Kutathimini Matumizi Ya Lugha Na Dhamira Katika Tamthilia Za .

1y ago
13 Views
2 Downloads
816.43 KB
95 Pages
Last View : 17d ago
Last Download : 3m ago
Upload by : Cannon Runnels
Transcription

KUTATHIMINI MATUMIZI YA LUGHA NA DHAMIRA KATIKATAMTHILIA ZA KINJEKETILE NA NYERERE NA SAFARI YAKANAANI: UTAFITI LINGANISHICYPRIAN FIDESTASNIFU ILIYOWASILSHWA IKIWA NI SEHEMU YA MASHARTI YAKUPATIWA SHAHADA YA UZAMILI YA (M.A KISWAHILI) YA CHUOKIKUU HURIA CHA TANZANIA2017

iiUTHIBISHOAliyetia sahihi hapa anathibitisha kuwa amesoma tasnifu hii iitwayo,Kutathminimatumizi ya lugha na dhamira katika tamthiliya za Kinjeketile na Nyerere naSafari ya Kanaani: Utafiti linganishi na kupendekeza ikubaliwe na Chuo KikuuHuria cha Tanzania kwa kwa ajili kukamilisha masharti ya Shahada ya Uzamili yaKiswahili (M.A) ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania. .Prof. Emmanuel D. Y. Mbogo(Msimamizi) Tarehe

iiiHAKIMILIKITasnifu hii au sehemu yake yoyote hairuhusiwi kukaririwa, kuhifadhiwa,kubadilishwa kwa mbinu yoyote ile: kieletroniki, kimekanika, kunakilishwa,kurudufiwa kwa utaratibu wowote ule katika hali yoyote ile bila idhini ya maandishikutoka kwa mwandishi wake au kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, kwa niabayake.

ivTAMKOMimi, Cyprian Fides, nathibitisha kwamba tasnifu hii ni kazi yangu halisi nahaijawahi kuwasilishwa katika chuo kikuu kingine kwa ajili ya kutunukiwa shahadayoyote. .Saini Tarehe

vTABARUKUKazi hii ninaitabaruku kwa wazazi wangu, familia yangu, walimu na wanafunziwenzangu ambao wamejitoa kwa hali na mali katika kufanikisha malengo yangu yakitaaluma ambayo yamenifikisha hatua hii ya kutunukiwa Shahada ya Uzamili katikaKiswahili.

viSHUKURANINamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai, nguvu na uwezo wa kukamilishakazi hii. Nawashukuru wote waliokuwa wakinipa ushauri na mawazo mbalimbalihasa walimu wangu wa shahada ya uzamili. Ni vigumu kuwataja wote ila sina budikuwaomba radhi wale nisiowataja. Napenda kutoa shukurani zangu za dhati kwamsimamizi wangu Profesa Emmanuel D. Y. Mbogo ambaye hakusita wala kuchokakunishauri katika hatua zote za ukamilishaji wa kazi hii. Kwa hakika alijitoa sanakatika kuniongoza, kunishauri, kunikosoa na kunielekeza katika hatua mbalimbali zautafiti wangu.Hivyo kutokana na ushauri wake ilinilazimu kutumia muda mwingikutafakari na kufanyia kazi maelekezo yake yaliyonisaidia kukamilisha utafiti huu.Nakushukuru sana Profesa Mbogo, nakuombea kwa Mungu akupe maisha marefuyenye baraka, amani na furaha tele. Pia napenda kuwashukuru wazazi wanguwapendwa, BwanaCyprian Abel Moshy na Bi Josephine Jacob Tengia kwakunisomesha hatua mbalimbali hadi kufikia kusoma Shahada ya Uzamili. Munguawabariki awape afya, amani na furaha katika maisha yenu yote.Aidha napenda kumshukuru mume wangu mpendwa Bwana Sixbert John Mahundikwa kunipa msaada wa hali na mali na kuniwezesha kukamilisha kazi hii. Pianawashukuru watoto wangu Alice, Stanley na Charles kwa kunipa ushirikiano katikakusoma kwangu na kuniwezesha kukumilisha kazi hii ya uzamili.Vilevilenawashukuru wanachuo wenzangu wa shahada ya uzamili, kwa ushirikianowalionipakwa kunihimiza na kunitia moyo bila kuchoka ili niweze kumalizashahada yangu ya uzamili Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

