِّذ ْك ِر إِ ْن َ َ َو َما أَرْ َس ْلنَا قَ ْبل ِ ُ ك إِ اَّل ِر َج اًال ن َ ُك ْنتُ ْم اَل تَ ْعلَ ُمون “Na hatukuwatuma kabla yako ila wanaume tuliowapawahyi. Basi waulizeni wenye kumbukumbu, ikiwa nyinyi hamjui.” (Anbiyaa; 21:7).Na katika hadithi tukufu imekuja: “Elimu ni hazinana ufunguo wake ni kuuliza, hivyo ulizeni MwenyeziMungu awarehemu. Hakika Yeye anawalipa humo watuwanne: Muulizaji, mwalimu, msikilizaji, na anaowapenda wao.”5Lakini watu kwa tabia yao wanahitalifiana katikakueleza ambayo yapo ndani yao na wanayoyasubiri katika hisia na fikira, hivyo maendeleo ya vyombo vyamawasiliano vinastahiki kusifiwa kwa kutoa fursa kwaambaye haya inamzuia au umahususi wa mas’ala unamzuia kuuliza moja kwa moja. Na hapa kuna nafasiya maulamaa na waelekezaji katika kubeba jukumu nakuamiliana na matatizo ya kijamii na mambo ya kiutamaduni ambayo yanawapata watu, hivyo tunakutatovuti zote za Maulamaa zina sehemu maalumu yakupokea maswali na kuyajibu.Tovuti ya Sheikh Hasan Saffar ni moja ya sehemuhizi zenye kufaulu na zenye kujijadidisha kwa mwen5Kanzul-Umaal, hadithi ya 28662.1012 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1011/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUdelezo, na Mwenyezi Mungu ameniwezesha kuwamshirika katika kitengo cha kujibu mas’ala chini yauangalizi wa Muadhamu Sheikh, kulingana na mfumowake katika majibu na uwasilishaji wake wa mamboambayo yanakuja katika tovuti kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni kote.Alama za mfumo:Nimepata katika majibu ya Muadhamu Sheikh umakiniwa ibara katika wingi wa elimu, na upeo mpana katikanasaha na mawaidha pamoja na hisia za upendo, huruma na upole, kwani ni mlango wa kutekeleza wajibuvyovyote itakavyoafikiana, bali kubeba katika madhumuni yake na mazingira yake maana tukufu, katika ukweli wa hisia na kupenda kheri, ikhlasi na nasaha.Na ninaweza kuona katika mfumo wa MuadhamuSheikh yafuatayo:Kwanza: Kumshajiisha muulizaji katika kutatua tatizo lake:Yeye wakati ule ule anapoweka hatua za utatuzi, anamhimiza mwenye tatizo kujitolea kufanya kazi nakujishughulisha kwa ajili ya kufikiria na kwenda mbiokutatua tatizo. Anambebasha jukumu na anamshiriki1112 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1111/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUsha katika fikira, na anamhimiza mwenye tatizo juu yakuandaa nguvu yake na kipaji chake kilichojificha nakutegemea nafsi yake katika kutatua.Pili: Kuzalisha fursa ya nasaha namawaidha:Kwa kawaida muulizaji anakuwa yuko tayari kushirikiana pamoja na mawaidha, na kwa hiyo Muadhamu Sheikh anatia mkazo juu ya nasaha za kuelekezana kuongoza. Na wala hatosheki na jawabu tu katikampaka wa swali, bali anaongeza majibu kwa kukumbusha na nasaha zenye matunda, kuanzia na kuamilianapamoja na maelekezo ya kidini na kuathirika kwake nahali ya kijamii, ambayo inahitaji kutoa juhudi kubwakatika kutoa nasaha, na juhudi za kikazi kwa kufanyakazi ya kubadilisha.Tatu: Kurejea kwenye fani na ubobezi:Katika mas’ala ya malezi au kimatibabu ya ubobezianatia mkazo Muadhamu Sheikh juu ya ulazima wakurejea kwa wabobezi, ili jawabu lifikie lengo lake,kama ambavyo anatia mkazo juu ya kujiepusha na watabiri na wachawi. Yanadhihirika hayo wazi kwa kutoa1212 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1211/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUushahidi wa rai za maulamaa katika nyanja ya ubobeziwao, na kurejea kwenye tafiti na masomo ya kisasa.Nne: Ufuatiliaji wa moja kwa moja:Baadhi ya hali maalumu zinahitaji ufuatiliaji wa mojakwa moja kutoka kwa Muadhamu Sheikh, na pamojana wingi wa kazi zake na