viiIKISIRILengo kuu la utafiti huu ni kutathmini matumizi ya lugha na dhamira zilizojitokezakatika tamthiliya za Kinjeketile na Nyerere na Safari ya Kanaani: Utafiti linganishi.Ili kufanikisha utafiti huu, mtafiti ametumia mbinu za maktabani katika kukusanyana kuwasiilisha data kimaelezo. Pia marejeleo mbalimbali kutoka tamthiliya zaKiswahili yalipitiwa.Nadharia ya fasihi ya jamiindiyo iliyotumika katikakufanikisha utafiti huu. Nadharia hii imemsaidia mtafiti kuweza kubaini mawazombalimbali ya waandishi katika tamthiliya zao za utafiti linganishi. Matokeo yauchanganuzi wa data yaliweza kujibu maswali ya utafiti. Tamthiliya hizi teulezimebainisha jamii yetu kabla ya uhuru na baada ya uhuru. Dhamira za uongozimbaya, rushwa na usaliti zimejitokeza. Matokeo mengine ni dhamira ya ukomboziiliyomfanya mkoloni aondolewe katika ardhi ya jamii ya watu wa Kusini ili wawehuru, kutumia ardhi yao na mali nyingine zilizopatikana katika jamii yao. Piauzalendo ulitakiwa kwa jamii kwa kuwapeleka vijana kwenye mafunzo ya Jeshi laKujenga Taifa na tohara. Tamthiliya za Kinjeketile na Nyerere na Safari yaKanaani zina mchango mkubwa katika jamii kwa kuwasilisha ujumbe ambao ni wakihistoria unaoiwezesha kujua matukio mbalimbali ya nchi kabla na baada ya uhuru

viiiYALIYOMOUTHIBISHO . iiHAKIMILIKI . iiiTAMKO . ivTABARUKU . vSHUKURANI . viIKISIRI . viiORODHA YA MAJEDWALI. xiiiSURA YA KWANZA . 1UTANGULIZI . 11.1Utangulizi . 11.2Usuli wa Mada . 21.3Tamko la Tatizo la Utafiti . 41.4Malengo ya Utafiti . 51.4.1Lengo Kuu . 51.5Maswali ya Utafiti . 51.6Umuhimu wa Utafiti. 61.7Mipaka ya Utafiti . 61.8Uzingativu wa Maadili . 61.9Vikwazo vya Utafiti . 71.10Utatuzi wa Vikwazo . 71.11Muundo wa Tasnifu . 81.12Hitimisho . 8

ixSURA YA PILI . 9MAPITIO YA KAZI TANGULIZI NA KIUNZI CHA NADHARIA . 92.1Utangulizi . 92.2Dhana ya Fasihi Linganishi . 92.3Tafiti kuhusu Tamthiliya za Kiswahili . 112.4Pengo la Utafiti . 142.5Matumizi ya Lugha . 142.5.1 Tamathali za semi. 142.5.2 Kejeli . 162.5.3 Sitiari . 162.5.4 Tashihisi . 172.5.5 Tashibiha . 172.5.6 Takriri . 172.5.8 Tashtiti . 182.5.9 Mdokezo . 182.6Dhana ya Dhamira . 192.7Kiunzi cha Nadharia. 202.7.1 Nadharia ya fasihi ya jamii. 212.8Hitimisho . 22SURA YA TATU . 23MBINU NA NJIA ZA UTAFITI . 233.1Utangulizi . 233.2Eneo la Utafiti . 233.3Kundi Lengwa . 23

x3.4Usampulishaji. 243.5Sampuli . 243.6Mbinu za ukusanyaji data . 243.6.1Mbinu ya Usomaji Matini mbalimbali . 243.7Zana za Utafiti . 253.7.1 Matini . 253.7.2 Kompyuta . 263.7.3 Simu ya mkononi . 263.8Hitimisho . 26SURA YA NNE . 27UWASILISHAJI NA UCHAMBUZI WA DATA . 274.1Utangulizi . 274.2Vipengele vya Lugha katika Tamthiliya Teule . 274.3Mdafao wa Ujitokezaji wa Vipengele vya Lugha katika Tamthiliya zaKinjeketile na Nyerere na Safari ya Kanaani . 284.4Uteuzi na Matumizi ya Tamathali za Semi . 294.4.2 Nidaa . 314.4.3 Tashibiha . 334.4.4 Tashihisi . 344.4.5 Sitiari . 354.4.6 Takriri . 374.4.7 Tashtiti . 384.4.8 Tanakali Sauti . 394.4.9 Kejeli . 40

xi4.4.10 Mdokezo. 414.5Misemo. 424.6Methali . 444.7Nahau . 454.8Tamathali za Semi katika Tamtiliya ya Kinjeketile . 464.8.1 Nidaa . 474.8.2 Takriri . 484.8.3 Sitiari . 504.8.4 Tashibiha . 514.8.5 Kejeli . 524.8.6 Tashtiti . 534.8.7 Tashihisi . 544.8.8Mdokezo. 544.9Methali . 554.10Misemo. 564.11Kuwasilisha Dhamira kuu za Tamthiliya . 574.12Kulinganisha na Kulinganua Vipengele vya lugha katika Tamthiliya zaKinjeketile na Nyerere na Safari ya Kanaani . 594.13Kufanana . 594.14Kutofautiana . 614.15Kufanana au Kutofautiana kwa Dhamira Zilizojitokeza katika TamthiliyaTeule . 624.15.1 Matabaka . 624.15.2 Uongozi Mbaya . 63

xii4.15.3 Nafasi ya Mwanamke . 634.15.4 Umaskini . 644.15.5 Rushwa na Usaliti. 644.15.6 Mapenzi . 654.15.7 Ukombozi . 654.15.8 Hitimisho . 66SURA YA TANO . 67MUHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO . 675.1Utangulizi . 675.2Muhtasari wa Matokeo ya Utafiti . 675.3Hitimisho . 715.4Mapendekezo . 73MAREJELEO . 74

xiiiORODHA YA MAJEDWALIJedwali Na 4.1: Vipengele vya lugha katika Nyerere na Safari ya Kanaani . 27Jedwali Na 4.2: Vipengele vya Lugha katika Tamthiliya ya Kinjeketile . 28Jedwali Na 4.3: Mdafao wa Ujitokezaji wa Vipengele vya Lugha katikaTamthiliya ya Kinjeketile na Nyerere na Safari yaKanaani . 28Jedwali Na 4.4: Ujitokezaji wa Tamathali za Semi katika Tamthiliya yaNyerere na Safari ya Kanani . 30Jedwali Na 4.5: Mdafao wa Ujitokezaji wa Tamathali za Semi katikaTamthiliya ya Nyerere na Safari ya Kanaani . 30Jedwali Na 4.6: Mifano ya baadhi ya Nidaa katika Tamthiliya ya Nyererena Safari yaKanaani. 32Jedwali Na 4.7: Tashibiha katika Tamthiliya ya Nyerere na Safari ya Kanaani . 33Jedwali Na 4.8: Baadhi yaTashihisi Zilizojitokeza katika Tamthilia ya Nyerere naSafari ya Kanaani . 35Jedwali Na 4.9: Sitiari katika Tamthiya ya Nyerere na Safari ya Kanaani . 36Jedwali Na 4.10: Ujitokezaji wa Takriri katika Tamthiliya ya Nyerere naSafari ya Kanaani . 37Jedwali Na 4.11: Ujitokezaji wa Tashtiti katika Tamthiliya ya Nyererena Safari ya Kanaani. 38Jedwali Na 4.12: Matumizi ya baadhi ya Tanakali Sauti katika Tamthiliyaya Nyerere na Safari yaKanaani . 40Jedwali Na 4.13: Ujitokezaji wa Kejeli katika Tamthiliya ya Nyererena Safari yaKanaani. 41