shughuli zake ila hakikakwa moyo na hima yake kubwa na moyo wake mpana anafuatilia, anauliza na anatia mkazo kukidhi hajaza watu. Na kiasi gani anajisikia uchungu MuadhamuSheikh anapojua tatizo la mmoja wa wananchi na hakuweza kuchangia katika utatuzi wake kutokana nasababu miongoni mwa sababu.Tano: Kubeba hima ya nchi kwa ujumla:Muadhamu Sheikh haangalii kadhia ambayo inamjiakwa mtazamo wa kimadhehebu maalumu. Hakika anatia mkazo kushirikiana na wananchi wote, kwa kufumbia macho mtazamo wa ufuasi wao wa kimadhehebu, namsomaji atakuta hayo wazi katika majibu yake kuhusubarua ambazo zinajadili mas’ala yenye ikhitilafu.Kama ambavyo Muadhamu ni mwenye kufuatiliamatukio yanayojiri na mambo mapya katika medani ya1312 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1311/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUkitaifa na kiulimwengu, ni jambo ambalo linamuwezesha kutoa mtazamo wa kina na sahihi.Sita: Upole na kumhurumia muulizaji:Baadhi ya barua zinabeba kukiri kwa wenye barua hizomadhambi na makosa waliyoyafanya, na Muadhamuanazipokea kwa maneno ya upole na huruma na maneno laini. Kwa mazungumzo ya upole, kwa manenoyenye uwiano yanayofungua mbele yake wigo kwaupana wa huruma ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, nakuwashajiisha kufungua ukarasa mpya katika maishana kufunga kurasa zilizopita.Hakika ni msadikishaji wa maneno ya Imamu Ali : “Fakihi hasa ni yule ambaye hawakatishi watutamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu, na hawakatishitamaa na huruma ya Mwenyezi Mungu na wala hawapimatumini na hila za Mwenyezi Mungu.”Kutokana na yote yaliyotangulia nimepata umuhimuwa kusambaza mkusanyiko huu wa Maswali na Majibu,ili faida yake iwaenee na wanufaike kwayo wasomajiwatukufu. Na hapa naashiria kwamba tovuti inafanyakazi ya kusambaza baadhi ya mas’ala yanayofaa baadaya kuondoa ibara zinazoonyesha watu wake.1412 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1411/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUKama ambavyo natumia fursa ya kuandika utangulizi huu ili kumshukuru Sheikh kwa shukrani nyingikiasi ambapo, amenipa fursa ya kufuatilia faili hili, nakujifunza kwake mbinu za kutatua kadhia za kijamii nakujua rai za mafakihi, na kuzidi kupata elimu mbalimbali. Ukiongezea kujua tabia ya matatizo ya kijamii nakuamiliana nayo kwa muundo wa kielimu kila siku.Namuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu anipe taufiki ya kutekeleza haki ya mwanachuoni huyu mtukufuambaye amempa upendo na heshima. Na namuombaMwenyezi Mungu amlinde na arefushe umri wake naaongoze nyendo zake. Hakika Yeye ni Msikivu Mjuzi.Mahdi Sulail,3 Rajab 1432 Hijiria.1512 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1511/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUَّ بِس ِْم ه َّح ِيم ِ للاِ الرَّحْ ٰ َم ِن الر MAS’ALA YA QUR’ANI1.Kupima kwa kutumia Qur’ani.2.Mama wa waumini.3.Haiguswi ila na waliotwaharika.4.Aya ya utakaso.5.Kupanga sura za Qur’ani tukufu.6.Ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha.7.Bismillahi katika Surat Tauba.8.Kutajwa Nabii Isa D pamoja na jina la mamayake.9.Maana ya kauli ya Nabii wa Mwenyezi Mungu IsaD: Tawafaitaniy.10. Mauti ya kwanza.11. Nini makusudio ya: Aali Yasin?1612 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1611/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUKupima kwa kutumia Qur’ani:Swali: Je, tunaweza kupima kwa kutumia Qur’ani ilituweze kujua sifa za mtu fulani au uhusiano wetu naye?Jibu: Katika Qur’ani tukufu kuna aya tukufu zinazofafanua kazi ya Qur’ani. Nayo ni kwa ajili ya kuongozana kurekebisha na kuratibu maisha ya watu, na sio kwaajili ya kupima au mengineyo ambayo hayakubaliwi naQur’ani yenyewe.