xivJedwali Na 4.14: Ujitokezaji wa Mdokezo Katika Tamthiliya ya Nyerere naSafari yaKanaani . 42Jedwali Na 4.15: Ujitokezaji wa Misemo katika Tamthiliya ya Nyerere naSafari yaKanaani . 43Jedwali Na 4.16: Ujitokezaji wa Methali katika Tamthiliya ya Nyerere naSafari yaKanaani . 44Jedwali Na 4.17: Ujitokezaji wa Nahau katika Tamthiliya ya Nyerere naSafari ya Kanaani . 45Jedwali Na 4.18: Mdafao wa Ujitokezaji wa Tamathali za Semi katikaTamthiliya ya Kinjeketile . 47Jedwali Na 4.19: Ujitokezaji wa Nidaa katika Tamthilia ya Kinjeketile . 48Jedwali Na 4.20: Ujitokezaji wa Takriri katika Tamthiliya ya Kinjeketile . 49Jedwali Na 4.21: Ujitokezaji wa Sitiari katika Tamthiliya ya Kinjeketile . 50Jedwali Na 4.22: Ujitokezaji wa Tashibiha katika Tamthiliya ya Kinjeketile . 51Jedwali Na 4.23: Ujitokezaji wa Kejeli kutoka katika Tamthiliya ya Kinjeketile . 52Jedwali Na 4.24: Ujitokezaji wa Tashititi katika Tamthiliya ya Kinjeketile. 53Jedwali Na 4.25: Ujitokezaji wa tashihisi katika Tamthiliya ya Kinjeketile. 54Jedwali Na 4. 26: Ujitokezaji wa Mdokezo katika Tamthiliya ya Kinjeketile . 55Jedwali Na 4.27: Ujitokeazji wa Methali katika Tamthiliya ya Kinjeketile . 56Jedwali Na 4.28: Ujitokezaji wa misemo katika Tamthiliya ya Kinjeketile . 56Jedwali Na 4.29: Ujitokezaji wa Dhamira katika Tamthiliya Teule . 57Jedwali Na 4.30: Ujitokezaji wa Dhamira katika Tamthiliya ya Kinjeketile . 58Jedwali Na 4.31: Vipengele vya Lugha Vinavyofanana katika Tamthiliya Teule . 60Jedwali Na 4.32: Vipengele vya Lugha Vinavyotofautiana katika Tamthiliya

xvTeule. 61Jedwali Na 4.33: Kufanana kwa Dhamira Zilizowasilishwa na Vipengelevya Lugha . 62Jedwali Na 4.34: Kutofautiana kwa Dhamira zilizowasilishwa na Vipengele vyaLugha. 64

1SURA YA KWANZAUTANGULIZI1.1UtanguliziSura hii tangulizi inatoa usuli wa mada katika utafiti huu. Sura hii inahusu usuliwa mada, tamko la tatizo la utafiti,malengo ya utafiti, maswali ya utafiti, umuhimuwa utafiti, mipaka ya utafiti, uzingativu wa maadili, vikwazo vya utafiti, utatuzi wavikwazo, muundo wa tasnifu na hitimisho. Kabla ya kuanza tupate historia fupi yawasanii wa tamthiliya za Kinjeketile na Nyerere na Safari ya Kanaani.Tamthiliya yaKinjeketile imetungwa na msanii Ebrahim Hussein (1969) ambaye ni msaniialiyeandika kazi hii ya kisanii kwa kutumia tukio la kihistoria lililotokea Kusinimwa Tanzania. Wananchi wa Kusini walipambana na Mjerumani ili kumwondoakatika ardhi yao. Mwandishi ameonesha jinsi wananchi walivyoamini kuwa maji nikinga ya vita kwa kuwa itafanya risasi kuwa maji. Kinjeketile aliaminiwa nawananchi wa Kusini na kuweza kuwaunganisha makabila ya Kusini kuwa kitukimoja na mshikamano na kupambana na Mjerumani. Mwandishi ameendeleakuonesha kuwa maji yalikuwa ni ishara ya umoja kwa kuwa kupitia imani ya majiwananchi waliweza kuungana na kupambana na Mjerumani. Msanii E. Husseinanafaa kuigwa kwa mchango wake katika fasihi ya Kiswahili.Tamthiliya ya Nyerere na Safari ya Kanaani imetungwa na msanii EmmanuelMbogo (2015) ambaye ameandika jambo la kihistoria baada ya Tanzania kupatauhuru. Msanii ametuonesha baada ya uhuru watu wachache walijilimbikizia malikwa muda mfupi na kuwa matajiri. Hvyo watu hawa walikuwa wamepingana na Rais