“Alif lam raa. Hiki ni Kitabu tulichokiteremsha kwakoili uwatoe watu gizani uwapeleke kwenye nuru .”(Surat Ibrahim; 14:1).“Hakika hii Qur’ani inaongoza kwenye yaliyonyookakabisa na inawabashiria waumini ambao wanatendamema kwamba watapata malipo makubwa.”(Surat Bani Israil; 17:9).1712 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1711/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBU“Hiki ni Kitabu, tumekuteremshia wewe, na kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhikewenye akili.” (Surat Swad 38:29).Qur’ani tukufu inamuongoza mwanadamu kwambinu iliyo bora katika kuamiliana na misimamo yawatu, lakini uongofu huu unahitaji kutafakari na ushirikiano na kuzisemesha aya tukufu, kila unapozidiushirikiano wa mwanadamu pamoja na Qur’ani tukufuinapatikana fursa kwake ya kuongoka na kunufaika.Katika upande mwingine, hakika uhusiano na watuna kushirikiana pamoja nao unatawaliwa na maelekezo ya kidini ambayo yanalingania katika wema nadhana nzuri. Ama akipatikana anayemfanyia ubaya naanayekwenda mbio kumuudhi ni juu ya mwanadamuajihadharishe kuamiliana naye.Mama za Waumini:Swali: Kuhusiana na aya“Nabii ni aula kwa waumini kuliko nafsi zao. Na wakezake ni mama zao. Na ndugu wa tumbo ni aula we1812 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1811/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUnyewe kwa wenyewe, katika Kitabu cha MwenyeziMungu kuliko waumini wengine na wahajiri. Ila muwemnafanya wema kwa maralfiki zenu. Hayo yamekwishaandikwa Kitabuni.”Kwa nini hapa wametajwa wake za Nabii baada yakutajwa Mtume 7, wakati waumini kulingana na ufahamu wangu katika aya wao ni Ali bin Abi Twalib D,naomba ufafanuzi wa kuniondolea mkanganyo?Jibu: Anasema Sheikh Naswir Makarim Shirazi katika Tafsiri yake: Qur’ani imetaja katika aya hii uborawa NabiiD kwa Waislamu kwa sura ya jumla, namaana ya hayo ni kwamba hakika Nabii ni bora kwamwanadamu Mwislamu kuliko nafsi yake katika maslahi yote ambayo anayamiliki mwanadamu katikahaki ya nafsi yake (al-Amthal, Juz. 12, Suratul-Ahzabaya 6).Ama kutajwa wanawake wa Nabii katika aya nakwamba wao ni kama mama za waumini baada yakutajwa Mtume 7, imekuja aya ili kutia mkazo kutokuwepo kurithi ila baina ya mahram wa kikweli kweli. Pamoja na kwamba Nabii ni kama mfano wa babawa waumini na wake zake ni mfano wa mama zao, ilahakuna kurithiana. Ukiongezea kutojuzu kuoa wake waNabii baada ya kufariki kwake.1912 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 1911/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUSheikh Naswiru Makarim Shirazi anasema katikatafsiri yake: Hukumu ya pili katika mlango huu inaambatana na wake wa Nabii ambapo wanazingatiwa nikama mama za Waumini wote, nayo bila shaka ni umama wa kimaanawiya na wa kiroho, kama ambavyo Nabii 7 ni baba wa kiroho na kimaanawi katika umma.Hakika athari ya mafungamano haya ya kimaanawiilikuwa imezingirwa katika mas’ala ya kuhifadhi heshima ya wake za Nabii na uharamu wa kuwaona kwao,kama ilivyokuja hukumu wazi katika uharamu wa kuwaoa wao baada ya kufariki Nabii 7 katika aya zaSura hii (al-Amthali, Juz. 13, Suratul-Ahzab, aya ya 6).Hawaigusi ila wenye kutwaharika:Swali: Katika kauli Yake (swt)“Hakika hii bila shaka ni Qur’ani Tukufu. Katika Kitabu kilichohifadhiwa. Hapana akigusaye ila waliotakaswa.” (Surat al-Waqia’ 56:77-79)”.Ni nani waliotwaharika katika aya tukufu?Jibu: Tunanukuu ambayo yamekuja katika kitabu chatafsiri ya al-Amthal cha Ayatullahi Naswir Makarim2012 17 (4-75 x 7) Maswali na Majibu 10 Nov 2017 .indd 2011/10/2017 6:51:32 PM