2Nyerere. Profesa E. Mbogo ni maarufu kwa uandishi wa Drama na FasihiyaKiswahili na mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.1.2Usuli wa MadaKatika fasihi yoyote ni lazima iwe na fani na maudhui. Katika fani kunakuwa namtindo, lugha, mandhari, na wahusika. Wasanii wa kazi za tamthiliya wanapendakutumia vipengele mbalimbali vya lugha katika kazi zao ili kufikisha ujumbe kwajamii. Kazi yoyote ya msanii ili iweze kueleweka vizuri lazima lugha ichambuliwekufuatana na jinsi ilivyotumika katika vipengele vyake mbalimbali kwa pamoja ilikuleta maana kamili iliyopo katika kazi hiyo. Kila msanii ana ubunifu wake katikakuandika kazi yake kwa kubuni mtindo atakaoutumia katika kazi yake kwa mfanokatika kuteua msamiati muundo na lugha. Katika kuchunguza kazi ya msanii ilikupata ujumbe wa kazi hiyo hatuna budi kuhusisha vipengele vya lugha katika kazihusika.Katika utafiti huu tumechunguza matumizi ya lugha iliyotumika kulingana navipengele vyake na dhamira zilizojitokeza katika tamthiliya ya Kinjeketileiliyoandikwa na Ebrahim Hussein na tamthiliya ya Nyerere na Safari ya Kanaaniiliyoandikwa na Profesa Emmanuel Mbogo. Katika kazi hii utafiti umetathminimatumizi ya lugha iliyotumika katika tamthiliya hizi ikiwa ni pamoja na vipengelevyakena dhamira zilizojitokezakatika kuwasilishaujumbe kwa jamii kwakuwalinganisha na kuwatofautisha waandishi hawa wawili. Utafiti huu umekuwawa kihistoria umetumia lugha kwa kupitia vipindi mbalimbali kuonesha mchangowa waandishi hawa katika kazi ya sanaa ya uandishi. Waandishi hawa wamechangiakukuza historia ya nchi yetu na kuiwezewesha jamii kuona umuhimu wa kusoma

3tamthiliya za kihistoria ili kupata maarifa ya kihistoria yaliyopo na kuweza kuonanchi imetoka wapi.Katika kutathmini matumizi ya lugha utafiti huu umewalinganisha wasanii wawiliambapo ni msanii E. Mbogo ambaye ni msanii nguli aliyebobea katika kuandikadrama na kuielimisha jamii kupitia tamthiliya zake. Kwa utafiti huu tumetumiakitabu chake cha Nyerere na Safari ya Kanaani (2015) ambapo ameelezea Nyererena harakati za kuimarisha vijana kabla ya kuanza kazi wawe wazalendo kwakulitumikia Jeshi la Kujenga Taifa. Vilevile kuwawezesha vijana kujitegemea hatapale ambapo hawatapata ajira.Tumefanya utafiti pia kwa kutumia tamthiliya yaKinjeketile iliyotungwa na msanii Ebrahim Hussein ambaye katika uandishi naye piaanaibua hisia za usomaji kwa kuandika tamthiliya za Kiswahili. Mwandishianaonesha Kinjeketile alivyokuwa akiwaunganisha wananchi wa Kusiniwakatiwakipambana na Wajerumani akitetea uhuru wa Waafrika, akilaani uonevu wawakoloni kwa Waafrika katika nchi yao kwa kubaguliwa na kutengwa kabisa nawazungu (Wajerumani). Kinjeketile alionesha maji yalivyotumiwa kama kinga dhidiya mashambulizi ya risasi zilizokuwa zikipigwa na Wajerumani. Kinjeketile alitumiamaji kwa kuwaunganisha wananchi kuwa kitu kimoja ili waweze kumshambuliaMjerumani kwa urahisi. Na alifanikiwa kuyaunganisha makabila ya Kusini mwaTanzania na kuwa na imani kuwa watamshinda Mjerumani.Tamthiliya hizi za Kinjeketile na Nyerere na Safari ya Kanaani ni tamthiliya zakihistoria kwa kuwa zinawazungumzia watu au wanaharakati wa kihistoria makuchayawakoloni.Wanaharakati hawa walikuwa na uchungu na nchi yao kwa uzalendo

4waliokuwa nao bila woga walitetea waziwazi uhuru wa nchi yao. Kupitia tamthiliyahizi jamii imejifunza jinsi nchi zilivyopitia misukosuko katika kuleta mabadilikokatika nchi yao.Kupitia kwa wasanii hawa jamii imeendelea kujifunza historia ya nchi kutoka kizazikimoja hadi kingine kwa kuwa historia hubaki kuwa historia wakati wote. Hivyowasanii huchangia kwa kiasi kikubwa muendelezo wa matukio mbalimbali ambayoyatabaki kuwa ni historia.Utafiti huu umechunguza na kutathmini matumizi ya lughana dhamira ikiwa ni pamoja na vipengele vya lugha kwa kulinganisha tamthiliya yaKinjeketile na Nyerere na Safari ya Kanaan. Aidha umechunguza kutofautiana aukufanana kwa wasanii hawa katika kufikisha ujumbe kwa jamii.1.3Tamko la Tatizo la UtafitiKatika kuelezea jambo la kihistoria katika jamii waandishi wa kazi za sanaawanaweza kutumia lugha kufikisha ujumbe uliokusudiwa kuwezesha kizazi kimojahadi kingine kujifunza historia.Waandishi wa wana jukumu la kutumialughainayomwezesha msomaji kupata ujumbe uliokusudiwa.Tatizo la utafiti ni kwamba tamthiliya za kihistoria hazijafanyiwa uchunguzi wa kinana kuweka wazi jinsi lugha na vipengele vyake vinavyoweza kumtofautisha nakumfananisha msanii mmoja na mwingine katika kuwasilisha ujumbe kwa jamii.Kwa utafiti huu tutaweza kuainisha matumizi ya lugha na dhamira zinazojitokezakatika tamthiliya teule.Pia kulinganisha na kulinganua matumizi ya lugha na dhamirazilizojitokeza katika tamthiliya hizo.

51.4Malengo ya UtafitiUtafiti huu umetathmini matumizi ya lugha na dhamirakatika tamthiliya zaKinjeketile (1970) na Nyerere na Safari ya Kanaani (2015) katika kuwasilisha kwanamna tofauti ujumbe uliokusudiwa kwa jamii.1.4.1Lengo KuuKutathmini matumizi ya lugha na dhamira katika tamthiliya teulevipengele vinavyotofautiana na vinavyofananakatikaili kubainikutumia lugha kufikishaujumbe katika mkabala wa fasihi linganishi.1.4.2Malengo MahsusiUtafiti huu una malengo mahususi yafuatayo:(i)Kuainisha vipengele vya lugha katika tamthiliya teule.(ii)Kulinganisha na kulinganua vipengele vya lugha katika tamthiliyateulekufikisha.(iii) Kuainisha dhamira zinazojitokeza katika tamthiliya teule.(iv) Kulinganisha na kulinganua dhamira zinazojitokeza katika tamtiliya teule.1.5Maswali ya Utafiti(i)Ni vipengele vipi vya lugha vinajitokeza katika tamthiliya teule?(ii)Uteuzi wa vipengele vya lugha katika tamthiliya teule unafanana aukutofautiana vipi katika kuwasilisha ujumbe kwa jamii?(iii) Ni dhamira zipi zinajitokeza katika tamthiliya teule?(iv) Uteuzi wa dhamira katika tamthiliya teule unafanana au kutofautianakatika kufikisha ujumbe kwa jamii?vipi

61.6Umuhimu wa UtafitiUtafiti ni sayansi ya uchunguzi ambao ni muhimu kwa jamii. Katika uchunguzi wamatumizi ya lugha katika tamthiliya za Kinjeketile na Nyrere na Safari yaKanaaniutafiti umesaidia kuelimisha jamii kuona jinsi gani hawa wapigania haki Nyerere naKinjeketile walivyokuwa wazalendo na dhamira ya ukombozi katika nchi yao.Utafitipia umeonesha jinsi Nyerere na Kinjeketile walivyohamasisha watu wao kupiganiauhuru wao. Kukataa kutawaliwa na kuonewa pasipo na sababu za msingi. Piaumegundua jinsi wananchi walivyokuwa na umoja katika kupigania uhuru waohadikujikomboa na kujitoa katika makucha ya wakoloni.Aidha utafiti huu utakuwa changamoto kwa watafiti wengine kufanya utafiti juu yatamthiliya za Kiswahili zilizojikita katika historia ya mambo mbalimbali yaliyotokeakatika jamii.1.7Mipaka ya UtafitiUtafiti huuumetathmini matumizi ya lugha na dhamira zilizojitokeza katikatamthiliya za Kinjeketile na Nyerere na Safari ya Kanaani.Zipo tamthiliya nyingi za kihistoria lakini kwa sasa nimeshughulikia tamthiliya zakihistoria za Kinjeketile iliyoandikwa na Ebrahim Hussein na Nyerere na Safari yaKanaani iliyoandikwa na Emmanuel Mbogo. Vipengele vya lugha tamathali zasemi,misemo, methali na nahau ndivyo vimetumika katika kujenga hii kazi ya fasihi.1.8Uzingativu wa MaadiliKatika utafiti huu kipengele hiki cha uzingativu wa maadili umejadili masualayaliyomwezesha mtafiti kuzingatia, na kudumisha maadili yake kabla na baada ya