MASWALI NA MAJIBUShirazi kuhusu aya tukufu “Hawaigusi ila waliotwaharika” iliyoko Suratul-Waqia’; 56:79.Wengi wa wafasiri wametaja – kufuatana na baadhi ya riwaya zilizopokewa kutoka kwa Maimamumaasumina G – kutojuzu kugusa maandishi yaQur’ani tukufu bila ya kuoga au bila ya kuw

MASWALI NA MAJIBU ميِحِرلا َّنِمَٰحْرلا َِّالل َّمِسِْب NENO LA MCHAPISHAJI M aswali na Majibu ni kitabu kinachotoa mwongo-zo kwa njia ya maswali na majibu. Kitabu hiki ni mkusanyiko wa maswali aliyoulizwa Sheikh Hasan al-Saffar katika programu yake ya maswali na majibu ili-yoandaliwa katika tovuti yake.

Related Documents:

4. Biblia inajibu maswali tunayojiuliza Mwanamke fulani alitambua kwamba Biblia ina majibu ya maswali yaliyomhangaisha kwa miaka mingi.OnyeshaVIDEO,kisha mzu-ngumzie maswali haya: Katika video hiyo, mwanamke huyo alijiuliza maswali gani? Kujifunza Biblia kulimsaidiaje? Biblia inatutia moyo tuulize maswali.SomaMathayo 7:7, kisha mzungumzie .

MWALIMU ONYANGO #DIRA SERIES, USHAIRI# KCSE 2007-2019. MASWALI NA MAJIBU. 0707311302 Soma shairi hili kisha ujibu maswali yayofuata: Kila Mchimba Kisima; Musa Mzenga 1. Tenda utendapo tendo, tenda tendo kwa hekima, Lindamane mwenendo, sawa na yakio kalmia, Kalmia yenye upendo, kufurahisha mtima, Kila mchimba kisima, budi hungia mwenyewe. 2.

maswali yako mengi iwezekavyo kuhusu Australia Tuanze kwa kujua nini haswa WEWE unachotaka kujua Tumia nafasi ya mstari iliyopo hapo chini ili kuandika maswali yako Wakati unaposikia majibu ya moja wapo ya maswali yako wakati upo kwenye AUSCO, andika majibu hayo AUSCO hukupatia wewe maelezo mengi na inaweza kuwa vigumu kukumbuka maelezo yote!

1. Pata orodha ya maswali yako na uifungue kwenye ukurasa wa kwanza. 2. Tumia habari katika mwongoza huu wa Kiswahili kuweka alama kwa majibu yako kwenye karatasi ya orodha ya maswali la Kiingereza. USIANDIKE MAJIBU YAKO KWENYE MWONGOZO HUU. 3. Kabla ya kujibu swali la kwanza, hesabu watu wanaoishi katika nyumba

Kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafa-nyayoKazi,Bukula2,kimekusudiwakumpamtotowenu kanuninzurisana za Kimaandiko. Ukitazama Yaliyomokati-ka ukurasa wa 4na 5utaona habari mbalimbali zinazozungu-mziwa katika kitabu hiki. Hata hivyo, kitabu hiki kimekusudi-wa kutimiza mengi zaidi. Fikiria mamboyafuatayo: (1) Kitabu hiki kinamhusisha .

Maswali na majibu Ufafanuzi Uchambuzi Maelezo Mifano Maswali na majibu Majadiliano JUMA 5. 219 KIPINDI SHABAHA NJIA ZA KUFUNDISHIA NYENZO ZA KUFUNDISHIA MADA KUU MADA NDOGO MAONI HAKIUZWI Yatumiwe na Kiswahili Fasaha Kiswahili, Kidato cha 2 Maazimio ya Kazi Muhula wa Kwanza 1 2 3

MASWALI & MAJIBU UTARATIBU, SIFA NA VIGEZO VYA UTOAJI MIKOPO KWA 2018/2019. Tunawawezesha Wahitaji 2 1. Swali: Ninapaswa kufanya nini ili niweze kuanza kuomba mkopo kwa njia ya mtandao (OLAMS)? Jibu: Soma mwongozo uliotolewa na Bodi ambao unapatikana katika tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz). Baada ya kuusoma Mwongozo, fungua mtandao

cowardice following a navel defeat in the Battle of Ushant to the French in 1 . Elsecar/Wentworth Circular Walk page 2 of 5 1778. Its entasis visibly bulges, due to a height adjustment caused by funding problems after the death of the Marquess 3. Take the right hand of two paths as it crosses a field and continues to climb. Cross the stile, then a further three fields (and stiles). The route .