7kukusanya data. Masuala ya kimaadili huibuka katika aina zote za utafiti usio wakitakwimu na ulio wa kitakwimu, Padget (2002) katika kip

katika tamthiliya za Kinjeketile na Nyerere na Safari ya Kanaani: Utafiti linganishi. Ili kufanikisha utafiti huu, mtafiti ametumia mbinu za maktabani katika kukusanya na kuwasiilisha data kimaelezo. Pia marejeleo mbalimbali kutoka tamthiliya za Kiswahili yalipitiwa. Nadharia ya fasihi ya jamii ndiyo iliyotumika katika

Related Documents:

Data zilirekodiwa katika kinasa sauti na kunukuliwa kwa maandishi. . Tofauti za Matumizi ya Lugha katika Miktadha Mbalimbali ya Mazungumzo 13 sehemu ya pili inahusu tofauti ya matumizi ya lugha katika miktadha mbalimbali. Sehemu ya tatu inafafanua mkabala wa kinadharia uliotumika katika uch

Nyenzo za kufundisha huwa viungo muhimu wakati wa utoaji wa mafunzo. Utafiti ulichunguza matumizi ya nyenzo katika ufundishaji wa Kiswahili katika shule za msingi za umma katika Jimbo la Nyandarua, Kenya. Madhumuni ya utafiti yalikuwa: Kuainisha nyenzo zinazotumika kufundisha Kiswahili, Kutathimini kiwango cha matumizi ya

inafuata mchango wa baadhi ya wanaisimu wa lugha ya Kiingereza, Kiarabu na Kiswahili walivyobainisha uwepo wa kategoria ya nomino (majina) katika lugha hizi. 1.1.2 Majina Katika Lugha ya Kiingereza Wataalamu mbalimbali wa lugha ya kiingereza wamebainisha kuwepo kw

Kukuza lugha. Aghalabu tungo zote za fasihi hutumia lugha. Isitoshe, fasihi hutumia mbinu nyingi za lugha. Wasimulizi na waandishi wa fasihi huhitaji kuwa na ukwasi wa lugha. Kuhifadhi mila, tamaduni na itikadi za jamii. Aghalabu kazi za fasihi (hasahasa Fasihi Simulizi) huambatanishwa na desturi mbalim

KI 214 UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI MBINU ZA UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI I. Malengo ya ufundishaji lugha kwa wageni Lengo kubwa ni kwamba ili mwanafunzi aweze kujua lugha hiyo kwa stadi zote za lugha ile. Stadi za lugha ni 1. Kusikiliza 2.kuzungumza

iii) Sauti iv) Ishara za mwili. Ni mfumo wa sauti za nasibu zinazotumiwa na wanadamu katika mawasiliano. Sifa za lugha. i) Hakuna lugha iliyo bora kushinda zingine. –zote ni sawa. ii) Kila lugha ina sifa zake. iii) Lugha hubadilika kutegemea mazingira, aina ya

kila lugha hutumia mfumo fulani wa sauti mahususi katika lugha hiyo pekee. 5. Fonetiki - huchunguza sauti zinazotamkwa na binadamu bila kuzingatia lugha yoyote. 6. Mofolojia - (au sarufi maumbo) ni tawi la isimu linalochunguza maneno ya lugha fulani, aina

Python for Scientific Programming Paul Sherwood CCLRC Daresbury Laboratory p.sherwood@dl.ac.uk. Overview Introduction to the language – (thanks to David Beazley) Some important extension modules – free tools to extend the interpreter – extending and embedding with C and C Chemistry projects in Python – some examples of science projects that use Python Our experiences – a GUI for .